Blog Rebranding Teaser_030826

Blog Rebranding Teaser_030826

Stanbic Bank Banner_070826

Stanbic Bank Banner_070826

Absa Loan Campaign_160426

Absa Loan Campaign_160426

Tuesday, 8 September 2026

MASHINDANO YA VODACOM CORPORATE MASTERS GOLF YAMALIZIKA KWA MAFANIKIO, YAIMARISHA MAHUSIANO YA KIBIASHARA

Washindi wa Vodacom Corporate Masters Golf Tournament 2026 katika makundi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa zawadi zao katika hafla iliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando (kulia), akikabidhi tiketi ya kwenda na kurudi Mauritius kwa mshindi wa jumla kwa upande wa wanaume, Khalid Shemndolwa (wa tatu kushoto), katika Vodacom Corporate Masters Golf Tournament 2026, iliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam.

Dar es Salaam, Septemba 5, 2026: Vodacom Tanzania PLC, kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited, imehitimisha kwa mafanikio mashindano ya Vodacom Corporate Masters Golf 2026, yaliyofanyika katika Uwanja wa TPDF Lugalo Golf Club jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo yaliwakutanisha takribani wachezaji 150 kutoka Tanzania na nchi jirani, wakiwemo viongozi wa biashara, wakurugenzi, wakuu wa kampuni pamoja na wapenzi wa mchezo wa gofu.

Katika mashindano hayo ya siku moja, Khalid Shemndolwa na Yvonne Ondari waliibuka washindi wa jumla kwa upande wa wanaume na wanawake, mtawalia. Shemndolwa alikusanya pointi 42, huku Ondari naye akifikisha pointi 42.

Katika madaraja mengine, Godfrey Abel alitwaa ubingwa wa Daraja A baada ya kupata pointi 42, akifuatiwa na Likuli Juma aliyemaliza na pointi 41.

Kwa upande wa Daraja B, Sigfrid Urassa aliibuka mshindi kwa pointi 40, akimzidi Godfrey Kilenga, ambaye pia alipata pointi 40, lakini Urassa akashinda kwa kutumia kanuni ya countback.

BENKI YA EXIM YAADHIMISHA MIAKA 29 YA UBORA KWA VITENDO KWA KUSAIDIA JUHUDI ZA USAFI KWA JAMII

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Bw. Stanley Kafu (wa pili kulia), akipeana mikono na Diwani wa Kata ya Kawe, Mheshimiwa Fabian Malima (katikati), baada ya kukabidhi vifaa vya usafi kwa Manispaa ya Kinondoni.

Shughuli hiyo ilifanyika kama sehemu ya kilele cha maadhimisho ya miaka 29 tangu kuanzishwa kwa Benki ya Exim Tanzania. Katika maadhimisho hayo, Benki pia ilishiriki katika zoezi la usafi wa fukwe za bahari katika maeneo ya Kawe.

Tukio hilo lilifanyika tarehe 5 Septemba 2026, jijini Dar es Salaam, na kushuhudiwa na Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Bi. Kauthar D'souza (kulia), Mkuu wa Kituo cha Polisi Kawe, ASP Ally Liviga (kushoto), pamoja na Afisa Usafishaji wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Alban Mugyabuso (wa pili kushoto).

DAR ES SALAAM, TANZANIA - Septemba 5, 2026: Benki ya Exim Tanzania inaadhimisha miaka 29 tangu kuanzishwa kwake chini ya kaulimbiu “Miaka 29 ya Ubora kwa Vitendo,” ikisherehekea karibu miongo mitatu ya ukuaji, uaminifu wa wateja, ushirikiano na mchango wake kwa jamii inazozihudumia.

Mwaka 1997, Benki ya Exim Tanzania ilianza safari yake ikiwa na idadi ndogo ya wateja na, hatua kwa hatua, ikajenga uwepo mkubwa katika soko la Tanzania. Kwa kipindi cha miaka 29, Benki hiyo imekua na kuwa miongoni mwa taasisi za kifedha zinazoongoza nchini, ikitambulika kwa ubunifu, suluhisho zinazomlenga mteja na mchango wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi.

Kwa sasa, Benki ya Exim ina zaidi ya matawi 30 nchini Tanzania, pamoja na uwepo katika masoko ya nje ya Tanzania, ikiwemo Comoro, Djibouti, Uganda na Ethiopia.

Kama sehemu ya safari hiyo, Benki ya Exim ilikuwa benki ya kwanza Tanzania kufungua matawi nje ya nchi, hatua iliyoifanya kuwa miongoni mwa benki chache za Tanzania zilizofanikiwa kupanua shughuli zake katika masoko ya kimataifa.

VODACOM DIGITAL ACCELERATOR NA BRIDGE FOR BILLIONS WAINGIA UBIA KUIMARISHA MFUMO WA UJASIRIAMALI TANZANIA

Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi (kulia), akizungumza wakati wa kutangazwa kwa ushirikiano wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na Bridge for Billions, unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini kwa kuwafikia zaidi ya wajasiriamali na wabunifu 1,000 na kusaidia biashara zaidi ya 40 kukua na kupanuka.

Ushirikiano huo ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3, 2026, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando.
Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, akizungumza wakati wa kutangazwa kwa ushirikiano mpya wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na Bridge for Billions, unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini na kuwawezesha wajasiriamali na wabunifu kukua.

Ushirikiano huo ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3, 2026, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi.

Dar es Salaam, Septemba 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc imeingia katika ubia wa miaka mitatu na Bridge for Billions, mtandao wa kimataifa wa ujasiriamali, kwa lengo la kupanua wigo na kuongeza matokeo ya mpango wa Vodacom Digital Accelerator (VDA) nchini Tanzania.

Kupitia ubia huo, taasisi hizo mbili zinalenga kujenga uwezo wa taasisi zinazosaidia wajasiriamali (Entrepreneurship Support Organizations – ESOs) kote nchini, hatua inayotarajiwa kuwawezesha kuwafikia zaidi ya wajasiriamali 1,000 na kusaidia biashara zaidi ya 40 kukua na kupanuka katika kipindi cha miaka mitatu.

KUWEKEZA KATIKA MFUMO WA UJASIRIAMALI

Ushirikiano huo unaashiria hatua mpya katika utekelezaji wa Vodacom Digital Accelerator, ambapo pamoja na kuendelea kusaidia biashara changa moja kwa moja, mpango huo sasa utawekeza pia katika kuimarisha taasisi na vituo vinavyowasaidia wajasiriamali.

Taasisi zitakazonufaika zitajumuisha vituo vya kulea na kukuza biashara changa, vituo vya ujasiriamali, vyuo vikuu pamoja na mashirika ya maendeleo ya biashara yanayowasaidia waanzilishi wa biashara.

BENKI YA EXIM YAZIDI KUIMARISHA UJASIRIAMALI KWA WANAWAKE KUPITIA WEP 2026

DAR ES SALAAM: Benki ya Exim Tanzania imehitimisha mafunzo ya Women Empowerment Programme (WEP) 2026, yaliyowaleta pamoja wanawake wajasiriamali 50 jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwajengea uwezo na kuwawezesha kuendesha na kukuza biashara zao kwa ufanisi zaidi.

Programu hiyo, inayotekelezwa kupitia mpango wa Benki wa kurejesha kwa jamii, Exim Cares, imelenga kuwapatia wanawake wajasiriamali maarifa na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwasaidia kukabiliana na changamoto za uendeshaji wa biashara na kutumia fursa zilizopo katika soko.

Monday, 7 September 2026

EQUITY BANK POWERS DIGITAL PAYMENTS FOR ZANZIBAR ENTREPRENEURS AT FAHARI YA ZANZIBAR 2026

Bank deepens investment in the Isles as Equity Lipa Namba helps traders receive digital payments and build transaction histories for future growth

ZANZIBAR, SEPTEMBER 5, 2026 – Equity Bank Tanzania is deepening its investment in Zanzibar’s enterprise economy by enabling businesses participating in Fahari ya Zanzibar 2026 to receive digital payments through Equity Lipa Namba.

Convened by the Zanzibar Economic Empowerment Agency (ZEEA), the third edition of the national trade fair is taking place from September 4 to 14, 2026, at Maisara Grounds, under the theme “Bidhaa Zetu Ndio Fahari Yetu” (Our Products Are Our Pride).

The 11-day festival has brought together more than 300 exhibitors and is expected to attract over 15,000 visitors. The festival was officially opened on September 5 by His Excellency Hemed Suleiman Abdulla, Second Vice President of Zanzibar.

DIGITAL PAYMENTS FOR SMALL BUSINESSES

At the heart of Equity Bank Tanzania’s participation is the small trader, who remains an important part of Zanzibar’s enterprise economy.

Through Equity Lipa Namba, participating businesses can receive payments instantly from customers using any bank or mobile network in Tanzania. The funds are credited directly to the merchant’s account, without collection charges being deducted from the amount received.

Beyond the immediate convenience of receiving payments, digital transactions can help entrepreneurs establish a visible and verifiable record of their business activity.

Abdulssamad Abdul Ayoub, Director of Operations at Equity Bank Tanzania, said digital payments can create a financial footprint that may become valuable when entrepreneurs seek financing in the future.

“Digital payments do more than complete a sale. Each transaction helps a trader build a verifiable record of business activity, a record that can support future conversations about financing. The eleven days at Fahari ya Zanzibar therefore represent more than daily sales; they give entrepreneurs a financial footprint they can carry forward.”

BUILDING A FINANCIAL FOOTPRINT

The benefits of digital payments extend across different categories of entrepreneurs participating in the festival.

A small trader selling spices, seaweed, dried fish, batik, furniture or processed foods, for example, can benefit from a faster way of receiving payments while building a transaction history.

Women entrepreneurs can explore access to capital, financial training and business protection through Mwanamke Plus and Equity’s bancassurance solutions.

BANK OF AFRICA TANZANIA, CFAO MOBILITY PARTNER TO BOOST BUSINESS GROWTH THROUGH VEHICLE FINANCING

Group photo featuring representatives from CFAO Mobility Tanzania and Bank of Africa Tanzania. From left to right: Mr. Asupya Nalingigwa, Head of Retail Banking, Bank of Africa Tanzania; Mr. Khalifa Zidadu, Head of Corporate Banking, Bank of Africa Tanzania; Mr. Ali Timimi, CEO, CFAO Mobility Tanzania; Ms. Tharaia Ahmed, Sales and Marketing Director, CFAO Mobility Tanzania; and Mr. Fabrice De Creisquer, CEO, CFAO Mobility East & Southern Region.

DAR ES SALAAM, TANZANIA; September 7, 2026 — Bank of Africa Tanzania and CFAO Mobility Tanzania Limited have entered into a new vehicle financing partnership aimed at helping entrepreneurs, professionals, SMEs and businesses expand their operations by improving access to vehicles as productive assets.

The collaboration will enable eligible customers to acquire new and eligible pre-owned vehicles from CFAO Mobility Tanzania while spreading the cost through structured financing. This will allow customers to preserve their cash flow while putting the acquired vehicles to productive use.

The initiative is expected to support business expansion, personal mobility, transportation, logistics, trade and tourism by making it easier for customers to access globally recognised vehicle brands distributed by CFAO Mobility Tanzania, including Mercedes-Benz, Suzuki and Fuso.

According to the two companies, the value of the partnership will ultimately be reflected in what customers are able to achieve with the vehicles they acquire, particularly through increased business capacity, improved distribution and logistics, and expansion of vehicle fleets.

CFAO: MOBILITY AS A DRIVER OF ECONOMIC OPPORTUNITIES

Speaking on the partnership, CFAO Mobility Tanzania Chief Executive Officer (CEO), Mr Ali Timimi, said the initiative would make mobility more accessible by connecting customers with the right vehicle and a practical financing solution.

“At CFAO Mobility Tanzania, we believe mobility is an important driver of economic opportunities. For many of our customers, a vehicle is not simply a means of transport; it is an asset that helps them run a business, serve their customers, grow their operations and create value. Our partnership with Bank of Africa Tanzania is about making that opportunity more accessible,” he said.

Mr Timimi added that the collaboration would create a more connected customer journey, from selecting the appropriate vehicle to accessing the financing required to put it to work.

“By bringing together BOA Tanzania’s financing capabilities with CFAO’s automotive expertise and range of trusted brands, we are creating a more connected customer journey; from choosing the right vehicle to accessing the right financing needed to put it to work,” he said.

SERENGETI BREWERIES YAIMARISHA DHAMIRA YAKE KATIKA DIRA 2050, KAMATI YA BAJETI YA BUNGE YATEMBELEA KIWANDA CHA MOSHI

Kilimanjaro, Tanzania, Septemba 6, 2026: Kampuni ya Bia Serengeti (SBL) imeeleza mchango wa uwekezaji wa sekta binafsi katika mageuzi ya kiuchumi ya Tanzania wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti katika kiwanda chake cha Kilimanjaro, Moshi.

Ziara hiyo iliipa kamati fursa ya kujionea moja kwa moja uwekezaji wa SBL nchini Tanzania, mchango wake katika sekta ya viwanda na uchumi kwa ujumla, pamoja na hatua zinazochukuliwa na kampuni katika kuunga mkono kilimo cha ndani, ajira, maendeleo ya ujuzi, jamii na uendelevu wa mazingira.

Ziara hiyo imefanyika wakati Tanzania ikiendelea kutekeleza Dira ya Maendeleo Tanzania 2050, ambayo inatambua sekta binafsi imara na yenye nguvu kama kichocheo muhimu cha mageuzi ya kiuchumi, kuongeza tija, kukuza ubunifu na uwekezaji, pamoja na uundaji wa ajira.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Serengeti, Dkt. Obinna Anyalebechi, alisema SBL inaona uwekezaji wake nchini Tanzania ukienda zaidi ya shughuli za uzalishaji na kugusa mnyororo mzima wa thamani pamoja na jamii ambazo kampuni inafanya nazo kazi.

“Tanzania inapoelekea mwaka 2050, sekta binafsi ina jukumu muhimu la kuhakikisha matarajio ya Dira 2050 ya nchi yetu yanageuka kuwa matokeo halisi. Kwa hiyo, tumefurahi kuwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti katika kiwanda chetu cha Moshi na kuwaonyesha moja kwa moja uwekezaji tunaoufanya katika uzalishaji wa ndani, watu wetu na mnyororo mpana wa thamani.

“Katika SBL, tunaendelea kujitolea kufanya kazi kwa ushirikiano na Serikali kuunga mkono ajenda ya viwanda ya Tanzania, kujenga na kuongeza ajira, kuimarisha minyororo ya thamani ya ndani na kuchangia ukuaji endelevu wa uchumi,” alisema Dkt. Anyalebechi.

CREDITINFO YAZINDUA MFUMO WA KUBAINI WAKOPAJI WADANGANYIFU TANZANIA

Mwenyekiti wa Bodi ya Creditinfo Tanzania, Israel Kamuzora (kushoto), akibadilishana mawazo na Deogratias Mnyamani kutoka Benki Kuu ya Tanzania (katikati), muda mfupi baada ya uzinduzi wa huduma mpya inayolenga kusaidia taasisi za fedha kuwabaini wakopaji wadanganyifu, inayojulikana kama Fraud and ID Solution. Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Creditinfo Tanzania, Edwin Urasa.
Deogratias Mnyamani kutoka Benki Kuu ya Tanzania akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya inayolenga kusaidia taasisi za fedha zinazokopesha kuwabaini wakopaji wadanganyifu, inayojulikana kama Fraud and ID Solution. Huduma hiyo inatolewa na kampuni ya Creditinfo Tanzania.

Dar es Salaam, Septemba 7, 2026: Benki na taasisi nyingine za fedha zinazojihusisha na utoaji wa mikopo sasa zitaweza kubaini kwa urahisi zaidi wakopaji wasio waaminifu wanaotumia mbinu mbalimbali kuficha taarifa zao halisi ili kujipatia mikopo kwa njia za udanganyifu.

Hayo yamekuja kufuatia kuzinduliwa kwa mfumo mpya unaojulikana kama Fraud and ID Solution, uliozinduliwa na kampuni ya Creditinfo Tanzania, ambao unalenga kusaidia taasisi za fedha kuthibitisha utambulisho wa wateja kabla ya kutoa mikopo.

Mfumo huo utawezesha taasisi za fedha kumtambua mteja anayehitaji mkopo na kubaini iwapo anatumia majina, nyaraka au utambulisho ambao si wake au si halali.

BENKI KUU YA TANZANIA YAUPONGEZA MFUMO

Akizungumza katika uzinduzi wa mfumo huo, Bw. Deogratias Mnyamani kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) alisema huduma hiyo itazisaidia taasisi za fedha nchini kupambana na udanganyifu unaohusiana na mikopo, huku ikichangia kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa wakopaji waaminifu.

Alisema kwa miaka mingi huduma za aina hiyo zimekuwa zikitolewa na kampuni za kimataifa zilizopo nje ya Tanzania.

“Leo tunaondokana na kutegemea huduma hii muhimu kutoka kwa makampuni yaliyopo nje ya nchi yetu. Hii ni mara ya kwanza huduma hii inatolewa na kampuni iliyopo hapa hapa Tanzania ambayo ina uelewa mpana wa soko letu, taasisi zetu za kifedha na watu wetu. Nawapongeza sana Creditinfo kwa kuja na huduma hii,” alieleza Bw. Mnyamani.

MABADILIKO YA KIDIJITALI YAMEONGEZA HATARI YA FRAUD

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Creditinfo Tanzania, Bw. Edwin Urasa, alisema mabadiliko makubwa katika sekta ya fedha, ambayo yamechochea upanuzi wa huduma za kibenki pamoja na mifumo mbalimbali ya malipo ya kidijitali, yameongeza pia changamoto ya udanganyifu wa kifedha.

Alisema kupitia Fraud and ID Solution, Creditinfo inatumia taarifa kutoka mamlaka mbalimbali kusaidia taasisi za fedha kuthibitisha iwapo utambulisho unaowasilishwa na mkopaji ni halali kabla ya taasisi kufanya uamuzi wa kutoa mkopo.

“Uaminifu ni jambo muhimu sana, hasa katika kipindi hiki ambacho taasisi zinafanya mawasiliano na wateja kwa njia ya kidijitali pasipo kulazimika kuonana. Kumjua kwa uhakika yule unayewasiliana naye ni muhimu katika kulinda biashara na wateja wake pia,” alisema Bw. Urasa.

Alifafanua kuwa huduma hiyo mpya inazipatia taasisi za fedha taarifa za kiintelijensia kuhusu wateja, jambo linaloweza kusaidia katika kufanya maamuzi sahihi zaidi wakati wa mchakato wa utoaji wa mikopo.

Sunday, 6 September 2026

SERENGETI BREWERIES YATAMBULIWA KWA UBORA WA UZALISHAJI KATIKA TUZO ZA 19 ZA PMAYA 2026

Dar es Salaam, Tanzania – Septemba 3, 2026: Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) imeshinda Tuzo ya Rais ya Wazalishaji Bora wa Mwaka (PMAYA) katika kundi la wazalishaji wakubwa wa vileo, katika hafla ya 19 ya tuzo hizo zilizolenga kutambua ubora na mchango wa wazalishaji katika maendeleo ya sekta ya viwanda nchini Tanzania.

Tuzo hiyo, iliyoandaliwa na Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI), inatambua juhudi za SBL katika kuendeleza uzalishaji unaozingatia ufanisi, uendelevu, ubunifu, uwajibikaji wa kibiashara na athari chanya kwa jamii.

Tuzo za mwaka huu zilitolewa chini ya kauli mbiu “Umahiri wa Kijani – Kusherehekea Uzalishaji Endelevu,”ikisisitiza umuhimu wa uzalishaji unaolinda mazingira huku ukichochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya viwanda.

KUIMARISHA MNYORORO WA THAMANI WA KILIMO

SBL inaendelea kuunga mkono mnyororo wa thamani wa kilimo nchini kupitia ununuzi wa malighafi zinazozalishwa ndani ya Tanzania, zikiwemo mtama, shayiri na mahindi.

Kwa kufanya hivyo, kampuni inachangia katika kuimarisha soko la mazao ya kilimo yanayozalishwa na wakulima wa ndani, huku ikiendeleza uhusiano kati ya sekta ya kilimo na viwanda.

Friday, 4 September 2026

VODACOM CUTS CARBON EMISSIONS BY 24% AS NETWORK MODERNISATION REACHES 27.7 MILLION CUSTOMERS

Vodacom Tanzania Plc Network Director, Andrew Lupembe (left), and the company’s Director of External Affairs & Regulatory, Zuweina Farah, speak during the launch of the company’s Environmental, Social and Governance (ESG) Report for the financial year ended March 2026. The report highlights a 24% reduction in carbon emissions and significant investment in network modernisation.

FY2026 ESG Snapshot shows diesel consumption down by two million litres and energy savings increasing more than six-fold

Dar es Salaam - September 3, 2026: Vodacom Tanzania Plc has released its Environmental, Social and Governance (ESG) Snapshot for the year ended 31 March 2026, reporting a 24% reduction in Scope 1 and 2 greenhouse gas emissions alongside the largest network modernisation programme in the company’s history.

During the year, the company invested TZS 3.5 billion in energy-efficiency initiatives, delivering energy savings of 18,340 megawatt-hours (MWh) — more than six times the 2,861 MWh saved in FY2025.

Scope 1 and 2 market-based emissions fell to 18,445.5 tonnes of carbon dioxide equivalent (tCO₂e), from a restated 24,285.6 tonnes. Diesel consumption also declined by 24%, from 8.6 million litres to 6.6 million litres.

The reductions were driven by a major network modernisation programme that replaced legacy radio equipment across 1,808 sites in just seven months — work equivalent to roughly three years of normal deployment — together with improved grid stability that significantly reduced generator runtime at the company’s data centres.

LESS ENERGY, WIDER REACH

Vodacom Tanzania’s network consumes approximately 169.5 GWh of energy annually across more than 3,800 sites, including 2,190 in rural areas. Base stations account for 78.9% of total energy consumption, making improvements in network equipment efficiency one of the company’s most significant opportunities for reducing its environmental footprint.

VODACOM TANZANIA YAPUNGUZA UZALISHAJI WA HEWA CHAFUZI (CARBON EMISSIONS) KWA 24%

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mtandao wa Vodacom Tanzania Plc, Andrew Lupembe (kushoto), na Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Zuweina Farah, wakizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Mazingira, Jamii na Utawala (ESG) ya kampuni hiyo kwa mwaka wa fedha ulioishia Machi 2026. Ripoti hiyo imeonesha kupungua kwa uzalishaji wa hewa chafuzi (carbon emissions) kwa asilimia 24, pamoja na uwekezaji mkubwa katika uboreshaji wa mtandao.

Mkurugenzi wa Miundombinu wa Vodacom Tanzania Plc, Andrew Lupembe, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Mazingira, Jamii na Utawala (ESG) ya kampuni hiyo kwa mwaka 2026.

DAR ES SALAAM | Septemba 3, 2026

VODACOM Tanzania Plc imepunguza uzalishaji wa hewa chafuzi kwa asilimia 24, huku maboresho makubwa ya mtandao yakifikia wateja milioni 27.7, ikiwa ni sehemu ya mafanikio yaliyoainishwa katika Ripoti ya Mazingira, Jamii na Utawala (ESG) ya kampuni kwa mwaka ulioishia Machi 31, 2026.

Vodacom Tanzania ilizindua ripoti hiyo Septemba 1, 2026, ikionesha hatua mbalimbali zilizopigwa katika kupunguza athari za kimazingira, kuboresha ufanisi wa nishati, kupanua huduma za kidijitali na kuimarisha ujumuishwaji wa kifedha nchini.

UZALISHAJI WA HEWA CHAFUZI WAPUNGUA KWA 24%

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, uzalishaji wa hewa chafuzi ulipungua hadi tani 18,445.5, kutoka tani 24,285.6 katika kipindi kilichotangulia.

Wakati huo huo, matumizi ya mafuta ya dizeli yalipungua kwa asilimia 24, kutoka lita milioni 8.6 hadi lita milioni 6.6.

Kupungua huko kulitokana na kubadilisha vifaa vya zamani vya mawasiliano ya redio katika maeneo 1,808 ndani ya kipindi cha miezi saba, pamoja na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa gridi ya taifa.

Hatua hizo zimepunguza muda ambao jenereta hutumika katika vituo vya kampuni na hivyo kupunguza matumizi ya mafuta pamoja na uzalishaji wa hewa chafuzi.

SHILINGI BILIONI 3.5 ZATUMIKA KATIKA UFANISI WA NISHATI

Katika mwaka huo, Vodacom Tanzania iliwekeza Shilingi bilioni 3.5 katika ufanisi wa nishati, na kufikisha uokoaji wa nishati hadi megawati 18,340, zaidi ya mara sita ya megawati 2,861 zilizookolewa mwaka 2025.

Mtandao wa Vodacom Tanzania unatumia takriban GWh 169.5 kwa mwaka katika maeneo zaidi ya 3,800 nchini, ambapo 2,190 kati yake yapo vijijini.

Vituo vya msingi vya mawasiliano vinachukua asilimia 78.9 ya matumizi yote ya nishati ya kampuni.

Katika mwaka huo, maeneo 169 yaliyokuwa nje ya gridi ya taifa yaliunganishwa kwenye gridi, hatua iliyosaidia kupunguza utegemezi wa jenereta.

Thursday, 3 September 2026

NMB FOUNDATION YATENGA SHILINGI BILIONI 1 KUWEZESHA VIJANA 50 KUPITIA ‘NURU YANGU SCHOLARSHIP AND MENTORSHIP’

NMBF YAFUNGUA MAOMBI YA UFADHILI WA MASOMO YA CHUO KIKUU NA MENTORSHIP

DAR ES SALAAM | September 3, 2026

VIJANA 50 wenye ufaulu wa juu kitaaluma lakini wanaotoka katika familia zenye uwezo mdogo kifedha watanufaika na ufadhili wa elimu ya chuo kikuu pamoja na maandalizi ya kuingia katika soko la ajira kupitia programu ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship.

NMB Foundation (NMBF), kwa kushirikiana na Benki ya NMB, imetenga Shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuwawezesha vijana hao katika dirisha la tatu la programu hiyo kwa mwaka wa masomo 2026/27.

Maombi ya programu hiyo yamefunguliwa na yatapokelewa kupitia tovuti rasmi ya NMB Foundation, foundation.nmbbank.co.tz, kuanzia Leo, September 3, hadi Septemba 18, 2026.

Programu hiyo inalenga Watanzania waliomaliza Kidato cha Sita mwaka 2026 kwa Daraja la Kwanza lenye pointi tatu hadi tano, ambao pia wana ushahidi wa uhitaji wa kifedha na wanatarajia kujiunga na taasisi za elimu ya juu zinazotambuliwa nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa NMB Foundation, Nelson Karumuna, alisema vijana hao watakaochaguliwa wataungana na wanufaika 101 waliowezeshwa kupitia awamu mbili zilizopita za programu hiyo.

Kwa kuongezwa kwa vijana hao 50, idadi ya wanufaika wa Nuru Yangu itafikia 151, huku NMBF ikiwa imetumia zaidi ya Shilingi bilioni 2.1 katika awamu zilizopita na kutenga Sh bilioni 1 kwa kundi jipya.

“Uwezeshaji huu utagharamia ada, fedha za kujikimu, mafunzo kwa vitendo, malipo ya lazima ya chuo na vifaa vya kujifunzia, ikiwemo kompyuta mpakato,” alisema Karumuna.

 

Alisema pamoja na kugharamiwa masomo, vijana hao watapatiwa pia malezi na ushauri wa kitaaluma, mafunzo ya uongozi, maandalizi ya kuingia katika soko la ajira na fursa za kujifunza kwa vitendo.

NMBF YATOA ONYO DHIDI YA UTAPELI

Karumuna alisisitiza kuwa maombi ya programu hiyo ni bure, akionya kuwa hakuna mtu wala taasisi iliyopewa mamlaka ya kuuza nafasi za Nuru Yangu.

Alisema mchakato wa uchaguzi utafanyika kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa pamoja na uhakiki wa kina ili kuhakikisha fursa hizo zinawafikia vijana wanaostahili.

NMB FOUNATION ALLOCATES TZS 1 BILLION TO EMPOWER 50 YOUNG TANZANIANS THROUGH NURU YANGU SCHOLARSHIP

DAR ES SALAAM | September 3, 2026

Fifty high-performing young Tanzanians from financially disadvantaged families are set to receive university education and career-readiness support after NMB Foundation (NMBF), in partnership with NMB Bank, allocated TZS 1 billion for the 2026/27 academic year.

The support will be provided through the third intake of the Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Programme, an initiative aimed at removing financial barriers that prevent academically capable young Tanzanians from pursuing higher education.

Applications are open from today, September 3, until September 18, 2026, and must be submitted through the official NMB Foundation website, foundation.nmbbank.co.tz

The programme targets Tanzanian students who completed Form Six in 2026 with a Division One score of between three and five points, demonstrate financial need and are preparing to join recognised higher learning institutions in Tanzania.

Speaking in Dar es Salaam, NMB Foundation General Manager Nelson Karumuna said the 50 successful applicants would join 101 students who benefited from the programme’s first two intakes.

Their inclusion will bring the total number of beneficiaries to 151 students. NMBF has invested more than TZS 2.1 billion in supporting the first two cohorts, with another TZS 1 billion committed to the 2026/27 intake.

“The support will cover tuition fees, living expenses, field practical training, compulsory university charges and learning materials, including laptops,” Karumuna said.

He added that beneficiaries would also receive academic mentorship, leadership development, employment preparation and practical learning opportunities designed to help them succeed both at university and in their future careers.

Karumuna emphasised that the application process is completely free, warning applicants against individuals or organisations claiming to facilitate or sell scholarship opportunities.

“No individual or organisation has been authorised to sell or facilitate scholarship places,” he said, adding that selection would be based on the published criteria and a detailed verification process to ensure the support reaches eligible students.

The Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Programme was launched on May 19, 2022, with the objective of addressing financial barriers that prevent academically talented young Tanzanians from accessing higher education.

Wednesday, 2 September 2026

STANBIC BANK TANZANIA COMMITS TZS 200 MILLION TO FAHARI YA ZANZIBAR 2026

From left: Tahir Mussa, Acting Deputy Director General of TanTrade; Juma Burhan, Executive Director of ZEEA; and Fatma Ahmed, Head of Enterprise Banking at Stanbic Bank Tanzania, during a press conference in Zanzibar to announce the partnership.

ZANZIBAR, TANZANIA – SEPTEMBER 2, 2026: Stanbic Bank Tanzania has committed TZS 200 million to support Fahari ya Zanzibar 2026, reinforcing its partnership with Zanzibar and its commitment to supporting businesses, entrepreneurs and communities across the Isles.

The third edition of Fahari ya Zanzibar will be held from September 4 to 14, 2026, at Maisara Grounds in Zanzibar under the theme “Bidhaa Zetu Ndio Fahari Yetu,” meaning “Our Products Are Our Pride.”

The festival is organised by the Zanzibar Economic Empowerment Agency and is expected to attract more than 15,000 visitors and over 300 exhibitors.

Fahari ya Zanzibar will bring together entrepreneurs, small and medium-sized enterprises (SMEs), investors, financial institutions, government agencies and members of the public, providing a platform to showcase locally produced goods and services, establish business connections and enhance access to financial and business development services.

The Grand Launch, scheduled for Saturday, September 5, is expected to be officiated by H.E. Dr Hussein Ali Mwinyi, President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council.

STANBIC TO CONNECT BUSINESSES WITH FINANCIAL SOLUTIONS

As a Platinum Sponsor, Stanbic Bank Tanzania will use its presence at the festival to connect entrepreneurs and businesses with practical financial solutions designed to support business growth.

Among the solutions to be showcased are trade solutions including CIPS and the Africa China Corridor, Biashara Exchange, guarantees and supply chain solutions, as well as agribusiness solutions, Vehicle and Asset Finance and digital solutions such as TXB, Lipa, Pokea and Agency Banking.

The Stanbic Biashara Incubator will also participate in the festival, bringing business development support closer to entrepreneurs and SMEs.

The Incubator team will engage entrepreneurs on areas including financial management, access to finance, business growth and market opportunities, helping businesses strengthen their capabilities and position themselves for sustainable growth.

SUPPORTING ZANZIBAR’S ENTREPRENEURIAL COMMUNITY

Speaking on the partnership, Fatma Ahmed, Head of Enterprise Banking at Stanbic Bank Tanzania, said the Bank's involvement reflects its ambition to play a practical role in Zanzibar's economic development.

“Fahari ya Zanzibar celebrates the entrepreneurs, businesses and locally produced goods that are contributing to Zanzibar’s growth. Our role goes beyond providing financial solutions. We want to help businesses build the knowledge, connections and capabilities they need to grow, compete and access new opportunities.”

VODACOM YAANGAZIA JINSI MTANDAO UNAVYOCHOCHEA USHIRIKI WA KIDIJITALI KUELEKEA DIRA YA MAENDELEO 2050

Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma, akizungumza katika Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, ambapo alielezea namna Vodacom inavyowaunganisha Watanzania na kuongeza tija kupitia huduma zake za “Zaidi ya Mtandao”, hususan kwa kuwawezesha watengeneza maudhui na watumiaji wa majukwaa ya mtandaoni kupata mtandao bora pamoja na simu janja zinazounga mkono ubunifu wao.
Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma (kulia), akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, baada ya kumaliza majadiliano kuhusu namna ya kuunganisha sauti za Watanzania, hususan watengeneza maudhui na watumiaji wa majukwaa ya mtandaoni.
Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited, Rosalynn Mndolwa-Mworia (wa pili kushoto), Meneja wa Uchunguzi wa Vodacom Tanzania, Joseph Mnyune (kushoto), na Meneja Biashara, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited, Tess Aloyce (wa pili kulia), wakizungumza wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026.

Ni katika Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026

DAR ES SALAAM - September 2, 2026: Vodacom Tanzania imeangazia mchango wa mtandao, ubunifu na ujasiriamali katika kuchochea ushiriki wa kidijitali na kufanikisha malengo ya Dira ya Maendeleo Tanzania 2050.

Hayo yameelezwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, tukio linalowakutanisha wabunifu, wajasiriamali, watunga sera, wawekezaji, vijana na wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili na kuibua fursa za kukuza uchumi wa kidijitali nchini.

IWTz 2026 imefanyika chini ya kauli mbiu “Kutoka Matarajio hadi Mageuzi: Kuibua Njia ya Tanzania Kuelekea Ustawi Jumuishi.”

VODACOM YASHIRIKI MJADALA WA UCHUMI WA KIDIJITALI

Katika wiki hiyo ya ubunifu, Vodacom Tanzania imeshiriki katika mijadala kuhusu uchumi wa watengeneza maudhui na majukwaa ya mtandaoni, maonesho, mikutano na wadau, pamoja na shughuli za kuelimisha jamii kuhusu usalama wa mtandao.

Ushiriki huo unaonesha nafasi ya sekta ya mawasiliano katika kuwezesha Watanzania kutumia teknolojia na huduma za kidijitali kama nyenzo za kujifunza, kufanya biashara, kubuni na kujenga fursa za kiuchumi.

Akizungumza katika mjadala kuhusu watengeneza maudhui na majukwaa ya mtandaoni, Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma, alisema thamani ya mtandao inaonekana zaidi kupitia fursa ambazo unawawezesha Watanzania kuzipata katika maeneo mbalimbali, ikiwemo elimu, biashara na ubunifu.

VODACOM YAWAWEZESHA WATENGENEZA MAUDHUI

Kupitia Vodacom Youth Base (VYB), Vodacom Tanzania inaendelea kuwawezesha vijana na watengeneza maudhui kutumia fursa zinazopatikana kupitia teknolojia na majukwaa ya kidijitali.

EQUITY WAITARA TROPHY 2026: ELEVATING THE GAME, LIFESTYLE AND POSSIBILITIES

Equity Bank Tanzania brings together golf, lifestyle and premium banking experiences

DAR ES SALAAM, September 2, 2026 — Equity Bank Tanzania is set to bring a new lifestyle experience to Tanzania’s golfing community through the Equity Waitara Trophy 2026, creating a platform that connects a shared passion for golf with networking, lifestyle experiences and opportunities for wealth creation.

The tournament is scheduled for September 19, 2026, at TPDF Lugalo Golf Club, bringing together golf enthusiasts, business leaders, entrepreneurs and professionals from across the country for a day that goes beyond competition to celebrate the lifestyle, relationships and opportunities surrounding the sport.

Through the sponsorship, Equity Bank Tanzania is strengthening its engagement with the High Net Worth Individual (HNI) segment by connecting customers with premium financial and lifestyle solutions designed to help them elevate how they live, travel, transact, invest and grow their wealth.

PREMIUM BANKING MEETS LIFESTYLE

At the centre of the experience is the Equity Mastercard World Elite Debit Card, complemented by Equity Bank's broader premium banking proposition.

The proposition offers customers access to personalised financial solutions, investment opportunities, asset financing, mortgages, insurance, regional banking services and selected lifestyle privileges.

Speaking on the partnership, Shumbana Walwa, Head of Brand and Product Marketing at Equity Bank Tanzania, said the tournament provides an opportunity for the bank to engage customers around a lifestyle and passion they value.

“Golf is more than a game; it is a lifestyle built around ambition, relationships, discipline and continuous growth. Through the Equity Waitara Trophy, we want to connect with Tanzania’s golf community through that shared passion and introduce experiences and solutions that can help them elevate both their game and their lives,” said Walwa.

HONOURING GENERAL GEORGE WAITARA

The annual Waitara Trophy honours retired General George Waitara, founder of TPDF Lugalo Golf Club.

Over the years, the tournament has grown into an important fixture within Tanzania's golfing community, attracting golfers and enthusiasts from different parts of the country.

Tuesday, 1 September 2026

TANZANIA TABLES MOVABLE ASSETS SECURED LENDING BILL 2026 IN PARLIAMENT TO EXPAND ACCESS TO CREDIT

The Minister for Finance, Hon. Ambassador Khamis Mussa Omar (MP), presenting to Parliament the Movable Assets Secured Lending Bill, 2026, which seeks to establish an effective framework for managing loans provided against movable assets as collateral.

DODOMA - August 31, 2026: Minister for Finance, Hon. Ambassador Khamis Mussa Omar (MP), has tabled the Movable Assets Secured Lending Bill, 2026 in Parliament, seeking to establish a comprehensive framework for the management of loans secured by movable assets.

Presenting the Bill in Parliament in Dodoma, Hon. Ambassador Omar said the proposed legislation is aimed at increasing the use of banking services in Tanzania from 22 percent in 2023 to 50 percent by 2030.

He said the Bill also seeks to increase private sector credit as a proportion of Gross Domestic Product (GDP) from 22.5 percent in 2024 to 50 percent by 2030, while supporting job creation and increasing the contribution of the financial sector to 20 percent by 2030, from 17.1 percent in 2024.

According to the Minister, the proposed legislation is important in expanding access to credit for individuals and businesses by allowing them to use movable assets as collateral, rather than relying predominantly on immovable assets such as land and buildings.

ADDRESSING CHALLENGES IN MOVABLE ASSET COLLATERAL

Hon. Ambassador Omar said one of the key challenges the Bill seeks to address is the absence of a unified registration system for movable assets that can be used as collateral.

The lack of such a system has created a situation where the same asset can potentially be used as collateral for multiple loans without other lenders being aware of existing claims over the asset. This could contribute to an increase in non-performing loans within the financial sector.

Other challenges include the absence of a coordinated system for managing movable assets used as collateral, as well as inadequate procedures for enforcing the rights of borrowers and lenders when such assets are sold.

Monday, 31 August 2026

MAENDELEO BANK PLC NAMED FASTEST GROWING SME BANK IN TANZANIA 2026


Global Banking & Finance Review recognition highlights the Bank’s growing focus on small and medium enterprises

DAR ES SALAAM, TANZANIA — August 31, 2026: Maendeleo Bank Plc has been named Fastest Growing SME Bank Tanzania 2026 by Global Banking & Finance Review, published by GBAF Publications Ltd, in recognition of the Bank’s rapid growth in serving small and medium enterprises (SMEs) across Tanzania.

The recognition reflects Maendeleo Bank’s deliberate strategic focus on supporting SMEs through products and services designed around their business needs.

Business growth, including SME growth, is one of the three key pillars of Maendeleo Bank’s Strategy 2025–2030. Over the past year, the Bank has expanded its branch network to six locations, while continuing to strengthen its services to SME customers.

The Bank also conducted its annual SME Clinic, an initiative designed to identify training and product needs directly from SME customers. In addition, Maendeleo Bank has developed a consolidated approach to SME product bundling, enabling SME customers to gain visibility into the full range of relevant banking products during a single visit.

RECOGNITION OF SME TEAM AND FRONTLINE STAFF

Commenting on the recognition, Maendeleo Bank Plc Managing Director, Mr. Lomnyaki Saitabau, said the award reflects the efforts of the Bank’s SME Unit and frontline staff working closely with small and medium enterprises.

“This recognition belongs to our SME Unit and to frontline staff across our branch network, whose work with small and medium enterprises earned it. It reflects a direction we set deliberately in our Strategy 2025 to 2030: build products and service around what SME customers actually need.”

Sunday, 30 August 2026

VODACOM TANZANIA YAGUSA MAISHA YA WANAFUNZI IHOWANJA KWA KUBORESHA MAZINGIRA YA USOMAJI

Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania PLC, Chiha Nchimbi (kulia), akikabidhi dawati kwa Diwani wa Kata ya Kilosampepo, Boniventure Killian Mwanga (kushoto). Dawati hilo ni mojawapo ya madawati 30 yaliyokabidhiwa katika Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro, kupitia mpango wa Classroom for Community Impact unaotekelezwa chini ya Vodacom Tanzania Foundation.

Kupitia mpango huo, Vodacom Tanzania imekarabati na kujenga jumla ya madarasa sita pamoja na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma za Vikindu (Mkuranga – Pwani), Ihowanja (Malinyi – Morogoro) na Mahilo (Songea – Ruvuma), kwa lengo la kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro.

Wengine katika picha ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ihowanja, Iddy Mgonja (wa pili kushoto), na Mtendaji wa Kijiji cha Ihowanja, Gotard Garus Mitti (wa pili kulia).

MALINYI, MOROGORO - Agosti 28, 2026: Vodacom Tanzania PLC kupitia programu ya Classroom for Community Impact, iliyo chini ya Vodacom Tanzania Foundation, imekabidhi madarasa mawili yaliyokarabatiwa, madawati 30 pamoja na vifaa muhimu vya shule kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro.

Msaada huo ni sehemu ya juhudi za kampuni katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi za umma nchini, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Makabidhiano hayo yaliyofanyika jana yanalenga kuchangia katika kuboresha miundombinu ya shule na kuweka mazingira salama na rafiki zaidi kwa wanafunzi na walimu.

MADARASA SITA, MADAWATI 90

Kupitia mpango huo, katika awamu hii Vodacom Tanzania imekarabati na kujenga jumla ya madarasa sita na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma zilizopo mikoa mbalimbali.

Shule hizo ni Vikindu wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Ihowanja wilayani Malinyi mkoani Morogoro na Mahilowilayani Songea mkoani Ruvuma.

Katika Shule ya Msingi Ihowanja, msaada huo umehusisha ukarabati wa madarasa mawili pamoja na utoaji wa madawati 30. Aidha, wanafunzi wamepatiwa mahitaji muhimu ya shule, ikiwemo madaftari, chupa za kubebea maji, kalamu na mabegi.

VODACOM YAWEKEZA KATIKA ELIMU JUMUISHI

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania PLC, Chiha Nchimbi, alisema mpango huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kusaidia jamii na kuboresha mazingira ambayo watoto wanapata elimu.

Alisema uwepo wa madarasa salama, madawati ya kutosha na mazingira rafiki ya kujifunzia ni muhimu katika kuwawezesha wanafunzi, hasa wenye mahitaji maalum, kushiriki kikamilifu katika masomo yao.