MALINYI, MOROGORO - Agosti 28, 2026: Vodacom Tanzania PLC kupitia programu ya Classroom for Community Impact, iliyo chini ya Vodacom Tanzania Foundation, imekabidhi madarasa mawili yaliyokarabatiwa, madawati 30 pamoja na vifaa muhimu vya shule kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro.
Msaada huo ni sehemu ya juhudi za kampuni katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi za umma nchini, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Makabidhiano hayo yaliyofanyika jana yanalenga kuchangia katika kuboresha miundombinu ya shule na kuweka mazingira salama na rafiki zaidi kwa wanafunzi na walimu.
MADARASA SITA, MADAWATI 90
Kupitia mpango huo, katika awamu hii Vodacom Tanzania imekarabati na kujenga jumla ya madarasa sita na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma zilizopo mikoa mbalimbali.
Shule hizo ni Vikindu wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Ihowanja wilayani Malinyi mkoani Morogoro na Mahilowilayani Songea mkoani Ruvuma.
Katika Shule ya Msingi Ihowanja, msaada huo umehusisha ukarabati wa madarasa mawili pamoja na utoaji wa madawati 30. Aidha, wanafunzi wamepatiwa mahitaji muhimu ya shule, ikiwemo madaftari, chupa za kubebea maji, kalamu na mabegi.
VODACOM YAWEKEZA KATIKA ELIMU JUMUISHI
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania PLC, Chiha Nchimbi, alisema mpango huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kusaidia jamii na kuboresha mazingira ambayo watoto wanapata elimu.
Alisema uwepo wa madarasa salama, madawati ya kutosha na mazingira rafiki ya kujifunzia ni muhimu katika kuwawezesha wanafunzi, hasa wenye mahitaji maalum, kushiriki kikamilifu katika masomo yao.

.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)









.jpeg)



















.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
