Dar es Salaam, Juni 6, 2024 – Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua kampeni maalum inayofahamika kama “Tunakuona Mbali”, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kuwawezesha Watanzania kutoka makundi mbalimbali ya kijamii kufikia malengo yao ya maendeleo kupitia huduma rasmi za kifedha.
Kampeni hiyo inalenga kuhamasisha utamaduni wa kuweka akiba, kuwekeza, kutumia huduma za kifedha kwa usahihi na kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu fursa zinazotolewa na benki katika kuboresha maisha yao. Kupitia kampeni hiyo, NBC inalenga kuwafikia wafanyakazi, wakulima, watoto, vijana, wanafunzi, wanawake, wastaafu, vikundi vya kijamii, taasisi za dini, Watanzania wanaoishi nje ya nchi pamoja na wafanyabiashara wadogo, wakati, na wakubwa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam mapema leo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa NBC, Bw. David Raymond, alisema kampeni hiyo imejengwa juu ya falsafa ya kutambua na kuunga mkono ndoto na juhudi za Watanzania katika hatua mbalimbali za maisha yao.
“Tunaposema ‘NBC Tunakuona Mbali’, tunamaanisha kuwa tunakupa zaidi ya huduma za kawaida za benki. Tunatambua kwamba kila Mtanzania ana ndoto na malengo ya kufikia mafanikio katika maisha yake; iwe ni kujenga nyumba, kukuza biashara, kusomesha watoto, kuanzisha uwekezaji au kujijengea usalama wa kifedha kwa sasa na siku zijazo. Ndiyo maana, kama taasisi ya kifedha, tunajiona kuwa mshirika wa safari hiyo ya maendeleo.
Akaunti ya NBC ni zaidi ya mahali pa kuhifadhi fedha; ni suluhisho kamili la kifedha mfano wa ‘wallet’ inayokuwezesha kufanya miamala ya kila siku kwa urahisi,ni mahali pa kuweka akiba, kutuma na kupokea pesa, kupata mikopo, kuwekeza katika masoko ya hisa na mifuko ya uwekezaji, pamoja na kuendesha biashara yako kwa ufanisi zaidi. Kupitia huduma hizi, tunalenga kukupa nyenzo na fursa zinazokusaidia kufikia malengo yako na kutimiza ndoto zako,” alisema.

.jpeg)









%20(1).jpg)





.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)



