Benki ya NMB imeendeleza jitihada zake za kujenga nguvu kazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa katika sekta ya fedha nchini kwa kusaidia mafunzo ya kitaaluma na utalaamu kwa vijana 100 kupitia mpango maalumu wa Graduate Banker Readiness Programme (GBRP) unaotekelezwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Kupitia mpango huo, NMB kwa kushirikiana na UDSM, inatoa mafunzo ya kitaaluma yanayochanganya nadharia na vitendo, yakilenga kuwajengea washiriki uelewa mpana na wa kina wa sekta ya fedha. Kundi la nne la washiriki, kama ilivyokuwa kwa makundi yaliyotangulia, limehitimu Ijumaa iliyopita baada ya kukamilisha mafunzo hayo.
Akizungumza kabla ya kuwakabidhi wahitimu vyeti, Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa NMB, Erica Hanson, alisema mpango huo ni matokeo ya ushirikiano wa kimkakati kati ya benki hiyo na UDSM kupitia Shule ya Biashara ya chuo hicho, ukiwa na lengo la kuunganisha elimu ya darasani na uhalisia wa kazi za benki.
Bi. Hanson alibainisha kuwa washiriki wamepata mafunzo katika maeneo muhimu ikiwemo uchambuzi wa kifedha, uendeshaji wa benki, usimamizi na udhibiti wa vihatarishi, uzingatiaji wa kanuni, utoaji bora wa huduma kwa wateja pamoja na mifumo ya benki ya kidijitali.
“Kuhitimu kwa vijana hawa leo kunaongeza nguvu katika dhamira ya NMB ya kuendelea kujijenga kama mwajiri pendwa nchini, jambo ambalo limethibitishwa kwa kutunukiwa Tuzo ya Mwajiri Bora kwa miaka mitatu mfululizo. Haya yote ni matokeo ya uwekezaji wa makusudi katika watu, vipaji na maendeleo endelevu ya rasilimali watu,” alisema Bi. Hanson.











.jpeg)


.jpeg)









.jpeg)





.jpg)

.jpg)

.jpeg)
.jpeg)
