Ushirikiano huu muhimu unaoungwa mkono na Benki ya Dunia unawanufaisha moja kwa moja wateja wa Access Bank Tanzania pamoja na jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania.
Dar es Salaam Jumanne 2 Juni 2026 Access Bank Group, ambayo ni mmiliki wa benki ya Access Bank Tanzania, imesaini makubaliano ya dola milioni 500 na Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC), ambayo ni tawi ya sekta binafsi yaKundi la Benki ya Dunia. Ushirikiano huo unalenga kuimarisha masoko ya mitaji ya sarafu za ndani na kupanua upatikanaji wa bei nafuu kwa biashara kote barani Afrika, na inaleta manufaa ya moja kwa moja kwa masoko ambayo Access Bank inafanya kazi, ikiwa ni pamoja na Tanzania.
Kwa biashara nchini Tanzania, makubaliano haya yanalenga kutatua changamoto za ubadilishaji wa fedha za kigeni. Kampuni zinapolazimika kukopa kwa sarafu za kigeni, mabadiliko ya viwango vya kubadilishia fedha yanaweza kupunguza faida, kuvuruga mipango ya kifedha, na hatimaye kukandamiza uwekezaji. Kupitia suluhisho hili la upatikanaji wa mikopo ya sarafu ya ndani—kiwango ambacho kinawezekana kwa upekee wa ushirikiano kati ya Access Bank na IFC—wateja wa Access Bank Tanzania, kuanzia wajasiriamali wadogo (SMEs) hadi makampuni makubwa, sasa wataweza kupata mikopo yenye gharama nafuu na inayotabirika ili kusaidia ukuaji wao wa muda mrefu.
“Makubaliano haya na IFC ni hatua muhimu kwetu, lakini manufaa yake makubwa yataonekana hapa nchini Tanzania,” alisema Imani John, Mkurugenzi Mtendaji wa Access Bank Tanzania.
“Wateja wetu, iwe wanaendesha biashara ndogo au wanasimamia shughuli za makampuni makubwa, wanahitaji huduma za kifedha ambazo hazitawaweka katika changamoto ya mabadiliko ya thamani ya sarafu. Ushirikiano huu unaimarisha uwezo wetu wa kutoa huduma hizo, huku tukiungwa mkono na uaminifu pamoja na ushawishi wa Kundi la Benki ya Dunia.”




.jpeg)









%20(1).jpg)





.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)



