Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Saturday 30 April 2022

JUMAMOSI HII NEWCASTLE VS LIVERPOOL NDANI YA DStv


Jumamosi hii ndani ya #EPL kupitia chaneli za SuperSport

Newcastle vs Liverpool
SS 223
8:30 Mchana

Kikosi kipi kuibuka na alama 3?

Lipia kifurushi chako mapema kwa kupiga *150*53#

#Birianiiendelee
#DStvEwaaaaah

GEITA GOLD MINE PAYS 4 BILLION TO TWO GEITA COUNCILS


Geita Gold Mining Limited (GGML) has paid a combined over Sh4 billion to Geita Town and Geita District Councils for the period July 2021 to March 2022 (3 quarters) as service levies. The service levy is a service charge that is payable to the respective councils in accordance with the law.

Commenting on the payments to the respective councils, AngloGold Ashanti – Geita Gold Mine Vice President for Tanzania and Ghana, Simon Shayo said the company recognizes and appreciates the importance of paying various taxes and levies to the government including service levies as revenue enables the government to bring development to their citizens.

"This contribution clearly illustrates how our company is at the forefront of paying various taxes and levies for the development of the people of Geita, it is also our responsibility to obey the laws of the Tanzanian government," said Shayo.



In addition to the various taxes and levies paid directly to the Central Government and our Councils, Geita Gold Mining Limited has also been contributing to community development through their Corporate Social Responsibility (CSR) plans.

Friday 29 April 2022

NOTICE TO USA BASED DIASPORA FROM NHC AND NMB BANK


BENKI YA NMB YAKUSANYA BILIONI 74.3 KUPITIA HATI FUNGANI YA ‘NMB JASIRI’

Naibu Katibu Mkuu - Sera, Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru, akigonga kengele kama ishara ya kuorodheshwa rasmi 'NMB Jasiri' kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Wakishuhudia ni; Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) - Moremi Marwa(kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB - Ruth Zaipuna na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Nicodemus Mkama (kulia).
Naibu Katibu Mkuu - Sera, Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji - CPA Nicodemus D. Mkama, Mkurugenzi Mkuu wa DSE - Moremi Marwa, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB - Ruth Zaipuna, Afisa Mkuu wa Fedha Benki ya NMB - Juma Kimori pamoja na wawakilishi kutoka FSD Africa, Ubalozi wa Uingereza, International Finance Co-operation (IFC), Orbit Securities Ltd na UN Women wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya kuorodhesha hati fungani ya NMB Jasiri katika Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE).

Benki ya NMB imefunga mauzo ya Hati Fungani ya Jasiri (NMB Jasiri Bond) kwa mafanikio makubwa Iliyoweka rekodi ya makusanyo Afrika Mashariki na Kati ya Shilingi Bilioni 74.27 na kuvuka lengo la Shilingi Bilioni 25, ufungaji ulioenda sambamba na kuiorodhesha rasmi hati hiyo katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Hafla hii ilihudhuriwa na Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu - Sera, Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru aliyemwakilisha Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande, ametangaza rasmi kuorodhozeshwa kwa hati fungani ya Jasiri na sasa kuanza kununuliwa na kuuzwa kupitia soko la hisa la Dar es salaam.

Akizungumza Mafuru aliipongeza NMB kwa ubunifu chanya wa Jasiri Bond, hati fungani iliyolenga kukusanya fedha ili kutoa mikopo kwa biashara ndogo ndogo na za kati zinazo milikiwa au kuongozwa na wanawake na biashara ambazo bidhaa au huduma zake zinamgusa mwanamke moja kwa moja.

“Hii sio mara ya kwanza kwa NMB kuja na Hati Fungani na kuvuka lengo la makusanyo, hii ni mara ya nne na kwa hati hii ambayo ni ya kipekee, kama jina lake lilivyo, kumekuwa na ujasiri mkubwa sana, kwani jina Jasiri linaashiria mambo mengi sana.

“Ujasiri wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), ya kuiruhusu Hati Fungani hii kuingia sokoni kabla hata ya sheria zake hazijawa tayari, jambo linalothibitisha imani ya mamlaka hii kwa NMB ilivyokuwa kubwa.

“Lakini pia, NMB ikalenga kupata Shilingi Bilioni 25 na hatimaye inafunga mauzo ikiwa imepata zaidi ya mara tatu ya lengo, hii ni kuthibitisha kwamba kuna nguvu kubwa ya kiuchumi miongoni mwa wanawake, tunachotakiwa ni kuweka mazingira wezeshi ya kuwaamini kama wenzetu NMB walivyofanya,” alisisitiza Mafuru.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna, alisema NMB ilipokea maombi 1,630 yaliyowezesha kukusanya Shilingi Bilioni 74.27 badala ya Bilioni 25 na kuwashukuru wateja na wawekezaji wote kwa kuiamini benki hio.

“Kuaminika kwa NMB katika hili kunathibitishwa na kuwa asilimia 96 ya waliotuma maombi ya kununua Hati Fungani, yamepitia katika matawi yetu, huku asilimia 4 tu yakifanyika kupitia Madalali wa Soko la Hisa waliosajiliwa”.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji (CMSA), Nicodemus Mkama, aliipongeza Bodi ya Wakurugenzi na Uongozi wa NMB, kwa kufanikisha uuzwaji wa ‘Jasiri Bond’ kwa Umma wa Watanzania na hatimaye kufikia hatua ya kuiorodhesha DSE, tayari kwa mauzo ya walionunua na manunuzi ya waliokosa katika mchakato uliofungwa.

Wengine waliohudhuria hafla hii ni Mkurugenzi Mkuu WA DSE, Moremi Marwa, pamoja na wawakilishi kutoka FSD Africa, Ubalozi wa Uingereza, International Finance Co-operation (IFC), UN Women na Orbit Securities Ltd.

Thursday 28 April 2022

AFRICAN DEVELOPMENT BANK GROUP CHIEF GARNERS STRONG GLOBAL SUPPORT FOR AFRICA

“I will be your strong advocate for G7 countries to do more for the African Development Fund and to put in more resources for Africa” – Melinda French Gates, co-chair of the Bill & Melinda Gates Foundation.

United States Assistant Treasury Secretary Alexia Latortue said the African Development Fund was critical to Africa’s the development landscape

ABIDJAN, Ivory Coast, April 25, 2022/ -- African Development Bank Group (www.AfDB.org) President Dr Akinwumi Adesina concluded a three-day official visit to Washington DC on Saturday. Alongside the Spring Meetings of the International Monetary Fund and World Bank, the visit included several bilateral engagements with stakeholders on African development.

Adesina garnered broad strong support for a robust 16th replenishment of the African Development Fund, the Bank Group’s concessionary lending arm that supports Africa’s low-income economies. Replenishment efforts continue through October, when partners are expected to make their pledges.

During bilateral meetings, United States Assistant Treasury Secretary Alexia Latortue said the African Development Fund was critical to Africa’s development landscape. She assured the Bank President that the US remains a strong and proud supporter of the Fund, which has strategic focus and delivers impact. Latortue applauded the leadership of Dr. Adesina in developing the Bank’s bold African emergency food production plan to avert the looming food crisis due to the Russian war in Ukraine and assured of the strong partnership of the US Treasury Department on the plan.

Dr. Adesina received similar strong support for the African Development Fund replenishment from other partners, including Sweden’s Minister for International Development Cooperation Matilda Ernkrans, Anne Beathe Tvinnereim, Norway’s Minister for International Development, Vicky Ford, Minister for Africa of the United Kingdom, and Paul Ryan, Director of International Finance and Climate of Ireland. They gave their strong support for the African Development Fund to be allowed to go to the market to leverage its equity and raise more financing for low-income and fragile states.

NMB YAIPA KIPAUMBELE ELIMU YA FEDHA KWA VIJANA NCHINI


Serikali chini ya Benki kuu ya Tanzania (BOT) waliweka kipaumbele utoaji wa elimu ya fedha kwa Watanzania hususani vijana kwa malengo ya kukuza jamii iliyo na uelewa na masuala ya fedha.

Kwa kutambua umuhimu huu, Benki ya NMB kupitia sera ya uwajibikaji kwa jamii, inatoa mafunzo ya elimu ya fedha kwa makundi tofauti katika maeneo mbalimbali hapa nchini huku elimu ikielekezwa katika ufunguaji wa akaunti za Benki na utunzaji wa Akiba kwa manufaa ya baadae.

Katika ziara ya maafisa wa Benki ya NMB kwa mikoa ya Tabora, Kigoma na Shinyanga, mbali na kutembelea na kujionea namna Benki hiyo imekuwa chachu ya kukua kwa sekta ya Elimu na Afya nchini, walitumia fursa hii kutoa Elimu ya fedha hasa kwa wanafunzi.



Afisa wa benki ya NMB idara ya uwajibikaji kwa jamii, Aloyce Kikois, aliwasisitiza wanafunzi juu ya uwekaji wa akiba na kutumia Benki kama sehemu sahihi ya kuhifadhi fedha kwani ni salama zaidi. Kwa mujibu wa Meneja wa Benki ya NMB idara ya Uwajibikaji kwa jamii, Lilian Kisamba alisema, Benki ya NMB tayari imetoa mafunzo hayo katika maeneo mbalimbali nchini huku zaidi ya watanzania 80,000 wakinufaika na elimu hii hasa katika ulimwengu wa sasa wa kiteknolojia.

ABSA BANK HOSTS AN IFTAR FOR CLIENTS IN ZANZIBAR

Absa Bank Tanzania Head of Retail Banking, Ndabu Lilian Swere speaks to the media during an  iftar meal hosted by the bank to its Zanzibar customers and stakeholders in the Isles over the weekend.
Absa Bank Tanzania Head of Business Banking, Melvin Saprapasen (right), serves an Iftar meal to one of the bank’s Zanzibar customers at an occasion to break the fast hosted by the bank for its customers and stakeholders in the Isles over the weekend.
Absa Bank Zanzibar Branch Manager, Rabia Abood (left), serves an Iftar meal to one of the bank’s customers, Nuru Mohamed Ali during the occasion.
Absa Bank Tanzania Citizenship Manager, Hellen Siria (left), serves an iftar meal to one of the bank’s Zanzibar customers, at the fast-breaking event.
Absa Bank Zanzibar Branch Manager, Rabia Abood, welcomes some of the invited guests to the Iftar meal hosted by the bank for its customers and stakeholders in the Isles.
Sheikh Khalid Ali Mfaume (second left), represented Zanzibar Chief Mufti at the Iftar meal hosted by Absa Bank. Looking on are Absa Bank  Tanzania Head of Business Banking, Melvin Saprapasen (right), Sheikh Salum Maridhia from Zanzibar Chief Mufti Office (left) and Absa Tanzania Director for Corporate and Investment Banking, Hugo Chilufya.

Absa Bank Tanzania has pledged to maintain the quality of services to its customers to ensure it sustainable growth, it has been revealed in Zanzibar over the weekend.

Speaking during an Iftar dinner hosted for the banks customers to break the fast during the on-going holy month of Ramadhan, Absa's Head of Business Banking, Melvin Saprapasen said: “We are confident about the future as we continue to innovate and come up with new products and solutions that are more digitalised that make it easier for our clients to access and enjoy our services.”

He pointed out the year 2021 had been a very good one from the financial performance perspective as the Bank was able to recover from a reported loss position of TZS 532 million in 2020 to register a Tsh 9.4 billion profit after tax (PAT) in 2021.

ABSA BANK REWARDS 'CARD ASSIST' CAMPAIGN WINNERS

Absa Bank Tanzania Premier Centre Manager, Agnes Mushi (third right), rewards Catherine Mwakisu, who represented James Samson Babala, with a 43 inch smart tv cum sound system after winning the bank’s English Premier League promotion christened ‘Absa Card Assist’ aimed at mobilizing customers to execute transactions using the bank’s card. The campaign ran from December 4, 2021 to January 31 2022. During the presentation ceremony in Dar es Salaam recently, the winner and 10 other participants at a specially set up rendezvous watched a live match of the on-going EPL league match.

Head of Products and Strategic Plans unit of Retail Customers section of Absa Bank Tanzania, Heristraton Genesis (third right), presents Catherine Mwakisu, on behalf of James Samson Babala, with a 43 inch smart tv and sound system prize after emerging tops in the bank’s English Premier League campaign dubbed ‘Absa Card Assist’ which focused on sensitizing customers to make business transactions using the bank’s card. 
The winner of ‘Absa Card Assist’ promotion, fellow participants and Absa staff erupt in cheers during the prize presentation ceremony to the winner of the campaign which was aimed at mobilizing the bank’s customers to use cards in transactions. 
Head of Products and Strategic Plans unit of Retail Customers section of Absa Bank Tanzania , Heristraton Genesis (right), Premier Centre Manager, Agnes Mushi (second right) presents Catherine Mwakisu, on behalf of James Samson Babala, with a 43 inch smart tv and sound system prize after emerging tops in the bank’s English Premier League campaign dubbed ‘Absa Card Assist’ which focused on sensitizing customers to make business transactions using the bank’s card. 
Absa Premier Centre Manager, Agnes Mushi (centre) speaks during a ceremony to present prizes to winners of the bank’s English Premier League campaign dubbed ‘Absa Card Assist’ which focused on sensitizing customers to make business transactions using the bank’s card. The campaign ran from December 4, 2021 to January 31 2022.

KATA BIMA YA AFYA KUPITIA TAWI LOLOTE LA BENKI YA NMB


Katika kuhakikisha afya za Watanzania zinakuwa salama na bora, Benki ya NMB imeshirikiana na Kampuni ya Bima ya Jubilee kukuletea bima ya afya ili kumkinga mteja dhidi ya magonjwa au ajali itakapotokea.

Kuna vifurushi viwili kwenye bima hii;

Bima ndogo (J-Afya) ambayo inamkinga mteja kwa ajili ya matibabu ya kutwa na kulazwa. Katika kifurushi hiki, Bima itagharamia mwanachama na familia yake kwa mwaka, Sh. Milioni 6 kwa matibabu ya kulazwa, na Milioni 1.2 ya kutwa.

Mtoto pekee yake atagharamiwa kwa Sh. Milioni 3. Kutakuwa na gharama za ziada endapo mwanachama atahitaji huduma zaidi ya zilizoainishwa kwenye mpango wake wa bima.

Aidha, Bima kubwa (J-care) imegawanyika katika makundi manne; Royal, Executive, Advanced na Premier, na malipo ya kila mwaka (Premium) yatategemea na ukubwa wa familia pamoja na umri wa mwanachama na mwenza wake.

Faida ya bima hii ni kupata matibabu ya kutwa na kulazwa, matibabu ya meno na macho, mkono wa pole endapo mwanachama atafariki, uzazi na vipimo vikubwa kama MRI.

Bima ya J-care inakupa huduma bora za matibabu kwa urahisi katika hospitali zilizoko kwenye mpango wa bima zinazopatikana nchi nzima.

Pata bima yako kupitia *150*68# au kupiga simu nambari 0800 002 002 bure Kabisa, barua pepe Bancassurance@nmbbank.co.tz au fika tawi la NMB lililopo karibu yako.

Umebima?- SiNgumuKihivyo!

Wednesday 27 April 2022

ALHAMISI HII, MAN. UNITED VS CHELSEA NDANI YA EPL



Ni wiki iliyoshamiri michezo mingi sana na Alhamis hii, Manchester United watavaana na Chelsea ndani ya EPL!

Ikiwa wewe ni shabiki wa Chelsea weka 🔵 na ikiwa wewe ni Manchester United weka 🔴.

Kisha lipia mapema kifurushi cha Compact 51,000/= tu na ufurahie mechi hii Live tena kwa Lugha Adhimu ya kiswahili ndani ya @dstvtanzania pekee.

Piga *150*53# kulipia kwa urahisi zaidi kifurushi chako ili usikose burudani hii.
@edgarkibwana

#DStvEwaaaaah

#BirianiIendeleee

TANZANIA COMMERCIAL BANK YAFADHILI UPIMAJI AFYA BURE

Meneja wa Tanzania Commercial Bank (TCB), Tawi la Mbagala, Edward Mwoleka (kati kati), akifanyiwa kipimo cha moyo na Mtaalam kutoka Alliance Insurance Group, Ravi Kumar, wakati Tanzania Commercial Bank waliposhirikiana na Alliance Insurance Group kutoa vipimo vya magonjwa mbalimbali kwa wakazi wa Mbagala na viunga vyake bure. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Alliance Insurance Group, KVA Krishnan. Hafla hiyo imefanyika katika ofisi za Tanzania Commercial Bank Tawi la Mbagala jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Benki ya Tanzania Commercial Bank, Edward Mwoleka (wapili kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Alliance Insurance Group, KVA Krishnan (kulia), wakiangalia mmoja ya wakazi wa Dar es Salaam, Joeseph John, akipatiwa huduma ya kipimo cha moyo na Mtaalam kutoka Alliance Insurance Group, Ravi Kumar.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza ili kupata vipimo hivyo.

Meneja wa Tanzania Commercial Bank Tawi la Mbagala, Edward Mwoleka (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Alliance Insurance Group, KVA Krishnan.

Mkazi wa Mbagala akifanyiwa kipimo cha shinikizo la damu na Mtaalamu kutoka Shirika la Bima Alliance Insurance incorporation Group, Ravi Kumar, kwa kushirikiana na Tanzania Commercial Bank walipokuwa wakitoa huduma ya vipimo vya magonjwa mbalimbali kwa wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake bila malipo.

Meneja wa Tanzania Commercial Bank (TCB) Tawi la Mbagala, Edward Mwoleka akishuhudia mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam akipata kipimo cha sukari kutoka kwa Mtaalamu wa Maabara, Husna Hassan wakati Benki ya Tanzania Commercial Bank ilipoungana na Kampuni ya Bima ya Alliance kutoa vipimo vya uchunguzi kwa wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake bila malipo.

Mamia ya wananchi leo wamejitokeza kupima afya zao bure Tanzania Commercial Bank tawi la Mbagala iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ikiwa ni sehemu ya Tanzania Commercial Bank pamoja na shirika la bima la Alliance Insurance Corporation kujali wateja wao na wananchi kwa ujumla.

Akizungumza katika hafla hiyo Meneja wa Benki ya Tanzania Commercial Bank Tawi la Mbagala Edward Mwoleka “Amesema kuwa kila mtanzania angependa kujua afya yake hivyo Tanzania Commercial Bank imeamua kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan hasa katika sekta ya afya kwa kutoa huduma ya vipimo bure bila malipo yoyote kwa wananchi wa mbagala.na viunga vyake”.

NOTICE TO USA BASED DIASPORA FROM NHC AND NMB BANK

THANK YOU FOR SUPPORTING THE NBC PREMIER LEAGUE


“The income generated from NBC Premier league-related transactions enables significant expenditure across supply chains, supports thousands of jobs, and creates progressive tax revenues. We couldn’t be prouder.” - Theobald Sabi.

By Theobald Sabi, Managing Director, NBC Bank.

As the NBC Premier League is getting closer to an exciting finale, I wish to extend our sincere gratitude to everyone who made it possible. The financial and non-financial gains that the league has collectively yielded, especially to those in the football value chain, have surpassed our expectations.

What started as a commercial decision resulted in a cross-sectoral empowerment platform that touches and improves lives amicably. Today, we stand tall, advocating our overriding objective: bringing possibilities to life.

On behalf of everyone at NBC, I wish to extend our special appreciation to the Government of Tanzania under Her Excellency President Samia Suluhu Hassan for unparalleled support, the fans for their unwavering passion, and appreciably, to the Tanzania Football Federation (TFF) for trusting and endorsing us to be their partners. Asanteni sana.

On a similar note, I wish to bring you up to speed on the recent value addition to the league players’ insurance covers. Thanks to our new agreement with TFF, we can now offer life and health insurance covers to all the NBC Premier leagues players, club staff, and their immediate families. Special thanks to our partners, Sanlam and Britam Insurance companies, for bringing these arrangements to life.

Tuesday 26 April 2022

FUTARI YA NMB, MIKOPO MAALUM KWA WABUNGE YAMKUNA SPIKA WA BUNGE

Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene (wa kwanza kutoka kulia), Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB - Filbert Mponzi na Afisa Mkuu wa Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa (kushoto) wakati wa Futari iliyofanyika katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katika mwendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Benki ya NMB iliandaa Futari iliyohudhuriwa na Waheshimiwa Wabunge, viongozi wa Dini mbalimbali, Uongozi wa NMB na baadhi ya wateja katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.


Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha wabunge iliyoandaliwa na Benki ya NMB katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

Hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu zaidi ya 500, ambapo mgeni rasmi alikuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Spika ameipongeza na kuishukuru NMB kwa kuandaa hafla hiyo ya Ibada iliyowakutanisha kwa upendo, imani na kuendeleza uhusiano mwema kati ya benki hiyo na Muhimili wa Bunge.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB - Filbert Mponzi akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha Jijini Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya NMB, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara - Filbert Mponzi alisema “Kwa kuandaa futari hii, sisi kama NMB tunaendelea kudumisha ukaribu na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa Serikali ya Mkoa wa Dodoma na wateja wetu. Huu ni wakati mzuri kwa ndugu zetu Waislamu na jamii kwa ujumla kutafakari juu ya upendo kwa familia zetu, shukrani kwa Mungu na toba za dhati”

Mponzi alibainisha kuwa hiyo ndio sababu ya NMB kuipa umuhimu mkubwa jambo hilo na wamekuwa wakifanya hivyo toka miaka ya nyuma. Kwa mwaka huu, tayari wameshatoa futari kwa mkoa wa Dar es Salaam, Dodoma na baadaye watafanya hivyo Visiwani Zanzibar.

Monday 25 April 2022

USIKOSE NUSU FAINALI ZA UEFA NDANI YA DStv PEKEE

 

Baada ya hekaheka za #EPL wikiendi iliyoisha Jumanne na Jumatano hii tunaendeleza Nusu Fainali za #UEFA ambapo Jumanne hii; 

⚽ Man City vs Real Madrid
📺 SS 222
🕰️ 4:00 usiku

Na Jumatano hii; 
⚽ Liverpool vs Villareal
📺 SS 222
🕰️ 4:00 usiku

Je ni kikosi gani kitakachoibuka kidedea katika mitanange hii?

Lipia mapema kifurushi chako kwa kupiga *150*53# kufurahia mechi hizi.

#DStvEwaaaaah

#Birianiiendeleee

BIMA YA MKONO WA POLE YA NMB INAVYOLETA MATUMAINI KWA WANAVIKUNDI

  • Mwanakikundi anaweza kuchangia kwanzia Sh.500 mpaka Sh.2,000 kila mwezi na kupata fidia pale janga la kifo litakapotea kwanzia Sh.1,000,000 mpaka Sh.5,000,000.
  • Bima hii imegawanyika katika makundi mawili yaani kifurushi vilivyo na wazazi na vifurushi na visivyo na wazazi.
  • Kila kifurushi kina aina tatu ambavyo ni Shaba, Fedha na Dhahabu.
  • Kikundi kinatakiwa kuchagua kifurushi kimoja kwa wanakikundi wote.
Benki ya NMB ikishirikiana na makampuni zaidi ya 10 ya Bima nchini, imekuja na huduma mbalimbali za bima kwa lengo la kumlinda mteja pale majanga yanapotokea.

Moja ya bima inayotolewa ni bima ya Mkono wa Pole kwa wanakikundi kuanzia watano na kuendelea wenye umri wa miaka 18 mpaka 75.

Bima hiyo imegawanyika katika vifurushi vya aina tatu ambavyo ni shaba, fedha na dhahabu, ambayo inamnufaisha mwanakikundi, wenzi na watoto pale janga la kifo litakapotea.

Katika kifurushi cha Bronze (Shaba), mwanakikundi mkuu atakuwa anachangia Sh.500 kwa mwezi ambapo yeye, mwenzi na watoto wake watapata Sh.Milioni 1.

Katika kifurushi cha Silva (Fedha), mwanakikundi atachangia Sh.1200 na iwapo akifariki atapata Sh.Milioni 3, mwenzi Sh.Milioni 2 na watoto Sh.Milioni 1.

Aidha, kifurushi cha Gold (Dhahabu), mwanakikundi atachangia Sh.2,000 kwa mwezi na iwapo atafariki atafidiwa Sh.Milioni 5, mwenzi Sh.Milioni 4 na watoto Sh.Milioni 1.

Kuhusu vifurushi vinavyojumuisha wazazi , kutakuwa na makundi matatu yale yale ambapo katika kifurushi cha Shaba mwanakikundi atachangia Sh.2,000 kwa mwezi na iwapo atafariki, Bima itatoa Sh.Milioni 1 kwake, kwa mwenzi, watoto, wazazi na wakwe.

Katika kifurushi cha Fedha mwanakikundi atatakiwa kuchangia Sh.5000 kwa mwezi na iwapo atafariki bima itatoa Sh.Milioni 3, mwenzi Sh.Milioni 2 na watoto, wazazi na wakwe Sh.Milioni 1.

Katika kifurushi cha Dhahabu mwanakikundi atachangia Sh.8000 na iwapo atafariki atapewa Sh.Milioni 5, mwenzi Sh.Milioni 4, watoto Sh.Milioni 1 na wazazi na wakwe Sh.Milioni 1.5.

Mahitaji ya kununua bima hii ni;
  • Kikundi kiwe na watu kuanzia watano. 
  • Kivuli cha kitambulisho chochote kinachotambuliwa na serikali mfano NIDA, leseni ya udereva n.k ya kila mwanakikundi. 
  • Orodha ya wanakikundi. 
  • Gharama ya malipo ya bima ya mwaka ( gharama italipwa kwa mwaka moja).
Tembelea tawi la NMB karibu nawe kujipatia Bima hii au kwa taarifa zaidi wasaliana na NMB huduma kwa wateja 0800 002 002.

ROSTAM AZIZ APPEALS FOR AfDB FUNDING TO AGRICULTURE

President of the African Development Bank Group, Dr. Akinwumi Adesina (left) shakes hands with Tanzanian business tycoon, Rostam Aziz in Washington DC after holding talks on agriculture development.

A local business mogul, Rostam Aziz has advised the African Development Bank (AfDB) to shore up financing to the agricultural sector so as to help Tanzania to become a major food exporting country.

He told the bank's president, Dr. Akinwumi Adesina during a meeting in Washington that Tanzania had a considerable potential to produce both food and cash crops for its domestic consumption as well as for export, but more investments were required to enhance productivity.

"Tanzania has a huge potential to produce food and cash crops for itself and the world. However, it is high time we stop singing about the potential and do actual investment in agriculture and its value chain", said Mr. Azizi who is visiting the United States as part of President Samia Suluhu Hassan's delegation.

KATA BIMA YA GARI KUPITIA BENKI YA NMB

Pata amani ya moyo ukiwa umebima gari lako kupitia Benki ya NMB.
  • Unaweza kupata mkopo wa bima na kuulipia kidogo kidogo kwa muda wa miezi 10
  • Janga litakapotokea, watasimamia na kuhakikisha madai yako yanalipwa ndani ya muda mfupi
  • Utapata huduma kwenye matawi yote ya NMB yaliyotapakaa nchi nzima


Kwa kuendelea kuwajali na kuwathamini Watanzania, Benki ya NMB ikishirikiana na makampuni ya Bima, inatoa huduma ya bima ya gari au chombo cha moto (gari, pikipiki n.k) kwa lengo la kutoa kinga dhidi ya hasara itokanayo na ajali, wizi, uharibifu na majeraha ya mwili au kifo kwa mtu mwingine.

Kuna aina mbili za bima hii, ndogo na kubwa. Bima ndogo (third party only) ina mkinga mwenye chombo dhidi ya majanga yaliyosababishwa kwa watumiaji wengine wa barabara ambayo ni kifo au majeruhi na uharibifu wa mali zao.

Wakati, Bima kubwa (comprehensive) inakinga uharibifu wa gari ya mteja kutokana na majanga ya barabarani, moto, wizi wa gari, mafuriko, kimbunga na majanga yote yanayofidiwa na Bima ndogo.

Unachohitaji ni;
  • Nakala ya kadi ya chombo na kitambulisho halali
  • Picha za chombo kwa wakati huo
  • Thamani ya chombo
Kata Bima hii kupitia *150*68# na endapo utahitaji kutoa taarifa za madai, basi fika tawi la NMB karibu yako au piga simu nambari 0800 002 002 bure kabisa!

Kwa barua pepe, tuma kwenda Bancassurance@nmbbank.co.tz

Umebima- SiNgumuKihivyo!

STANBIC BANK HOSTS AN IFTAR FOR ITS CUSTOMERS

Stanbic Bank Tanzania Chief Executive, Kevin Wingfield speaks during an iftar ceremony organized by the bank for its Muslim customers, held at Hyatt Hotel in Dar es Salaam recently. The ceremony was attended by Mufti Hon. Sheikh Aboubakary Zubeiry, top dignitaries from the National Muslim Council of Tanzania (BAKWATA) and various stakeholders of the bank including customers and the bank’s employees. During the event, Stanbic Bank reiterated its commitment to upholding its culture of inclusivity while servicing its clients with utmost dedication by creating tailor-made solutions.

Sunday 24 April 2022

STANDARD CHARTERED KUTOA FEDHA ZAIDI UJENZI WA SGR

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa tatu kushoto), na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango- Zanzibar Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb) (wa pili kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Benki ya Standard Chartered, baada ya kumalizika kwa mkutano wao uliofanyika katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Standard Chartered Tanzania Bw. Sanjay Raghani, Katibu Mkuu, Fedha na Mipango Zanzibar Dkt. Juma Malik Akil, Mwenyekiti wa Standard Chertered, Bw. Jose Vinals.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (katikati), na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb) (wa tano kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Benki ya Standard Chartered Pamoja na Ujumbe wa Tanzania, baada ya kumalizika kwa mkutano wao uliofanyika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kushoto), akisalimiana na Mwenyekiti wa Benki ya Standard Chartered duniani Bw. Jose Vinals, baada ya kumalizika kwa mkutano wao uliofanyika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kushoto), na Mwenyekiti wa Benki ya Standard Chartered Bw. Jose Vinals, wakibadilishana kadi za mawasiliano baada ya kumalizika kwa mkutano wao kuhusu uwekezaji kwenye miradi ya kimkakati nchini Tanzania, uliofanyika Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb), akisalimiana na Mwenyekiti wa Benki ya Standard Chartered Bw. Jose Vinals, baada ya kumalizika kwa majadiliano kati ya Ujumbe wa Tanzania na Benki hiyo kuhusu upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miradi uliofanyika Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango- Zanzibar Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb), akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Standard Chertered Tanzania, Bw. Sanjay Rughani, baada ya kumalizika kwa majadiliano kati ya Ujumbe wa Tanzania na Benki hiyo kuhusu upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo, uliofanyika katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Jijini Washington DC, Marekani.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao kati ya ujumbe wa Tanzania na Ujumbe wa Benki ya Standard Chartered kuhusu upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya kimkakati nchini Tanzania. Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Washington DC, Marekani. Kushoto ni Mwenyekiti wa Benki hiyo duniani Bw. Jose Vinals.

Benny Mwaipaja, Washington DC

Benki ya Standard Chartered imeihakikishia Tanzania kuwa iko tayari kutoa fedha zaidi kwenye miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali ikiwemo Reli ya kisasa ya SGR na ujenzi wa miundombinu ya viwanja vya ndege.

Ahadi hiyo imetolewa na Uongozi wa Benki hiyo ukjongozwa na Mwenyekiti wake Bw. Jose Vinals, ulipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Tanzania, ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb). kando ya mikutano ya majira ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), inayofanyika Jijini Washington DC, Marekani.

Akizungumza baada ya kikao hicho kilichofanyika katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Washington DC, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba alisema kuwa Benki hiyo ilitoa mkopo unaotumika kujenga reli ya kisasa ya SGR kutoka Morogoro hadi Makutupora, mkoani Singida, na kwamba hivi sasa Serikali iko kwenye mazungumzo na Benki hiyo ili itoe mkopo mwingine kwa ajili ya vipande vingine vya reli hiyo.