Foreign Exchange Rates

Equity Bank Advert_12 February 2026

CRDB Bank Advert_070325

Global Sanctions Compliance Masterclass

Saturday, 21 February 2026

BENKI YA EQUITY YAINGIA UBIA WA KIMKAKATI NA MIXX BY YAS KUPANUA HUDUMA ZA KIFEDHA NCHINI

Dar es Salaam – Katika hatua muhimu ya kuimarisha ujumuishaji wa kifedha, Equity Bank Tanzania imetangaza ushirikiano wa kimkakati na Mixx by Yas unaolenga kusogeza huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi kupitia mtandao mpana wa mawakala wa Mixx by Yas uliosambaa nchi nzima.

Ushirikiano huu unaimarisha juhudi za benki katika kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa haraka, urahisi na uaminifu, popote walipo – mijini na vijijini.


Huduma za Kuweka na Kutoa Fedha Kupitia Mawakala

Kupitia ushirikiano huu, wateja wa Equity sasa wanaweza:

  • Kuweka fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao za Equity
  • Kutoa fedha kwa matumizi mbalimbali

Huduma hizi zinapatikana kupitia mawakala wa Mixx by Yas waliopo kote Tanzania.

Kwa wateja wenye simu janja, miamala inafanyika kwa urahisi kupitia Equity Mobile App, huku watumiaji wa simu za kawaida wakihudumiwa kupitia USSD code *150*07#.

Huduma hii imebeba kauli mbiu:

“Weka Pesa, Toa Pesa” – Equity Bank kwa kushirikiana na Mixx by Yas.


Kauli ya Uongozi

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Bi. Isabela Maganga, alisema:

Ushirikiano huu na Mixx by Yas una thamani ya kimkakati inayokwenda mbali zaidi ya utoaji wa huduma za kibenki. Ni hatua mahsusi ya kuwafikia wateja kwa urahisi zaidi, kupunguza umbali kati yao na huduma za benki, na kuwaletea huduma karibu na maeneo wanayoishi na kufanyia kazi.

 

Kupitia mtandao mpana wa mawakala wa Mixx by Yas, wateja hawatalazimika tena kusafiri umbali mrefu kufika matawi ya benki. Wanaweza kuweka na kutoa fedha kwa urahisi, gharama nafuu na usalama mkubwa kupitia mawakala wanaowaamini.”

Kwa mujibu wa benki hiyo, ushirikiano huu:

  • Unarahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wateja
  • Unafungua fursa mpya za kiuchumi kwa mawakala
  • Unaongeza mzunguko wa fedha katika uchumi wa ndani
  • Unachochea wananchi kushiriki kikamilifu katika mfumo rasmi wa kifedha


Kwa upande wake, Angelica Pesha, CEO wa Mixx by Yas, alisema:

Kwa kuunganisha uzoefu wa kibenki wa Equity na nguvu ya jukwaa la Mixx pamoja na mtandao mpana wa mawakala wetu, tunabadilisha vituo vya huduma vilivyo karibu na jamii kuwa milango kamili ya huduma za kibenki.

 

Kupitia ushirikiano huu, ikiwemo upanuzi wa huduma za utoaji fedha za kimataifa (IMT), tunaongeza upatikanaji, urahisi na uaminifu kwa mamilioni ya Watanzania. Kwa pamoja, tunajenga mfumo wa kifedha ulio jumuishi zaidi, unaounganishwa kidijitali na wenye kuwezesha uchumi wa taifa.”


Mwelekeo Mpya wa Sekta ya Kifedha

Ushirikiano kati ya Equity Bank Tanzania na Mixx by Yas unaakisi mwelekeo wa sekta ya kifedha wa kuunganisha huduma za benki na majukwaa ya kidijitali ili kuwafikia wateja kwa ukaribu zaidi.

BOLT YATOA UFAFANUZI KUHUSU MFUMO WA KAMISHENI NA PUNGUZO KWA MADEREVA TANZANIA

Meneja Mkuu wa Bolt Afrika Mashariki, Dimmy Kanyankole.

Dar es Salaam, Tanzania – Februari 16, 2026 – Kampuni inayoongoza kwa huduma za usafiri mtandao nchini, Bolt, imekutana na waandishi wa habari katika mkutano maalum na wa kina ili kutoa ufafanuzi kuhusu mfumo wake wa kamisheni na punguzo la nauli kwenye app, kufuatia maandamano ya hivi karibuni kutoka kwa baadhi ya madereva.

Akizungumza na vyombo vya habari, Meneja Mkuu wa Bolt Afrika Mashariki, Dimmy Kanyankole, alieleza kuwa madereva hawabebi gharama za punguzo wanazopewa abiria kupitia ofa za matangazo.

Alifafanua kuwa pale abiria anapopata punguzo — kwa mfano asilimia 40 — abiria hulipa kiasi kilichooneshwa kwenye programu, huku Bolt ikimrejeshea dereva sehemu ya fedha iliyopunguzwa mara baada ya safari kukamilika. Kwa utaratibu huo, dereva hupokea mapato yake kamili ya safari husika bila kuathiriwa na ofa yoyote inayoendelea.

Madereva ni mhimili wa jukwaa letu. Uwezo wao wa kupata kipato cha uhakika na endelevu ni msingi wa mafanikio yetu ya muda mrefu. Tumejizatiti kuendesha mfumo wenye haki na uwazi, unaolinda mapato ya madereva huku ukihakikisha huduma inabaki nafuu kwa abiria,” alisema Kanyankole, akisisitiza kuwa uwazi ni nguzo kuu ya uendeshaji wa kampuni hiyo.

Muundo wa Kamisheni na Ulinganifu wa Kikanuni

Kuhusu muundo wa kamisheni, kampuni ilieleza kuwa inatoza kamisheni ya asilimia 20 — kiwango kilicho ndani ya wigo wa asilimia 15 hadi 25 unaoruhusiwa na Land Transport Regulatory Authority (LATRA).

Aidha, Bolt hutoza ada ya kuhifadhi safari (booking fee) ya asilimia 2 pekee, ambayo huoneshwa wazi kwenye risiti ya kila safari inayokamilika. Licha ya madai ya baadhi ya waandamanaji kuwa kamisheni imeongezwa, kampuni imethibitisha kuwa kiwango cha asilimia 20 kimekuwa kikitumika kwa miaka kadhaa sasa.

NMB YATOA MISAADA YA SAMANI ZA SHULE YENYE THAMANI YA SH. MILIONI 21.6 WILAYANI MALINYI

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Sebastian Waryuba (wa pili kushoto), akionyesha ishara ya shukrani baada ya Benki ya NMB kukabidhi vifaa vya shule kwa wilaya hiyo vyenye thamani ya Sh. milioni 21.6 katika hafla iliyofanyika Shule ya Sekondari Kilosa Mpepo, mkoani Morogoro. Wa kwanza kutoka kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango; wengine ni wanafunzi wa shule hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Sebastian Waryuba (wa tatu kushoto), akikabidhiwa moja ya meza 100 na Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango (wa pili kulia), katika hafla ya benki hiyo ya kukabidhi vifaa vya shule wilayani Malinyi vyenye thamani ya Sh. milioni 21.6, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Kilosa Mpepo, mkoani Morogoro. Kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Malinyi, Anderson Lyatuu, na kushoto ni wawakilishi wa shule zilizonufaika na msaada huo.

Katika kuendeleza dhamira yake ya kurejesha kwa jamii na kuchochea maendeleo endelevu, NMB Bank Plc kupitia Programu yake ya Uwekezaji kwa Jamii (CSR), imekabidhi misaada ya madawati 100, viti 100 na meza 100 kwa shule mbili za msingi na moja ya sekondari wilayani Malinyi, mkoani Morogoro. Misaada hiyo ina thamani ya Shilingi Milioni 21.6.

Hatua hiyo ni sehemu ya Shilingi Bilioni 7.4 zilizotengwa na benki hiyo kwa mwaka 2026 kwa ajili ya miradi ya kijamii katika sekta za Elimu, Afya na Mazingira — sawa na asilimia moja ya Faida Baada ya Kodi kwa mwaka wa fedha ulioishia Desemba 31, 2025.

Mgao wa Misaada kwa Shule Husika

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Kilosa Mpepo, Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Bi. Janeth Shango, alisema:

  • Shule ya Msingi Madibila Chini imepokea madawati 50
  • Shule ya Msingi Salamiti imepokea madawati 50
  • Shule ya Sekondari Kilosa Mpepo imepokea viti 100 na meza 100 kwa ajili ya wanafunzi

Bi. Shango alikabidhi misaada hiyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Mhe. Sebastian Waryuba, aliyepokea kwa niaba ya walimu wakuu wa shule hizo.

Alisisitiza kuwa msaada huo ni uthibitisho wa ushiriki wa benki katika maendeleo ya kijamii, akieleza kuwa kupitia uwekezaji huo, NMB inaendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya elimu nchini.

Thursday, 19 February 2026

STANBIC BANK AND UWEZO LAUNCH 45 SCHOOL LIBRARIES TO BOOST FOUNDATIONAL LEARNING IN LUDEWA

Senior Manager for External Affairs, Communication and Reputation at Stanbic Bank Tanzania, Dickson Senzi (right), and Uwezo Tanzania Executive Director, Baraka Mgohamwende (left), jointly handed over books funded by Stanbic Bank to Ludewa District Executive Director, Sunday Deogratius, for the establishment of 45 school libraries in primary schools across Ludewa District. The brief ceremony was held in Dar es Salaam.

In a major step toward strengthening foundational education in Tanzania, Stanbic Bank Tanzania has partnered with Uwezo Tanzania to launch a transformative library programme that will establish 45 school libraries across primary schools in Ludewa District, Njombe Region.

The initiative is expected to benefit an estimated 33,619 children every year, equipping young learners with the tools they need to master literacy and numeracy at the most critical stage of their academic journey.


Strengthening the Foundations of Learning

At the heart of the programme is a simple but powerful belief: Reading, Writing, and Arithmetic (RWA) form the bedrock of a child’s entire education journey.

When children acquire these foundational skills early, they move confidently through school. Without them, they risk falling behind from the very beginning.

The libraries will be stocked with:

  • Curriculum-aligned learning materials
  • Age-appropriate literacy and numeracy books
  • Storytelling and extracurricular reading materials

The goal is to improve classroom engagement while also encouraging reading at home — creating a culture of learning that extends beyond school walls.


Aligned with National Education Priorities

This initiative directly supports the National Scientific Strategy for Building Reading, Writing, and Arithmetic (RWA) Proficiency, launched in January 2026 by H.E. Samia Suluhu Hassan, President of the Tanzania.

Implementation will follow Uwezo Tanzania’s My Village (Kijiji Changu) model, a community-based approach that promotes:

  • Village-level library access
  • Active parental engagement
  • Community ownership of learning outcomes

By embedding libraries within schools while encouraging family participation, the programme ensures education becomes a shared responsibility.


Phase I: Investing in Human Capital

Under Phase I, Stanbic Bank Tanzania is funding the acquisition of curriculum-aligned and storytelling books designed to increase learner engagement both in classrooms and at home.

According to Dickson Senzi, Senior Manager for External Affairs, Communication and Reputation at Stanbic Bank Tanzania:

This partnership reflects Stanbic Bank’s commitment to investing in human capital in line with Tanzania’s Vision 2050. By expanding access to quality learning resources in underserved communities, we are strengthening the foundation for a skilled, productive and innovative generation capable of driving inclusive national growth. Tanzania is our home, and we are committed to driving her growth.”

BOLT CLARIFIES COMMISSION STRUCTURE AND DISCOUNT POLICY AMID DRIVER CONCERNS

Dimmy Kanyankole, Senior General Manager of Bolt East Africa.

Dar es Salaam, Tanzania – February 16, 2026 – Bolt, one of Tanzania’s leading ride-hailing platforms, has held a detailed press conference in Dar es Salaam to clarify how commissions and ride discounts operate on its platform.

The briefing comes in response to recent unrest among members of the driver community, with concerns raised over promotional discounts and commission rates.

Drivers Do Not Bear the Cost of Discounts

Speaking to journalists, Dimmy Kanyankole, Senior General Manager of Bolt East Africa, emphasized that drivers do not absorb the cost of passenger discounts.

He explained that when a rider receives a promotional offer — for example, 40 percent off a trip — the passenger pays the reduced fare shown in the app. Bolt then reimburses the discounted portion directly to the driver after the trip is completed.

This structure ensures that drivers receive their full trip earnings, regardless of any active promotions.

Drivers are at the heart of our platform. Their ability to earn reliably and sustainably is fundamental to our long-term success. We are committed to maintaining a fair and transparent system that balances affordability for riders with income protection for drivers,” said Kanyankole.

The company reiterated that transparency remains central to its operations.

Commission Structure Explained

Bolt also addressed concerns regarding its commission rates, firmly stating that it charges a 20 percent commission — a rate it says is lower than that of other major competitors operating in Tanzania.

According to the company, the commission framework aligns with guidelines set by the Land Transport Regulatory Authority (LATRA), which permit ride-hailing companies to charge commissions within a range of 15 to 25 percent.

Bolt’s structure is as follows:

  • 20% commission per trip
  • 2% booking fee
  • Full breakdown reflected in every trip receipt accessible to drivers

Wednesday, 18 February 2026

BANKING STOCKS POWER MARKET RALLY AT THE DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE

Dar es Salaam, 16 February 2026 – Equity markets closed the week on a strong note as banking stocks led a broad-based rally on the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE), underscoring renewed investor confidence in the financial sector.

Indices Post Strong Gains

The DSE’s key indices recorded solid advances:

  • DSEI rose by 5.9% to close at 3,756.82 points
  • TSI gained 7.19% to 8,421.38 points
  • The Bank, Finance & Investment Index climbed an impressive 10.06% to 18,066.11 points

The parallel appreciation of both the DSEI and TSI suggests that the rally was not confined to a handful of counters but reflected broader market participation.

Market analysts noted that the upward momentum was largely driven by sustained demand for tier-one banking stocks.


Banking Counters Take Centre Stage

Performance was led by:

  • CRDB Bank Plc
  • NMB Bank Plc
  • Maendeleo Bank Plc (MCB)
  • Mkombozi Commercial Bank Plc (MKCB)
  • Mwalimu Commercial Bank Plc (MBP)

Among the standout performers:

  • MCB surged 46.46% to 930/-
  • MKCB jumped 43.51% to 5,310/-
  • MBP rose 40.49% to 2,290/-
  • NMB gained 10.22%, closing at 12,730/-

The rally was supported by strong earnings sentiment, particularly following NMB’s recently announced pre-tax profit performance. Analysts note that robust profitability across tier-one banks has reinforced investor appetite for banking counters.

EQUITY BANK TAKES BANKING CLOSER TO THE PEOPLE THROUGH MIXX BY YAS AGENT NETWORK

Dar es Salaam, 17 February 2026 – In a major boost to financial inclusion, Equity Bank Tanzania has announced a strategic partnership with Mixx by Yas aimed at bringing banking services closer to millions of Tanzanians through the extensive nationwide network of Mixx agents.

The collaboration marks a significant step in expanding access to convenient, secure, and reliable financial services across both urban and rural communities.


Bringing Banking Closer to the People

Through this partnership, Equity Bank customers can now:

  • Deposit money directly into their Equity accounts (Cash-In)
  • Withdraw cash for personal and business needs (Cash-Out)

These services are available at Mixx by Yas agents located across Tanzania, eliminating the need for customers to travel long distances to bank branches.

Customers can transact using:

  • 📱 Equity Mobile App (for smartphone users)
  • 📞 USSD Code *150*07# (for basic phone users)

All transactions are conducted securely under the banner:

“Equity Bank – Deposit Cash, Withdraw Cash with Mixx by Yas.”



Leadership Perspective: A Strategic Move for Inclusion

Speaking during the launch, the Managing Director of Equity Bank Tanzania, Ms. Isabela Maganga, emphasized the broader impact of the partnership:

“This partnership with Mixx by Yas holds strategic value that extends far beyond the provision of banking services. It is a concrete step to enhance our services by reaching customers conveniently and reducing the distance between customers and banking services by bringing services closer to where they live and work.”

She noted that through the widespread Mixx by Yas agent network:

  • Customers will no longer need to travel long distances.
  • Banking services will be accessible easily, affordably, and securely.
  • Communities will benefit from stronger money circulation within the local economy.

“Our vision is to make banking services a part of everyday life, and this step is crucial in achieving that mission.”

 


Transforming Community Agents into Financial Gateways

On her part, Mixx by Yas CEO Ms. Angelica Pesha highlighted how the partnership transforms agent outlets into full-service financial access points:

“By combining Equity's banking expertise with the strength of the Mixx platform and our extensive agent network, we are transforming community-based service points into comprehensive gateways for banking services.”

She further noted that the collaboration will:

  • Expand International Money Transfer (IMT) services
  • Increase accessibility and convenience
  • Strengthen reliability for millions of Tanzanians
  • Accelerate digital financial integration nationwide

Tuesday, 17 February 2026

BENKI YA EXIM YATANGAZA WASHINDI WA KAMPENI YA ‘CHANJA KIJANJA, DILI NDIO HILI’

Dar es Salaam, Februari 16, 2026 – Exim Bank Tanzania imehitimisha kampeni yake ya ‘Chanja Kijanja, Dili Ndio Hili’ kwa hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi, iliyofanyika katika tawi jipya la Ubungo.

Kampeni hiyo ya miezi miwili ililenga kuhamasisha matumizi ya kadi za benki katika malipo ya kila siku na kukuza utamaduni wa miamala ya kidijitali isiyotumia fedha taslimu.


🏆 Washindi Wakuu

Katika droo ya mwisho:

  • Asif K. Dhalla – Shilingi milioni 15 (Zawadi Kuu)
  • Aliakber Zoeb Hakimjee – Shilingi milioni 10 (Mshindi wa Pili)
  • John Estomih Kweka – Shilingi milioni 5 (Mshindi wa Tatu)

AIR FRANCE-KLM WAWEKEZA KATIKA NDOTO ZA MAMA VIJANA

Meneja Mkaazi wa Air France–KLM nchini Tanzania, Rajat Kumar (kulia), akikabidhi moja ya mashine za kushonea kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Forward Motion (FOMO), Vivian Sirikwa, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo. Kushoto ni Meneja wa Air France–KLM Ukanda wa Afrika Mashariki, Viyalrth Abbas.

Katika jamii nyingi, kuwa mama katika umri mdogo huambatana na changamoto kubwa—kutengwa kijamii, ukosefu wa kipato na kukatizwa kwa masomo. Hata hivyo, kupitia ushirikiano kati ya Air France–KLM Group na Forward Motion (FOMO), zaidi ya mama vijana 20 nchini Tanzania sasa wana sababu mpya ya kutazama kesho kwa matumaini.

Kupitia mchango wa mashine 15 za kushona, programu ya mafunzo ya ushonaji ya FOMO imepata nguvu mpya. Huu si msaada wa vifaa pekee—ni uwekezaji katika ujuzi na mustakabali wa maisha. Mafunzo ya ushonaji yanawawezesha washiriki kujenga stadi za vitendo zinazofungua milango ya ajira binafsi, ubunifu wa bidhaa na hatimaye kipato cha kujitegemea.

Wawakilishi wa Air France–KLM Group hawakukabidhi tu mashine hizo; walitumia muda wao kuzungumza na mama vijana hao, wakitoa ushauri na kuwatia moyo. Kwa wengi wao, ujumbe kwamba wanathaminiwa na kuaminiwa ulikuwa na uzito mkubwa sawa na msaada wa kifaa chenyewe. Hii ni ishara kuwa uwekezaji wa kweli hauishii kwenye rasilimali, bali pia kwenye mahusiano na kujenga kujiamini.

AKIBA COMMERCIAL BANK PARTNERS WITH THE MEDIA TO ADVANCE FINANCIAL EDUCATION & INCLUSION

Dar es Salaam; 16th February 2026 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) has strengthened its collaboration with media stakeholders as part of its ongoing commitment to promoting financial education and accelerating financial inclusion across Tanzania.

Recognizing the media as a vital bridge between financial institutions and the public, the Bank underscored the important role journalists and media houses play in amplifying financial literacy messages. Through print, broadcast, and digital platforms, the media have the reach and influence to simplify complex financial concepts, helping individuals and businesses make informed financial decisions.

Speaking during the engagement session, Dora Saria, Head of Marketing and Communications at ACB, emphasized that financial education remains a strategic priority for the Bank. She noted that the initiative is designed to empower communities with practical knowledge on savings, responsible borrowing, digital financial services, investment opportunities, and sound financial management practices.

According to Saria, promoting responsible financial service provision and encouraging prudent use of financial products are central to ACB’s mission of supporting economic wellbeing and strengthening long-term financial resilience.

She further highlighted that an informed public is better positioned to utilize financial services responsibly, manage risks effectively, and contribute meaningfully to national economic growth. As Tanzania’s financial landscape continues to evolve—particularly with the rapid adoption of digital financial services—the demand for accessible, accurate, and consistent financial education has become increasingly critical.

NMB YAITANGAZA SEKTA YA MADINI YA TANZANIA KATIKA MINING INDABA 2026, AFRIKA KUSINI

Wajumbe kutoka Benki ya NMB wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde (wa tatu kushoto), pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. James Bwana (wa nne kushoto), wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji katika Mnyororo wa Thamani wa Madini Tanzania lililofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini.
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, akizungumza wakati wa Kongamano la Uwekezaji katika Mnyororo wa Thamani wa Madini Tanzania, lililoandaliwa na Breakthrough Attorneys kwa ushirikiano na Benki ya NMB.

Benki ya NMB imewakilisha kikamilifu Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya uwekezaji wa madini ya Mining Indaba 2026, yaliyofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini kuanzia Februari 8 hadi 11, 2026.

Kupitia maafisa wake waandamizi, wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Makampuni, Bw. Nelson Karawa, pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mauzo – Idara ya Hazina, Bw. Jeremiah Lyimo, NMB ilitumia jukwaa hilo kuitangaza Tanzania na sekta yake ya madini mbele ya wawekezaji wa kimataifa.

Katika maonesho hayo, NMB ilisisitiza nafasi ya Tanzania kama moja ya nchi zenye rasilimali nyingi za madini na fursa lukuki za uwekezaji barani Afrika, huku ikiweka bayana utayari wa sekta ya fedha nchini kuunga mkono miradi mikubwa ya kimkakati.

Kuonesha Uwezo wa Kifedha na Uzoefu wa Kibenki

Sambamba na ushiriki wake katika mikutano na makongamano ya kimataifa, NMB ilieleza mchango wake katika maendeleo ya sekta ya madini nchini na utayari wake wa kushiriki katika kufadhili miradi mikubwa kupitia suluhisho bunifu za kifedha.

Katika kongamano hilo, Bw. Lyimo alieleza kuwa NMB ina uwezo mkubwa wa kifedha, uzoefu wa kusimamia mikataba mikubwa, pamoja na mtandao mpana wa ndani na nje ya nchi unaowezesha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya madini. Alisisitiza pia nafasi muhimu ya benki katika kuunganisha rasilimali za ndani na kimataifa ili kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa.

Monday, 16 February 2026

TANZANIA’S MINING GROWTH ENTERS A DECISIVE EXECUTION PHASE

Dar es Salaam, Tanzania – 16 February 2026

Tanzania’s mining sector is entering a more decisive phase of growth — one increasingly defined by execution, infrastructure readiness, and access to long-term capital. As the country positions itself for sustained value creation, attention is shifting from opportunity-driven expansion toward disciplined delivery and long-term investment alignment.

Mining now contributes approximately 10 percent of Tanzania’s Gross Domestic Product (GDP), a significant rise from just 4 percent in 2007. The sector has also become the country’s second-largest foreign exchange earner after tourism, underlining its growing strategic importance to the national economy.

Gold continues to anchor the industry, with leading producers recording a combined output of around 335,000 ounces by the third quarter of 2025.

As the curtains close on Mining Indaba 2026 in Cape Town, Tanzania’s trajectory is drawing attention as an example of how mining jurisdictions are transitioning from exploration-led growth to execution-focused development.

The conversation around mining has evolved,” said Elias Ngunangwa, Head of Client Coverage for Corporate and Investment Banking at Stanbic Bank Tanzania. “The focus today is on whether projects can be delivered efficiently, supported by the right infrastructure, financing structures and operating environment.”


Infrastructure and Energy Shape Competitiveness

Infrastructure and energy reliability are increasingly central to mining competitiveness.

Ongoing investments in transport corridors — including roads and rail networks — are improving the movement of minerals, consumables, and heavy equipment. At the same time, stronger power connectivity is reducing operational uncertainty across mining operations.

More mining companies are now connecting to the national electricity grid, lowering dependence on diesel-powered generation and stabilising operating costs. For investors, these developments significantly influence how project risk and long-term viability are assessed.

Infrastructure and power are no longer background considerations,” Ngunangwa noted. “They directly affect timelines, costs and the ability of mining projects to move from development into steady production.”


Financing Across the Mining Value Chain

As the sector matures, financing needs are also evolving. Capital is no longer required solely for mine development, but across the broader mining ecosystem that sustains operations.

According to Edgar Mwasha, Vice President, Diversified Industries at Stanbic Bank Tanzania, sustainable growth depends on financing models that reflect operational realities.

Mining functions as an ecosystem,” Mwasha said. “Beyond extraction, there are suppliers, contractors, logistics providers and service companies that need access to capital to keep operations running smoothly. Financing must support that full chain if growth is to be sustained.”

SERENGETI PREMIUM APPLE YAONGOZA SHAMRASHAMRA ZA SIKU YA VALENTINE JIJINI DAR ES SALAAM

Serengeti Breweries Limited (SBL) imeendelea kuimarisha mkakati wake wa ubunifu kupitia uzinduzi na uendelezaji wa Serengeti Premium Apple — kinywaji chake kipya kilichotengenezwa hapa hapa Tanzania — kwa kuongoza shamrashamra za Siku ya Valentine kupitia matukio maalum jijini Dar es Salaam.

Ikiwa imelenga kuwashirikisha zaidi wateja na watumiaji wake kupitia uzoefu wa moja kwa moja (experiential marketing), chapa hiyo iliendesha mfululizo wa hafla katika maeneo mbalimbali ya jiji, ikilenga makundi tofauti ya walaji na mitindo yao ya maisha.

Galentine’s Johari Rotana: Urafiki, Mafanikio na Ubunifu wa Kitanzania

Tukio kuu lilikuwa Galentine’s iliyofanyika katika hoteli ya Johari Rotana, likiwaleta pamoja wateja, washirika na wageni waalikwa kusherehekea urafiki, mafanikio na ujio wa kinywaji kipya chenye hadhi ya juu kinachoendana na maisha ya kisasa.

Kupitia hafla hiyo, Serengeti Premium Apple iliimarisha nafasi yake kama ubunifu wa Kitanzania unaokidhi mahitaji yanayobadilika ya walaji — hasa kizazi cha vijana wanaothamini ubora, muonekano na uzoefu wa kipekee wa chapa.

Balozi wa kinywaji hicho, Flaviana Matata, alihudhuria hafla hiyo, akiongeza mvuto wa chapa na kuimarisha uhusiano kati ya bidhaa na wateja wake. Uwepo wake uliendana na taswira ya kinywaji hicho kama alama ya kujiamini, mafanikio na mtindo wa kisasa.

Upanuzi wa Uzoefu: Upper Deck, Serena na Zaidi

Mkakati huo uliendelea kupitia matukio mengine kama Galentine’s Brunch iliyofanyika katika mgahawa wa The Upper Deck Gastro Pub, pamoja na ushirikiano maalum wa Bravo Coco na Serena Hotel Dar es Salaam — yote yakiongozwa na Serengeti Premium Apple kama chapa kinara.

Jumapili, tukio la Big Brunch lililofanyika katika Ramada Resort Dar es Salaam liliongozwa na kinywaji cha Serengeti Lemon, likionyesha upana wa bidhaa za SBL katika kuendana na ladha na mitindo tofauti ya walaji.

Wakati huo huo, Smirnoff Ice iliwafikia wale waliokuwa bado ‘single’ kupitia tukio la “Valentine’s Is a Vibe – Singles Rave.” Chapa nyingine zikiwemo The Singleton na Gordon's Gin nazo ziliongeza nguvu katika kuwapatia wateja burudani na vibe la kipekee katika matukio ya wikiendi hiyo.

Saturday, 14 February 2026

STRENGTHENING TANZANIA’S FINANCIAL MARKETS: KEY INSIGHTS FROM THE AFMI 2025 REPORT

By Irene Rwegalulira, Director of Global Markets, Absa Bank Tanzania

The recent launch of the Absa Africa Financial Markets Index 2025 (AFMI) in Dar es Salaam provided an important opportunity to reflect on Tanzania’s progress in developing its financial markets — and to assess where further reforms can accelerate growth.

For nine years, the AFMI has become one of Africa’s most respected tools for evaluating financial market development across the continent. Beyond ranking countries, the Index offers policymakers, regulators and financial institutions a data-driven framework to understand what is working well, where gaps remain, and which reforms can deliver the greatest impact.

The 2025 report shows that Tanzania continues to move forward steadily. While important foundations are firmly in place, the findings also highlight opportunities to deepen and broaden the market further.


A Strong Foundation of Stability and Transparency

One of the most encouraging findings in this year’s report is Tanzania’s continued strength in macroeconomic stability. The country has benefited from steady and predictable monetary policy, low and stable inflation, and increasingly transparent communication from policymakers.

These elements are critical in building investor confidence. Stability reduces uncertainty, supports long-term planning, and creates a reliable environment for both businesses and households.

The report also reflects ongoing improvements in market infrastructure and the regulatory framework. Efforts to strengthen governance, align regulatory standards with international best practice, and enhance transparency across key segments of the financial system are beginning to yield measurable results.

This progress is not accidental. It reflects sustained commitment from policymakers and regulators to build a credible, resilient and investable financial ecosystem.


Growing Market Depth and Product Diversification

The AFMI 2025 further highlights gradual but meaningful advances in market depth. Tanzania’s financial markets are becoming more diversified, with a broader range of instruments and increased use of capital market solutions.

While bank financing remains dominant, the expanding role of bonds, structured products and risk management tools signals a shift toward a more balanced financial system.

TZS 500 MILLION FINANCING WINDOW OPENS FOR YOUTH UNDER CRDB BANK'S GO GREEN WITH IMBEJU

Dodoma, February 12, 2026 – The Minister of State, President’s Office – Planning and Investment, Hon. Prof. Kitila Mkumbo, has commended CRDB Bank Foundation and CRDB Bank for launching the Go Green with IMBEJU programme, describing it as a strategic initiative that directly aligns the Government’s green economy agenda with youth empowerment.

Speaking during the launch event held at the Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC), Prof. Mkumbo said the programme is fully aligned with Tanzania’s National Development Vision 2050, which emphasizes building an inclusive, competitive, and climate-resilient economy while positioning youth at the centre of national transformation.

The Government has placed strong emphasis on empowering youth economically, promoting a green economy, and strengthening collaboration between the public and private sectors. Youth-led environmental projects like the ones we see today are a direct and practical implementation of Vision 2050,” said Prof. Mkumbo.

 

He underscored that private sector participation remains a critical pillar in transforming young people’s innovative ideas into sustainable enterprises that create jobs and contribute meaningfully to national development.


Parliament Backs Green Economy Framework

The Deputy Speaker of the National Assembly of the United Republic of Tanzania, Hon. Daniel Sillo, noted that Parliament has laid a strong legal foundation to support environmental protection and the growth of the green economy.

He described the programme as a practical example of aligning policy direction, financial capital, and youth innovation to deliver tangible development outcomes.


Financing Youth Innovation in Key Green Sectors

The Go Green with IMBEJU programme is designed to support youth-led innovative projects across key sectors, including:

  • Climate-smart agriculture
  • Renewable and clean energy
  • Water technologies
  • Waste management
  • Environmental conservation
  • Digital innovation

Under the initiative, young entrepreneurs will access affordable financing ranging from TZS 500,000 to TZS 500 million, depending on the size and scale of their projects.


Bridging International Climate Finance and Youth Innovation

Speaking at the event, CRDB Bank Managing Director, Abdulmajid Nsekela, said the programme acts as a bridge between international climate finance and innovative young entrepreneurs who often lack collateral or formal credit history required under traditional banking systems.

Through Go Green with IMBEJU, we believe more young people will be reached, prepared, and empowered to actively participate in the green economy. This is a strategic linkage between international climate finance and the innovation of Tanzanian youth,” said Nsekela.

BENKI YA NMB YADHAMINI TRI-NATIONS LIVESTOCK EXPO KWA SHILINGI MILIONI 300

Mkurugenzi wa Mbogo Ranches, Naweed Bulla (kushoto), akipokea mfano wa hundi ya Sh. milioni 300 kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa NMB Bank Plc, Nsolo Mlozi (kulia), mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Fabian Madele (katikati). Udhamini huu ni wa miaka mitatu kwa ajili ya maonesho ya Tri-Nations Livestock Expo (2026–2028).

Katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kukuza sekta ya mifugo na kuimarisha uchumi wa kilimo, NMB Bank Plc imesaini makubaliano ya udhamini wa miaka mitatu kwa ajili ya Maonesho ya Kimataifa ya Mifugo – Tri-Nations Livestock Expo – kwa thamani ya Shilingi milioni 300.

Maonesho hayo yatakayoshirikisha wafugaji na wadau kutoka Tanzania, Kenya na Namibia, hufanyika kila mwaka. Kwa mwaka huu, yatafanyika kuanzia Juni 19 hadi 21 katika eneo la Ubena Zomozi, Chalinze mkoani Pwani.


Uwekezaji wa Kimkakati katika Sekta ya Ufugaji

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa makubaliano hayo, Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa NMB, Nsolo Mlozi, alisema benki hiyo inajivunia mafanikio ya maonesho ya miaka ya 2024 na 2025, yaliyochochea uamuzi wa kuingia katika mkataba mpya wa muda mrefu aliouita uwekezaji wa kimkakati.

Mkataba huu ni uwekezaji wa kimkakati unaolenga kukuza sekta ya ufugaji na kuboresha maisha ya Watanzania wanaojihusisha na sekta ya kilimo — mnyororo wa thamani unaojumuisha kilimo, uvuvi na ufugaji,” alisema Mlozi.

Alibainisha kuwa hadi kufikia mwaka 2025, NMB ilikuwa imekopesha zaidi ya Shilingi bilioni 100 katika sekta hiyo, hatua inayodhihirisha dhamira ya benki hiyo katika kuchochea maendeleo ya kilimo na mifugo nchini.


Serikali Yaunga Mkono Ushirikiano

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mbogo Ranches, Naweed Bulla, aliishukuru NMB kwa kukubali kudhamini maonesho hayo kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa mchango huo utaongeza hadhi na wigo wa maonesho kimataifa.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Fabian Madele, aliipongeza NMB kwa kuendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuendeleza maonesho hayo, akiahidi kuwa Serikali itaendelea kuyaunga mkono katika kipindi chote cha miaka mitatu ya mkataba huo.


Jukwaa la Ushirikiano, Ubunifu na Biashara

Maonesho ya Tri-Nations Livestock Expo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la ushirikiano, ubunifu na biashara kwa wafugaji na wadau wa mnyororo mzima wa thamani. Kupitia maonesho hayo, washiriki hupata:

  • Mbinu bora za ufugaji
  • Elimu kuhusu bima na huduma za kifedha
  • Fursa za mikopo na uwezeshaji
  • Uunganishwaji na masoko ya kitaifa na kimataifa

Udhamini wa NMB kwa kipindi cha miaka mitatu unaashiria kuimarika kwa ushirikiano kati ya sekta ya fedha, sekta binafsi na Serikali katika kukuza uchumi wa mifugo — moja ya nguzo muhimu za maendeleo ya Tanzania.

Friday, 13 February 2026

CRDB BANK FOUNDATION YAZINDUA "GO GREEN NA IMBEJU", VIJANA KUPATA MITAJI HADI SH. MIL. 500

Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati), akiwa na viongozi wengine wa Serikali, Bunge na Benki ya CRDB, wakipata maelezo kutoka kwa mwanzilishi wa kampuni ya Aquafresh iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana, wakati wa hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati), akipokelewa na kikundi cha ngoma za asili wakati alipowasili katika uzinduzi wa programu ya Go Green na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Wengine pichani ni, kushoto kwake, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo; Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori; na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.

Dodoma, 12 Februari 2026 – Waziri wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo, ameipongeza CRDB Bank Foundation na Benki ya CRDB kwa kuanzisha programu ya Go Green na IMBEJU, akisema ni hatua ya kimkakati inayounganisha ajenda ya Serikali ya uchumi wa kijani na uwezeshaji wa vijana.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma, Prof. Mkumbo alisema mpango huo unaendana kikamilifu na Dira ya Taifa 2050, ambayo imeweka mkazo katika uchumi jumuishi, shindani na himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi huku ikitambua vijana kama msingi wa mafanikio ya Taifa.

Serikali imeweka mkazo mkubwa katika kuwawezesha vijana kiuchumi, kukuza uchumi wa kijani na kujenga mifumo imara ya ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi. Miradi ya vijana inayolinda mazingira kama tunavyoiona leo ni utekelezaji wa moja kwa moja wa Dira ya Taifa 2050 kwa vitendo,” alisema Prof. Mkumbo.

Alisisitiza kuwa ushiriki wa sekta binafsi ni nguzo muhimu katika kuhakikisha mawazo bunifu ya vijana yanageuzwa kuwa biashara endelevu zenye ajira na tija kwa Taifa.


Mitaji Nafuu Kuanzia Shilingi 500,000 hadi Milioni 500

Programu ya Go Green na IMBEJU inalenga kuwawezesha vijana wenye miradi bunifu inayohusiana na:

  • Kilimo himilivu
  • Nishati safi na jadidifu
  • Teknolojia za maji
  • Usimamizi wa taka
  • Uhifadhi wa mazingira
  • Ubunifu wa kidijitali

Kupitia dirisha hili, vijana wanaweza kupata mitaji nafuu kuanzia Shilingi 500,000 hadi Shilingi milioni 500, kulingana na ukubwa na mahitaji ya mradi.


Daraja Kati ya Fedha za Tabianchi na Ubunifu wa Vijana

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema mpango huo ni daraja kati ya fedha za kimataifa za tabianchi na vijana wabunifu ambao mara nyingi hukosa dhamana au historia ya mikopo inayohitajika katika mifumo ya kawaida ya kifedha.

Kupitia Go Green na IMBEJU tunaamini vijana wengi zaidi watafikiwa, kuandaliwa na kuwezeshwa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kijani. Huu ni muunganiko wa kimkakati kati ya ufadhili wa kimataifa wa tabianchi na ubunifu wa vijana wa Tanzania,” alisema Nsekela.

BENKI YA EXIM YAONGEZA MCHANGO KWA SEKTA YA UTALII KAMA MDHAMINI MKUU WA Z-SUMMIT 2026

Zanzibar | 11 Februari 2026

Benki ya Exim Tanzania imedhihirisha tena dhamira yake ya muda mrefu katika kuchochea ukuaji na ustawi wa sekta ya utalii kwa kudhamini Z-Summit 2026 kama Mdhamini Mkuu. Hafla hiyo imefanyika tarehe 11–12 Februari 2026 katika Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), Tunguu.

Huu ni mwaka wa nne mfululizo kwa benki hiyo kudhamini mkutano huu tangu kuanzishwa kwake.


Jukwaa Muhimu la Biashara na Uwekezaji

Z-Summit imejipatia umaarufu kama jukwaa kuu la biashara na uwekezaji katika utalii Zanzibar. Hukutanisha wawekezaji wa utalii, waendeshaji wa watalii, wamiliki wa hoteli, mawakala wa usafiri, watunga sera na watoa huduma kutoka Tanzania, Afrika Mashariki na mataifa mengine duniani.

Mkutano huu una mchango mkubwa katika:

  • Kujenga ushirikiano wa kimkakati
  • Kufungua fursa mpya za uwekezaji
  • Kuweka mwelekeo wa maendeleo endelevu ya utalii Zanzibar


Suluhisho za Kifedha kwa Sekta ya Utalii

Mbali na akaunti maalum kwa waendeshaji wa watalii na huduma za bima, Benki ya Exim imeendelea kubuni suluhisho za kisasa za malipo ya kidijitali.

Benki hii ilikuwa ya kwanza nchini kuzindua Kadi ya Exim TANAPA, inayowawezesha waendeshaji wa watalii kufanya malipo ya kielektroniki kwa viingilio vya hifadhi na huduma nyingine kupitia Tanzania National Parks Authority (TANAPA).