Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 31 March 2020

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI WAIUNGA MKONO WIZARA YA AFYA KUSAMBAZA UJUMBE JUU YA COVID-19

Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), John Wanyancha (kulia) akipokea sehemu ya vipeperushi vyenye ujumbe wa kuelimisha umma juu ya homa kali ya mapafu maarufu kama COVID-19 kutoka kwa Zaidan Wilfred ambaye ni afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. SBL imejitolea kuisaidia Serikali kusambaza vipeperushi hivyo nchi nzima. 
Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), John Wanyancha (kulia) akipokea moja ya kipeperushi chenye ujumbe wa kuelimisha umma juu ya homa kali ya mapafu maarufu kama COVID-19 kutoka kwa Zaidan Wilfred ambaye ni afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. SBL imejitolea kuisaidia Serikali kusambaza vipeperushi hivyo nchi nzima.

BENKI YA DCB YAUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA CORONA

Mkurugenzi Msaidizi wa Afya Mazingira wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khalid Massa (wa pili kushoto), akitakasa mikono yake katika moja ya vifaa 100 vya kutakasia mikono vyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 30 vilivyotolewa na Benki ya Biashara ya DCB vitakavyowekwa katika vituo mbalimbali vya daladala na mwendokasi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa homa ya mapafu wa Corona (Covid-19). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za wizara jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa. Wa tatu kushoto ni Mfamasia Mkuu wa Serikali, Daudi Msasi.
Mfamasia Mkuu wa Serikali, Daudi Msasi (katikati), akitakasa mikono yake katika moja ya vifaa 100 vya kutakasia mikono vyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 30 vilivyotolewa na Benki ya Biashara ya DCB vitakavyowekwa katika vituo mbalimbali vya daladala na mwendokasi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa homa ya mapafu wa Corona (Covid-19). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za wizara jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Afya Mazingira wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khalid Massa. 
Mfamasia wa Wizara ya Afya, Neema Nagu (katikati), akitakasa mikono yake katika moja ya vifaa 100 vya kutakasia mikono vyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 30 vilivyotolewa na Benki ya Biashara ya DCB vitakavyowekwa katika vituo mbalimbali vya daladala na mwendokasi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa homa ya mapafu wa Corona (Covid-19). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za wizara jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Afya Mazingira wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khalid Massa.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa (kushoto), akiweka kitakasa mikono katika chupa katika hafla ambayo DCB ilikabidi vifaa vifaa 100 vya kutakasia mikono vyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 30 vilivyotolewa na Benki ya Biashara ya DCB vitakavyowekwa katika vituo mbalimbali vya daladala na mwendokasi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa homa ya mapafu wa Corona (Covid-19). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za wizara jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Afya Mazingira wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khalid Massa na Mfamasia Mkuu wa Serikali, Daudi Masasi.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa (wa tatu kushoto), akikabidhi baadhi ya vitakasa 100 nyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 30 vilivyotolewa na benki hiyo vitakavyowekwa katika vituo mbalimbali vya daladala na mwendokasi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa homa ya mapafu wa Corona (Covid-19). Vifaa hivyo vilipokelewa katika ofisi za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam hivi karibuni na Mkurugenzi Msaidizi wa Afya Mazingira wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khalid Massa (wa tatu kulia), Mfamasia Mkuu wa Serikali, Daudi Masasi (wan ne kulia) pamoja na maofisa wengine.

KILI PHOTO CANVAS, CUTTING-EDGE TECHNOLOGY IN PHOTOGRAPHY USED FOR THE FIRST TIME IN THE WORLD BY A LOCAL COMPANY



Each year, Tanzanians and Citizens from all corners of the world meet in Moshi in Kilimanjaro to participate in the famous "Kili Marathon" that is sponsored by Tanzania Breweries Limited (TBL) through its Kilimanjaro Premium Lager beer. Kilimanjaro has been sponsoring the event and bringing refreshing moments to Tanzanians in Moshi for 18 years now.

In March this year, Kilimanjaro Premium Lager decided to do something different and introduced for the first time, an advanced photography technology during the marathon that placed the brand as an innovation leader globally. This technology developed by AIMGroup Tanzania is known as Kili Photo Canvas and is a unique system that captured runners' photos as they were running the marathon and sent it directly to their phone via WhatsApp.

BENKI YA NMB YATOA MSAADA WA SH. MILIONI 100 KWA AJILI YA MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA CORONA

Kama mchango wa Benki ya NMB katika kudhibiti na kupambana dhidi ya virusi vya Corona, Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna amekabidhi msaada wa kifedha wa shilingi Milioni 100 kwa Mhe. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali. Makabidhiano hayo yamefanyika mwishoni mwa wiki katika ofisi ya Waziri Mkuu, Dar es Salaam.

Benki ya NMB ikiwa na maadhimio sawa ya kuudhibiti ugonjwa huu, mchango huu utaisaidia serikali katika mapambano dhidi ya virusi hivi.

Tunasisitizwa kuendelea kutumia njia stahiki kujikinga na maambukizi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (wa tatu kushoto) akipokea hundi ya Sh. Milioni 100 kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (wa nne kutoka kushoto). Kushoto ni Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa wa Serikali wa NMB Alfred Shao na kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na uongozi wa Benki ya NMB.

Sunday 29 March 2020

KAMPUNI YA MULTICHOICE KUTOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 10 KUSAIDIA WAZALISHAJI WA MAUDHUI WAKATI WA JANGA LA COVID-19

Afisa Mtendaji Mkuu wa kundi
la makampuni ya MultiChoice,
Calvo Mawela.
Wakati hali ya janga la ugonjwa wa virusi vya Corona (Covid-19) likiendelea kuitikisa dunia, Kampuni ya MultiChoice imetangaza mpango wake wa kutoa randi milioni 80 (sawa na takriban shilingi bilioni 10.5) kusaidia wazalishaji wa maudhui katika kipindi hiki cha kupambana na virushi vya Corona.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Afisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya MultiChoice Calvo Mawela amesema “dhamira yetu ni kuhakikisha watu wote wanaofanya uzalishaji wa maudhui yetu kote barani Afrika wanaendelea kupata kipato chao bila kuathirika katika wakati huu. Tunataka wadau wetu hawa muhimu wasiathiriwe vibaya na hali ya sasa ambapo kazi nyingi za uazalishaji zimesimama.

Taarifa hiyo pia imebainisha kuwa kwa kupitia programu yake ya MultiChoice Talent Factory (MTF) kampuni hiyo itazindua ulingo wa mafunzo maalum kwa njia ya mtandao (online learning portal) itakayowezesha zaidi ya watu 40,000 wa tasnia ya uzalishaji maudhui kupata mafunzo ya kawaida na mafunzo maalum (master classes). Mafunzo haya yatawafanya wana tasnia waendelee kujifunza huku wakizingatia maagizo ya mamlaka za afya yanayowataka watu kuepuka mikusanyiko na kukaa nyumbani katika kipindi hiki cha mlipuko wa virusi vya corona.

Kwa sasa kila sekta kote ulimwenguni imekuwa ikipitia kipindi cha mabadiliko na changamoto nyingi zinazotokana na maradhi haya na kwakuwa MultiChoice ni mdau mkubwa katika sekta ya habari na burudani nayo imeamua kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa inasimama na wadau wake pamoja hata katika nyakati ngumu kama hizi.


Saturday 28 March 2020

BENKI YA CRDB YATOA MILIONI 30 KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA CORONA (COVID-19)

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kulia) akimkabidhi Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Elisha Osati, mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. Milioni 30, ikiwa ni mchango wa Benki ya CRDB kusaidia kampeni ya kuelimisha juu ya mapambano ya ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona. Makabidhiano hayo yalifanyika katika tawi la Benki ya CRDB Azikiwe, jijini Dar es Salaam jana.
Benki ya CRDB imetoa msaada wa shilingi milioni 30 kwa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kusaidia mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya corana. Akizungumza katika hafla fupi na waandishi wa habari iliyofanyika katika tawi la Azikiwe, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema msaada huo unakwenda kusaidia kampeni maalum inayoendeshwa na chama hicho katika kuelimisha Watanzania juu ya kujikinga na ugonjwa wa Corona (COVID-19) ijulikanayo “TUNAWEZA KUJIKINGA”.

Nsekela alisema katika kipindi hiki ambacho dunia inapambana na ugonjwa wa Corona hakunabudi kwa taasisi na mashirika yote kuungana na Serikali na wataalamu wa afya katika kutoa elimu kwa Watanzania itakayosaidia kupunguza maambukizi na kuondokana kabisa na ugonjwa huo wa Corona.

“Benki yetu ya CRDB tayari imeshachukua hatua mbalimbali zinazosaidia kuwakinga wafanyakazi na wateja wetu, ikiwamo kuweka dawa za kusafisha mikono (hand sanitizer) katika ofisi zetu, matawi pamoja na ATM,” alisema Nsekela huku akishukuru Wizara ya Afya na Chama cha Madaktari kwa kuwa nao bega kwa bega katika kutoa elimu kwa wafanyakazi na wateja wa benki hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, akinawa mikono kwa kutumia vitakasa mikono wakati wa hafla ya kukabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. Milioni 30 kwa Chama cha Madaktari Tanzania, ikiwa ni msaada wa benki hiyo kusaidia kampeni ya uelimisha juu ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona.
Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Elisha Osati, akinawa mikono ikiwa ni tahadhari ya kupata maambukizi ya virusi vya corona.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada wa Sh. Milioni 30 kwa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), kwa ajili ya kusaidia kampeni ya uelimisha juu ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona. 
"Tunaagana"

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, akizungumza na wateja wa Tawi la Azikiwe jijini Dar es Salaam.
Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dkt. Elisha Osati aliishukuru Benki ya CRDB kwa mchango huo wa shilingi milioni 30 huku akisema kuwa hela hiyo itaelekezwa katika kuelekezwa katika utoaji elimu kwa watumishi wa sekta ya afya husasan katika huduma za afya za msingi kuanzia Zahanati na Vito vya Afya itakayowasaidia kutambua wagonjwa na hatua za kuchukua pindi wanapopata mgonjwa. Dkt. Osati alisema zoezi hilo linaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Madaktari kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Wanafanzi (TAMSA), ambapo zoezi hilo tayari limeshaanza katika mkoa wa Dar es Salaam.

Friday 27 March 2020

NINI MAANA YA MAFANIKIO KATIKA MTAZAMO WA MAENDELEO BARANI AFRIKA? LAWRENCE MAFURU ATAKUWA MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI LEO USIKU


Nini maana ya Mafanikio katika Mtazamo wa Maendeleo barani Afrika?

Ungependa kufunguliwa kifikra juu ya hili?

Ungana nasi Kwenye Mtazamo Round Table Ijumaa hii saa 2 hadi 3 kamili usiku huku tukio zima ukiliona LIVE kupitia @cloudsplus DStv Channel namba 294

#MtazamoRoundTable
#KilaMtuMachokodo

CORONA VIRUS: DSTV ASSURES CUSTOMERS OF EXTENDED INFORMATION, EDUCATION AND ENTERTAINMENT

DStv is setting out how it will ensure its customers are informed, educated, and entertained during the coronavirus ordeal.

MutliChoice Tanzania has announced its plan to continue providing its DStv customers with access to invaluable content during this time of disruption.

This strategy is a major move for DStv on its mission to ensure Tanzanians are up to date with all that is happening around them, and also goes a long way in keeping families educated, entertained and reliably informed.

This plan comes in the wake of many recent changes and adjustments in the daily lives of Tanzanians, which include closure of schools and colleges and restrictions in travels and gatherings which compel families to spend hours in isolation at home.

Thursday 26 March 2020

DSTV KUMENOGA. PATA KUJUA YANAYOJIRI ULIMWENGUNI


DStv kumenoga

Pata kujua yanayojiri ulimwenguni, kwa kutazama na kufuatilia habari kupitia chaneli za habari CNN 401 Africa News 417 pamoja na Euro News 414 zilizoshushwa mpaka kifurushi cha Bomba TShs. 19,000 tu.

Hatuishii hapo ndani ya kifurushi cha Bomba, mtoto wako atafurahia na kujifunza kupitia chaneli ya watoto Da Vinci 318 pamoja na Cartoon Network 309

Na kwa wewe mpenzi wa michezo utapata kuburudika na makali mbalimbali ya kimchezo kupitia Supersport ReLive. Supersport 1 imeshushwa mpaka kifurushi cha Compact ikiwa imebeba matukio muhimu yaliyowahi kujitokeza katika michezo, huku Supersport 4 ikishuka mpaka kifurushi cha Family.

Hakikisha unalipia mapema kifurushi chako ili usipitwe na burudani hii!

Wednesday 25 March 2020

VODACOM YASAIDIA JAMII KUPAMBANA NA COVID-19

Dar es Salaam, Machi 24, 2020 - Hivi karibuni, Watanzania wengi wameungana na dunia nzima katika kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 (maarufu Corona). Katika miezi na wiki zijazo juhudi za pamoja zinahitajika ili kusaidiana na serikali katika kupambana na athari za mlipuko wa ugonjwa huu.

Jihitada za kuisaidia jamii kutatua changamoto mbalimbali kama ilivyo kwa janga hili la COVID-19 ni mojawapo ya majukumu ya Vodacom Tanzania PLC katika kusaidia jamii na wadau wake. Kipaumbele cha Vodacom ni afya na usalama wa wafanyakazi wake zaidi ya 560, na wakati huo huo kuendelea kutoa huduma, kuunganisha na kusaidia wateja wake kwa kuzingatia miongozo ya serikali na wizara zake.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Hisham Hendi anasema, “Vodacom ina majukumu muhimu katika kipindi hiki kisicho cha kawaida. Tuna mkakati wa kuhakikisha kuwa biashara yetu inakuwa endelevu wakati wote. Niwahakikishie Watanzania kuwa wataendelea kupata huduma zetu kwa kuunganishwa na marafiki na familia na kwamba biashara itaendelea kufanyika kwa kutumia njia za kidijitali kupitia mtandao wetu ulioboreshwa.”

Hendi aliongeza kuwa, “Wakati huo huo tunaweka juhudi za pamoja, kuwasaidia wanafunzi ambao kwa sasa wamefunga shule ili waweze kupata nyenzo za kujisomea kwa njia ya kidijitali kwa kutumia mitaala inayokubalika kimataifa. Kupitia mfumo uliopitishwa kimataifa wa Khan Academy http://instantschools.vodacom.co.tz/user/#/signin wanafunzi ambao wako nyumbani kutokana na janga hili wanaweza kuendelea kujisomea ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua stahiki za kujikinga na ugonjwa wa COVID-19.”

CRDB BANK DONATES TSHS 30 MILLION FOR CORONAVIRUS AWARENESS CAMPAIGN

CRDB Bank Managing Director, Abdulmajid Nsekela (right), presents a TShs. 30 million dummy cheque to Medical Association of Tanzania (MAT) President, Dr. Elisha Osati (left) being part of the bank's support towards a campaign against Coronavirus. The handing over ceremony was held in Dar es Salaam yesterday.
CRDB Bank has become the first Financial Institution to donate money to fight against the novel coronavirus in the country.

The bank yesterday donated TShs. 30 million to the Medical Association of Tanzania (MAT) to assist in combating the pandemic.

CRDB Bank Managing Director, Abdulmajid Nsekela said the donation is for an awareness campaign that is aimed at stopping the spread of the virus.

Continue Reading >>>

DSTV KUSOGEZA BURUDANI KWA WATOTO KATIKA KIPINDI HIKI AMBAPO WAPO NYUMBANI

@dstvtanzania inajali na kuthamini watoto na kwa kuzingatia hilo katika kipindi hiki ambapo wapo nyumbani @dstvtanzania inawasogezea burudani watoto kupitia chaneli Cartoon Network 301, huku ikizidi kuwapa kujifunza kupitia chaneli Da Vinci 318 ambazo sasa zimeshushwa mpaka kifurushi cha Bomba TShs. 19,000 tu.

Haiishi hapo kwani kuanzia tarehe 29 Machi 2020 kupitia kifurushi hiki cha Bomba TShs. 19,000 tu watoto watazidi kupata burudani kupitia chaneli maalum iitwayo "Toonami SuperHero".

Hakikisha unalipia mapema kifurushi chako ili mtoto wako aweze kufaidi burudani hii!

CLYDE & CO UPDATER - TANZANIA ELECTRICITY RULES 2019

The Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) recently released new rules to govern various electricity matters. These relate to the development of small power projects (SPPs), generation, transmission and distribution activities along with supply services. The new rules attempt to address some of the challenges contained in the previous (repealed) rules by providing less procedural requirements. In this article, we provide an overview of the recently released Electricity Rules and how this affects businesses in Tanzania.

Tuesday 24 March 2020

CORONA VIRUS: DSTV YAPANUA WIGO WA HABARI, ELIMU NA BURUDANI KWA WATEJA WAKE

Ni katika jitihada za kuhakikisha jamii inapata habari za uhakika, elimu ya kutosha na burudani kipindi hikicha mapambano dhidi ya corona

Pamoja na changamoto iliyopo duniani kwa sasa, MultiChoice inawahakikishia wateja wake wa DStv kuwa inayazingatia mahitaji yao has ukizingatia kuwa kwa sasa watu wengi wanalazimika kukaa nyumbani katika jitihada za kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.

“Tutaendelea kukupa wigo mpana zaidi wa kupata habari za uhakika kwa kufungua chaneli za habari kwenye vifurushi vyetu. Tunazingatia mawasiliano ya mara kwa mara na mamlaka husika na tutashiriki kikamilifu katika kupambana na kuenea kwa ugonjwa wa Covid-19. Ni muhimu sana sote tuzingatie maelekezo na maagizo yanayotolewa na mamlaka sahihi na wataalamu wetu ili kuhakikisha kuwa tunalinda afya zetu na za wenzetu” amesema Jacqueline Woiso, Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania

Mkurugenzi huyo ametangaza rasmi kwamba kuanzia sasa;

  • Fahamu kinachoendelea 
Ili kukuwezesha kupata habari na taarifa za uhakika katika kipindi hiki, tunapanua wigo wa habari kwa kufungua chaneli kubwa za habari katika vifurushi vyetu. Kuanzia leo chaneli ya CNN (401) na Euronews (414) zitafunguliwa kwa wateja wa vifurushi vyote kuanzia kile cha chini kabisa cha DStv Bomba. Pia tumefungua chanel maarufu ya habari za Afrika Africanews(chaneli 417) kwenye vifurushi vyetu vyote hadi tarehe 1 Mei ambapo chaneli hii itakuwa inapatikana kuanzia kifurushi cha DStv Family.
  • Kwa watoto
Kwa kuzingatia kuwa Watoto wetu wako likizo kipindi hiki, maudhui ya elimu yamezingatiwa ambapo chaneli ya elimu ya Da Vinci(Chaneli 318) na ile ya burudani ya Cartoon Network(channel 310) sasa zimefunguliwa kwa vifurushi vyote kuanzia cha chini kabisa cha DStv Bomba. Hii ni katika jitihada za kuhakikisha watoto wetu wanaendelea kupata elimu na burudani wakati huu wakiwa nyumbani.


UBONGO TO PROVIDE RESOURCES AND SUPPORT HOME LEARNING INITIATIVES AMID CORONAVIRUS OUTBREAK AND SCHOOLS SHUT DOWN

BENKI YA NMB YAKABIDHI MSAADA WA VITI, MEZA NA MADAWATI VYA THAMANI YA SH. 15M/- KWA AJILI YA SHULE ZA SEKONDARI WILAYANI UBUNGO

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd (kushoto) akimkabidhi msaada wa madawati, viti na meza 150 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kisare Makori (kulia) katika Shule ya Sekondari Kibamba. Vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 15 vimetolewa na Benki ya NMB kuzisaidia Shule tatu za Manispaa ya Ubungo ambazo ni Kibamba, Kinzudi Sekondari pamoja na Shule ya Msingi Makuburi Jeshini zote za jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Kisare Makori (kulia mwenye suti) pamoja na Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd (wa pili kushoto) wakikata utepe kuzinduwa madawati, viti na meza 150 katika Shule ya Sekondari Kibamba, vilivyotolewa na Benki ya NMB kuzisaidia Shule tatu za Manispaa ya Ubungo ambazo ni Kibamba na Kinzudi Sekondari na Shule ya Msingi Makuburi Jeshini kutatua changamoto za madawati leo katika Manispaa ya Ubungo.
Benki ya NMB, imekabidhi msaada wa viti, meza na madawati vyote vikiwa na thamani ya Sh. Milioni 15 kwa ajili ya Shule za Sekondari Kibamba na Kinzudi na Shule ya Msingi Makuburi Jeshini, zilizoko wilayani Ubungo jijini Dar es Salaam.

Hafla ya kukabidhi msaada huo ilifanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kibamba, ambako Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd alimkabidhi msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori (aliyekuwa mgeni rasmi).

Alisema Kibamba Sekondari yenye wanafunzi 1,365, ilikuwa na changamoto ya uhaba wa viti na meza na kwamba msaada wa NMB unaenda kupunguza kwa kiasi kikubwa adha ya wanafunzi kusoma katika mazingira yasiyo rafiki.

Naye Ofisa Elimu (Sekondari) Wilaya ya Ubungo, Hilda Shalanda, alisema kinachofanywa na benki ya NMB katika wilaya yake kwenye sekta ya elimu, ni kitu cha kupongezwa na kinachopaswa kuungwa mkono na wadau wengine kwa kuzifikia shule mbalimbali zenye uhitaji.

NATIONAL BANK OF COMMERCE REQUEST FOR EXPRESSION OF INTEREST FOR CONSULTANCY SERVICES - MIGRATION OF ITS SERVICES HOSTED AT THE SHARED ENVIRONMENT IN SOUTH AFRICA TO TANZANIA

LET’S ENCOURAGE CREATIVITY AND INNOVATION TO FUEL TANZANIA’S DRIVE TOWARDS INDUSTRIALISATION

Last week saw the opening of an exhibition at Mbeya University of Science and Technology. The exhibition brought together numerous students and staff from colleges and institutions across the Mbeya region, to discuss the opportunities that arise from innovation.

Speaking at the exhibition, Dr John, the Acting President of the Faculty of Science and Technical Education at Mbeya University, called on Tanzania’s Commission for Science and Technology to develop special funds to help identify and support universities and their students with research and development.

Dr John highlighted that creating these funds will help encourage business creativity, which will benefit the nation in its pursuit of becoming an industrial economy. We are all well aware that becoming an industrialised economy is high on the President’s agenda.

Monday 23 March 2020

BAADA YA LIGI KUSITISHWA, DSTV KUPITIA KAMPENI YA "SUPERSPORT RELIVE" INAKUHAKIKISHIA BURUDANI KUPITIA ULIMWENGU WA KIMICHEZO WA SUPERSPORT


Baada ya Ligi kusitishwa, @dstvtanzania kupitia kampeni ya Supersport Relive inakuhakikishia burudani kupitia ulimwengu wa kimichezo wa Supersport.

Supersport 1 itashushwa mpaka kifurushi cha Compact ikiwa imebeba matukio muhimu yaliyowahi kujitokeza katika michezo, huku Supersport 4 ikishuka mpaka kifurushi cha Family.

Pata kutazama makala mbalimbali za kimichezo ikiwemo, Golf, Tennis, Masumbwi, mechi kali kutoka katika ligi mbalimbali.

Lipia sasa kifurushi chako na ufurahie ulimwengu huu wa kimichezo

#SupersportRelive

DSTV KUMENOGA!!! PATA KUJUA YANAYOJIRI ULIMWENGUNI, KWA KUTAZAMA NA KUFUATILIA HABARI KUPITIA CHANELI ZA HABARI


DStv kumenoga!!!

Pata kujua yanayojiri ulimwenguni, kwa kutazama na kufuatilia habari kupitia chaneli za habari CNN 401 pamoja na Euro News 414 zilizoshushwa mpaka kifurushi cha Bomba 19,000 tu.

Hatuishii hapo ndani ya kifurushi cha Bomba, mtoto wako atafurahia na kujifunza kupitia chaneli ya watoto Da Vinci 318 pamoja na Mind Set 319

Hakikisha unalipia mapema kifurushi chako ili usipitwe na burudani hii!

BAADA YA LIGI KUSIMAMISHWA, DSTV TUNAKUHAKIKISHIA BURUDANI KUPITIA ULIMWENGU WA KIMICHEZO SUPERSPORT



Supersport ReLive
Baada ya Ligi kusimamishwa, tunakuhakikishia burudani kupitia ulimwengu wa kimichezo Supersport.

Supersport 1 itashushwa mpaka kifurushi cha Compact ikiwa imebeba matukio muhimu yaliyowahi kujitokeza katika michezo.

Supersport 2 - Grand Prix
Supersport 3 - Matukio ya #EPL
Supersport 4 - Pata kufurahia WWE
Supersport 5 - Golf
Supersport 6 - Tennis
Supersport 7 - Soka ( Kifurushi Bomba)
Supersport 8 - Boxing 🥊
Supersport 9 - Soka la Africa
Supersport 10 - Soka zaidi
Supersport 11 - Rugby 🏉 na Cricket 🏏
Supersport 12 - Boxing 🥊

Friday 20 March 2020

JOB VACANCY AT A COMMERCIAL BANK - HEAD OF RETAIL BANKING

NATIONAL BANK OF COMMERCE TENDER NOTICE - REQUEST FOR PROPOSAL FOR VARIOUS SERVICES

JOB VACANCY AT VODACOM - M-PESA DECISION SCIENTIST

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 19-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

Role purpose:

To develop fit-for-purpose predictive and affordability models, execute and analyse our markets to determine the most effective way to increase customer base whilst minimizing customers at risk of churning, increase customer acquisition, conversion and retention; cross selling and upselling, customer behaviour segmentation, analyse customer feedback from call centre, social network analysis. Increase of M-Pesa product penetration, customer engagement, increase M-Pesa ARPU and sharing insights.

JOB VACANCY AT VODACOM - SENIOR REGULATORY AFFAIRS SPECIALIST

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 17-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

Role Purpose
The Regulatory / Public Policy Lead focusses upon the development and provision of expert regulatory policy, economic analysis and cost modelling in support of policy development and advocacy within specialist areas with reference to the particular risks and goals of Vodafone and identification of areas within Vodafone where new policy is required. They are recognised as a technical expert providing policy advice on all matters within area of expertise and demonstrate strong public policy understanding in specialist area and the implications of this across wider Vodafone teams. Ensuring compliance with the key regulatory requirements and/or the regulatory compliance programme/matrix across the company.

JOB VACANCY AT VODACOM - ON-GROUND ACTIVATIONS & SPONSORSHIPS SPECIALIST

Posting Country: TZ
Date Posted: 17-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

Job Profile

  • Assist the business development efforts by planning Trade Activations activities (sales and marketing) on the ground, to acquire new and retain subscribers. 
  • Management of all on ground activations , events and sponsorship mechanics as per individual business plans
  • In having customer satisfaction as main priority, he/she is the contact point between marketing department and sales team to ensure achievement of sales objectives.
  • On-ground Activations & Sponsorships Specialist will ensure growth of both revenue and customer base according to the set overall company and division strategies.

JOB VACANCY AT VODACOM - HOD: MERCHANT PAYMENTS

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 17-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

JOB PROFILE

Responsible for creating and executing merchant payment strategy provision of expert knowledge. Interacts with other teams within the function or work area, plans and controls resources required for delivery.

KEY ACCOUNTABILITIES
  • Create and execute merchant acquisition strategy (both online merchants and offline)
  • Create and execute marketing strategy to increase customer adoption
  • Create and execute e-commerce strategy
  • Identify opportunities and develop new products, using data and insight to establish the consumer’s problem or unmet need
  • Oversee the attracting, recruiting, deployment and retention of “A” players for the department

JOB VACANCY AT VODACOM - HEAD OF NETWORK OPERATIONS

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 11-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

Role purpose:
  • Formulation and execution of the overall network technology strategy aligned with the Group Technology blueprint and roadmap and with the local market business strategy to ensure network coverage and quality differentiation and service user-experience superiority.
  • To lead the entire Network Operations team toward excellent performance standards by monitoring, analysing and controlling end-to-end Network architecture and service design, site rollout and program management, KPI’s and SLA assurance to ensure operational excellence and adherence to company strategy, goals and Regulatory compliance. 
  • Network CAPEX & OPEX budget planning and execution through implementation of cost optimization initiatives, effective program management and commercially driven network investment for maximization of financial returns.

JOB VACANCY AT VODACOM - HEAD OF NETWORK ENGINEERING

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 11-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent

Role purpose:
  • Formulation and execution of the overall network technology strategy aligned with the Group Technology blueprint and roadmap and with the local market business strategy to ensure network coverage and quality differentiation and service user-experience superiority.
  • To lead the entire Network Engineering team toward excellent performance standards by monitoring, analysing and controlling end-to-end Network architecture and service design, site rollout and program management, KPI’s and SLA assurance to ensure operational excellence and adherence to company strategy, goals and Regulatory compliance. 
  • Network CAPEX & OPEX budget planning and execution through implementation of cost optimization initiatives, effective program management and commercially driven network investment for maximization of financial returns.

JOB VACANCY AT VODACOM - HEAD OF NETWORK PERFORMANCE

Posting Country: Tanzania, United Republic of
Date Posted: 11-Mar-2020
Full Time / Part Time: Full Time
Contract Type: Permanent


Role purpose:

  • Formulation and execution of the overall network technology strategy aligned with the Group Technology blueprint and roadmap and with the local market business strategy to ensure network coverage and quality differentiation and service user-experience superiority.
  • To lead the entire Network Performance team toward excellent performance standards by monitoring, analysing and controlling end-to-end Network architecture and service design, site rollout and program management, KPI’s and SLA assurance to ensure operational excellence and adherence to company strategy, goals and Regulatory compliance. 
  • Manage end-to-end quality of experience and SLA for the Vodacom enterprise clients through Customer Support Operations Centre (CSOC)

TANZANIA BANKERS ASSOCIATION IN A JOINT MEETING WITH MINISTRY OF HEALTH AND BANK OF TANZANIA OFFICIALS

Tanzania Bankers Association (TBA) members in a joint meeting with Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children and Bank of Tanzania officials in Dar es Salaam yesterday, to discuss various measures that can be taken by TBA and the government in ensuring availability of safety measures to combat COVID-19 in the country.


Thursday 19 March 2020

AIRTEL KENYA WAIVES MOBILE MONEY TRANSACTION FEES ACROSS ALL BANDS

Airtel Kenya has waived the transaction fees across all bands on its mobile money service.

The telco announced Monday that starting Tuesday, all person to person money transfer will be free for the next 90 days as the country works to combat the potential spread of coronavirus.

The company has also increased the transaction limits and the amounts individuals can hold in their mobile wallets.

Airtel has increased the daily transaction limit from Ksh70,000 ($700) to Ksh150,000 ($1500) while the daily limit for mobile money transactions is up to Ksh300,000 ($300) from Ksh140,000 ($1,400).

NMB: HUDUMA YA BIMA KUPITIA BENKI HUKUZA BIASHARA ENDELEVU

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi, Biashara Ndogo na za Kati, Filbert Mponzi akizungumza na wateja waliohudhuria mkutano wa NMB Business Club kupata maoni yao kuhusu huduma na bidhaa za NMB.
Meneja wa Mikopo ya Nyumba NMB, Miranda Lutege akielezea mikopo ya nyumba wakati wa mkutano wa NMB Business Club. 
Meneja Mwandamizi wa Bima wa Benki ya NMB, Martine Massawe akielezea kuhusu Bima ‘Bancassuarance’ wakati wa mkutano wa NMB Business Club.
Benki ya NMB imesisitiza umuhimu wa wafanyabiashara kukata bima ya biashara zao ili ziwe endelevu kwa kuzilinda dhidi ya hatari (risks) zinazoweza kujitokeza.

Akizungumza katika semina iliyohudhuriwa na wajasiriamali wapatao 300 wanaounda Klabu ya Biashara ‘NMB Business Club’ ya Mkoa wa Dar es Salaam, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi, Biashara Ndogo na za Kati wa NMB, Filbert Mponzi, alisema kuwa biashara hukabiliwa na hatari (risk) mbali mbali ambazo kinga yake ni kuzikatia bima. Majanga kama moto, wizi na mafuriko ni baadhi ya hatari zinazozikabili biashara na kudumaza ukuaji endelevu wake.

Ikiwa na matawi 225 nchini kote, NMB inayo nafasi bora ya kufikisha huduma za bima kwa watu wote (wateja wake na wasio wateja wake) popote walipo.

Benki ya NMB inatoa huduma za bima (Bancassurance) katika matawi yake yote 225 nchini kote kupitia ushirikiano wake na kampuni za bima za Sanlam, UAP, Shirika la Bima la Taifa (National Insurance Corporation - NIC), Jubilee, Shirika la Bima la Zanzibar (Zanzibar Insurance Corporation – ZIC) na Reliance.

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA SADC

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akifungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika uliofanyika kwa njia ya video kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Machi 2020. 
Mhe. Waziri Mkuu akitoa salamu kwa Nchi Wanachama wa SADC ambao ni wajumbe wa Mkutano huo unaoongozwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa jumuiya hiyo. Pamoja na salamu hizo za ufunguzi Mhe. Waziri Mkuu alipongeza jitihada zinazofanywa na Nchi Wanachama katika kukabiliana na majanga mbalimbali ikiwemo la ugonjwa wa virusi vya CORONA ambao umewezesha nchi wanachama kushirikiana kutafuta namna bora ya kuendelea na shughuli za utekelezaji kwa ustawi wa kanda na watu wake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, Mhe. Palamagamba John Kabudi akitoa hotuba ya utangulizi kumkaribisha Waziri Mkuu ili aweze kufungua mkutano wa wa Baraza hilo uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jinini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC, Dkt. Stergomena Tax akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu ya jumuiya hiyo wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC.
Wajumbe wa Mkutano huo ambao ni Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine waandamizi wakifuatilia hafla ya ufunguzi.