Kupungua kwa zaidi ya asilimia 90 kwa muda wa upakuaji wa shehena kunadhihirisha mabadiliko ya kiutendaji yaliyofanyika ndani ya miaka miwili ya mageuzi ya uendeshaji
DAR ES SALAAM, TANZANIA – 7 July 2026: Bandari ya Dar es Salaam imeshuhudia mapinduzi makubwa kiutendaji baada ya kampuni ya DP World kuweka rekodi mpya ya kasi ya kuhudumia meli na kupunguza muda wa kushusha mizigo kwa zaidi ya asilimia 90. Mafanikio haya ni hatua kubwa katika mageuzi ya bandari hiyo tangu kampuni hiyo ianze uendeshaji wake rasmi mnamo Aprili 2024.
Chini ya mkataba wa uendeshaji wa miaka 30, kampuni ya DP World inaendelea kuwekeza katika ukarabati na upanuzi wa bandari hiyo ili kuunga mkono malengo ya muda mrefu ya nchi kiuchumi na kibiashara.
Kupitia uhamishaji wa mifumo ya kisasa ya uendeshaji wa meli za mizigo ya magari (RoRo) unaowezesha bandari kuhudumia meli kubwa na zenye mahitaji ya hali ya juu kwa usalama zaidi, huku ikipunguza gharama za mnyororo wa ugavi, huku ikiongeza ushindani wa kibiashara na kuchochea ukuaji wa uchumi.
Mageuzi haya yameleta mapinduzi makubwa kwa kupunguza muda wa kushusha mizigo ya aina hiyo kwa zaidi ya asilimia 90—kutoka zaidi ya saa 300 hadi chini ya saa 28. Hatua hii imeweka kiwango kipya kabisa cha ufanisi katika bandari hiyo.
Meli hiyo yenye urefu wa mita 240, ndiyo meli ndefu zaidi kuwahi kutia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam, ikiwa na uwezo wa kubeba hadi magari 7,790. Ilitumia muda wa saa 27 tu kukamilisha zoezi la kushusha shehena ya magari 779, ambayo mengi yake yalikuwa ni magari makubwa na mitambo mizito.
Akizungumzia hatua hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa DP World nchini Tanzania, Martin Jacob, alisema: “Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, tumefanya mapinduzi makubwa katika mfumo wa usafirishaji wa shehena kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Kasi kubwa ya kuhudumia meli, kuongezeka kwa uwezo wa bandari, na uwezo wa kupokea meli kubwa zaidi zenye mizigo mchanganyiko, kunazidi kuimarisha nafasi ya Tanzania kama lango kuu la biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku kukileta tija kwa wateja, wafanyabiashara na uchumi kwa ujumla.”
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)




.jpeg)












