DAR ES SALAAM: Agosti 8, 2026 - Kampuni ya Halotel imeshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane 2026, kwa kuendesha shughuli zake katika mikoa saba ya Tanzania ambayo ni Dodoma, Zanzibar, Arusha, Mwanza, Mbeya, Kagera na Tabora.
Maonesho hayo ya kitaifa yamefanyika kuanzia Agosti 1 hadi 8, 2026, chini ya kaulimbiu “Kutambua Soko, Kuongeza Uzalishaji, Kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”
Kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo, Halotel imeendelea kuonyesha namna teknolojia na huduma za mawasiliano zinavyoweza kusaidia wakulima, wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla katika kuongeza tija na fursa za kiuchumi.
Katika mabanda yake katika maeneo hayo saba, Halotel imeonyesha bidhaa na huduma mbalimbali, zikiwemo router za 5G, huduma ya intaneti ya nyumbani kupitia FTTH, huduma za fedha kwa njia ya simu ya HaloPesa, pamoja na vifurushi vya mawasiliano vyenye gharama nafuu.
Wakulima, wafanyabiashara wa mazao na wananchi wanaotembelea maonesho wamepata fursa ya kuona na kujifunza namna huduma hizo zinavyoweza kuwasaidia kuunganisha nyumba, maduka na ofisi zao kwa huduma za mawasiliano zenye kasi, ubora na uhakika.
TEKNOLOJIA KUUNGANISHA WAKULIMA NA MASOKO
Kwa kuzingatia kaulimbiu ya Nane Nane ya mwaka huu, inayolenga kuwawezesha wakulima kutambua masoko na kuongeza uzalishaji, timu za Halotel katika kila eneo la maonesho zimekuwa zikieleza namna teknolojia inavyoweza kuwa sehemu muhimu ya mnyororo wa thamani wa kilimo.
Kupitia huduma zake, wakulima wanaweza kupata taarifa kuhusu bei za mazao, kufanya malipo kupitia HaloPesa, kuwafikia wanunuzi wa bidhaa zao, pamoja na kupata huduma na taarifa mbalimbali za ugani kupitia mtandao.













.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpg)






.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)