Kitomari Banking & Finance Blog
Kitomari Banking & Finance Blog is a premier site for banking, finance, business, economic, investment and stock market news as well as selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the World. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.
Friday, 11 July 2025
MAKAMU WA RAIS DR. MPANGO AIPONGEZA NMB KWA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI
Arusha – Julai 10, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, ameipongeza Benki ya NMB kwa ushirikiano wake wa karibu na Serikali katika kufanikisha matukio mbalimbali ya kijamii na kiuchumi nchini.
Akizungumza jijini Arusha alipotembelea banda la maonyesho la NMB kabla ya kufungua Mkutano wa 14 wa Watunga Sera wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Afrika, unaofanyika katika ukumbi wa AICC, Dkt. Mpango alieleza kufurahishwa kwake na mchango wa benki hiyo kwa taifa.
“Kila ninapoiona NMB ikishiriki katika matukio mbalimbali yanayoandaliwa na Serikali kama mshirika wa karibu, roho yangu inasuuzika kwa sababu najua kazi wanazofanya na uwezo walionao,” alisema Dkt. Mpango.
WITO WA KUWEKEZA ZAIDI VIJIJINI
Makamu wa Rais alitumia fursa hiyo kuitaka NMB kuongeza uwekezaji katika miundombinu ya benki vijijini, ili kuhakikisha Watanzania wanaoishi maeneo ya pembezoni wanapata huduma sawa na wale wa mijini.
“Ni muhimu benki kama NMB kuhakikisha kuwa huduma zake zinafika kila kona ya nchi, ili kila Mtanzania apate haki ya kifedha bila kujali eneo analoishi,” alisisitiza.
NMB YATOA ZAIDI YA BILIONI 6.4 KUISAIDIA JAMII
Akiwasilisha taarifa ya huduma za kijamii, Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa NMB, Baraka Ladislaus, alisema benki hiyo hutenga asilimia moja ya faida yake kila mwaka kwa ajili ya kuisaidia jamii.
“Kwa mwaka huu pekee, tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 6.4 kusaidia sekta ya Afya, Elimu na Mazingira. Lengo letu ni kurejesha faida kwa jamii inayotuzunguka na kushirikiana na serikali kuhudumia wananchi,” alisema Baraka.
NMB YAUNGA MKONO MIFUKO YA JAMII
Baraka aliongeza kuwa NMB inaendesha kampeni maalum ya kuunga mkono kazi za mifuko ya hifadhi ya jamii katika kuimarisha uchumi wa wanachama, kupunguza utegemezi na kuinua maisha ya wazee.
“Tuna bidhaa maalum kama NMB Hekima Plan, inayolenga wastaafu na wale wanaotarajia kustaafu. Kupitia mpango huu, tunatoa elimu ya kifedha ikiwemo uwekezaji na utunzaji wa mafao ili yawasaidie kwa muda mrefu,” alieleza.
NMB YAZINDUA HUDUMA YA KIDIJITALI YA UNUNUZI NA UUZAJI WA HISA KUPITIA NMB MKONONI
Dar es Salaam – Julai 10, 2025
Benki ya NMB kwa kushirikiana na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) wamezindua rasmi ushirikiano wa kimkakati na wa kidijitali wa ununuzi na uuzaji wa hisa za kampuni mbalimbali zilizoorodheshwa DSE, kupitia huduma mpya inayopatikana ndani ya aplikesheni ya NMB Mkononi.
Huduma hiyo mpya, matokeo ya ubunifu wa muda mrefu kati ya NMB na DSE, inahusisha uunganishaji wa mifumo ya kidijitali ya NMB Mkononi na Hisa Kiganjani, hatua inayowezesha wateja wa NMB kununua, kuuza hisa, kupata taarifa za soko na thamani ya uwekezaji wao kwa urahisi zaidi kupitia simu zao.
TEKNOLOJIA YA KISASA KUWEZESHA USHIRIKI WA KIFEDHA
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna, alisema kuwa huduma hiyo ni hatua kubwa katika kujumuisha Watanzania kwenye masoko ya mitaji kwa njia salama, rahisi na ya kisasa.
“Huduma hii ni matokeo ya ubunifu na ushirikiano baina ya wataalamu wa TEHAMA kutoka NMB na DSE. Wateja sasa wataweza kujisajili, kununua na kuuza hisa, kufanya malipo moja kwa moja kupitia akaunti zao za NMB na kupata taarifa za mwenendo wa soko kwa wakati halisi,” alisema Zaipuna.
Aliongeza kuwa huduma hiyo inathibitisha dhamira ya NMB katika kukuza ushirikishwaji wa kifedha kupitia teknolojia, na inatarajiwa kuongeza kasi ya ushiriki wa Watanzania kwenye sekta ya masoko ya mitaji.
SERIKALI YAIPONGEZA NMB NA DSE
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, aliizindua rasmi huduma hiyo na kupongeza mashirika hayo kwa ubunifu unaoenda sambamba na malengo ya Taifa ya kuimarisha huduma kwa wananchi.
“Huduma hii inachangia moja kwa moja katika maeneo manne muhimu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa: kuimarisha upatikanaji wa huduma, kubadili mitazamo ya wananchi, kuelimisha jamii kuhusu uwekezaji na kuchochea ushirikiano miongoni mwa taasisi za ndani,” alisema Prof. Mkumbo.
Alisisitiza kuwa huduma hii ni hatua muhimu ya kuhamasisha utamaduni wa kuwekeza miongoni mwa Watanzania, hasa vijana, na kuongeza uelewa kuwa utajiri unaweza pia kupatikana kupitia umiliki wa hisa.
DSE: HATUA MUHIMU KATIKA KUJENGA KESHO BORA
Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE, Peter Nalitolela, alisema huduma hiyo inapanua wigo wa ushiriki wa wananchi katika masoko ya mitaji, na kwamba DSE inajivunia kuwa sehemu ya mabadiliko haya ya kidijitali.
ACER PURSUES MARKET GROWTH IN EAST AFRICA WITH CUTTING-EDGE TECHNOLOGY & CHANNEL EXPANSION
“Our goal is to empower East Africa’s businesses, schools, and households with technology that drives productivity, creativity, entertainment, and connectivity,” said Grigory Nizovsky, Vice President of Acer Middle East and Africa. “With technology’s constant evolution, we are focused on breaking barriers between people to address a variety of needs. The region’s digital transformation is accelerating, and we are excited to support this growth with dependable commercial and education solutions, which will enhance efficiency and innovation.”
Acer has established itself as a trusted partner in education by providing reliable, easy-to-manage devices and solutions that empower both students and educators. With a broad portfolio of Chromebooks, laptops, and classroom technologies, Acer supports digital learning environments in schools and universities worldwide. The education vertical is a key focus for Acer because it drives long-term growth, fosters digital inclusion, and helps build future-ready communities—aligning with their mission to break barriers through technology – specifically in education.
VODACOM NA STANBIC WAKABIDHI MISAADA YA KIJAMII KATIKA SHULE YA MSINGI MINGA, SINGIDA
Singida – Julai 10, 2025
Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania, Chiha Nchimbi (kulia), pamoja na Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Benki ya Stanbic Tanzania, Geofrey Mwijage (kushoto), wamekabidhi miche 100 ya miti kwa Mkuu wa Divisheni ya Awali na Msingi wa Manispaa ya Singida, Omari Maje, katika Shule ya Msingi Minga, mkoani Singida.
Hafla hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya msafara wa Twende Butiama, unaoendelea nchini na uliozinduliwa rasmi mnamo Julai 3, 2025.
Mbali na miche hiyo ya miti, msafara huo pia umetoa msaada wa magodoro 30, vitanda 5, mashuka 20, madawati 10, pamoja na vitimwendo 6 (wheelchairs) kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum katika shule hiyo.
Kwa pamoja, Vodacom Tanzania na Benki ya Stanbic Tanzania wanadhamini msafara huu, ambao umebeba ujumbe wa kuhimiza uzalendo, mshikamano na kusaidia jamii kupitia shughuli mbalimbali za kijamii na mazingira.
"Tunaamini kuwa kusaidia shule zetu na mazingira ya kujifunzia ni msingi wa kujenga taifa lenye elimu bora na kizazi chenye maadili. Kupitia msafara huu, tutaendelea kutoa msaada na kugusa maisha ya Watanzania wengi zaidi," alisema Chiha Nchimbi wa Vodacom.
Kwa upande wake, Geofrey Mwijage alisisitiza dhamira ya Stanbic katika kuwa mshirika wa maendeleo endelevu kwa Watanzania:
“Tunajivunia kushirikiana na Vodacom katika kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii. Uwekezaji katika elimu na ustawi wa watoto ni sehemu ya mkakati wetu wa kuwainua wananchi kiuchumi na kijamii.”
Msafara wa Twende Butiama utaendelea katika mikoa mbalimbali nchini, ukiambatana na shughuli za kijamii, michezo, na elimu kwa jamii, ikiwa ni kumbukizi ya historia na maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
NMB BANK UNVEILS MOBILE STOCK TRADING PLATFORM TO BOOST ACTIVITY AT DSE
By Staff Reporter – Dar es Salaam
In a strategic move to deepen capital markets participation in Tanzania, NMB Bank Plc has partnered with the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) to launch a groundbreaking mobile trading solution — the ‘Hisa Kiganjani’ mini app, now integrated into the NMB Mkononi App.
Launched yesterday in Dar es Salaam, the innovation aims to democratize access to stock trading, making it easier for both seasoned and first-time investors to buy and sell shares directly from their smartphones. The initiative is expected to stimulate trading activity, enhance market liquidity, and lower the entry barriers historically associated with investing on the DSE.
One-Click Access to DSE
The new platform allows users to access real-time trading data, buy and sell stocks of all DSE-listed companies, and manage their investments securely and efficiently — all within a unified digital ecosystem. This seamless integration not only reduces transaction costs but also eliminates the need for physical visits to stockbrokers.
Speaking during the launch event, NMB Bank CEO Ruth Zaipuna described the new platform as a milestone in the bank’s digital transformation journey, emphasizing its role in boosting financial inclusion and capital market participation.
“This new platform will help facilitate the processes of buying and selling shares. It offers real-time market data and is equipped with robust security features, delivering a seamless and secure trading experience,” she said.
Zaipuna also acknowledged the collaborative efforts of the ICT teams from NMB and DSE, which led to the successful integration of the apps.
“We will continue investing in technology to ensure a smarter, faster, and more user-friendly experience for our customers,” she added. “And we remain committed to promoting financial literacy, including stock market education, to empower more Tanzanians.”
A New Era for Market Participation
Echoing her sentiments, DSE CEO Peter Nalitolela highlighted the app’s potential to transform the trading experience at the bourse.
“This new app will empower users to navigate the DSE market more efficiently while enjoying a personalized trading experience. Now, millions of Tanzanians can buy and sell stocks with a single click,” he said.
He further encouraged citizens — particularly the youth — to embrace investment opportunities in the stock market, noting that large capital is not a prerequisite to start trading.
Government Endorsement and Future Outlook
Minister for Planning and Investment, Prof. Kitila Mkumbo, who officiated the launch as guest of honor, lauded the platform for its promise to enhance efficiency and transparency in the market.
“This will be a catalyst for increased trade at the Dar es Salaam Stock Exchange,” he noted. “However, the key challenge remains changing mindsets so that more Tanzanians adopt stock market trading.”
Thursday, 10 July 2025
NMB NA SAVE THE CHILDREN WAZINDUA PROGRAMU YA SEED KWA AJILI YA UJASIRIAMALI NA AJIRA
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam
Serikali yaipongeza Benki ya NMB na Save the Children kwa kushirikiana katika kuwainua vijana wa Kitanzania kupitia ujuzi na mitaji ya ujasiriamali.
Serikali imepongeza uzinduzi wa Programu ya Ujuzi kwa Maendeleo ya Ujasiriamali na Ajira (SEED), iliyoanzishwa kwa ushirikiano kati ya NMB Foundation na Save the Children Tanzania, kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata maarifa ya kujitegemea kiuchumi kupitia mafunzo ya vitendo na msaada wa mitaji ya kuanzisha biashara.
Programu hiyo, inayotekelezwa kwa mara ya kwanza jijini Dar es Salaam, inalenga vijana 200 kutoka vyuo vya ufundi vya VETA Dar es Salaam, Kipawa ICT Center na Kigamboni Folk Development College.
Serikali Yapongeza Ushirikiano wa Sekta Binafsi
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisema kuwa mpango huo unaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, za kujenga vyuo vya ufundi katika kila wilaya nchini.
“Ninapongeza NMB Foundation na Save the Children kwa kubuni mpango huu ambao utarahisisha kurasimisha ujuzi wa vijana walioko mtaani. Hii ni nguvu tunayohitaji ili kuhakikisha vyuo vinavyojengwa vina tija kwa jamii,” alisema Prof. Mkenda.
Aliongeza kuwa changamoto ya ajira ni kubwa, hivyo kuna haja ya kuwa na ubunifu wa pamoja kati ya Serikali, mashirika na sekta binafsi ili kuwaandaa vijana kwa soko la ajira na kujiajiri.
NMB: SEED Ni Suluhisho la Ajira Kwa Vijana
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB na Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Bi. Ruth Zaipuna, alisema programu ya SEED ni matokeo ya maono ya pamoja kati ya benki yake na wizara, yenye lengo la kuwaandaa vijana kujitegemea kiuchumi.
“SEED ni zaidi ya mafunzo. Tunawapa vijana maarifa ya kuanzisha biashara, kutambua fursa, usimamizi wa fedha na biashara, na vifaa vya kazi badala ya pesa taslimu,” alisema Bi. Zaipuna.
Alifafanua kuwa vijana wa TEHAMA watapewa kompyuta, printer na mashine za kunakili, wakati wale wa useremala watapatiwa vifaa vinavyohusiana na fani yao, huku wale wa ushonaji wakipokea verehani na vifaa vya kushonea.
NMB Foundation Yajibu Wito wa Kitaifa
Mkurugenzi wa NMB Foundation, Bw. Nelson Karumuna, alisema msukumo wa programu hii umetokana na takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya 2022, zilizoonesha kuwa vijana wanawakilisha asilimia 34.5 ya Watanzania, ambapo kati ya kila vijana 10, wanne hawana ajira wala fursa za kiuchumi.
GOVERNMENT APPLAUDS NMB FOUNDATION, SAVE THE CHILDREN FOR YOUTH EMPOWERMENT
By Special Correspondent
The government has praised a new youth empowerment initiative launched jointly by NMB Foundation and Save the Children Tanzania, describing it as a strategic and timely boost to national efforts aimed at reducing unemployment and promoting inclusive economic growth.
Speaking during the official launch of the Skills for Entrepreneurship and Employment Development (SEED) programme in Dar es Salaam yesterday, the Minister of Education, Science and Technology, Prof. Adolf Mkenda, said the initiative aligns with the country’s broader development agenda to equip youth with relevant skills to thrive in an evolving economy.
“With a growing middle class and a national drive to transform local industries for both domestic and export markets, the SEED programme is a timely and strategic intervention,” said Prof. Mkenda. “It reflects our shared commitment across government, civil society, and the private sector to invest in Tanzania’s most valuable asset: its youth.”
He highlighted the programme’s potential to address youth unemployment, especially in urban centres where joblessness remains a pressing concern.
Prof. Mkenda also applauded the collaboration between NMB Foundation—the philanthropic arm of NMB Bank—and Save the Children, calling it a model for effective public-private partnerships in youth empowerment.
According to the minister, the SEED initiative supports several of Tanzania’s long-term development goals, especially those related to quality education, gender equality, and decent employment for young people.
“This programme doesn’t just prepare young people for jobs. It prepares them to shape a more sustainable, inclusive, and prosperous Tanzania,” he added.
Initially, SEED will be piloted in Dar es Salaam, targeting 200 youth aged 18 to 35, with a focus on those from underprivileged backgrounds, including the unemployed and youth in vocational training facing financial hardship.
In her address, NMB Bank CEO Ruth Zaipuna, who also chairs the NMB Foundation Board, said the programme is designed to equip young Tanzanians with practical business tools and vocational skills to enable self-employment and enhance competitiveness in the job market.
Wednesday, 9 July 2025
TANZANIA SET TO LAUNCH VISION 2050: A NEW ERA OF TRANSFORMATION BEGINS
![]() |
Minister of State in the President’s Office (Planning and Investment), Prof. Kitila Mkumbo. |
Dar es Salaam, July 8, 2025 – A bold new chapter is unfolding for Tanzania as President Samia Suluhu Hassan is set to officially launch the Tanzania Development Vision 2050 (TDV 2050) in Dodoma on July 17, 2025. This long-term strategy seeks to elevate the nation into an upper-middle-income economy over the next 25 years.
The launch, to be held at the Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC), follows over two years of intensive, inclusive consultations and surveys involving 13 key stages that shaped this historic, non-partisan national vision — the second of its kind in the country’s history.
“The Tanzania We Want” – A Bold National Ambition
Under the theme “The Tanzania We Want,” the TDV 2050 targets a significant rise in national prosperity. The country aims to increase its per capita income from the current USD 1,157.89 (approx. TZS 3.06 million) to USD 7,000 (approx. TZS 18 million) by the year 2050.
National Unity and Inclusiveness at the Core
Announcing the launch during a briefing with editors and journalists in Dar es Salaam, Minister of State in the President’s Office (Planning and Investment), Prof. Kitila Mkumbo, described the launch as a landmark event for Tanzania’s development agenda.
“This will mark a crucial and historic day for the country,” he said, highlighting that the vision document had passed all formal stages including Cabinet and Parliamentary approval.
STANBIC YAWAZAWADIA WATEJA 28 FEDHA TASLIMU KUPITIA DROO YA SALARY SWITCH
Dar es Salaam, 3 Julai 2025 – Stanbic Bank Tanzania imewazawadia wateja 28 waliobahatika zawadi za fedha taslimu hadi kufikia TZS 500,000 kupitia droo ya pili ya kampeni yake ya Salary Switch. Droo hiyo imefanyika ikiwa ni miezi miwili tangu kuzinduliwa kwa kampeni inayolenga kuhamasisha wafanyakazi nchini kuhamishia mishahara yao kwenye akaunti za Stanbic Bank.
Tukio hilo limefanyika katika makao makuu ya benki jijini Dar es Salaam, likishuhudiwa na Bi. Irene Kawili, mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, pamoja na wanahabari — kama sehemu ya kudhihirisha uwazi na uadilifu wa mchakato huo.
Wateja Waendelea Kupewa Thamani ya Kweli
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Sarah Odunga, Meneja wa Thamani kwa Wateja wa Stanbic Bank, alisema:
“Tunaendelea kuhamasika na mwitikio mkubwa na imani ambayo wateja wetu kote nchini wanaendelea kutuonesha. Droo hii ni sehemu ya ahadi yetu ya kuwapatia thamani ya kweli wale wanaochagua kuhamishia mishahara yao Stanbic. Kwa kufanya hivyo, wanapata si tu huduma za kifedha, bali pia fursa halisi za maendeleo.”
Faida Lukuki kwa Wateja Washiriki
Kampeni ya Salary Switch inawawezesha wateja kupata huduma na faida mbalimbali zikiwemo:
- Mkopo wa mshahara hadi asilimia 60 ya kipato chao
- Bima ya msiba bure kwa mteja na familia yake
- Ushauri binafsi wa kifedha kupitia programu ya Financial Fitness Academy
- Ushiriki wa moja kwa moja kwenye droo za kila mwezi zenye zawadi za pesa taslimu
BENKI YA NMB YATUZWA NA WCF KWA UONGOZI BORA KATIKA MASUALA YA RASILIMALI WATU
Dar es Salaam
Benki ya NMB imeendelea kuthibitisha uongozi wake katika usimamizi bora wa rasilimali watu baada ya kutunukiwa tuzo maalum na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa kuzingatia kikamilifu kanuni pamoja na uwasilishaji wa michango kwa wakati.
Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa maadhimisho ya miaka 10 ya WCF, yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa serikali, waajiri, wadau wa ajira na mifuko ya hifadhi ya jamii kutoka sekta mbalimbali nchini.
Kwa niaba ya Benki ya NMB, Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu, Onesmo Kabeho, alipokea tuzo hiyo.
Waziri Mkuu Majaliwa Apongeza Mafanikio ya WCF
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), aliipongeza menejimenti ya WCF kwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kipindi cha miaka 10. Vilevile, alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma, kwa uongozi wake mahiri tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo.
Tuesday, 8 July 2025
BENKI YA STANBIC YATOA ELIMU YA BIMA KWA WANANCHI WA TANGA
Tanga, Tanzania – 4 Julai 2025
Ili kuhamasisha elimu ya kifedha na kuongeza uelewa wa bima miongoni mwa Watanzania, Stanbic Bank Tanzania kwa kushirikiana na Alliance Life Insurance na Jubilee Allianz Insurance, waliandaa kliniki ya bure ya elimu ya bima mbele ya tawi la benki hiyo jijini Tanga.
Katika kliniki hiyo, wakazi wa Tanga walipata fursa ya kuzungumza ana kwa ana na wataalamu wa sekta ya bima na benki, kuhusu huduma mbalimbali kama bima ya maisha, afya na mali, wakifundishwa namna ya kutumia bima kulinda maisha na rasilimali zao.
“Bima mara nyingi huonekana kama ya watu wachache, lakini ni msingi wa usalama wa maisha ya muda mrefu,” alisema Jumanne Mbepo, Meneja Mwandamizi wa Bima wa Stanbic Bank Tanzania.
Stanbic Bank inaendesha pia vipindi vya mtandaoni vya elimu ya bima, ili kuwafikia wananchi wengi zaidi kote nchini kwa njia rahisi na ya kidijitali.
Wakazi wengi wa Tanga walifurahishwa na tukio hilo. Kennedy Wanga, mmoja wa washiriki, alisema:
“Nilidhani bima ni kwa watu wenye fedha tu. Leo nimeelewa kuwa hata mimi naweza kujilinda na kusaidia familia yangu.”
Tukio hili ni sehemu ya jitihada za Stanbic Bank za kuimarisha ujumuishaji wa kifedha, na kuonesha dhamira yake ya kuchochea maendeleo endelevu kwa kauli mbiu:
“Tanzania ni nyumbani kwetu, tunachochea maendeleo yake.”
NMB YABORESHA HUDUMA ZA KIDIJITALI KWA UJUMUISHAJI MPANA WA KIFEDHA
Dar es Salaam, Julai 7, 2025
Benki ya NMB imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kuwekeza kwenye mifumo ya huduma za kidijitali ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi, kwa lengo la kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kupunguza utegemezi wa matawi ya benki.
Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (DITF), Meneja Mwandamizi wa Mauzo Kidijitali, Hezbon Mpate, alisema kuwa jukwaa la NMB Mkononi limebadilisha kabisa namna Watanzania wanavyopata huduma za kifedha — kwa urahisi, haraka na usalama.
“Kupitia NMB Mkononi, huduma zipo popote ulipo, bila vikwazo vya umbali au muda,” alisema Mpate.
Mpate alibainisha kuwa:
- Zaidi ya wateja milioni 4.7 hutumia NMB Mkononi
- Asilimia 96 ya miamala ya mwaka 2024 ilifanyika kidijitali
- Matumizi ya jukwaa yameongezeka kwa asilimia 16
.jpeg)
Huduma Zinazobadilisha Maisha
Kupitia huduma ya MshikoFasta, wateja wanaweza kupata mikopo hadi Sh milioni 1 bila dhamana, ndani ya dakika 10.
Tangu 2022, zaidi ya mikopo milioni 3 imetolewa kwa karibu wateja milioni 1, wakiwemo mama lishe, wamachinga na watoa huduma wa kati.
Ili kuboresha usalama, NMB imeanzisha alama za vidole kwa kuingia na kufanya miamala, pamoja na kuongeza ukomo wa miamala ya kila siku kutoka Sh milioni 5 hadi Sh milioni 30.
Teknolojia ya Chatbot na Takwimu za Kitaifa
NMB pia imezindua NMB Jirani Chatbot, inayopatikana kwenye WhatsApp, tovuti ya benki na mitandao ya kijamii. Chatbot hiyo huchakata asilimia 78 ya maswali ya wateja papo kwa papo, na imepunguza mzigo wa maulizo kwa asilimia 22.
NMB BANK BOOSTS DIGITAL INVESTMENT TO EXPAND FINANCIAL INCLUSION
Dar es Salaam, July 7, 2025
NMB Bank has reiterated its commitment to digital innovation as a key driver of financial inclusion in Tanzania. Through its mobile platform, NMB Mkononi, the bank is transforming how millions of Tanzanians access financial services — quickly, securely, and without the need to visit a branch.
Speaking during the 49th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF), NMB’s Senior Manager for Digital Sales, Mr. Hezbon Mpate, highlighted that over 4.7 million customers now use the NMB Mkononi app. In 2024 alone, 96% of transactions were processed digitally, reflecting a 16% year-on-year growth.
“Our aim is to eliminate the barriers of time and distance. With NMB Mkononi, we’re ensuring banking services are truly accessible to all,” said Mpate.
Enhancements for Greater Access & Security
To further support customer needs, NMB has:
- Upgraded biometric login with fingerprint authentication.
- Increased daily limits from TZS 5 million to TZS 30 million for higher-value transactions via MshikoFasta.
- Expanded instant micro-loans, allowing users to borrow up to TZS 1 million in under 10 minutes, collateral-free.
Since 2022, MshikoFasta has disbursed over 3 million loans, benefitting nearly 1 million Tanzanians, including food vendors, small traders (wamachinga), and service providers.
Embracing AI for Efficiency
NMB has also launched an AI-powered chatbot, NMB Jirani, available on WhatsApp, the bank’s website, and social media. The bot currently handles 78% of customer queries in real-time and has reduced customer care traffic by 22%.
VIONGOZI WA VODACOM WATEMBELEA BANDA LAO SABASABA NA KUANGALIA TEKNOLOJIA YA KISASA
Dar es Salaam, 7 Julai 2025
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (mwenye tisheti nyeupe), pamoja na Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa Sheria, Agapinus Tax (wa kwanza kushoto), wametembelea banda la Vodacom katika viwanja vya Sabasaba na kupatiwa maelezo kuhusu televisheni janja (smart screen) inayotoa taarifa juu ya bidhaa na huduma mbalimbali za kampuni hiyo.
Tukio hilo limefanyika katika maadhimisho ya Siku ya Sabasaba, wakati wa Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere.
Vodacom inaendelea kutumia maonesho haya kama jukwaa la kuelimisha na kuhamasisha wateja kuhusu suluhisho za kidijitali na bidhaa bunifu zinazoboreshwa kila siku kwa mahitaji ya soko la kisasa.
Sunday, 6 July 2025
VODACOM NA STANBIC WABORESHA SHULE YA MSINGI MKATA KUPITIA MSAFARA WA TWENDE BUTIAMA
Mkata, Handeni Vijijini — 5 Julai 2025
Mkuu wa Kanda ya Kaskazini wa Vodacom Tanzania PLC, George Venanty (pichani kushoto), amemkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mkata kiti cha ulemavu ikiwa ni sehemu ya msaada mkubwa uliotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana na Benki ya Stanbic Tanzania kupitia msafara wa Twende Butiama.
Katika hafla hiyo, shule imenufaika kwa kupokea:
- Matundu ya choo 10,
- Vitanda 20,
- Magodoro 40, na
- Viti maalum 47 vya walemavu.
Msaada huo unalenga kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi, hasa wale wenye mahitaji maalum, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya Vodacom na Stanbic katika kusaidia maendeleo ya elimu na ustawi wa jamii.
Aidha, kama sehemu ya juhudi za kulinda mazingira, msafara huo uliweza kupanda miti 100 katika kata ya Mkata, Wilaya ya Handeni Vijijini, Mkoa wa Tanga.
Msafara wa Twende Butiama, ulioanza rasmi Julai 3, 2025, unaendelea kupitia maeneo mbalimbali ya Tanzania ukiwa na lengo la kuhimiza mshikamano wa kitaifa, utunzaji wa mazingira, na kuchochea maendeleo ya kijamii kupitia miradi ya kijamii na misaada ya kijamii yenye tija.
Saturday, 5 July 2025
NMB FOUNDATION YAWAWEZESHA WAKULIMA WA KOROSHO NEWALA NA RUANGWA
Wakulima kutoka Newala na Ruangwa, mkoani Mtwara, wamehitimu mafunzo ya uongezaji thamani wa zao la korosho yaliyoandaliwa na NMB Foundation kwa ushirikiano na Rabo Foundation na kampuni ya Prosperity Agro Industries Ltd.
Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo, Meneja Mkuu wa NMB Foundation, Nelson Karumuna, alisema kuwa lengo la mafunzo ni kuwajengea wakulima uwezo wa kuongeza thamani ya mazao ili waongeze kipato na kustawi kiuchumi.
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Newala Alhaji Rajabu Kundya, aliipongeza NMB Foundation na wadau wake kwa jitihada hizo na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na serikali katika kuleta mapinduzi ya kilimo.
Wakulima waliokamilisha mafunzo walikabidhiwa vyeti vya ushiriki, ikiwa ni pamoja na Asha Juta, Laurent Muya, Ismail Chibumbui, Rehema Saidi, na Asha Abrahmani.
Meneja Ubanguaji wa Bodi ya Korosho (CBT), Mangile Malegesi, alisisitiza nafasi ya teknolojia na uongezaji thamani katika kukuza soko la korosho ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Prosperity Agro, Haroun Maarifa, aliwahakikishia wakulima ushirikiano endelevu kwenye uzalishaji na usindikaji.
Friday, 4 July 2025
TRA NA SICPA WATUMIA TEKNOLOJIA KULINDA WALAJI NA KUSAIDIA MAENDELEO YA TAIFA
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam
04 Julai 2025
Katika kuendeleza dhamira yake ya kuimarisha uwazi, uwajibikaji, na uchumi jumuishi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa kushirikiana na SICPA Tanzania, inaendelea kuelimisha umma kuhusu nafasi ya teknolojia katika kulinda walaji, kuhakikisha ulipaji sahihi wa kodi, na kulinda uchumi wa Taifa.
Kukabiliana na Bidhaa Bandia kwa Teknolojia ya Kisasa
Katika mazingira ya biashara yanayobadilika kwa kasi, Watanzania wanakabiliwa na changamoto ya bidhaa bandia na biashara haramu ambazo si tu kwamba zinahatarisha afya na usalama wa walaji, bali pia zinapunguza mapato ya serikali yanayotumika kufadhili huduma muhimu za jamii.
TRA, kupitia majukwaa kama Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), inatumia fursa hii kuelimisha wananchi juu ya njia rahisi za kuchangia mapambano dhidi ya bidhaa bandia na kuunga mkono maendeleo ya Taifa.
Wananchi Wanapata Nini?
Katika ushiriki wake kwenye Sabasaba, TRA inawawezesha wananchi kwa kutoa:
- Maarifa kuhusu mfumo wa kisasa wa Stempu za Kodi za Kielektroniki (ETS) – unaosaidia kutambua bidhaa halali kwa urahisi na kuwalinda walaji dhidi ya bidhaa hatarishi.
- Mafunzo ya vitendo ya kutumia programu ya Hakiki Stempu – programu ya simu janja inayowawezesha watumiaji kuthibitisha uhalali wa bidhaa kama vinywaji, vileo na sigara kwa sekunde chache.
- Uelewa wa uhusiano kati ya kodi na maendeleo ya Taifa – ikielezwa wazi kuwa kila bidhaa halali inayonunuliwa huchangia ujenzi wa shule, hospitali, barabara, na huduma nyingine muhimu.