Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 31 March 2022

DP WORLD YAZINDUA JUKWAA LA BIASHARA MTANDAONI

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Biashara, Viwanda na Uwekezaji, Prof. Godius Kahyarara (aliyesimama kushoto) na Naibu Balozi wa UAE nchini, Mohammad Al Bahri wakishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano kati ya TCCIA na DP World katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Machi, 2022. Wanaotia saini makubaliano hayo ni Rais wa TCCIA, Paul Koyi, (aliyeketi kushoto) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dubai Trade World, Mahmood Al Bastaki.
  • DUBUY.com ambayo ni sehemu ya watoa huduma wa kimataifa wa DP World inafungua ukanda mpya wa biashara ya kidijitali nchini Tanzania na katika Ukanda wa Afrika Mashariki.
  • Jukwaa hilo la biashara mtandaoni linaleta ufanisi na uhakika katika biashara za jumla kwa wafanyabiashara nchini Tanzania, kwa kuwezesha upatikanaji wa masoko kwa biashara za ukubwa mbalimbali.
  • Ukanda mpya wa biashara za kidijitali unaoundwa na DUBUY.com unaenda sambamba na kanda za usafirishaji ambazo DP World imejenga katika bara zima la Afrika, ikijumuisha bandari, gati na huduma za usafirishaji.
Dar es Salaam, 29 Machi 2022 – DP World imezindua rasmi jukwaa lake la biashara za jumla mtandaoni liitwalo DUBUY.com nchini Tanzania. Soko hilo la mtandaoni litawapa wafanyabiashara wa Kitanzania nafasi ya kushiriki katika masoko ya kimataifa. Jukwaa hilo pia litakuza usalama na uhakika katika biashara, kupitia bandari na mtandao wa huduma za usafirishaji zinazoendeshwa na DP World.

Jukwaa hili jipya linawezesha wafanyabiashara wa Kitanzania kuuza bidhaa za jumla za aina mbalimbali ndani na nje ya nchi. Mbali na teknolojia ya hali ya juu, DUBUY.com inawapa watumiaji fursa ya kipekee ya kufaidika na miundombinu inayoendeshwa na DP World - ikiwemo Bandari ya Berbera nchini Somalia - katika kutatua vikwazo mbalimbali vya ukuaji wa biashara ya mtandaoni barani Afrika. Hii ni pamoja na uhakika katika ukamilishaji wa mauzo au manunuzi, usalama katika miamala ya kifedha, na usalama katika usafirishaji wa bidhaa.

Uzinduzi wa DUBUY.com nchini Tanzania umekuja baada ya uzinduzi wa jukwaa hilo nchini Kenya na Rwanda mnamo mwaka jana, na kuunda jumuiya ya wafanyabiashara mtandaoni inayowaunganisha zaidi ya wafanyabiashara hai 1,500. Ujio wa DUBUY.com nchini Tanzania unathibitisha dhamira ya jukwaa hilo katika kuunda lango la kimkakati la biashara katika nchi za Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania.

VODACOM NA WWF WAADHIMISHA WASAA WA MAZINGIRA

Vodacom Tanzania Foundation imeshirikiana na WWF kuadhimisha wasaa wa mazingira (Earth Hour ) kwa kupanda miti wilayani Kisarawe.

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo (katikati) akiwa kwenye zoezi la upandaji miti katika kampeni ya Wasaa wa Mazingira (Earth Hour) yenye lengo la kuhamasisha upandaji miti ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Kampeni hiyo ilifanyika Wilayani Kisarawe, taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation ambayo ni mdau wa mazingira wameshirikiana na WWF katika kupanda na kusimamia miti Wilayani humo. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Vodacom Tanzania Foundation, Sandra Oswald.




Wednesday 30 March 2022

BENKI KUU YA ETHIOPIA NA SAFARICOM WAJIFUNZA HUDUMA ZA KIFEDHA ZA M-PESA VODACOM ZINAVYOFANYA KAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc, Sitholizwe Mdlalose akizungumza na maofisa kutoka Benki Kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Safaricom Ethiopia namna huduma za kifedha kwa njia ya mtandao zinavyoleta tija kwa jamii na kuongeza pato la taifa kwa kufuata sheria na mamlaka husika za nchi. Ujumbe huo umekuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kujifunza huduma jumuishi za kifedha kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi.
Mkurugenzi wa Vodacom M-Pesa, Epimack Mbeteni akiwaelimisha maofisa kutoka Benki Kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Safaricom Ethiopia namna huduma za kifedha kwa njia ya mtandao zinavyoleta tija kwa jamii na kuongeza pato la taifa kwa kufuata sheria na mamlaka husika za nchi. Ujumbe huo umekuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kujifunza huduma jumuishi za kifedha kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi.
Meneja Uendeshaji Kituo cha Huduma kwa Wateja Vodacom Tanzania, Deogratius Massawe akiwaelezea maofisa kutoka Benki Kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Safaricom Ethiopia namna kituo hicho kinavyofanya kazi za kuweka usalama na kutunza taarifa za wateja wao.
Mkuu wa Mauzo Vodacom Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Shirima akiwa kwenye kituo cha mafuta kwa ajili ya kuwaonesha maofisa kutoka Benki Kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Safaricom Ethiopia namna ambavyo wateja wanaweza kulipia kwa kutumia huduma ya "Lipa kwa simu" ikiwa ni sehemu ya kuwaonesha namna huduma ya kulipa kidijitali kupitia M-Pesa inavyofanya kazi.

Tuesday 29 March 2022

BENKI YA CRDB YASAINI MKATABA WA SH. BILIONI 182 NA PROPARCO KUWEZESHA WAJASIRIAMALI NCHINI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Proparco Afrika Mashariki, Jean Bendit-Du Chalard (kulia) wakionyesha mikataba ya makubaliano ya mkopo na dhamana za mikopo yenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 182 kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali nchini, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB. Mkopo na dhama hizo zilizotolewa na Proparco zitaiwezesha Benki ya CRDB kutoa mikopo kwa wajasiriamali wa sekta ya kilimo, wajasiriamali wanawake, pamoja na wajasiriamali walioathirika na janga la UVIKO-19.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Proparco Afrika Mashariki, Jean Bendit-Du Chalard (kulia) wakisaini mikataba wa makubaliano ya mkopo na dhamana za mikopo yenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 182 kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali nchini, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB. Mkopo na dhama hizo zilizotolewa na Proparco zitaiwezesha Benki ya CRDB kutoa mikopo kwa wajasiriamali wa sekta ya kilimo, wajasiriamali wanawake, pamoja na wajasiriamali walioathirika na janga la UVIKO-19.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Proparco Afrika Mashariki, Jean Bendit-Du Chalard (kulia) wakibadilishana mikataba ya makubaliano ya mkopo na dhamana za mikopo yenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 182 kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali nchini, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) na Mkurugenzi Mkuu wa Proparco Afrika Mashariki, Jean Bendit-Du Chalard (wapili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Balozi wa Ufaransa Tanzania, Alex David Gullion (wapili kulia), Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya, Mihaela Marcu (wakwanza kushoto), na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Benki ya CRDB wakati wa hafla ya kusaini mikataba ya makubaliano ya mkopo na dhamana za mikopo yenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 182 kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali nchini, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB. 

Benki ya CRDB imeingia makubaliano ya uwezeshaji wajasiriamali wadogo na wakati (MSMEs) wenye thamani ya Shilingi bilioni 182 na shirika la fedha la nchini Ufaransa la Proparco.

Makubaliano hayo ambayo yanajumuisha mkopo na dhamana za mikopo kwa wajasiriamali, itasaidia kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na mpango wa maendeleo wa Taifa, kwa kuzingatia zaidi wajasiriamali wanawake, wajasiriamali katika sekta ya kilimo, pamoja na wajasiriamali ambao wameathirika kwa kiasi kikubwa na janga la UVIKO-19.

Proparco, ni kampuni tanzu ya shirika la maendeleo la UfaransaAgence Française de Développement Group (AFD Group), ambalo limejikita katika kutoa ufadhili na usaidizi kwa biashara na taasisi za kifedha barani Afrika, Asia, Amerika Kusini na Mashariki ya Kati.

Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano hayo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka na utasaidia kwa kiasi kikubwa kufufua sekta ya ujasiriamali nchini na kuchochea ukuaji wa uchumi.

"Nidhahiri kuwa katika kipindi cha mitatu iliyopita wajasiriamali wengi wameathirika na janga la UVIKO-19. Tunatarajia kuwa fedha pamoja na dhamana hizi tunazozipata leo, pamoja na huduma zetu bunifu kwa ajili ya wajasiriamali, zitasaidia kuwainua na kuwawezesha wajasiriamali nchini kuboresha biashara,” amesema Nsekela.

TANZANIA YAISHUKURU OPEC FUND KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akimkabidhi zawadi yenye picha ya baadhi ya vivutio vya utalii vilivyopo nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa OPEC, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo, ofisini kwake, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa OPEC, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, baada ya kukamilika kwa mazungumzo yao, ofisini kwa Waziri wa Fedha, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa OPEC, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh (wa tatu kulia), Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa (kulia), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhe. Nadhifa Kemikimba, na Mkurugenzi Mkuu Msadizi anayesimamia Idara ya Sekta Binafsi (OFID), Bw. Fuad Albassam (wa pili kushoto), jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa OPEC, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh (wa nne kushoto), pamoja na ujumbe wa Tanzania na OPEC FUND, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa OPEC, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, zawadi yenye picha ya kazi zinazofanywa na Serikali katika kuwaondolea wananchi umasikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF, ofisini kwake, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia), akipokea zawadi ya kisahani chenye alama ya shughuli zinazofanywa na Mfuko wa OPEC, kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo, Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, alipomtembelea Waziri wa Fedha, Ofisini kwake, Jijini Dodoma.

Na Benny Mwaipaja, Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameushukuru Mfuko wa nchi zinazozozalisha Mafuta kwa wingi Duniani (OPEC FUND), kwa kuwekeza hapa nchini zaidi ya dola za Marekani milioni 218, sawa na shilingi za Tanzania, bilioni 504, kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.

Dkt. Nchemba, alitoa shukrani hizo Jijini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Shirika hilo ulioongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wake Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, ambapo walijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Mfuko huo.

Alisema kuwa fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi mbalimbali, ukiwemo mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe, mradi wa barabara ya Kazilambwa-Chagu, barabara ya Uvinza-Ilunde – Malagarasi pamoja na kufadhili mradi wa kupambana na Umasikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -TASAF. 

“OPEC FUND, mmekuwa msaada mkubwa katika maendeleo ya nchi yetu katika kukuza uchumi wa nchi, kupunguza umasikini wa wananchi nana kuwaletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii watu wetu” alisema Dkt. Nchemba.

Monday 28 March 2022

NMB YAZINDUA HUDUMA YA WAKALA KWA SIMU ZA MKONONI

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi (wapili kushoto), kutoka kushoto - Kaimu Mkuu wa Uthibiti Hatari na Utekelezaji, Oscar Nyirenda, Afisa Mkuu wa Teknolojia na Mabadiliko ya Kidigitali, Kwame Makundi na Mkuu wa Idara ya Bidhaa, Aloyse Maro.

Benki ya NMB imezindua huduma maalumu ya kuweka na kutoa pesa kirahisi kupitia wakala watakao tumia simu zao za mkononi tu.

Huduma hiyo ya NMB Pesa Wakala imezinduliwa jijini Dar es Salaam, ikilenga kusogeza ‘Karibu Zaidi’ huduma za kifedha kwa wananchi, pamoja na kutoa fursa za ajira kwa Watanzania, lengo likiwa kuongeza idadi ya mawakala kutoka 11,000 wa sasa, hadi 100,000 miaka mitano ijayo. 



Huu ni muendelezo wa utoaji wa suluhishi za kidijitali zilizo rahisi na salama kwa wateja ili kuwafanya kuendelea kufurahia huduma zao popote walipo.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alivitaja vigezo vya mtu kuomba uwakala wa NMB Pesa Wakala kuwa ni pamoja na Leseni ya Biashara, Kitambulisho cha Taifa (NIDA) na simu ya mkononi ya aina yoyote (smartphone au kitochi).



Sasa Wakala anaweza kutumia huduma hii kupitia simu yake ya mkononi tu, bila kuhangaika kupata mashine za PoS ambazo zinatumia kadi. Kwa mteja, hakikisha umejiunga na NMB Mkononi kuweza kufurahia huduma hii kiurahisi.

MBEYA STUDENTS GET SET FOR A BRIGHTER FUTURE WITH DONATION OF CLASSROOM FURNITURE FROM COCA-COLA

Coca-Cola Kwanza’s Sustainability and Communications Specialist, Victor Byemelwa (right) sits on one of the 100 desks donated by Coca-Cola Kwanza Ltd which is the subsidiary of Coca-Cola Beverages Africa (CCBA) to Ilunga Secondary School in Mbeya. Coca-Cola Kwanza Ltd donated classroom furniture including 100 desks, ten tables and ten chairs to Ilunga Secondary School in Mbeya to support improved education the government’s focus on creating an improved education environment in rural areas. Left is Mbeya District Commissioner Dr Rashid Chauchua. (Photo courtesy of Coca-Cola Kwanza.

Mbeya, Sunday 27 March 2022 - Students at Ilunga Secondary School in Mbeya will be able to concentrate on learning in comfort after Coca-Cola Kwanza Ltd donated classroom furniture including 100 desks, ten tables and ten chairs to support improved education in rural areas.

The donation by the subsidiary of Coca-Cola Beverages Africa (CCBA), valued at 12 million Tanzanian shillings, will help to address the desk shortage, and support the government’s focus on creating an improved education environment in rural areas.

Speaking at the handover event, Coca-Cola Kwanza’s Sustainability and Communications Specialist, Victor Byemelwa, said the company’s donation was intended to create greater shared opportunity for the business and communities.

“Opportunity is more than just money, it’s about a better future for people and their communities everywhere on the African continent.

“Coca Cola Kwanza's vision is to refresh and improve the lives of Tanzanians every day. We do business the right way for a better-shared future, and this support will benefit 200 students to give them the best chance for a successful education,” he said.

NCBA YASHIRIKI JUKWAA LA FINANCIAL WOMEN FORUM

Unwanaobong David, Mkuu wa Usimamizi wa Mikopo Hatarishi wa Benki ya NCBA akishiriki kwenye kungamano la kuadhimisha mchango wa viongozi wanawake kwenye sekta ya fedha kwenye jukwaa lijulikanalo kama Financial Women Forum.


Nasikiwa Berya, Msaidizi wa Chapa - Benki ya NCBA (kulia) akipokea tuzo ya Meneja Masoko bora wa mwaka kwa niaba ya Caroline Mbaga, Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uraia wa Benki ya NCBA kutoka jukwaa lijulikanalo kama Financial Women Forum.

Unwanaobong David, Mkuu wa Usimamizi wa Mikopo Hatarishi wa Benki ya NCBA akipokea tuzo ya Mkuu wa Rasilimali watu wa mwaka kwa niaba ya Zainab Mushi, Mkuu wa Rasilimali Watu kutoka Benki ya NCBA kwenye jukwa la Financial Women Forum.

BENKI YA NCBA KUIMARISHA UWEZESHWAJI WA WANAWAKE ZAIDI KUPITIA UVUMBUZI WA KIFEDHA

Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya NCBA, Margaret Karume akipokea tuzo ya Kiongozi Mwanamke ijulikanayo kama Women in Management (WIMA) kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula.
Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya NCBA, Margaret Karume (katikati) akiwa na Caroline Mbaga, Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uraia wa NCBA (kushoto) na Mansoor Baragama, Mkuu wa Rasilimali wa NCBA (kulia).
Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa NCBA Bank, Margaret Karume akiwa na tuzo yake kutoka WIMA.
Wafanyakazi wa NCBA kwenye picha ya pamoja katika kumpongeza Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya NCBA, Margaret Karume baada ya kupokea tuzo yake ya WIMA.

Dar es Salaam - Benki ya NCBA imesisitiza dhamira yake ya kuwawezesha wanawake zaidi kupitia uvumbuzi wa kifedha ili kukuza ari yao ya ujasiriamali na biashara. Ahadi hiii ilitolewa Machi 26, 2022 kwenye hafla ya kuwapongeza Wanawake kwenye uongozi, maarufu kama Women in Management (WIMA).

Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya NCBA, Margaret Karume alikuwa miongoni mwa wanawake waliotunukiwa tuzo ya heshima kwenye hafla hio alikaririwa akisema, "uwezeshwaji wa wanawake kwenye kazi zao ni kipaumbele chetu, iwe ni kwenye biashara, ujasiriamali au kazi za kawaida. Hii ni kwasababu benki yetu ina uwezo mkubwa wa kifedha, uwekezaji, na uvumbuzi hivyo kuwa na nafasi kubwa ya kuwa kama mhamasishaji, msaidizi, muongozaji, na mshirika wao kwenye kila hatua zao za mafanikio’.

DStv INAKULETEA USIKU WA MAKOROKOCHO



Usiku wa Makorokocho

@dstvtanzania inakueletea usiku wa kuvunja mbavu na wakali wa Vichekesho kutoka Tanzania, Uganda na Nigeria.

Kutana na Wakongwe kazini Original comedy wakiongozwa na Masanja Mkandamizaji, Mwarabu wa Dubai Mpoki, Mac Regan Kipara Mwanaumee na Wakuvwanga aka Mama Imma wanarudi kwenye Jukwaa la Stand Up comedy kwa mara ya kwanza baada ya miaka zaidi ya 7 ya kukosekana.

Original comedy watapata support kutoka kwa Mzee Shayo, Deogratius na Munga kutoka kundi la @watubaki. Na kutoka Uganda anashuka Salvador wakati Nigeria itawakilishwa na Kevin Pam.

Usiku wa Makorokocho utafanyika siku ya Alhamisi, tarehe 31 March 2022 na utarushwa LIVE na DStv pekee kupitia Maisha Magic Poa inayopatikana ndani ya kifurushi cha POA kwa TShs.9,900 tu kwa mwezi.

Makorokocho comedy night, hakika hii si ya kukosa! Piga *150*53# kulipia kifurushi chako cha DStv sasa!
@str8upvibes_

Friday 25 March 2022

USIKOSE IRELAND VS BELGIUM JUMAMOSI HII

 


Hapa Ireland hapa Beligium, je nani kufanya kufuru Jumamosi hii?

Mchongo ni huu, kupitia Ofa ya Panda Tukupandishe wewe mteja wa Poa panda sasa na lipia kifurushi cha Bomba na @dstvtanzania itakupandisha mpaka Shangwe bila malipo ya ziada uweze kutazama mechi hii Live.

VigezoNaMashartiKuzingatiwa @edgarkibwana

#PandaTukupandishe
#BirianiIendelee

Thursday 24 March 2022

LETSHEGO AFRICA DELIVERS DOUBLE DIGIT GROWTH

Omar S. Msangi, Letshego Bank Tanzania’s Acting CEO.
  • LETSHEGO AFRICA DELIVERS DOUBLE DIGIT GROWTH IN PROFITS, BUILDING THE @LETSGONATION TO SUPPORT ECONOMIC DEVELOPMENT ACROSS FOOTPRINT
Access Letshego Africa Results FACT SHEET for FULL YEAR 2021 below

1. Screen friendly version: Letshego_group_financials_december_2021.pdf

2. Print friendly version: Book 1.indb (letshego.com)

DAR ES SALAAM, TANZANIA 15th March, 2022 — Pan-African inclusive finance entity, Letshego Holdings Limited (“Letshego Africa” / “Letshego Group”) has announced positive Full Year Results for the year ended 31 December 2021 this last Thursday 3 March 2022. The Group’s consolidated performance for 2021 has been strong with double digit growth in profits: Profit before tax was up 11% year-on-year to P1.147 billion, and Profit after tax climbed 16% for the same comparative period, to P730 million.

Asset quality remains strong with the Group’s Loan Loss Ratio (LLR) at -0.1% for the year, or 0.5% excluding once-off deductions. The Group’s Non-performing loans ratio increased marginally to 5.9% for the year (FY2020: 5.3%), reiterating stability in the Group’s credit and risk management framework. Performance for the year was largely driven by 17% growth in net customer advances, totalling P11.9 billion.

Other financial performance highlights include:
  • NET INTEREST INCOME up 6% to P1.989 billion (FY 2020: P1.861billion)
  • TOTAL ASSETS increased by 30% year-on-year to P15.8 billion (FY 2020: P12.2billion)
  • CUSTOMER DEPOSITS increased by 77% year-on-year to P1.2 billion (FY 2020: P664 million)
  • COST TO INCOME RATIO of 52% (FY 2020: 50%), in line with expectation due to heightened digital investment and insurance costs in Namibia 
  • EFFECTIVE TAX RATE (ETR) improved to 36% (FY 2020: 39%)

TANZANIA COMMERCIAL BANK DEBUTS POPOTE VISA CARD

VISA Card East Africa Vice President, Corine Nana (right), and Tanzania Commercial Bank (TCB Bank) Chief Executive Officer, Sabasaba Moshingi press a button to mark the official launch of the Popote Visa Card to enable the Bank's customers access to services and wherever they are in and out of the country. The launch event took place in Dar es Salaam.
VISA Card East Africa Vice President, Corine Nana (center) with TCB Bank Chief Executive Officer, Sasabasa Moshingi (second left) showing the POPOTE VISA CARD model during the official launch of the card. From left is TCB Bank - Telecommunications and Operations Director, Jema Msuya, CEO of UBX Tanzania LTD, Seronga Wangwe and TCB Bank - Internet Banking Senior Manager, Allen Manzi.
TCB Bank Chief Executive Officer, Sabasaba Moshingi, speaking during the official launch of the Popote Visa Card in Dar es Salaam.
  • VOWS TO SUPPORT DIGITAL TANZANIA AGENDA
The government’s aspiration for a cashless economy got yet another vital digital finance shot in the arm following the official debut of an internationally accepted electronic payments card in the market by Tanzania Commercial Bank (TCB Bank).

The bank has partnered with Visa International to introduce the new service that elevates its commercial clout in international trade finance circles and enables its customers to transact anywhere any time in the world.

Speaking at the launch ceremony of the Popote Visa Card, the Chief Executive Officer of TCB Bank, Sabasaba Moshingi, said the debit card has all it takes to make universal financial services to be within reach in Tanzania.

The Popote debt card partners vowed to support efforts for a less cash national economy by championing and promoting responsible and innovative digital payment solutions that are more convenient, safe and offer better money management options.

“Any efforts like the international debit card that we have launched today and our partnership with Visa are mportant to the government’s digital economy and cashless society ambitions,” Moshingi noted.

He said the bank opted for the Visa partnership because the American multinational was the giant of digital payments in the world with an unmatched network of 61 million merchants.

FAINALI NMB MASTABATA - MILIONI 90/- KWA WASHINDI 30


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya Nmb, Filbert Mponzi (wa tatu kulia) akibonyeza kitufe kuashiria kuchezesha Droo ya mwisho ya msimu wa tatu wa Kampeni ya NMB MastaBata Kivyako Vyako. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi Benki ya NMB, Aikansia Muro na Mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania, Elibariki Sengasenga, (kulia) ni Meneja Mwandamizi kitengo cha Kadi, Manfredy Kayala na Balozi wa Kampeni hiyo, Masoud Kipanya.

Miezi mitatu ya Kampeni ya ‘NMB MastaBata – Kivyako Vyako,’ iliyoendeshwa na Benki ya NMB, imefikia tamati leo kwa wateja 30 kujinyakulia kitita cha Sh. Mil. 90 (sawa na Mil. 3 kila mmoja), hivyo kukamilisha kinyang’anyiro kilichobeba zawadi ya pesa taslimu Sh. Mil. 240.



Hitimisho ‘Grand Finale’ la kampeni hiyo, limefanyika NMB Tawi la Sinza jijini Dar es Salaam, kufikia ukomo kwa mchakato uliowanufaisha wateja 1,080, kati yao 1,000 wakijinyakulia Sh. Milioni 100 (sawa na Sh. 100,000 kila mmoja), huku 50 wakitwaa Sh. Mil. 50 (sawa na Mil. 1 kila mmoja) na 30 wa fainali wakishinda Mil. 90 hizo.



Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi, alisema malengo ya kampeni hiyo, ambayo ni kuhamasisha matumizi ya kadi badala ya pesa taslimu, yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kumekuwa na ongezeko la asilimia 10 ya watumiaji wa kadi.



Huu sio mwisho, kampeni hizi zitaendelea na tutaendelea kutoa elimu kwa jamii itambue umuhimu wa kutumia kadi badala ya pesa taslimu, kwa sababu ni rahisi, nafuu na salama zaidi.

Wednesday 23 March 2022

RAIS SAMIA ATEMBELEA BANDA LA BENKI YA EQUITY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan alitembelea banda la Benki ya Equity lililopo Mlimani City apo Jana kwenye maadhinisho ya Wiki ya Maji ambako alipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bi. Isabela Maganga, namna Benki ya Equity ilivyo mstari wa mbele kuhakikisha inachangia juhudi za serikali katika upatikanaji wa maji safi.

KILOMBERO YAWAHAKIKISHIA WANANCHI UPATIKANAJI WA SUKARI KATIKA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Fimbo Butallah akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Mauzo, Harshid Chavda na kushoto ni Meneja Usambazaji, Johannes Rugalema.

"Tunawasihi wafanyabiashara kote nchini kutopandisha bei ya sukari katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuepuka taharuki inayoweza kujitokeza"

23 Machi 2022: Dar es Salaam — Kampuni ya Sukari ya Kilombero na kusambaza sukari chini ya chapa ya “Bwana Sukari” inapenda kuwatoa hofu wananchi, hususani wapenzi na watumiaji wa sukari ya Kilombero “Bwana Sukari” kuhusu upungufu wa sukari katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi Aprili.

Hayo yamesemwa na Fimbo Butallah, Mkuu wa Idara ya Biashara siku ya Jumatano, 23 Machi, 2022 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.

Tamko hilo limekuja kutokana na historia ya kupanda kwa bei za bidhaa nyingi za vyakula kila uanzapo mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kusababisha adha kubwa kwa wananchi, hususan waumini wanaofunga katika mwezi huo. Kutokana na hilo, kampuni ya Sukari ya Kilombero imewasihi wafanyabiashara wote, wa jumla na rejareja wanaouza bidhaa za “Bwana Sukari” kutopandisha bei, jambo ambalo limekuwa likiwakandamiza watumiaji wa sukari ambapo matumizi yake huongezeka zaidi katika mfungo wa Ramadhani.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Fimbo alisema, “Tunafahamu kuwa katika uchumi wa soko huria, sisi kama wazalishaji haturuhusiwi kuwapangia wafanyabiashara bei ya kuuza bidhaa. Hata hivyo tunao wajibu mkubwa wa kuwashauri kuhusu upandishaji holela wa bei, haswa pale ambapo sisi kama wazalishaji wa sukari hatujapandisha bei ya bidhaa hiyo. Tunawasihi wafanyabiashara kote nchini kutopandisha bei za sukari katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuepuka taharuki inayoweza kujitokeza.”

Akizungumzia suala la uhaba wa sukari ambao mara nyingi hujitokeza katika mfungo wa Ramadhani, Fimbo alisema kuwa Kampuni ya Sukari ya Kilombero inayo akiba ya kutosha kulivusha taifa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuongezea kuwa tayari kampuni imepata kibali cha kuagiza sukari kutoka nje ya nchi ili kuziba pengo la uzalishaji.

“Tumekwishaanza taratibu za uagizaji wa sukari ambayo inatarajiwa kuanza kuingia nchini muda wowote kuanzia hivi sasa. Tunapenda kuwatoa hofu wananchi kuhusu upandaji holela wa bei ya sukari, hususan chapa ya “Bwana Sukari” kwani kampuni imeandaa mikakati thabiti kukabiliana na tatizo hilo katika msimu huu”, alisema Fimbo.

Kampuni ya Sukari ya Kilombero, ambayo inamilikiwa na Kampuni ya Illovo Sugar Africa kwa Asilimia 75 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 25 ipo katika maandalizi ya mradi wake wa upanuzi ambao utakuza uwezo wa kampuni hiyo wa kutengeneza sukari na kupunguza uhaba wa sukari nchini kupitia chapa yake ya “Bwana Sukari”.

Mawasiliano:

Fimbo Butallah, Mkuu wa Idara ya Biashara
Namba ya Simu: +255 687 610 662
Barua pepe: fbutallah@illovo.co.za

SMILE EXPANDS ULTRA-FAST INTERNET TO ZANZIBAR

Zuweina Farah, Smile Country Manager with Zanzibar's Minister of State President's Office Responsible for Economy and Investment, Hon. Mudrick Soraga celebrating the launch of Smile 4G LTE broadband ultra fast internet services, launched in Zanzibar yesterday.

Smile Tanzania CEO, Zuweina Farah in discussion with TENMET Board Chairperson, Faraja Nyalandu on existing Smile Tanzania Investment Opportunities in Zanzibar and how to use them. This discussion was part of the Opening of 4G LTE Network in Zanzibar earlier yesterday.

Zanzibar - Smile Communications announced its expansion in Zanzibar, providing reliable, fast 4G LTE mobile broadband internet services across the Island.

Smile Communications, is an African telecommunications group with operations in Tanzania, Nigeria, Uganda, and the Democratic Republic of the Congo.

“Following Smile Tanzania's recent investment in network expansion, we are excited to bring the best 4G LTE broadband internet services to customers in Zanzibar”, said Zuweina Farah Smile's Country Manager.



Adding on Mr. Ahmad Farroukh, Smile Group’s Chief Executive Officer said "Dar es Salaam was the first city in Africa to experience true 4G LTE when Smile launched its internet services there in May 2013. Today, the people of Zanzibar can celebrate another first, enabled by the latest 4G LTE technology, when they connect to Smile internet with data speeds of up to 50Mbps".

Zuweina Farah, Director of Smile Tanzania presenting the 4G LTE Award to the Minister of State President's Office Responsible for Economy and Investment, Hon. Mudrick Soraga to demonstrate that this is the Official Opening of Smile Tanzania and the service is now available in Zanzibar.