Bahi, Dodoma
Serikali imeipongeza NMB Bank Plc kwa kukamilisha ujenzi wa shule ya sekondari ya bweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Wilaya ya Bahi, Mkoa wa Dodoma, mradi wenye thamani ya Shilingi bilioni 5 ambao umekamilika kwa asilimia 100.
Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu, Atupele Mwambene, alipotembelea na kukagua mradi huo, akisema shule hiyo imejengwa kwa viwango vya juu vinavyokidhi mahitaji ya wanafunzi wenye uhitaji maalumu nchini.
Kwa mujibu wa Mwambene, shule hiyo imewekewa miundombinu yote muhimu ikiwemo mabweni, vitanda, madawati na vifaa vingine vinavyohitajika kwa mazingira bora ya kujifunzia na kuishi kwa wanafunzi.
"Shule hii imejengwa kwa kiwango cha juu sana na imekamilika kwa asilimia 100. Ina uwezo wa kuhudumia wanafunzi 160 na inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi mwezi Januari 2027 mara baada ya kukamilika kwa taratibu za usajili," alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uhusiano na Wawekezaji, Uendelevu na Mawasiliano wa NMB Bank Plc, Innocent Yonazi, alisema mradi huo ni sehemu ya dhamira ya benki hiyo ya kuimarisha upatikanaji wa elimu kwa makundi maalumu na kuchangia maendeleo endelevu ya jamii.
Alisema NMB inaamini elimu ni nyenzo muhimu ya kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, ndiyo sababu imeendelea kuwekeza katika miradi inayoongeza fursa za elimu kwa watoto wenye mahitaji maalumu na makundi mengine yanayohitaji msaada.
"Mradi huu una lengo la kupanua fursa za elimu kwa watoto wenye mahitaji maalumu na kuhakikisha wanapata mazingira bora ya kujifunzia. Hii ni sehemu ya mchango wetu katika maendeleo ya taifa kupitia uwekezaji wa kijamii," alisema Yonazi.
Aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, NMB Bank imetoa zaidi ya Shilingi bilioni 24 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya jamii nchini kupitia programu zake za uwajibikaji kwa jamii.
.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)


%20copy.jpeg)
.jpeg)










.jpeg)


.jpeg)

.jpg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
