Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 28 June 2023

NBC DODOMA MARATHON 2023: A PARAMOUNT OF CORPORATE PHILANTHROPY

By Godwin Jaha Semunyu

Marathoners have a special way of teaching us about endurance and defying limits. Eliud Kipchoge's world record redefined human boundaries, while John Akhwari's superhuman finish in Mexico in 1968, despite injury, a dislocated knee, inspires.

In our everyday lives, we require this resolute spirit and mentality to confront challenges head-on. Ultimately, life unfolds as a marathon, demanding our enduring commitment and steadfastness to reach our goals.

NBC Dodoma Marathon 2023. Here for improved maternal health:

We are excited to invite you to the upcoming fourth edition of the NBC Dodoma Marathon on Sunday, July 23, 2023, in Dodoma.

This extraordinary event is dedicated to generating funds for enhanced maternal health through cervical cancer awareness initiatives and providing valuable scholarship opportunities to aspiring midwifery scholars in Tanzania.

Raising Awareness for Cervical Cancer:

Cervical cancer claims the most lives among women in developing countries, often due to late-stage diagnoses stemming from limited awareness and inadequate screening.

To combat this dire situation, we have partnered with the Ocean Road Cancer Institute (ORCI) to amplify awareness efforts. Our goal is to reach a broader audience, encourage regular screenings, and offer financial aid for medical expenses.

WAZIRI NAPE AZINDUA OFISI YA KISASA YA VODACOM JIJINI DODOMA

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye (katikati) akizungumza na viongozi wa Vodacom Tanzania wakati wa uzinduzi wa ofisi mpya yenye ubora na uwezo sawa na ya makao makuu ya Dar es Salaam ikiwemo kuhudumia wasioona na kusikia pamoja na chumba maalum cha wajawazito na waliojifungua, makao makuu ya nchi, jijini Dodoma. Wakimsiliza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mh. Selemani Kakoso wakati kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara, Linda Riwa, Mkuu wa Kanda ya Kati, Joseph Sayi, na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (kwa nyuma).

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania, Joseph Sayi (kushoto), wakati wa uzinduzi wa ofisi mpya ya kampuni hiyo yenye ubora na uwezo sawa na ya makao makuu ya Dar es Salaam ikiwemo kuhudumia wasioona na kusikia pamoja na chumba maalum cha wajawazito na waliojifungua, makao makuu ya nchi, jijini Dodoma. Akimfuatia kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mh. Selemani Kakoso Pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Vodacom Tanzania, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo.

Dodoma – Juni 28, 2023: Waziri Mkuu wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye amepongeza jitihada za Vodacom Tanzania kwa kufungua ofisi ya kisasa katika makao makuu ya nchi, Dodoma ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali kuhamishia sehemu ya shughuli zake jijini humo pamoja na kusambaza huduma za mawasiliano na kiteknolojia nchini kote.



Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ofisi hiyo mpya ya kisasa makao makuu ya nchini mkoani Dodoma, Mheshimiwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia na Habari, Mh. Nape Nnauye amepongeza jitihada hizo zikiwa zinalenga kuwasogezea Watanzania huduma bora na za uhakika popote walipo kama serikali inavyofanya kuhamishia baadhi ya shughuli zake katika makao makuu ya nchi ili kuwapunguzia usumbufu wa kusafiri umbali mrefu mpaka Dar es Salaam.



Friday 23 June 2023

HUDUMA YA NBC CONNECT YAGONGA HODI MKOANI DODOMA

Meneja wa NBC tawi la Dodoma Japhet Fungo akiuelezea Mfumo wa NBC Connect namna unavyoweza kurahisisha ufanyaji wa miamala kidigitali kwa wateja wa benki hiyo katika Hafla ya Uzinduzi wa mfumo huo iliyofanyika jijini Dodoma.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Ally Gugu (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa meneja wa benki ya NBC tawi la Dodoma Japhet Fungo muda mfupi baada ya uzinduzi wa huduma ya NBC Connect katika Hafla ya Uzinduzi wa huduma hiyo iliyofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi wa huduma ya NBC Connect inayowezesha kufanya miamala kwa urahisi kwa njia ya kidigitali. Hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo ilifanyika jijini Dodoma.

Mgeni rasmi katika uzinduzi wa huduma ya NBC Connect, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Ally Gugu (watatu kulia)akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa benki ya NBC na baadhi ya wateja walioalikwa kwenye uzinduzi wa huduma ya NBC Connect inayowezesha kufanya miamala kwa urahisi kwa njia ya kidigitali. Hafla hiyo imefanyika jijini Dodoma.

Dodoma Juni 21, 2023: Makampuni pamoja na taasisi mbali mbali ambazo ni wateja wa Benki ya Taifa ya Biashara ya (NBC) mkoani Dodoma, sasa wanaweza kupata uzoefu mpya wa huduma za kibenki kupitia huduma ya kibenki kwa njia ya kidigitali inayojulikana kama ‘NBC Connect’

NBC Connect, ni huduma ya kisasa ya kidigitali kwa makampuni na taasisi mbali mbali, ambayo huwezesha huduma salama za kibenki kufanyika sehemu yoyote, muda wowote kwa njia ya mtandao.

Huduma hii ni sehemu ya mchango wa benki katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuongeza ujumuifu katika huduma za kifedha (financial inclusion) kwa makundi mbali mbali.

Uzinduzi wa huduma ya NBC Connect Dodoma, ni wa tatu baada ya uzinduzi uliofanyika kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya na wa Kanda ya ziwa uliofanyika Mwanza.

USIKOSE ORIGINO KOMEDI NDANI YA MAISHA MAGIC POA


Jumapili hii ndani ya Origino Komedy, maji yamepanda bei, mganga wa kienyeji anaumbuka......

#Unakosaje visa vya Origino Komedi ndani ya Maisha Magic Poa, 144?

Piga *150*53# kulipia kifurushi chako cha Poa TShs 10,000 tu.

#tvnidstv

WATEJA WA TOTALENERGIES KURUDISHIWA 10% KUPITIA USHIRIKIANO NA LIPA KWA M-PESA

Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom Tanzania PLC, Bi. Harriet Lwakatare (kushoto) na Meneja Masoko wa TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, Caroline Kakwezi (kulia) wakifurahia baada ya uzinduzi wa ushirikiano utakaowawezesha wateja wa TotalEnergies kulipa kwa LIPA kwa M-Pesa masaa 24, siku 7 za wiki kwenye vituo vyote vya kutolea huduma na maduka yote ya Bonjour nchini kote uliofanyika Oysterbay jijini Dar es Salaam. Pia, wateja watarudishiwa 10% ya pesa watakapolipia kwa kutumia M-Pesa kwa siku 15 zijazo na kila Jumamosi kwa miezi mitatu ijayo.

Mteja wa TotalEnergies, Bw. Ambrose Kumbila (mwenye bodaboda) akifurahia pamoja na Meneja Masoko wa TotalEnergies Marketing Tanzania Limited, Caroline Kakwezi (wa kwanza kulia), Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom Tanzania PLC, Bi. Harriet Lwakatare (wa pili kulia), na Meneja Uendeshaji wa Mtandao wa TotalEnergies, Bw. Thomas Meitaron (katikati), pamoja na Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa Sheria, Bw. Agapinus Tax (wa kwanza kushoto) mara baaya ya kulipia mafuta kwa kutumia LIPA kwa M-Pesa muda mfupi baada ya kuzinduliwa rasmi kwa huduma hiyo ikiwa ni ushirikiano baina ya huduma ya M-Pesa ya Vodacom na TotalEnergies kuwawezesha wateja wa TotalEnergies kufanya malipo kwa masaa 24, siku 7 za wiki kwenye vituo vyote vya kutolea huduma na maduka yote ya Bonjour nchini kote. Pia, wateja watarudishiwa 10% ya pesa watakapolipia kwa kutumia M-Pesa kwa siku 15 zijazo na kila Jumamosi kwa miezi mitatu ijayo.


Dar es Salaam - Juni 21, 2023: Kupitia dhamira ya kuendeleza mfumo wa maisha wa kutotumia pesa taslimu nchini, huduma ya M-Pesa ya Vodacom na TotalEnergies Marketing Tanzania Limited wamezindua ushirikiano wa kimkakati ili kuwawezesha wateja kufanya malipo bila ya kutumia pesa taslimu kwa usalama na urahisi katika vituo vyote vya kutolea huduma vya TotalEnergies.

Kupitia ushirikiano huu mpya, wateja watafurahia faida tofauti ikiwemo kurudishiwa 10% ya pesa watakapolipia kwa kutumia M-Pesa kwa siku 15 zijazo. Ofa hii itaendelea mbele zaidi kwa kila Jumamosi kwa miezi mitatu ijayo. Zaidi ya hapo, kupitia ushirikiano huu, pia wateja watapata huduma ya M-Pesa kwa shughuli za kibiashara ikiwamo kuweka, kutoa, na kutuma pesa wakiwa katika katika vituo vya kutolea huduma vya TotalEnergies.

Ushirikiano wa TotalEnergies na huduma ya M-Pesa ya Vodacom umekuja katika muda muafaka, sio kuwapa Watanzania njia rahisi na ya uhakika ya kutumia pesa bali pia kuunga mkono jitihada za kidigitali za serikali hususani kuchochea mabadiliko kuelekea kwenye uchumi wa kidigitali ambapo bado matumizi ya pesa taslimu yanaendelea kutumika na kukubalika maeneo mengi nchini kote.

Wednesday 21 June 2023

AIRTEL KICKS OFF 5G ROLL OUT IN 3 COUNTRIES


Lagos, June 20, 2023: Airtel Africa, a leading provider of telecommunications and mobile money services with a presence in 14 countries across Africa, today in Nigeria began rolling out 5G network to deliver an enhanced experience to its customers.

The 5G network will initially go live in three countries starting in Nigeria and followed by Tanzania and Zambia, with plans underway to rollout in the rest of the markets.

With 5G, customers can now enjoy immersive real-time gaming, streaming live content among other uses on the ultra-fast, ultra-reliable network for home internet. The greater and seamless connectivity will also power businesses, particularly those that run on web-based applications as well as facilitate virtual meetings.

USIKOSE TAMTHILIA YA JUA KALI JUMATANO HADI IJUMAA NDANI YA MAISHA MAGIC BONGO



Maria na Frank ❤️ linazidi kutaradadi, Eva anamwambia Suzy mjini hapafai je Suzy atakubali kubaki kijijini?

Usikose Tamthilia ya Jua Kali Jumatano hadi Ijumaa ndani ya Maisha Magic Bongo, 160 saa 3:30 usiku... Umelipia?

Piga *150*53# kulipia kifurushi cha BombaTShs 23,000 tu ufurahie tamthilia hii @dstvtanzania pekee.

#TvniDStv
#Unakosaje

PROF. SYLVIA TEMU APPOINTED AS BOARD CHAIRPERSON FOR THE BOARD OF TRUSTEES OF PASS TRUST

BENKI YA STANDARD CHARTERED KUKAMILISHA HATUA ZA FEDHA ZA MRADI WA SGR

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiagana na mgeni wake ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal, baada ya mkutano kati yao, jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akielezea umuhimu wa Reli ya Kisasa wakati wa mkutano kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal (hayupo pichani), jijini Dodoma.

Ujumbe kutoka Benki ya Standard Chartered ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal Benki ya Standard Chartered (kulia) ukifuatilia maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani) kuhusu upatikanaji wa fedha za kujenga vipande vya reli ambavyo havijakamilika.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal Benki ya Standard Chartered, akieleza kufikiwa kwa hatua za mwisho za upatikanaji wa fedha za ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa kiwango cha Kimataifa (SGR), alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), jijini Dodoma.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa tano kushoto) na ujumbe wa Benki ya Standard Chartered ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal, ukiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano kati yao uliofanyika jijini Dodoma.

Na Peter Haule, WFM, Dodoma

Benki ya Standard Chartered ipo katika hatua za mwisho za utaratibu wa kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa vipande vilivyobakia vya reli ya kisasa kwa Kiwango cha Kimataifa (SGR) ikiwa ni pamoja na kipande cha Makutopora-Tabora, Tabora-Isaka, Isaka-Mwanza na kipande cha kuanzia Tabora hadi Kigoma.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered anayesimamia nchi za Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. Sunil Kaushal.

Dkt. Nchemba alisema kuwa Tanzania na Benki ya Standard Chartered, imekuwa na ushirikiano mzuri katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ya reli ambayo inaendelea vizuri.

“Tumekuwa na majadiliano kuhusu vipande vya reli ambavyo taratibu za kupata fedha zilikuwa hazijakamilika kikiwemo kipande cha Makotopora-Tabora, Tabora-Isaka, Isaka-Mwanza na kipande cha kuanzia Tabora hadi Kigoma”, alisema Dkt. Nchemba

Tuesday 20 June 2023

VODACOM YAZINDUA MNARA WA MAWASILIANO MAKUNDUCHI, ZANZIBAR

Mkurugenzi wa Wakala wa Mkongo Zanzibar (ZICTIA), Bw. Shukuru Awadh Suleiman (katikati) pamoja na Mkuu wa Mauzo wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania PLC Bi. Brigita Shirima (wa pili kulia) wakikata utepe wakati wa uzinduzi wa mnara wa mawasiliano wa Vodacom Tanzania katika mji wa Makunduchi, uliopo ndani ya Mkoa wa Kusini Unguja. Pamoja nao wakati wa uzinduzi ambao ni sehemu ya jitihada za kampuni hiyo kuunga mkono azma ya serikali ya kupanua na kuimarisha huduma za mawasiliano nchini kote, kutoka kushoto ni Meneja Mauzo Mwandamizi Liston Chale, Katibu Tawala Wilaya ya Kusini - Unguja, Baraka Omary Kaengeo na kulia ni Meneja Mauzo Fadhili Linga.

Zanzibar - June 15, 2023 - Katika kuunga mkono azma ya serikali ya kupanua na kuimarisha huduma za mawasiliano nchini kote, kampuni ya teknolojia na mawasiliano ya Vodacom Tanzania imezindua mnara wa mawasiliano katika mji wa Makunduchi, uliopo ndani ya Mkoa wa Kusini Unguja.


Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mnara huo mgeni rasmi Bw. Shukuru Awadh Suleiman Mkurugenzi wa Wakala wa Mkonga Zanizibar (ZICTIA) aliipongeza Vodacom kwa kuiunga mkono serikali katika kufikisha huduma za mawasiliano na intaneti kila kona ya nchi hususan vijijini ambapo wananchi wengi bado hawajafikiwa.


“Nimefurahi kuwa uzinduzi wa leo unafanyika wakati si muda mrefu umepita tangu utiaji saini wa mradi wa Tanzania ya Kidijitali ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan jijini Dodoma. Katika hotuba yake, Mh. Rais aliwataka watoa huduma za mawasiliano kuyapa kipaumbele maeneo ya vijijini, akisisitiza kuwa maeneo hayo yana watu wengi hali kadhalika yamesahaulika kwa muda mrefu. Aidha alibainisha kuwa kuboreshwa kwa mawasiliano kutachochea sekta mbalimbali za kiuchumi zikiwemo afya na kilimo ambazo ni msingi kwa maendeleo ya nchi yetu.” alinukuliwa Bw.Suleiman.

BANK OF TANZANIA NOTICE TO THE PUBLIC - DEALING IN FOREIGN CURRENCY WITHIN THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Monday 19 June 2023

JIUNGE NA UENDELEE KUBURUDIKA NA DStv



Mapinduzi makubwa katika tasnia…

Kaa tayari kwa tamthilia nzuri yenye kusisimua ya Wimbi itajayoanza tarehe 03 Julai kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo 160 ndani ya DStv pekee!

Lipia mapema kifurushi cha Bomba TShs 23,000/= tu ili usikose burudani hii.

@dstvtanzania
#TVNiDStv
#Unakakosaje

SERENGETI BREWERIES RECEIVES AN AWARD FOR CLEAN WATER PROJECTS


Bankrolling water projects with the sole purpose of bringing about relief to water stressed areas in the country, has been one of SBL’s key targets as part of the brewer’s corporate social responsibility initiatives for the past 13 years. To date, SBL has funded implementation of a total of 24 water projects in various parts of the country, something that has ultimately provided free, clean and safe water to more than 2,000,000 Tanzanians.

SBL’s commitment in funding water projects is in line with the brewer’s ‘Water of Life’ pillar whereas SBL has set itself a goal of enabling the provision of free, clean and safe water in water stressed areas. Recognising the significance of establishing strategic partnerships in project implementation, SBL has been partnering with Water Aid Tanzania, an NGO that specializes in provision of clean water, decent sanitation and good hygiene.

SBL’s commitment and immense investments in the sector is what attributed the brewer to scoop an award of recognition from the government and Water Aid Tanzania as the best private sector organisation that leads the way in initiatives for WASH for sustainable return to the community. Prime Minister, Kassim Majaliwa, who was representing President Dr. Samia Suluhu Hassan, handed over the award to SBL which was represented by SBL Communications and Sustainability Manager, Rispa Hatibu. The occasion took place on June 13th in Dar es Salaam.

VODACOM NA SILABU WASHIRIKIANA KUWEZESHA MASOMO MTANDAONI

Kamishna wa Elimu - Wizara ya Elimu, Sayansi, na Teknolojia, Dr. Lyabwene Mutahaba (kushoto) akipata maelekezo kutoka kwa Mwanzilishi Mwenza wa SILABU, Adam Duma (kulia) namna applikesheni ya SILABU inavyofanya kazi ambapo alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wake kuwawezesha wanafunzi na watanzania kujifunza mtandaoni. Akifuatilia katikati ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom Tanzania, Bi. Harriett Lwakatare. SILABU ni matokeo ya programu ya ‘Vodacom Digital Accelerator’, ambayo huzisaidia kampuni changa za kibunifu za kiteknolojia kutatua changamoto za kijamii.

Kamishna wa Elimu - Wizara ya Elimu, Sayansi, na Teknolojia, Dr. Lyabwene Mutahaba (kushoto) akipata maelekezo kutoka kwa Mwanzilishi Mwenza wa SILABU, Adam Duma (kulia) namna applikesheni ya SILABU inavyofanya kazi ambapo alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wake kuwawezesha wanafunzi na watanzania kujifunza mtandaoni. Wakifuatilia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom Tanzania, Bi. Harriett Lwakatare na Mkurugenzi wa Huduma za Kidigitali, Bw. Nguvu Kamando kutoka Vodacom Tanzania. SILABU ni matokeo ya programu ya ‘Vodacom Digital Accelerator’, ambayo huzisaidia kampuni changa za kibunifu za kiteknolojia kutatua changamoto za kijamii.

Katika jitihada za kujenga jamii ya kidigitali inayounganisha sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa ubunifu wa kiteknolojia, Vodacom Tanzania PLC kwa kushirikiana na SILABU wamezindua huduma itakayowarahisishia Watanzania kujifunza masomo na taaluma mbalimbali kwa ngazi tofauti nchini kwa njia ya mtandao muda na mahali popote walipo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika ofisi za Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH), Kamishna wa Elimu - Wizara ya Elimu, Sayansi, na Teknolojia, Dr. Lyabwene Mutahaba amepongeza jitihada za Vodacom na SILABU kwa ubunifu wa huduma ya kujifunza mtandaoni inayoendana na mahitaji ya soko la elimu nchini na duniani kote kwa sasa.

“Elimu ya sasa haitulazimishi kuwepo moja kwa moja darasani ili tuweze kujifunza. Uwepo wa nyenzo za kidigitali unarahisishia wanafunzi na watu wa taaluma mbali mbali kujisomea na kujifunza kwa njia ya mtandao. Ongezeko la vifaa vya kidijiti kama simu janja, kompyuta na vishkwambi pamoja na miundominu ya intaneti vinaendelea kuwa chachu ya mapinduzi ya kidijitali katika sekta ya elimu. Niipongeze Vodacom kwa hatua hii kwani nimefahamishwa kuwa SILABU ni matokeo ya programu ya ‘Vodacom Digital Accelerator’, ambayo huzisaidia kampuni changa za kibunifu zinazotumia teknolojia kutatua changamoto zinazoikumba jamii yetu ya Watanzania,” alisema Dr. Mutahaba.

VODACOM YAZINDUA DUKA JIPYA LA HUDUMA KWA WATEJA SONGWE

Mkuu wa Wilaya ya Songwe Mkoani Songwe, Mh. Solomon Itunda (katikati) akifanya muamala mara baada ya kufanya ufunguzi wa duka la huduma kwa wateja la Vodacom Tanzania PLC lililopo katika Mji wa Mkwajuni mwishoni mwa wiki. Kulia kwake ni Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Happines Shuma na Msimamizi wa maduka Nyanda za Juu Kusini, Dorice Mwambagi, kutoka Vodacom Tanzania PLC.

Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Mh. Solomon Itunda (katikati) akikata keki kuashiria ufunguzi wa duka la huduma kwa wateja la Vodacom Tanzania PLC lililopo katika Mji wa Mkwajuni Wilaya Songwe mwishoni mwa wiki. Pamoja naye kushoto ni Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Happines Shuma wa Vodacom Tanzania PLC.


Mkuu wa Wilaya ya Songwe Mkoani Songwe, Mh. Solomon Itunda (pili kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa duka la huduma kwa wateja la Vodacom Tanzania PLC lililopo katika Mji wa Mkwajuni Wilayani Songwe mwishoni mwa wiki. Pamoja naye (kushoto) ni Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Happines Shuma wa Vodacom Tanzania PLC.

Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa Vodacom Tanzania PLC, Happines Shuma akizungumza wakati ya ufunguzi wa duka la huduma kwa wateja katika Mji wa Mkwajuni Wilayani Songwe Mkoani Songwe.

Baadhi ya wateja wakipewa huduma katika duka jipya la huduma kwa wateja la Vodacom Tanzania PLC lililo zinduliwa katika Mjia wa Mkwajuni Wilayani Songwe Mkoani Songwe mwishoni mwa wiki.

BENKI YA DCB YAZIDI KUJIIMARISHA KIMTAJI NA KUENDELEA KUPATA FAIDA

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga (wa tatu kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe wa bodi ya benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo 2023 jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mwanasheria wa benki hiyo, Alex Mgongolwa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Isidori Msaki na wajumbe wengine; Dk. Amina Baamary, Cliff Maregeli na David Shambwe.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga akifungua Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Isidori Msaki akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Amina Baamary (kulia) akizungumza na baadhi ya wanahisa na wajumbe wengine wa bodi hiyo, baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya wanahisa wa Benki ya DCB wakihudhuria Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam.

Benki ya Biashara ya DCB imeendelea kujivunia kuongezeka kwa mtaji wake huku ikijiendesha kwa faida inayoongezeka kila mwaka licha ya changamoto kadhaa za kiuchumi, wanahisa wa benki hiyo wameelezwa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa DCB, 
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga alisema benki yao ipo imara kimtaji unaofikia kiasi cha Shs 28.5 bilioni unaovuka vigezo vya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) vya Shs 15 bilioni vilivyowekwa kwa benki za biashara.

“Benki yetu ilipata faida baada ya kodi ya Shs 747 milioni kwa mwaka 2022, faida iliyochangiwa na mapato yasiyotoka na riba ya Shs 10.3 bilioni ambayo ni mafanikio ya asilimia 111 ya malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2022, huku mapato yatokanayo na riba yakifika Shs 28.6 bilioni ikiwa ni asilimia 86 ya malengo tuliyojiwekea".

NMB YATENGA BILIONI 2.5 KWA AJILI YA UJENZI WA SHULE



Benki ya NMB yaacha Alama!

Kama ishara na kumbukumbu ya kuadhimisha miaka 25 ya mafanikio, NMB imetoa TShs. bilioni 2.5 kwa ajili ya kujenga Shule ya mfano katika eneo na Mkoa atakayoelekeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Dkt. Samia Suluhu Hassan. NMB inaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuinua sekta ya Elimu nchini.

#Miaka25YaNMB
#NMBKaribuYako

NMB YATOA GAWIO LA BILIONI 45.5, RAIS SAMIA APONGEZA

Rais Samia Suluhu Hassan akipokea Gawio la Serikali la TShs. Bilioni 45.5 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Dk. Edwin Mhede (wa pili kulia) na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna (wa pili kushoto) wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 25 ya mafanikio ya benki hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Katikati ni Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba na kushoto ni Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu.

Benki ya NMB imeandika historia!

Benki ya NMB imetoa gawio la TShs. Bilioni 45.5, ikiwa ni gawio kubwa zaidi kuwahi kutolewa na Taasisi ya kifedha kwa Serikali. Gawio hili kwa serikali ni kiashiria tosha cha Azma yetu ya kuhakikisha tunaleta tija na faida kubwa kwa wawekezaji wetu wote, ikiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NMB - Dkt. Edwin Mhede pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu - Ruth Zaipuna, wamemkabidhi Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Dkt. Samia Suluhu Hassan mfano wa hundi ya gawio hilo katika sherehe ya maadhimisho ya mikaa 25 ya mafanikio ya Benki ya NMB katika ukumbi wa Mlimani City – Dar es Salaam. Wakishuhudia ni Waziri wa Fedha na Mipango - Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba, Msajili Wa Hazina - Nehemiah Mchechu, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania - Emmanuel Tutuba pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

UBONGO LAUNCHES NEW SHOW "NUZO AND NAMIA" TO PROMOTE INCLUSIVE LEARNING AND CELEBRATE DIVERSE AFRICAN CULTURES


Dar es Salaam, 19th June 2023 - Ubongo, Africa's leading edutainment organization, is proud to announce the highly anticipated launch of its groundbreaking new show, Nuzo and Namia. This one-of-a-kind program aims to encourage learning through play, promote inclusivity, and raise awareness about neurodiversity across the continent.


Neurodiversity recognizes that individuals perceive and engage with the world in diverse ways, acknowledging that there is no singular "correct" way of thinking, learning, or behaving. It celebrates differences rather than viewing them as shortcomings or deficits. In African households, neurodivergent children often face challenges, including parental concerns, being labeled as slow learners, and even exclusion from schools. Ubongo firmly believes that every child has a unique way of learning and that no child should be left behind in education. With this vision in mind, Ubongo embarked on a journey to create a new show that focuses on the diverse ways in which children can learn while emphasizing the universal language of play.


“We have partnered with The LEGO Foundation, a global leader in children's play and learning, to develop a groundbreaking early learning program specifically designed for, and with, African children aged 6 to 9 that celebrates different ways of thinking and learning. This partnership has provided us with invaluable insights and expertise that have directly shaped our approach to curricula, pedagogy, content creation, and product design across all of our programs,” said Iman Lipumba, Ubongo’s Director of Communications and Development.


Through this transformative collaboration, Ubongo is committed to equipping every African child with the necessary support to thrive. Ubongo’s organizational goal is to become the leading inclusive, play-based edutainment producer in Africa, improving engagement, learning experiences, and outcomes for all audiences, including neurodivergent children. Additionally, Ubongo aims to increase awareness of Autism, ADHD, and the benefits of Learning Through Play among millions of African families.

Friday 16 June 2023

TANZANIA VS NIGER #AFCON2023 JUMAPILI HII NDANI YA DStv!!!


Tanzania ndani ya michuano ya kufuzu #AFCON2023 na mechi ya kwanza watacheza dhidi ya Niger katika viwanja vya nyumbani.

@dstvtanzania wanakupa kutazama mtanange huu LIVE kupitia chaneli ya SuperSport 225 ndani ya kifurushi cha Poa TShs 10,000/= tu.

Piga *150*53# kulipia kwa urahisi zaidi ili usikose burudani hii.

#TVNiDStv
#Unakosaje