Dar es Salaam – Katika hatua muhimu ya kuimarisha ujumuishaji wa kifedha, Equity Bank Tanzania imetangaza ushirikiano wa kimkakati na Mixx by Yas unaolenga kusogeza huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi kupitia mtandao mpana wa mawakala wa Mixx by Yas uliosambaa nchi nzima.
Ushirikiano huu unaimarisha juhudi za benki katika kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa haraka, urahisi na uaminifu, popote walipo – mijini na vijijini.
Huduma za Kuweka na Kutoa Fedha Kupitia Mawakala
Kupitia ushirikiano huu, wateja wa Equity sasa wanaweza:
- Kuweka fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao za Equity
- Kutoa fedha kwa matumizi mbalimbali
Huduma hizi zinapatikana kupitia mawakala wa Mixx by Yas waliopo kote Tanzania.
Kwa wateja wenye simu janja, miamala inafanyika kwa urahisi kupitia Equity Mobile App, huku watumiaji wa simu za kawaida wakihudumiwa kupitia USSD code *150*07#.
Huduma hii imebeba kauli mbiu:
“Weka Pesa, Toa Pesa” – Equity Bank kwa kushirikiana na Mixx by Yas.
Kauli ya Uongozi
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Bi. Isabela Maganga, alisema:
“Ushirikiano huu na Mixx by Yas una thamani ya kimkakati inayokwenda mbali zaidi ya utoaji wa huduma za kibenki. Ni hatua mahsusi ya kuwafikia wateja kwa urahisi zaidi, kupunguza umbali kati yao na huduma za benki, na kuwaletea huduma karibu na maeneo wanayoishi na kufanyia kazi.
Kupitia mtandao mpana wa mawakala wa Mixx by Yas, wateja hawatalazimika tena kusafiri umbali mrefu kufika matawi ya benki. Wanaweza kuweka na kutoa fedha kwa urahisi, gharama nafuu na usalama mkubwa kupitia mawakala wanaowaamini.”
Kwa mujibu wa benki hiyo, ushirikiano huu:
- Unarahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wateja
- Unafungua fursa mpya za kiuchumi kwa mawakala
- Unaongeza mzunguko wa fedha katika uchumi wa ndani
- Unachochea wananchi kushiriki kikamilifu katika mfumo rasmi wa kifedha
Kwa upande wake, Angelica Pesha, CEO wa Mixx by Yas, alisema:
“Kwa kuunganisha uzoefu wa kibenki wa Equity na nguvu ya jukwaa la Mixx pamoja na mtandao mpana wa mawakala wetu, tunabadilisha vituo vya huduma vilivyo karibu na jamii kuwa milango kamili ya huduma za kibenki.
Kupitia ushirikiano huu, ikiwemo upanuzi wa huduma za utoaji fedha za kimataifa (IMT), tunaongeza upatikanaji, urahisi na uaminifu kwa mamilioni ya Watanzania. Kwa pamoja, tunajenga mfumo wa kifedha ulio jumuishi zaidi, unaounganishwa kidijitali na wenye kuwezesha uchumi wa taifa.”
Mwelekeo Mpya wa Sekta ya Kifedha
Ushirikiano kati ya Equity Bank Tanzania na Mixx by Yas unaakisi mwelekeo wa sekta ya kifedha wa kuunganisha huduma za benki na majukwaa ya kidijitali ili kuwafikia wateja kwa ukaribu zaidi.





.jpeg)


.jpeg)









.jpeg)





.jpg)

.jpg)

.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)



