![]() |
| Wadau na washiriki wa Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) wakipiga makofi kuashiria kufurahia uzinduzi wa mashindano ya mbio za Vodacom Coastal Classic. |
DAR ES SALAAM - Agosti 6, 2026: Vodacom Tanzania Plc kwa kushirikiana na Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA) wametangaza rasmi kubadilishwa kwa jina la msafara wa baiskeli wa Twende Butiama na kuwa Nyerere Cycling Tour, hatua inayolenga kuenzi urithi wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere huku ikiupa mchezo wa baiskeli nchini mwelekeo mpya wa kimataifa.
Sambamba na mabadiliko hayo, Vodacom pia imezindua mashindano mapya ya Vodacom Coastal Classic, mbio za kilomita 109 zinazotarajiwa kuwa moja ya mashindano makubwa ya baiskeli nchini na kuvutia washiriki kutoka Tanzania, Afrika Mashariki na mataifa mbalimbali duniani.
Tangazo hilo limetolewa leo, Agosti 6, 2026, jijini Dar es Salaam.
Miaka 10 ya Kuendeleza Elimu Kupitia Baiskeli
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, msafara huo umekuwa ukitumia mchezo wa baiskeli kama chombo cha kuhamasisha maendeleo ya elimu kwa kuenzi maono ya Mwalimu Nyerere ya kutoa fursa sawa kwa kila mtoto.
Kupitia kampeni hiyo, zaidi ya shule 107 zimefikiwa huku zaidi ya wanafunzi 75,000 wakinufaika na ujenzi wa madarasa jumuishi, miundombinu ya vyoo pamoja na upatikanaji wa vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Vodacom Tanzania Foundation ilianza kushirikiana na CHABATA kufadhili msafara huo miaka minne iliyopita, ambapo katika kipindi hicho ushiriki umeongezeka mara nne na kuvutia waendesha baiskeli kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Nyerere Cycling Tour Kuanza Oktoba
Msafara wa mwaka huu utafanyika kuanzia Oktoba 5 hadi 14, 2026, ukianzia Bagamoyo kuelekea Butiama.

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpg)






.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



