Blog Rebranding Teaser_030826

Blog Rebranding Teaser_030826

Absa Banner_170926

Absa Banner_170926

Stanbic Bank Banner_070826

Stanbic Bank Banner_070826

Sunday, 20 September 2026

‘NMB THE GOAT’ ATAMBA MBIO ZA MBUZI, AMSHINDA MPINZANI WA BOWMANS

DAR ES SALAAM; Septemba 20, 2026 — Mbuzi wa Benki ya NMB, ‘NMB the GOAT’, ameibuka mshindi katika mashindano ya mbio za mbuzi yaliyopewa jina la ‘NMB unGOATable Race’, yaliyofanyika Septemba 19, 2026, akimshinda mbuzi wa Bowmans katika tukio lililolenga kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia elimu ya juu kwa vijana.

Mashindano hayo, maarufu kama Goat Races, yamelenga kuchangisha Sh200 milioni zitakazosaidia vijana 150 wenye changamoto za kifedha kupata fursa ya kuendelea na elimu ya juu.

NMB Bank imeshiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo ikiwa miongoni mwa wadhamini wakuu, huku ushindi wa ‘NMB the GOAT’ ukiongeza mvuto katika ushiriki wa benki hiyo kwenye tukio hilo la kijamii.

Akizungumza baada ya ushindi huo, Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa Wateja Maalumu wa NMB, Getrude Mallya, alisema ushindi huo umefanya ushiriki wa kwanza wa benki katika mashindano hayo kuwa wa kipekee.

Mallya alisema NMB inajivunia kuunga mkono tukio linalounganisha burudani na uchangishaji wa fedha kwa ajili ya kuwasaidia vijana wanaokabiliwa na changamoto za kifedha katika kuendelea na masomo yao.

“Zaidi ya furaha ya ushindi, ushiriki wetu katika mashindano haya unaakisi dhamira ya Benki ya NMB ya kuunga mkono jitihada zinazofungua fursa kwa vijana wa Kitanzania. Mashindano haya yanatuunganisha kwa lengo muhimu la kuchangisha fedha kusaidia elimu,” alisema Mallya.

 

Kwa upande wake, Rais wa Rotary Club ya Dar es Salaam Oysterbay, Paul Muhato, alisema wanafunzi 350 wamewezeshwa kuendelea na masomo tangu klabu hiyo ilipoanza kusimamia rasmi mashindano hayo mwaka 2018.

Saturday, 19 September 2026

PUMA ENERGY TANZANIA REACHES 100 FUEL STATIONS AS EMPLOYEES CELEBRATE THE MILESTONE

Dar es Salaam, 19 September 2026: Employees of Puma Energy Tanzania gathered in Dar es Salaam for a special event to celebrate the company’s milestone of reaching 100 fuel stations and additional service facilities across the country.

The event brought together employees from different departments and locations to celebrate the achievement, recognise their contribution to the company’s growth, strengthen teamwork and discuss the business outlook and growth plans for the period ahead.

The gathering also featured activities aimed at strengthening collaboration, workplace relationships and teamwork among employees.

Reaching 100 fuel stations and additional service facilities provides Puma Energy Tanzania with an expanded network through which it can continue providing its services to customers across different parts of the country.

The milestone comes as Puma Energy Tanzania continues to maintain a significant position in the country’s fuel market. According to the company, the Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) has recognised Puma Energy Tanzania as the leading company by market size in Tanzania’s fuel market for four consecutive years.

Employees Recognised for Their Contribution

Speaking during the event, Puma Energy Tanzania Managing Director, Ms. Fatma M. Abdallah, said reaching 100 fuel stations was an important milestone for the business, but also a reflection of the efforts and collaboration of employees across the company.

“Reaching 100 fuel stations and additional services is an important milestone in the growth of our business, but it is also the result of the work of the people behind this achievement. We have reached this point through the commitment and collaboration of employees across different areas of the company. Today is an opportunity to recognise that contribution, strengthen our relationships and look together at the next step.”

PUMA ENERGY TANZANIA YAFIKISHA VITUO 100 VYA MAFUTA, WAFANYAKAZI WAADHIMISHA HATUA HIYO

Dar es Salaam, 19 Septemba 2026: Wafanyakazi wa Puma Energy Tanzania wamekutana jijini Dar es Salaam katika tukio maalum la kuadhimisha hatua ya kampuni hiyo kufikisha vituo 100 vya mafuta na huduma za ziada nchini.

Tukio hilo liliwakutanisha wafanyakazi kutoka idara na maeneo mbalimbali ya kampuni kwa lengo la kusherehekea mafanikio hayo, kutambua mchango wa wafanyakazi katika ukuaji wa kampuni, kuimarisha ushirikiano pamoja na kujadili mwelekeo na mipango ya biashara katika kipindi kijacho.

Mbali na kusherehekea hatua hiyo, tukio hilo liliambatana na shughuli mbalimbali zilizolenga kuimarisha mshikamano, mahusiano ya kikazi na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi.

Kufikisha vituo 100 vya mafuta na huduma za ziada kunaipa Puma Energy Tanzania nafasi ya kuendelea kupanua upatikanaji wa huduma zake kwa wateja katika maeneo mbalimbali nchini.

Hatua hiyo pia imekuja wakati kampuni hiyo ikiendelea kutambuliwa kwa nafasi yake katika soko la mafuta nchini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeitambua Puma Energy Tanzania kama kampuni inayoongoza kwa ukubwa katika soko la mafuta nchini kwa miaka minne mfululizo.

Wafanyakazi wachangia mafanikio ya vituo 100

Akizungumza katika tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Bi. Fatma M. Abdallah, alisema kufikisha vituo 100 ni hatua muhimu katika ukuaji wa biashara, lakini pia ni matokeo ya juhudi na ushirikiano wa wafanyakazi.

“Kufikisha vituo 100 vya mafuta na huduma za ziada ni hatua muhimu katika ukuaji wa biashara yetu, lakini pia ni matokeo ya kazi ya watu walio nyuma ya mafanikio haya. Tumefikia hapa kutokana na kujituma na ushirikiano wa wafanyakazi katika maeneo mbalimbali ya kampuni. Leo ni fursa ya kutambua mchango huo, kuimarisha mahusiano yetu na kuangalia kwa pamoja hatua inayofuata.”

KCB BANK TANZANIA LAUNCHES ZED 360 DIGITAL SYSTEM TO STREAMLINE SCHOOL FEE COLLECTION

BAGAMOYO, Tanzania – 17 September 2026 – KCB Bank Tanzania has officially launched ZED 360, a digital solution designed to improve school fee collection, payment reconciliation and financial information management for educational institutions across Tanzania.

The ZED 360 platform has been developed to help schools address ongoing challenges in revenue management, including difficulties in payment reconciliation, monitoring collections, maintaining financial records and accessing real-time financial information.

Speaking during the launch ceremony, KCB Bank Tanzania Managing Director, Cosmas Kimario, said the bank continues to put customers at the centre of its services by leveraging technology to provide solutions that simplify day-to-day operations for different customer segments.

“Through ZED 360, schools will have greater visibility in managing their revenues, reduce reliance on manual processes and make decisions using accurate, real-time information. The system has been designed to improve efficiency and strengthen accountability within educational institutions,” said Kimario.

ZED 360 Simplifies School Fee Management

ZED 360 simplifies the entire school fee management process, including invoice generation, fee collection, payment reconciliation and real-time financial reporting.

The system also benefits parents and guardians by enabling them to receive invoices conveniently and make school fee payments securely through multiple channels.

Through ZED 360, parents and guardians can pay school fees through all KCB Bank Tanzania branches, the KCB Mobile App, KCB agents and Mixx by Yas agents across the country.

TOL GASES OPENS TZS 8.17 BILLION RIGHTS ISSUE TO EXPAND PRODUCTION CAPACITY

CPA Daniel Warungu, Managing Director of TOL PLC (fourth left), together with Mr. Leonard Kitoka, Chairman of the Board of Directors of TOL PLC (fifth left), speaking to journalists during a meeting held at the TOL PLC offices in Dar es Salaam regarding the launch of a Rights Issue aimed at raising TZS 8.17 billion from the company’s shareholders. The funds will be used to construct a new Carbon Dioxide (CO₂) gas production facility.

DAR ES SALAAM - September 17, 2026: TOL Gases PLC has officially opened a TZS 8.17 billion Rights Issue to expand its carbon dioxide (CO₂) production capacity, marking the next phase in the growth and transformation of one of Tanzania’s longest-established industrial and medical gases companies.

Under the Rights Issue, TOL Gases is offering 11,501,193 new ordinary shares at TZS 710 per share to eligible existing shareholders.

Eligible shareholders are entitled to one new share for every five ordinary shares held as at the Record Date of Monday, September 14, 2026.

The offer opened on Thursday, September 17, 2026, and will close at 4:00 p.m. on Thursday, October 8, 2026.

The new shares are expected to be listed and commence trading on the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) on Thursday, October 22, 2026, subject to applicable listing requirements.

Capital to expand CO₂ production

The proceeds of the Rights Issue will primarily be used to expand TOL Gases’ carbon dioxide production capacity and related infrastructure.

The investment will cover the design, procurement, installation and commissioning of a new CO₂ production facility, together with supporting logistics and operational requirements.

The capital raise comes as demand for TOL’s products continues to grow beyond the capacity of its existing production facilities, limiting the company’s ability to fully serve domestic requirements and regional opportunities.

Chairperson of the TOL Gases Board of Directors, CPA Leonard Kitoka, said the Rights Issue represents an important transition for the company from business recovery to its next phase of investment and growth.

NMB YATOA SH47.6 MILIONI KUPUNGUZA UHABA WA VIFAA SHULENI KONDOA, CHEMBA MKOANI DODOMA

KONDOA, DODOMA - Septemba 18, 2026: Juhudi za kuboresha mazingira ya kujifunzia na kupunguza uhaba wa vifaa vya shule katika Wilaya za Kondoa na Chemba mkoani Dodoma zimepata msukumo baada ya Benki ya NMB kukabidhi vifaa vyenye thamani ya Sh47.6 milioni kwa shule nane za msingi na sekondari.

Msaada huo unalenga kusaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa vifaa muhimu vya shule na umehusisha madawati, viti, meza, vitanda vya ghorofa pamoja na magodoro.

Akizungumza wakati wa kupokea msaada huo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kwadero, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Fatuma Nyangasa, alisema vifaa hivyo vitasaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuishi kwa wanafunzi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Hassan Mnyika, alisema baadhi ya shule katika wilaya hiyo bado zinakabiliwa na uhaba wa madawati, hali ambayo imekuwa ikiwalazimu baadhi ya wanafunzi kukaa chini wakati wa masomo.

Alisema msaada kutoka NMB utasaidia kupunguza changamoto hiyo na kuwezesha wanafunzi kupata mazingira bora zaidi ya kujifunzia.

Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango, alisema elimu ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayoungwa mkono na benki hiyo kwa kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za kijamii.

Alisema NMB itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika kusaidia kupunguza changamoto za vifaa vya kujifunzia na kuboresha mazingira ya elimu kulingana na mahitaji yaliyopo katika maeneo mbalimbali nchini.

Friday, 18 September 2026

NYOTA BIGI MSIMU WA PILI YARUDI TENA: SERENGETI LITE NA KUNTA AFRICA WATAFUTA NYOTA MPYA MKUBWA NCHINI TANZANIA

DAR ES SALAAM, TANZANIA – 17 Septemba 2026: Je, umewahi kujikuta ukifanya kazi ambayo unajua kabisa siyo kwa ajili yako? Au kujiuliza kama kile unachokifanya kwa kujifurahisha ukiwa nyumbani, njiani au wakati wako wa mapumziko kinaweza kuwa zaidi ya burudani?

Serengeti Lite, kinywaji kutoka Kampuni ya Vinywaji ya Serengeti, kwa kushirikiana na KUNTA Africa, wamezindua rasmi Nyota Bigi Msimu wa Pili, mpango unaolenga kusaka na kukuza nyota mpya wa Tanzania wenye vipaji mbalimbali vya ubunifu.

Katika msimu huu, usaili utafanyika katika mikoa minne ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Dodoma, ambapo safari ya kusaka vipaji itaanza jijini Dar es Salaam tarehe 3 Oktoba 2026, ikifuatiwa na Mwanza tarehe 10 Oktoba, Arusha tarehe 17 Oktoba, na Dodoma tarehe 24 Oktoba 2026.

Nyota Bigi Msimu wa Pili unalenga kuwafikia waimbaji, wacheza muziki, waigizaji, wachekeshaji, wabunifu, wanamitindo pamoja na wenye vipaji vingine vya ubunifu ambavyo bado havijagunduliwa na kupata nafasi ya kuonekana hadharani.

Mpango huo ni sehemu ya kampeni ya Serengeti Lite inayojulikana kama “Lite Your Imagination”, inayolenga kuwahamasisha vijana kuchukulia ubunifu wao kwa uzito, kujieleza na kutambua uwezo wa vipaji vyao katika kujenga maisha na fursa za kiuchumi.

Jukwaa la kugundua vipaji vipya

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Nyota Bigi Msimu wa Pili jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoko na Ubunifu wa Kampuni ya Vinywaji ya Serengeti, Henry Esiaba, alisema jukwaa hilo limeanzishwa kwa kutambua kuwa vipaji vipo kila mahali na kinachohitajika ni fursa ya kuvionyesha.

“Tuna vipaji vingi katika kila kona ya nchi hii. Ila kinachokosekana wakati mwingine ni nafasi ya kuonekana. Nyota Bigi ipo kwa ajili ya kuwapa vijana wa Tanzania jukwaa hilo. Tumerudi kwa msimu wa pili, pamoja na washirika wetu KUNTA Africa, kwa sababu tunataka kugundua vipaji zaidi, kuviweka mbele ya hadhira kubwa na kuvipa msukumo unaostahili, popote vilipo,” alisema Esiaba.

NMB KUONGEZA UFADHILI SEKTA BINAFSI KUHARAKISHA DIRA 2050

NMB Yajipanga Kufungua Zaidi Milango ya Mitaji Kuelekea Dira 2050

ARUSHA - Septemba 17, 2026: Benki ya NMB imejipanga kupanua ufadhili kwa wafanyabiashara na wawekezaji ili kuongeza upatikanaji wa mitaji na kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inategemea kwa kiasi kikubwa sekta binafsi kubeba sehemu kubwa ya uwekezaji unaohitajika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Akizungumza na waandishi wa habari pembezoni mwa Kongamano la Kitaifa la Wanamipango lililofanyika jijini Arusha, Septemba 17, 2026, Mkurugenzi wa Mipango wa NMB, Francis Haraka Mittah, alisema matarajio ya sekta binafsi kuchangia takribani asilimia 70 ya mahitaji ya uwekezaji yanaipa sekta ya fedha jukumu muhimu la kuwezesha upatikanaji wa mitaji.

Alisema jukumu hilo linahusisha kuwawezesha wawekezaji wakubwa pamoja na wafanyabiashara wadogo kupata fedha zinazohitajika kukuza shughuli zao na kuongeza mchango wao katika uchumi.

“Sekta binafsi ikiwa inatarajiwa kuchangia takribani asilimia 70 ya mahitaji ya uwekezaji, basi sekta ya fedha ina jukumu kubwa la kuhakikisha mitaji inapatikana kwa ajili ya uwekezaji huo,” alisema Mittah.

NMB Kupanua Fursa kwa Wafanyabiashara Wadogo

Mittah alisema NMB inaendelea kubuni njia mbalimbali za kuongeza upatikanaji wa fedha kwa wafanyabiashara, ikiwamo kupitia bidhaa zitakazowawezesha wafanyabiashara wadogo wanaokidhi vigezo kupata mitaji kwa masharti yanayoendana na uwezo wao.

Alisema benki pia inaangalia njia nyingine za kutathmini uwezo wa mteja kulipa, hatua inayoweza kusaidia kupanua wigo wa wafanyabiashara wanaoweza kupata huduma za kifedha.

Kwa mujibu wa Mittah, biashara ndogo na za kila siku, zikiwamo shughuli za mama na baba lishe, zina nafasi muhimu katika uchumi kwa kuwa zinachangia uzalishaji wa kipato na ajira.

Thursday, 17 September 2026

NMB TO EXPAND PRIVATE-SECTOR FINANCING TO SUPPORT TANZANIA VISION 2050

ARUSHA - September 17, 2026: NMB Bank has outlined plans to expand financing to businesses and investors as Tanzania turns to the private sector to deliver the bulk of investment required to implement the country’s Development Vision 2050.

The Vision places the private sector at the centre of Tanzania’s economic transformation, with approximately 70 percent of the financing required for its implementation expected to come from private sources as the country pursues its ambition of building a US$1 trillion economy by 2050.

Speaking to journalists on the sidelines of the National Planners’ Conference in Arusha on September 17, 2026, NMB Director of Planning, Francis Haraka Mittah, said the financing structure places banks and other financial institutions at the heart of Vision 2050 implementation.

“Within that 70 percent, the financial sector is directly required to play its part, from large investors to, particularly, small businesses,” Mittah said.

He said NMB was developing financing approaches aimed at increasing access to capital for investments aligned with national development priorities, while also expanding financing opportunities for smaller businesses that generate jobs and household incomes.

Mittah cited small food vendors as an example of enterprises whose individual operations may be modest, but whose collective contribution to employment and income generation makes them an important part of the economy.

He said the bank was also working on products that could enable qualifying small businesses to access financing with lower collateral requirements and through alternative approaches to assessing customers’ ability to repay, subject to the bank’s lending criteria.

The financing push comes as the Government seeks to reposition the private sector as the principal engine of investment under Vision 2050.

TBL NA VODACOM WAJENGA UWEZO WA WAFANYABIASHARA 150 MWANZA KUPITIA MAFUNZO YA GRIT

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji, Vodacom Business, Joseph Sayi, akizungumza na wafanyabiashara wa rejareja wa bidhaa za Tanzania Breweries PLC (TBL) wakati wa semina ya kuwajengea uwezo kupitia Mpango wa Maendeleo ya Wafanyabiashara wa Rejareja (GRIT), iliyofanyika jijini Mwanza. Mafunzo hayo, yaliyowashirikisha wafanyabiashara 150, yalilenga kuwaongezea ujuzi katika usimamizi wa biashara, fedha na matumizi ya suluhisho za kidijitali. Semina hiyo ni sehemu ya ushirikiano wa miaka miwili kati ya TBL na Vodacom Tanzania, unaolenga kuwafikia zaidi ya wafanyabiashara 24,000 nchini.

MWANZA - Septemba 17, 2026: Zaidi ya wafanyabiashara 150 jijini Mwanza wameshiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo katika usimamizi wa biashara, fedha na kuongeza faida, kupitia Mpango wa Maendeleo ya Wafanyabiashara wa Rejareja (GRIT), unaotekelezwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa ushirikiano na Vodacom Tanzania Plc.

Mafunzo hayo yamewakutanisha wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali ya Mwanza, kwa lengo la kuwapatia maarifa na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwasaidia kuboresha uendeshaji wa biashara zao, ikiwemo kupanga matumizi ya fedha, kudhibiti bidhaa, kusimamia gharama na kufanya maamuzi yanayoweza kuchochea ukuaji wa biashara.

Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Michelle Kilpin, alisema GRIT ni sehemu ya juhudi za kampuni kuwawezesha wafanyabiashara wanaofanya kazi nazo kwa kuwapatia maarifa na ujuzi unaoweza kuwasaidia kusimamia biashara zao kwa ufanisi zaidi.

Alisema uwezo wa kusimamia fedha, bidhaa na shughuli za kila siku ni muhimu katika kuiweka biashara katika nafasi nzuri ya kukua na hivyo kuchangia maendeleo ya wafanyabiashara, familia zao na jamii kwa ujumla.

Maarifa ya Usimamizi wa Biashara

Miongoni mwa wakufunzi katika mafunzo hayo alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dkt. Patrokil Kanje, aliyewafundisha washiriki namna ya kuendesha biashara kwa ufanisi, kusimamia gharama na kutambua maeneo yanayoweza kusaidia kuongeza faida.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Dkt. Kanje aliwasisitiza wafanyabiashara kuwa na uelewa wa kina kuhusu biashara zao, hasa katika kufuatilia mauzo, gharama na faida.

Alieleza kuwa mfanyabiashara anapaswa kufahamu si tu kiasi anachouza, bali pia gharama anazotumia na faida anayobaki nayo, kwa kuwa taarifa hizo ni muhimu katika kufanya maamuzi sahihi, kudhibiti matumizi na kupanga ukuaji wa biashara.

VODACOM CHAMPIONS DIGITAL INFRASTRUCTURE & REGIONAL CONNECTIVITY AT ITW & DATACLOUD AFRICA 2026

NAIROBI, KENYA - September 17, 2026: Africa’s next phase of digital transformation will require more than expanding connectivity. Stronger fibre networks, data centres, cloud infrastructure, reliable energy and an enabling investment environment will be essential to support the continent’s rapidly growing digital economy.

This was among the key messages emerging from ITW & Datacloud Africa 2026, held from September 7 to 10 in Nairobi, Kenya. The event brought together stakeholders from across the digital infrastructure and technology ecosystem to discuss connectivity, data centres, cloud computing, artificial intelligence (AI), investment, energy, sustainability and regulation.

Against this backdrop, Vodacom Tanzania used the forum to emphasise that Africa’s digital transformation must move beyond connectivity towards a more integrated digital ecosystem capable of supporting businesses, governments and communities.

Connectivity as the Foundation of Digital Transformation

Nguvu Kamando, Director, Vodacom Business, said Africa must move beyond simply expanding connectivity and focus on leveraging digital infrastructure, AI and enterprise solutions to drive economic growth.

He said connectivity remains the foundation of Africa’s digital transformation, but the greater opportunity lies in what businesses and institutions can build on top of reliable connectivity.

“Connectivity is everything. It is the foundation of the digital transformation we are looking for across Africa. But the real opportunity is what we build on top of it to drive Africa’s digital economy,” Kamando said.

He noted that cloud services, digital platforms, data-driven decision-making and AI-powered systems are increasingly essential for enterprises competing in domestic, regional and global markets.

KCB BANK TANZANIA YAZINDUA ZED 360 KUBORESHA UKUSANYAJI WA ADA SHULENI

BAGAMOYO, Tanzania – 17 Septemba 2026 – KCB Bank Tanzania imezindua rasmi mfumo wa kidijitali wa ZED 360, unaolenga kuboresha ukusanyaji wa ada, upatanisho wa malipo na usimamizi wa taarifa za kifedha katika taasisi za elimu nchini.

Mfumo huo umebuniwa kusaidia shule kukabiliana na changamoto mbalimbali katika usimamizi wa mapato, ikiwemo ugumu wa kufanya upatanisho wa malipo (payment reconciliation), ufuatiliaji wa makusanyo, utunzaji wa kumbukumbu za kifedha na upatikanaji wa taarifa kwa wakati halisi.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa ZED 360, Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Bank Tanzania, Cosmas Kimario, alisema benki hiyo inaendelea kumweka mteja mbele kwa kutumia teknolojia kuleta suluhisho zinazorahisisha shughuli za kila siku kwa makundi mbalimbali ya wateja.

“Kupitia ZED 360, shule zitapata uwazi mkubwa zaidi katika usimamizi wa mapato yao, kupunguza utegemezi wa michakato ya mikono na kufanya maamuzi kwa kutumia taarifa sahihi zinazopatikana kwa wakati halisi. Mfumo huu umeundwa kuboresha ufanisi na kuongeza uwajibikaji katika taasisi za elimu,” alisema Kimario.

ZED 360 Yarahisisha Usimamizi wa Ada

ZED 360 inarahisisha mchakato mzima wa usimamizi wa ada, kuanzia utoaji wa ankara, ukusanyaji wa ada, upatanisho wa malipo hadi utoaji wa taarifa za kifedha kwa wakati halisi.

Mfumo huo pia unalenga kurahisisha maisha ya wazazi na walezi kwa kuwawezesha kupokea ankara za ada kwa urahisi na kufanya malipo kupitia njia mbalimbali za kidijitali na kifedha.

Kupitia ZED 360, wazazi na walezi wanaweza kulipa ada kupitia matawi yote ya KCB Bank Tanzania, KCB Mobile App, mawakala wa KCB pamoja na mawakala wa Mixx by Yas kote nchini.

Teknolojia Katika Mageuzi ya Sekta ya Elimu

Uzinduzi wa ZED 360 ni sehemu ya mkakati wa KCB Bank Tanzania wa kuendelea kuwekeza katika mageuzi ya kidijitali, kwa lengo la kuboresha uzoefu wa wateja, kuongeza ufanisi wa shughuli za taasisi na kuchangia maendeleo ya sekta mbalimbali za uchumi.

Katika sekta ya elimu, suluhisho hilo linatarajiwa kusaidia taasisi kuwa na mifumo yenye uwazi zaidi katika usimamizi wa mapato na taarifa za kifedha, huku ikiwezesha uongozi wa shule kupata taarifa muhimu kwa wakati na kufanya maamuzi yanayozingatia takwimu.

KCB Bank Tanzania pia imewashukuru uongozi wa Shule ya Marian kwa kushiriki katika majaribio ya awali ya mfumo huo, ambayo yalisaidia kutoa mrejesho muhimu katika kuboresha ZED 360 kabla ya uzinduzi wake rasmi.

NBC CALLS FOR WIDER TANZANIAN PARTICIPATION IN CAPITAL MARKETS

NBC Managing Director Theobald Sabi (holding the microphone) speaks during a special webinar organised by the bank in collaboration with key stakeholders in the financial sector. The webinar aimed to encourage Tanzanians to take advantage of opportunities available in the country’s capital and stock markets, particularly through mobile technology.

Seated at the high table from left are Ibrahim Nzutu, Head of Business Advisory, NBC (Webinar Moderator); Peter Nalitolela, Chief Executive Officer, Dar es Salaam Stock Exchange (DSE); Theobald Sabi, Managing Director, NBC; Emmanuel Akaro, Director of Financial Markets, Bank of Tanzania (BoT); and CPA Alfred Mkombo, Director of Research, Policy and Planning, Capital Markets and Securities Authority (CMSA).

DAR ES SALAAM, September 16, 2026 — National Bank of Commerce (NBC) has called for greater participation by Tanzanians in the country’s capital markets, highlighting the growing role of digital financial services in making investment opportunities more accessible to ordinary citizens.

The call was made during a webinar hosted by NBC to provide the public with practical information on how individuals can use banking services and digital platforms to access opportunities in the capital and stock markets.

The webinar, broadcast live from NBC’s headquarters in Dar es Salaam, brought together representatives from key financial sector institutions, including the Bank of Tanzania (BoT), the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) and the Capital Markets and Securities Authority (CMSA).

Banks Can Be Gateways to Investment

Speaking during the webinar, NBC Managing Director Theobald Sabi said financial institutions should increasingly be viewed not only as places to save and borrow money, but also as important gateways to investment opportunities and financial education.

He said technological developments were enabling banks to connect customers more easily with capital market products, allowing people with different levels of income to participate in investment.

“This is why, as a bank, we are investing more in systems that enable our customers to participate in capital market investments. A bank is now more than a place to save and borrow; it is also an important link to financial education and services that provide access to capital and stock markets,” Sabi said.

Sabi cited NBC Kiganjani, which is integrated with DSE Kiganjani, as one of the platforms enabling customers to access investment opportunities digitally.

Investment platforms operated by UTT and iTrust have also been integrated with NBC Kiganjani, while additional services are being considered for integration.

NCBA CHAMPIONS DIGITAL AND CASH-FLOW-BASED FINANCING TO UNLOCK SME GROWTH IN TANZANIA

ZANZIBAR, Tanzania – September 16, 2026 — NCBA Bank Tanzania has called for a shift in how financial institutions approach small and medium-sized enterprise (SME) financing, emphasising the potential of digital technology, transaction data and innovative financing models to make credit more accessible, affordable and responsive to the realities of growing businesses.

The call was made during the Tanzania Bankers Association (TBA) Research and Financial Inclusion Conference 2026, held at Kwanza Resort Hotel in Zanzibar on September 3–4, 2026.

NCBA Bank Tanzania Chief Executive Officer, Alex Mziray, participated in a high-level panel discussion themed “Catalysing SME Growth: The Role of Innovative and Digital Financing Solutions,” alongside leaders from across the financial services ecosystem.

The discussion explored how innovation and digitalisation can address some of the longstanding barriers limiting SMEs' access to finance, with Mziray highlighting how commercial banks can leverage technology, data and alternative financing models to better serve businesses.

Moving beyond traditional collateral

Mziray noted that one of the fundamental challenges in SME financing is not necessarily a lack of appetite among financial institutions, but rather the economics of serving smaller businesses through conventional lending models.

Many SMEs do not have audited financial statements or traditional forms of collateral such as titled property. At the same time, increasingly digitised businesses are generating valuable transaction footprints through mobile money, electronic payments, point-of-sale transactions, invoices, supplier payments and credit bureau records.

According to Mziray, these data points create an opportunity for financial institutions to assess the actual cash flows and behaviour of businesses rather than relying predominantly on physical assets.

“Digital, for me, is not a channel story. It is what makes small-ticket lending commercially viable in the first place,” Mziray said.

 

This transition towards cash-flow-based lending has the potential to broaden access to finance for businesses with viable operations but limited conventional collateral.

Wednesday, 16 September 2026

NBC YAENDESHA SEMINA MTANDAO (WEBINAR) KUHAMASISHA UWEKEZAJI KATIKA MASOKO YA MITAJI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (aliyeshika kipaza sauti), akizungumza wakati wa semina mtandao (webinar) maalum iliyoandaliwa na benki hiyo kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya fedha. Semina hiyo imelenga kuhamasisha Watanzania kuchangamkia fursa zinazopatikana katika masoko ya mitaji na hisa nchini, hususan kupitia teknolojia ya simu za mkononi.

Waliopo meza kuu, kutoka kushoto, ni Ibrahim Nzutu, Mkuu wa Idara ya Ushauri wa Biashara wa NBC (Muendesha Semina); Peter Nalitolela, Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE); Theobald Sabi, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC; Emmanuel Akaro, Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT); na Alfred Mkombo, Mkurugenzi wa Utafiti, Sera na Mipango wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE), Peter Nalitolela (aliyeshika kipaza sauti), akizungumza wakati wa semina mtandao (webinar) maalum iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya fedha. Semina hiyo imelenga kuhamasisha Watanzania kuchangamkia fursa za masoko ya mitaji na hisa nchini, hususan kupitia teknolojia ya simu za mkononi.

Kushoto kwake meza kuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, na Ibrahim Nzutu, Mkuu wa Idara ya Ushauri wa Biashara wa NBC (Muendesha Semina).

DAR ES SALAAM, Septemba 16, 2026 — Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeendesha semina mtandao (webinar) maalum kwa lengo la kuwahamasisha Watanzania kutumia fursa zinazopatikana katika masoko ya mitaji na hisa nchini, hususan kupitia maendeleo ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma hizo kwa kutumia simu za mkononi.

Semina hiyo, iliyorushwa moja kwa moja mtandaoni kutoka makao makuu ya NBC, iliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka taasisi zinazosimamia na kuwezesha masoko ya mitaji, wakiwemo Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

NBC Yasisitiza Benki Kuwa Kituo cha Elimu ya Uwekezaji

Akizungumza katika semina hiyo, iliyojadili pamoja na mambo mengine namna wananchi, hususan wenye kipato cha chini, wanavyoweza kutumia akaunti zao za benki kufikia masoko ya mitaji, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, alisema wakati umefika kwa Watanzania kutumia taasisi za fedha kama vituo vya kupata elimu kuhusu fursa mbalimbali za uwekezaji.

Alisema taasisi za fedha hazipaswi kuonekana kama sehemu za kuweka akiba na kukopa pekee, bali pia kama kiungo muhimu cha kuwawezesha wananchi kupata elimu na huduma za uwekezaji.

“Na hii ndiyo sababu kama benki tunawekeza zaidi kwenye mifumo inayowawezesha wateja wetu kushiriki katika uwekezaji wa masoko ya mitaji. Yaani kwamba sasa benki ni zaidi ya kuweka akiba na kukopa, bali ni kiungo muhimu cha elimu na huduma za kuyafikia masoko ya mitaji na soko la hisa,” alisema Sabi.

Sabi alitolea mfano huduma ya NBC Kiganjani, ambayo imeunganishwa na DSE Kiganjani, huku mifumo ya mifuko ya uwekezaji ya UTT na iTrust nayo ikiwa imeunganishwa na huduma hiyo. Alisema huduma nyingine ziko katika hatua mbalimbali za kuunganishwa.

Alitoa wito kwa Watanzania wenye fedha kutafuta fursa za kuzalisha thamani kupitia uwekezaji badala ya kuzihifadhi bila kuzalisha thamani, akitaja miongoni mwa fursa hizo uwekezaji katika hisa na hati fungani za Serikali.

Tuesday, 15 September 2026

NMB FOUNDATION YAWAHIMIZA WAHITIMU WA VIJIJINI KUOMBA UFADHILI WA NURU YANGU

Dar es Salaam - Septemba 15, 2026: NMB Foundation imewahimiza wahitimu wa Kidato cha Sita mwaka 2026 wenye sifa, hususan wanaotoka vijijini na familia zenye uwezo mdogo, kutumia fursa ya kuomba ufadhili wa masomo kupitia Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Programme kabla ya dirisha la maombi kufungwa Septemba 18, 2026.

Katika awamu hii, NMB Foundation imetenga Shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuwawezesha vijana 50 wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza, waliopata pointi kati ya tatu na tano, na wanaotarajia kujiunga na taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania.

Ufadhili huo unalenga kupunguza changamoto za kifedha zinazoweza kuwazuia vijana wenye vipaji na ufaulu mzuri kuendelea na masomo ya elimu ya juu.

Ufadhili wa Masomo na Maendeleo ya Kitaaluma

Kupitia programu hiyo, wanufaika watapatiwa ufadhili unaojumuisha ada na tozo za chuo, fedha za kujikimu, gharama za mafunzo kwa vitendo pamoja na kompyuta mpakato kwa ajili ya kuwawezesha katika safari yao ya elimu.

Mbali na msaada wa kifedha, programu hiyo pia inajumuisha malezi elekezi na maandalizi ya kuwawezesha vijana kuingia katika soko la ajira baada ya kumaliza masomo yao.

Hatua hii inaifanya Nuru Yangu kuwa zaidi ya mpango wa kugharamia masomo, kwa kuwa inalenga pia kuwaandaa vijana kujenga uwezo, kujiamini na kuwa tayari kwa fursa za ajira na maendeleo ya kitaaluma.

Wito kwa Vijana wa Vijijini

NMB Foundation imewataka wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii kuhakikisha taarifa kuhusu fursa hiyo zinawafikia vijana wenye sifa, hasa wale wanaoishi maeneo ya vijijini ambao huenda wasipate taarifa za fursa kama hizi kwa wakati.

Kwa vijana waliomaliza Kidato cha Sita mwaka 2026 na wanaokidhi vigezo, fursa hii inaweza kuwa hatua muhimu katika kufanikisha ndoto zao za kuendelea na elimu ya juu.

Maombi Yafungwa Septemba 18

Maombi ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Programme yanaendelea kupokelewa kupitia tovuti ya NMB Foundation, foundation.nmbbank.co.tz, hadi Ijumaa, Septemba 18, 2026.

Vijana wenye sifa wanashauriwa kutoweka maombi yao hadi dakika za mwisho na kuhakikisha wanawasilisha taarifa zote zinazohitajika ndani ya muda uliowekwa.

Kwa wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii, kuwafikishia vijana taarifa kuhusu fursa hii kunaweza kuwa mchango muhimu katika kufungua milango ya elimu na maisha bora kwa kizazi kijacho.

BEYOND THE FAIRWAY: NCBA GOLF SERIES DRIVES COMPETITION, OPPORTUNITY AND IMPACT IN ARUSHA

ARUSHA, Tanzania - September 15, 2026: The NCBA Golf Series 2026 continued its journey in Arusha over the weekend, bringing together golfers, customers, business leaders and partners at Kili Golf for a tournament that combined competitive sport with a broader commitment to creating opportunities and supporting communities.

The Arusha leg was held in partnership with the Diplomatic Golf Tournament, an initiative aimed at raising funds to support school fees for students from low-income families, giving the tournament a purpose that extended well beyond the fairway.

The tournament was graced by NCBA Group Managing Director and CEO John Gachora, alongside NCBA Bank Tanzania Managing Director Alex Mziray and other senior leaders and stakeholders, underscoring the Group’s commitment to using sport as a platform for connection, talent development and meaningful community impact.

Beyond supporting the Diplomatic Golf Tournament’s education cause, NCBA will also sponsor the overall winner to participate in the NCBA Golf Series, providing an opportunity for the golfer to advance their journey through the wider Series.

Speaking during the tournament, Mziray said the partnership reflects NCBA’s philosophy of “Banking on Belief – Empowering Ambition”, by creating opportunities that enable people and communities to move forward.

“Golf gives us an opportunity to connect with our customers and partners, but its impact can go much further. Through this partnership, we are supporting education while creating an opportunity for golfing talent to progress. This is what empowering ambitions means to us — recognising potential and taking practical steps to help it move forward,” said Mziray.

The Arusha tournament follows the opening Tanzania leg held at Dar es Salaam Gymkhana and forms part of the wider NCBA Golf Series taking place across markets where NCBA Group operates.

The Tanzania series will culminate in Dar es Salaam, with qualifying golfers progressing to the NCBA Group Grand Finale in Nairobi at the end of November.

Through the Series, NCBA continues to position golf as more than a sporting competition. It is a platform for building relationships, opening opportunities and bringing together customers, partners and communities around shared ambitions.