Wachimbaji, Wakandarasi Kunufaika na Mpango Mpya wa Ufadhili wa Mitambo
DAR ES SALAAM – Benki ya NMB Plc na Mantrac Tanzania Limited zimeingia katika ushirikiano wa kimkakati utakaorahisisha upatikanaji wa mikopo ya kununua na kuhudumia mitambo kwa wachimbaji, wakandarasi na wafanyabiashara wanaofanya shughuli katika sekta za madini, ujenzi, miundombinu, nishati na viwanda.
Makubaliano hayo yanachanganya uwezo wa kifedha wa NMB, benki yenye mtandao wa zaidi ya matawi 250 nchini, na uzoefu wa Mantrac Tanzania katika usambazaji wa mitambo ya Caterpillar pamoja na huduma za matengenezo na msaada wa kiufundi, hatua inayotarajiwa kuongeza upatikanaji wa mitaji kwa miradi mikubwa ya maendeleo.
Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano ilisainiwa jijini Dar es Salaam na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Uendeshaji wa Mantrac Kanda ya Afrika Mashariki, Levite Dongmo.
Ufadhili wa Mitambo kwa Masharti Rafiki
Kupitia mpango huo, wateja watakaokidhi vigezo vya mkopo wataweza kufadhili ununuzi wa mitambo kwa kuchangia asilimia 20 hadi 25 ya gharama za awali, huku NMB ikiandaa mifumo ya ufadhili na ratiba za marejesho kulingana na mtiririko wa fedha, aina ya biashara na mahitaji ya mradi husika.
Akizungumza wakati wa utiaji saini, Mponzi alisema gharama kubwa za ununuzi wa mitambo zimekuwa changamoto kwa wafanyabiashara wengi wenye miradi yenye tija, lakini wasiokuwa na mtaji wa kutosha.
"Tunapofadhili mitambo, hatufadhili mashine pekee. Tunawezesha ujenzi wa barabara, migodi, viwanda, ajira na uwezo wa Tanzania kujenga mustakabali wake wa kiuchumi," alisema.


.jpeg)
.jpeg)










.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

