Foreign Exchange Rates

Equity Bank Advert_12 February 2026

CRDB Bank Advert_070325

Global Sanctions Compliance Masterclass

Tuesday, 17 February 2026

BENKI YA EXIM YATANGAZA WASHINDI WA KAMPENI YA ‘CHANJA KIJANJA, DILI NDIO HILI’

Dar es Salaam, Februari 16, 2026 – Exim Bank Tanzania imehitimisha kampeni yake ya ‘Chanja Kijanja, Dili Ndio Hili’ kwa hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi, iliyofanyika katika tawi jipya la Ubungo.

Kampeni hiyo ya miezi miwili ililenga kuhamasisha matumizi ya kadi za benki katika malipo ya kila siku na kukuza utamaduni wa miamala ya kidijitali isiyotumia fedha taslimu.


🏆 Washindi Wakuu

Katika droo ya mwisho:

  • Asif K. Dhalla – Shilingi milioni 15 (Zawadi Kuu)
  • Aliakber Zoeb Hakimjee – Shilingi milioni 10 (Mshindi wa Pili)
  • John Estomih Kweka – Shilingi milioni 5 (Mshindi wa Tatu)

AIR FRANCE-KLM WAWEKEZA KATIKA NDOTO ZA MAMA VIJANA

Meneja Mkaazi wa Air France–KLM nchini Tanzania, Rajat Kumar (kulia), akikabidhi moja ya mashine za kushonea kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Forward Motion (FOMO), Vivian Sirikwa, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo. Kushoto ni Meneja wa Air France–KLM Ukanda wa Afrika Mashariki, Viyalrth Abbas.

Katika jamii nyingi, kuwa mama katika umri mdogo huambatana na changamoto kubwa—kutengwa kijamii, ukosefu wa kipato na kukatizwa kwa masomo. Hata hivyo, kupitia ushirikiano kati ya Air France–KLM Group na Forward Motion (FOMO), zaidi ya mama vijana 20 nchini Tanzania sasa wana sababu mpya ya kutazama kesho kwa matumaini.

Kupitia mchango wa mashine 15 za kushona, programu ya mafunzo ya ushonaji ya FOMO imepata nguvu mpya. Huu si msaada wa vifaa pekee—ni uwekezaji katika ujuzi na mustakabali wa maisha. Mafunzo ya ushonaji yanawawezesha washiriki kujenga stadi za vitendo zinazofungua milango ya ajira binafsi, ubunifu wa bidhaa na hatimaye kipato cha kujitegemea.

Wawakilishi wa Air France–KLM Group hawakukabidhi tu mashine hizo; walitumia muda wao kuzungumza na mama vijana hao, wakitoa ushauri na kuwatia moyo. Kwa wengi wao, ujumbe kwamba wanathaminiwa na kuaminiwa ulikuwa na uzito mkubwa sawa na msaada wa kifaa chenyewe. Hii ni ishara kuwa uwekezaji wa kweli hauishii kwenye rasilimali, bali pia kwenye mahusiano na kujenga kujiamini.

AKIBA COMMERCIAL BANK PARTNERS WITH THE MEDIA TO ADVANCE FINANCIAL EDUCATION & INCLUSION

Dar es Salaam; 16th February 2026 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) has strengthened its collaboration with media stakeholders as part of its ongoing commitment to promoting financial education and accelerating financial inclusion across Tanzania.

Recognizing the media as a vital bridge between financial institutions and the public, the Bank underscored the important role journalists and media houses play in amplifying financial literacy messages. Through print, broadcast, and digital platforms, the media have the reach and influence to simplify complex financial concepts, helping individuals and businesses make informed financial decisions.

Speaking during the engagement session, Dora Saria, Head of Marketing and Communications at ACB, emphasized that financial education remains a strategic priority for the Bank. She noted that the initiative is designed to empower communities with practical knowledge on savings, responsible borrowing, digital financial services, investment opportunities, and sound financial management practices.

According to Saria, promoting responsible financial service provision and encouraging prudent use of financial products are central to ACB’s mission of supporting economic wellbeing and strengthening long-term financial resilience.

She further highlighted that an informed public is better positioned to utilize financial services responsibly, manage risks effectively, and contribute meaningfully to national economic growth. As Tanzania’s financial landscape continues to evolve—particularly with the rapid adoption of digital financial services—the demand for accessible, accurate, and consistent financial education has become increasingly critical.

NMB YAITANGAZA SEKTA YA MADINI YA TANZANIA KATIKA MINING INDABA 2026, AFRIKA KUSINI

Wajumbe kutoka Benki ya NMB wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde (wa tatu kushoto), pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. James Bwana (wa nne kushoto), wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji katika Mnyororo wa Thamani wa Madini Tanzania lililofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini.
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, akizungumza wakati wa Kongamano la Uwekezaji katika Mnyororo wa Thamani wa Madini Tanzania, lililoandaliwa na Breakthrough Attorneys kwa ushirikiano na Benki ya NMB.

Benki ya NMB imewakilisha kikamilifu Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya uwekezaji wa madini ya Mining Indaba 2026, yaliyofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini kuanzia Februari 8 hadi 11, 2026.

Kupitia maafisa wake waandamizi, wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Makampuni, Bw. Nelson Karawa, pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mauzo – Idara ya Hazina, Bw. Jeremiah Lyimo, NMB ilitumia jukwaa hilo kuitangaza Tanzania na sekta yake ya madini mbele ya wawekezaji wa kimataifa.

Katika maonesho hayo, NMB ilisisitiza nafasi ya Tanzania kama moja ya nchi zenye rasilimali nyingi za madini na fursa lukuki za uwekezaji barani Afrika, huku ikiweka bayana utayari wa sekta ya fedha nchini kuunga mkono miradi mikubwa ya kimkakati.

Kuonesha Uwezo wa Kifedha na Uzoefu wa Kibenki

Sambamba na ushiriki wake katika mikutano na makongamano ya kimataifa, NMB ilieleza mchango wake katika maendeleo ya sekta ya madini nchini na utayari wake wa kushiriki katika kufadhili miradi mikubwa kupitia suluhisho bunifu za kifedha.

Katika kongamano hilo, Bw. Lyimo alieleza kuwa NMB ina uwezo mkubwa wa kifedha, uzoefu wa kusimamia mikataba mikubwa, pamoja na mtandao mpana wa ndani na nje ya nchi unaowezesha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya madini. Alisisitiza pia nafasi muhimu ya benki katika kuunganisha rasilimali za ndani na kimataifa ili kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa.

Monday, 16 February 2026

TANZANIA’S MINING GROWTH ENTERS A DECISIVE EXECUTION PHASE

Dar es Salaam, Tanzania – 16 February 2026

Tanzania’s mining sector is entering a more decisive phase of growth — one increasingly defined by execution, infrastructure readiness, and access to long-term capital. As the country positions itself for sustained value creation, attention is shifting from opportunity-driven expansion toward disciplined delivery and long-term investment alignment.

Mining now contributes approximately 10 percent of Tanzania’s Gross Domestic Product (GDP), a significant rise from just 4 percent in 2007. The sector has also become the country’s second-largest foreign exchange earner after tourism, underlining its growing strategic importance to the national economy.

Gold continues to anchor the industry, with leading producers recording a combined output of around 335,000 ounces by the third quarter of 2025.

As the curtains close on Mining Indaba 2026 in Cape Town, Tanzania’s trajectory is drawing attention as an example of how mining jurisdictions are transitioning from exploration-led growth to execution-focused development.

The conversation around mining has evolved,” said Elias Ngunangwa, Head of Client Coverage for Corporate and Investment Banking at Stanbic Bank Tanzania. “The focus today is on whether projects can be delivered efficiently, supported by the right infrastructure, financing structures and operating environment.”


Infrastructure and Energy Shape Competitiveness

Infrastructure and energy reliability are increasingly central to mining competitiveness.

Ongoing investments in transport corridors — including roads and rail networks — are improving the movement of minerals, consumables, and heavy equipment. At the same time, stronger power connectivity is reducing operational uncertainty across mining operations.

More mining companies are now connecting to the national electricity grid, lowering dependence on diesel-powered generation and stabilising operating costs. For investors, these developments significantly influence how project risk and long-term viability are assessed.

Infrastructure and power are no longer background considerations,” Ngunangwa noted. “They directly affect timelines, costs and the ability of mining projects to move from development into steady production.”


Financing Across the Mining Value Chain

As the sector matures, financing needs are also evolving. Capital is no longer required solely for mine development, but across the broader mining ecosystem that sustains operations.

According to Edgar Mwasha, Vice President, Diversified Industries at Stanbic Bank Tanzania, sustainable growth depends on financing models that reflect operational realities.

Mining functions as an ecosystem,” Mwasha said. “Beyond extraction, there are suppliers, contractors, logistics providers and service companies that need access to capital to keep operations running smoothly. Financing must support that full chain if growth is to be sustained.”

SERENGETI PREMIUM APPLE YAONGOZA SHAMRASHAMRA ZA SIKU YA VALENTINE JIJINI DAR ES SALAAM

Serengeti Breweries Limited (SBL) imeendelea kuimarisha mkakati wake wa ubunifu kupitia uzinduzi na uendelezaji wa Serengeti Premium Apple — kinywaji chake kipya kilichotengenezwa hapa hapa Tanzania — kwa kuongoza shamrashamra za Siku ya Valentine kupitia matukio maalum jijini Dar es Salaam.

Ikiwa imelenga kuwashirikisha zaidi wateja na watumiaji wake kupitia uzoefu wa moja kwa moja (experiential marketing), chapa hiyo iliendesha mfululizo wa hafla katika maeneo mbalimbali ya jiji, ikilenga makundi tofauti ya walaji na mitindo yao ya maisha.

Galentine’s Johari Rotana: Urafiki, Mafanikio na Ubunifu wa Kitanzania

Tukio kuu lilikuwa Galentine’s iliyofanyika katika hoteli ya Johari Rotana, likiwaleta pamoja wateja, washirika na wageni waalikwa kusherehekea urafiki, mafanikio na ujio wa kinywaji kipya chenye hadhi ya juu kinachoendana na maisha ya kisasa.

Kupitia hafla hiyo, Serengeti Premium Apple iliimarisha nafasi yake kama ubunifu wa Kitanzania unaokidhi mahitaji yanayobadilika ya walaji — hasa kizazi cha vijana wanaothamini ubora, muonekano na uzoefu wa kipekee wa chapa.

Balozi wa kinywaji hicho, Flaviana Matata, alihudhuria hafla hiyo, akiongeza mvuto wa chapa na kuimarisha uhusiano kati ya bidhaa na wateja wake. Uwepo wake uliendana na taswira ya kinywaji hicho kama alama ya kujiamini, mafanikio na mtindo wa kisasa.

Upanuzi wa Uzoefu: Upper Deck, Serena na Zaidi

Mkakati huo uliendelea kupitia matukio mengine kama Galentine’s Brunch iliyofanyika katika mgahawa wa The Upper Deck Gastro Pub, pamoja na ushirikiano maalum wa Bravo Coco na Serena Hotel Dar es Salaam — yote yakiongozwa na Serengeti Premium Apple kama chapa kinara.

Jumapili, tukio la Big Brunch lililofanyika katika Ramada Resort Dar es Salaam liliongozwa na kinywaji cha Serengeti Lemon, likionyesha upana wa bidhaa za SBL katika kuendana na ladha na mitindo tofauti ya walaji.

Wakati huo huo, Smirnoff Ice iliwafikia wale waliokuwa bado ‘single’ kupitia tukio la “Valentine’s Is a Vibe – Singles Rave.” Chapa nyingine zikiwemo The Singleton na Gordon's Gin nazo ziliongeza nguvu katika kuwapatia wateja burudani na vibe la kipekee katika matukio ya wikiendi hiyo.

Saturday, 14 February 2026

STRENGTHENING TANZANIA’S FINANCIAL MARKETS: KEY INSIGHTS FROM THE AFMI 2025 REPORT

By Irene Rwegalulira, Director of Global Markets, Absa Bank Tanzania

The recent launch of the Absa Africa Financial Markets Index 2025 (AFMI) in Dar es Salaam provided an important opportunity to reflect on Tanzania’s progress in developing its financial markets — and to assess where further reforms can accelerate growth.

For nine years, the AFMI has become one of Africa’s most respected tools for evaluating financial market development across the continent. Beyond ranking countries, the Index offers policymakers, regulators and financial institutions a data-driven framework to understand what is working well, where gaps remain, and which reforms can deliver the greatest impact.

The 2025 report shows that Tanzania continues to move forward steadily. While important foundations are firmly in place, the findings also highlight opportunities to deepen and broaden the market further.


A Strong Foundation of Stability and Transparency

One of the most encouraging findings in this year’s report is Tanzania’s continued strength in macroeconomic stability. The country has benefited from steady and predictable monetary policy, low and stable inflation, and increasingly transparent communication from policymakers.

These elements are critical in building investor confidence. Stability reduces uncertainty, supports long-term planning, and creates a reliable environment for both businesses and households.

The report also reflects ongoing improvements in market infrastructure and the regulatory framework. Efforts to strengthen governance, align regulatory standards with international best practice, and enhance transparency across key segments of the financial system are beginning to yield measurable results.

This progress is not accidental. It reflects sustained commitment from policymakers and regulators to build a credible, resilient and investable financial ecosystem.


Growing Market Depth and Product Diversification

The AFMI 2025 further highlights gradual but meaningful advances in market depth. Tanzania’s financial markets are becoming more diversified, with a broader range of instruments and increased use of capital market solutions.

While bank financing remains dominant, the expanding role of bonds, structured products and risk management tools signals a shift toward a more balanced financial system.

TZS 500 MILLION FINANCING WINDOW OPENS FOR YOUTH UNDER CRDB BANK'S GO GREEN WITH IMBEJU

Dodoma, February 12, 2026 – The Minister of State, President’s Office – Planning and Investment, Hon. Prof. Kitila Mkumbo, has commended CRDB Bank Foundation and CRDB Bank for launching the Go Green with IMBEJU programme, describing it as a strategic initiative that directly aligns the Government’s green economy agenda with youth empowerment.

Speaking during the launch event held at the Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC), Prof. Mkumbo said the programme is fully aligned with Tanzania’s National Development Vision 2050, which emphasizes building an inclusive, competitive, and climate-resilient economy while positioning youth at the centre of national transformation.

The Government has placed strong emphasis on empowering youth economically, promoting a green economy, and strengthening collaboration between the public and private sectors. Youth-led environmental projects like the ones we see today are a direct and practical implementation of Vision 2050,” said Prof. Mkumbo.

 

He underscored that private sector participation remains a critical pillar in transforming young people’s innovative ideas into sustainable enterprises that create jobs and contribute meaningfully to national development.


Parliament Backs Green Economy Framework

The Deputy Speaker of the National Assembly of the United Republic of Tanzania, Hon. Daniel Sillo, noted that Parliament has laid a strong legal foundation to support environmental protection and the growth of the green economy.

He described the programme as a practical example of aligning policy direction, financial capital, and youth innovation to deliver tangible development outcomes.


Financing Youth Innovation in Key Green Sectors

The Go Green with IMBEJU programme is designed to support youth-led innovative projects across key sectors, including:

  • Climate-smart agriculture
  • Renewable and clean energy
  • Water technologies
  • Waste management
  • Environmental conservation
  • Digital innovation

Under the initiative, young entrepreneurs will access affordable financing ranging from TZS 500,000 to TZS 500 million, depending on the size and scale of their projects.


Bridging International Climate Finance and Youth Innovation

Speaking at the event, CRDB Bank Managing Director, Abdulmajid Nsekela, said the programme acts as a bridge between international climate finance and innovative young entrepreneurs who often lack collateral or formal credit history required under traditional banking systems.

Through Go Green with IMBEJU, we believe more young people will be reached, prepared, and empowered to actively participate in the green economy. This is a strategic linkage between international climate finance and the innovation of Tanzanian youth,” said Nsekela.

BENKI YA NMB YADHAMINI TRI-NATIONS LIVESTOCK EXPO KWA SHILINGI MILIONI 300

Mkurugenzi wa Mbogo Ranches, Naweed Bulla (kushoto), akipokea mfano wa hundi ya Sh. milioni 300 kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa NMB Bank Plc, Nsolo Mlozi (kulia), mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Fabian Madele (katikati). Udhamini huu ni wa miaka mitatu kwa ajili ya maonesho ya Tri-Nations Livestock Expo (2026–2028).

Katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kukuza sekta ya mifugo na kuimarisha uchumi wa kilimo, NMB Bank Plc imesaini makubaliano ya udhamini wa miaka mitatu kwa ajili ya Maonesho ya Kimataifa ya Mifugo – Tri-Nations Livestock Expo – kwa thamani ya Shilingi milioni 300.

Maonesho hayo yatakayoshirikisha wafugaji na wadau kutoka Tanzania, Kenya na Namibia, hufanyika kila mwaka. Kwa mwaka huu, yatafanyika kuanzia Juni 19 hadi 21 katika eneo la Ubena Zomozi, Chalinze mkoani Pwani.


Uwekezaji wa Kimkakati katika Sekta ya Ufugaji

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa makubaliano hayo, Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa NMB, Nsolo Mlozi, alisema benki hiyo inajivunia mafanikio ya maonesho ya miaka ya 2024 na 2025, yaliyochochea uamuzi wa kuingia katika mkataba mpya wa muda mrefu aliouita uwekezaji wa kimkakati.

Mkataba huu ni uwekezaji wa kimkakati unaolenga kukuza sekta ya ufugaji na kuboresha maisha ya Watanzania wanaojihusisha na sekta ya kilimo — mnyororo wa thamani unaojumuisha kilimo, uvuvi na ufugaji,” alisema Mlozi.

Alibainisha kuwa hadi kufikia mwaka 2025, NMB ilikuwa imekopesha zaidi ya Shilingi bilioni 100 katika sekta hiyo, hatua inayodhihirisha dhamira ya benki hiyo katika kuchochea maendeleo ya kilimo na mifugo nchini.


Serikali Yaunga Mkono Ushirikiano

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mbogo Ranches, Naweed Bulla, aliishukuru NMB kwa kukubali kudhamini maonesho hayo kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa mchango huo utaongeza hadhi na wigo wa maonesho kimataifa.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Fabian Madele, aliipongeza NMB kwa kuendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuendeleza maonesho hayo, akiahidi kuwa Serikali itaendelea kuyaunga mkono katika kipindi chote cha miaka mitatu ya mkataba huo.


Jukwaa la Ushirikiano, Ubunifu na Biashara

Maonesho ya Tri-Nations Livestock Expo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la ushirikiano, ubunifu na biashara kwa wafugaji na wadau wa mnyororo mzima wa thamani. Kupitia maonesho hayo, washiriki hupata:

  • Mbinu bora za ufugaji
  • Elimu kuhusu bima na huduma za kifedha
  • Fursa za mikopo na uwezeshaji
  • Uunganishwaji na masoko ya kitaifa na kimataifa

Udhamini wa NMB kwa kipindi cha miaka mitatu unaashiria kuimarika kwa ushirikiano kati ya sekta ya fedha, sekta binafsi na Serikali katika kukuza uchumi wa mifugo — moja ya nguzo muhimu za maendeleo ya Tanzania.

Friday, 13 February 2026

CRDB BANK FOUNDATION YAZINDUA "GO GREEN NA IMBEJU", VIJANA KUPATA MITAJI HADI SH. MIL. 500

Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati), akiwa na viongozi wengine wa Serikali, Bunge na Benki ya CRDB, wakipata maelezo kutoka kwa mwanzilishi wa kampuni ya Aquafresh iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana, wakati wa hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati), akipokelewa na kikundi cha ngoma za asili wakati alipowasili katika uzinduzi wa programu ya Go Green na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Wengine pichani ni, kushoto kwake, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo; Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori; na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.

Dodoma, 12 Februari 2026 – Waziri wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo, ameipongeza CRDB Bank Foundation na Benki ya CRDB kwa kuanzisha programu ya Go Green na IMBEJU, akisema ni hatua ya kimkakati inayounganisha ajenda ya Serikali ya uchumi wa kijani na uwezeshaji wa vijana.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma, Prof. Mkumbo alisema mpango huo unaendana kikamilifu na Dira ya Taifa 2050, ambayo imeweka mkazo katika uchumi jumuishi, shindani na himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi huku ikitambua vijana kama msingi wa mafanikio ya Taifa.

Serikali imeweka mkazo mkubwa katika kuwawezesha vijana kiuchumi, kukuza uchumi wa kijani na kujenga mifumo imara ya ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi. Miradi ya vijana inayolinda mazingira kama tunavyoiona leo ni utekelezaji wa moja kwa moja wa Dira ya Taifa 2050 kwa vitendo,” alisema Prof. Mkumbo.

Alisisitiza kuwa ushiriki wa sekta binafsi ni nguzo muhimu katika kuhakikisha mawazo bunifu ya vijana yanageuzwa kuwa biashara endelevu zenye ajira na tija kwa Taifa.


Mitaji Nafuu Kuanzia Shilingi 500,000 hadi Milioni 500

Programu ya Go Green na IMBEJU inalenga kuwawezesha vijana wenye miradi bunifu inayohusiana na:

  • Kilimo himilivu
  • Nishati safi na jadidifu
  • Teknolojia za maji
  • Usimamizi wa taka
  • Uhifadhi wa mazingira
  • Ubunifu wa kidijitali

Kupitia dirisha hili, vijana wanaweza kupata mitaji nafuu kuanzia Shilingi 500,000 hadi Shilingi milioni 500, kulingana na ukubwa na mahitaji ya mradi.


Daraja Kati ya Fedha za Tabianchi na Ubunifu wa Vijana

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema mpango huo ni daraja kati ya fedha za kimataifa za tabianchi na vijana wabunifu ambao mara nyingi hukosa dhamana au historia ya mikopo inayohitajika katika mifumo ya kawaida ya kifedha.

Kupitia Go Green na IMBEJU tunaamini vijana wengi zaidi watafikiwa, kuandaliwa na kuwezeshwa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kijani. Huu ni muunganiko wa kimkakati kati ya ufadhili wa kimataifa wa tabianchi na ubunifu wa vijana wa Tanzania,” alisema Nsekela.

BENKI YA EXIM YAONGEZA MCHANGO KWA SEKTA YA UTALII KAMA MDHAMINI MKUU WA Z-SUMMIT 2026

Zanzibar | 11 Februari 2026

Benki ya Exim Tanzania imedhihirisha tena dhamira yake ya muda mrefu katika kuchochea ukuaji na ustawi wa sekta ya utalii kwa kudhamini Z-Summit 2026 kama Mdhamini Mkuu. Hafla hiyo imefanyika tarehe 11–12 Februari 2026 katika Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), Tunguu.

Huu ni mwaka wa nne mfululizo kwa benki hiyo kudhamini mkutano huu tangu kuanzishwa kwake.


Jukwaa Muhimu la Biashara na Uwekezaji

Z-Summit imejipatia umaarufu kama jukwaa kuu la biashara na uwekezaji katika utalii Zanzibar. Hukutanisha wawekezaji wa utalii, waendeshaji wa watalii, wamiliki wa hoteli, mawakala wa usafiri, watunga sera na watoa huduma kutoka Tanzania, Afrika Mashariki na mataifa mengine duniani.

Mkutano huu una mchango mkubwa katika:

  • Kujenga ushirikiano wa kimkakati
  • Kufungua fursa mpya za uwekezaji
  • Kuweka mwelekeo wa maendeleo endelevu ya utalii Zanzibar


Suluhisho za Kifedha kwa Sekta ya Utalii

Mbali na akaunti maalum kwa waendeshaji wa watalii na huduma za bima, Benki ya Exim imeendelea kubuni suluhisho za kisasa za malipo ya kidijitali.

Benki hii ilikuwa ya kwanza nchini kuzindua Kadi ya Exim TANAPA, inayowawezesha waendeshaji wa watalii kufanya malipo ya kielektroniki kwa viingilio vya hifadhi na huduma nyingine kupitia Tanzania National Parks Authority (TANAPA).

ABSA GROUP ANNOUNCES EXECUTIVE APPOINTMENTS FOLLOWING PAN-AFRICAN STRATEGY RESET

Absa Group has announced a series of strategic executive leadership appointments aimed at strengthening its organisational capability, governance framework and customer-led growth ambitions across the continent.

The changes follow the finalisation of the Group’s refocused Pan-African Strategy and underscore its commitment to enhanced strategic execution, succession planning and deeper leadership bench strength.


Sitoyo Lopokoiyit Appointed Chief Executive: Personal and Private Banking

Absa has appointed Sitoyo Lopokoiyit as Chief Executive: Personal and Private Banking, effective 1 April 2026.

Lopokoiyit is widely recognised as one of Africa’s leading fintech executives, bringing extensive experience in financial services, telecommunications, customer value propositions and large-scale business transformation.

He most recently served as Managing Director of M-PESA Africa and Chief Financial Services Officer at Safaricom, where he led the strategy and growth of Africa’s largest fintech platform. Under his leadership, M-PESA scaled to serve over 56 million customers and more than 5 million businesses across the continent.

Since joining Safaricom in 2011, Lopokoiyit held several senior leadership roles, including Head of M-PESA Strategy and Business Development, and led operations in Tanzania. He also spearheaded major innovations such as the M-PESA Super App, Fuliza, and partnerships with global platforms including PayPal and Alipay.

His contribution to advancing financial inclusion earned him induction into the 11:FS Hall of Fame, recognising industry leaders who have significantly transformed financial services through innovation and resilience.

Commenting on the appointment, Kenny Fihla, Group Chief Executive Officer of Absa Group, said:

This appointment demonstrates Absa’s strategic focus on delivering integrated, customer-centric solutions across our Personal and Private Banking franchise while unlocking new growth opportunities.”


Strengthening Governance and Assurance Leadership

In line with Absa’s commitment to robust governance and regulatory excellence, several additional appointments have been confirmed, effective 1 March 2026.

Thursday, 12 February 2026

REGION’S FIRST ENTERPRISE-GRADE SANCTIONS RISK MASTERCLASS FOR BANKS IN EAST & SUB-SAHARAN AFRICA


Dar es Salaam to Host Global Sanctions Compliance Masterclass, 30–31 March 2026

Sanctions compliance is rapidly evolving from a back-office obligation into a strategic enterprise risk for banks across Africa. With increasing global enforcement, tightening correspondent banking relationships, and rising cross-border scrutiny, financial institutions are under growing pressure to strengthen their sanctions risk frameworks.

To address this gap, the Global Sanctions Compliance Masterclass will take place in Dar es Salaam, Tanzania, on 30–31 March 2026.

This marks the region’s first mid-to-senior level, bank-focused sanctions programme designed to equip financial institutions with the tools to identify, assess, investigate, and govern sanctions risk end-to-end — aligned with global enforcement expectations.


Why This Matters

Across East and Sub-Saharan Africa, sanctions risk now affects:

  • Correspondent banking access
  • Cross-border payments and trade flows
  • Revenue sustainability
  • Enterprise risk management
  • Board accountability

Despite this, many institutions continue to face:

  • Limited understanding of jurisdictional reach
  • Fragmented Financial Crime Compliance (FCC) structures
  • Weak frontline ownership
  • Gaps in investigative capability

This masterclass aims to bridge those gaps.


Programme Highlights

Day One: Sanctions Risk Identification & Exposure

  1. Global FCC Landscape & Repositioning Sanctions Risk
  2. Global Sanctions Architecture & Jurisdictional Reach
  3. Sanctions Risk Identification & Assessment (SRA)
  4. Sanctions Evasion Techniques
  5. Sanctions Investigations & Four-Eye Principles

Day Two: Sanctions Risk Mitigation & Governance

  1. Controls, Asset Freezes, Licensing & Reporting
  2. Screening Excellence Across Payments, Trade & Digital Assets
  3. First Line Ownership & Escalation Frameworks
  4. Sanctions in ERM, Risk Appetite & Board Oversight
  5. Designing an Enterprise-Grade Sanctions Framework (Capstone)


Certification & Target Audience

Participants will receive an Advanced Global Sanctions Compliance Certificate (AGSCC).

The programme is designed for:
Compliance (FCC & Regulatory), Trade Finance, Treasury, Payments, Risk, Legal, Audit, Business Units, Quality Controls and Technology teams.


A Strategic Question for Bank Leaders

Is sanctions risk treated merely as a compliance checklist — or as a core enterprise risk owned by the business and the board?


Registration & Further Information

📧 Email: evarist.muhaya@globalriskas.com
📱 WhatsApp: +255 765 565 031
🌐 Website: www.globalriskas.com

BANK OF TANZANIA SELLS USD 15.75 MILLION IN FOREX MARKET INTERVENTION

Dar es Salaam, 10 February 2026 – The Bank of Tanzania (BoT) has intervened in the Interbank Foreign Exchange Market (IFEM), selling USD 15.75 million through an auction aimed at providing liquidity and stabilising the foreign exchange market.

According to a public notice issued by the BoT’s Directorate of Financial Markets, the intervention was conducted in line with the Foreign Exchange Intervention Policy, 2023.

Strong Demand from Banks

The auction attracted significant participation from the banking sector:

  • Currency: USD
  • Offered Amount: USD 15 million
  • Tendered Amount: USD 27 million
  • Successful Amount: USD 15.75 million
  • Number of Participating Banks: 30
  • Number of Successful Banks: 18

The fact that banks tendered USD 27 million against an initial offer of USD 15 million indicates strong demand for foreign currency liquidity within the market.

Exchange Rate Details

The auction results showed:

  • Weighted Average Exchange Rate: TZS 2,572.56 per USD
  • Highest Bid Rate: TZS 2,580.00
  • Lowest Bid Rate: TZS 2,560.00
  • Highest Accepted Bid: TZS 2,580.00
  • Lowest Accepted Bid: TZS 2,570.00

The weighted average rate of TZS 2,572.56 reflects the market-clearing price determined through the competitive bidding process.

What This Means for the Market

The intervention is part of the central bank’s ongoing efforts to:

  • Maintain orderly conditions in the foreign exchange market
  • Address short-term liquidity pressures
  • Support exchange rate stability

By supplying dollars into the interbank market, the Bank of Tanzania helps ease demand pressures and ensures smoother functioning of foreign exchange transactions among commercial banks.

Such interventions are a key monetary tool used globally by central banks to manage volatility and reinforce confidence in the financial system.


Source: Bank of Tanzania – Public Notice, 10 February 2026.

EQUITY BANK YAZINDUA “WEZESHA AKAUNTI” KUKUZA UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI WA KIFEDHA

Dar es Salaam – 11 Februari 2026

Benki ya Equity Tanzania imezindua rasmi “Wezesha Akaunti”, akaunti ya amana ya muda maalum inayolenga kuwahamasisha Watanzania kuanza uwekezaji leo kwa ajili ya kesho iliyo bora kifedha.

Akaunti hii imeundwa kwa ajili ya watu binafsi, wajasiriamali, vikundi, vyama na taasisi, ikiwawezesha kukuza na kulinda mitaji yao kupitia uwekezaji salama unaotoa faida ya asilimia 13 kwa mwaka, inayolipwa kila mwezi.

Vigezo vya Wezesha Akaunti

  • Kima cha chini cha uwekezaji: TZS 500,000
  • Muda wa uwekezaji: Miaka mitatu
  • Faida: 13% kwa mwaka (malipo ya kila mwezi)
  • Inaweza kutumika kama dhamana ya hadi 80% ya thamani ya amana kupata mkopo

Kupitia kipengele cha dhamana, mteja anaweza kupata mkopo bila kuvunja uwekezaji wake — hatua inayowapa wawekezaji unafuu wa kifedha huku wakiendelea kunufaika na faida ya amana yao.

Uzinduzi wa Wezesha Akaunti umefanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau wa sekta ya fedha, wateja pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari. Dirisha la kuwekeza limefunguliwa rasmi, tarehe 11 Februari 2026, na litafungwa tarehe 30 Aprili 2026.


Fursa kwa Makundi Mbalimbali

Wezesha Akaunti inalenga kugusa makundi mbalimbali ya jamii:

  • Wajasiriamali – kupata mapato ya ziada kupitia riba ya kila mwezi na kutumia amana kama dhamana ya kukuza biashara.
  • Wafanyabiashara – kulinda na kukuza mali zao kwa faida thabiti ya 13% kwa mwaka.
  • Wanawake na vijana – kujenga uhuru wa kifedha kupitia mapato ya uhakika na fursa za mikopo.
  • Taasisi na wawekezaji – kutumia hadi 80% ya thamani ya amana kama dhamana ya mikopo kwa ajili ya miradi na fursa mpya.

Kwa mujibu wa Benki ya Equity, lengo ni kukusanya jumla ya TZS bilioni 200, hatua itakayosaidia kuimarisha uwezo wa benki katika utoaji wa mikopo, hususan kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (MSMEs).

Wednesday, 11 February 2026

EQUITY BANK LAUNCHES "WEZESHA ACCOUNT" TO BOOST INVESTMENT AND FINANCIAL EMPOWERMENT

Dar es Salaam, February 11, 2026

Equity Bank Tanzania Limited (EBTL) has officially launched the “Wezesha Account,” a strategic fixed deposit product designed to empower Tanzanians by transforming savings into a disciplined, high-yield investment opportunity.

The new product targets individuals, entrepreneurs, and institutions seeking a secure and predictable way to grow their capital while maintaining flexibility.

Turning Savings into Predictable Income

The Wezesha Account offers an attractive 13% annual interest rate, paid monthly, providing customers with a reliable income stream and enhanced financial predictability. With consistent monthly returns, the product is structured to support long-term wealth creation while encouraging disciplined savings.

Key Features of the Wezesha Account:

  • Interest Rate: 13% per annum
  • Interest Payment: Monthly payouts
  • Tenor: 3 years
  • Minimum Deposit: TZS 500,000
  • Loan Access: Deposit can serve as collateral for loans of up to 80% of its value

A standout feature of the Wezesha Account is the ability for customers to leverage their fixed deposit as collateral. This enables clients to access up to 80% of their deposit value in loans without liquidating their investment — offering flexibility for entrepreneurs and businesses that require liquidity while preserving capital growth.

Strategic Growth and Economic Impact

Equity Bank aims to mobilize TZS 200 billion through the Wezesha Account, strengthening its lending pipeline and supporting its broader strategic growth objectives.

Speaking at the launch, Equity Bank Commercial Director, Mr. Prosper Nambaya, emphasized the bank’s long-term vision and commitment to financial empowerment:

Our purpose is to transform lives, give dignity, and expand opportunities for wealth creation. The Wezesha Account is a tangible expression of this commitment. It provides a trusted and empowering tool for Tanzanians to make their money work harder, earn predictable returns, and unlock financial freedom. This initiative is central to our strategy of growing our balance sheet responsibly to position among Tanzania's top-tier banks.”

Responding to Market Dynamics

The launch comes at a time when banks are focusing on strengthening liquidity and building stable funding bases. The Wezesha Account is strategically designed to:

  • Improve the bank’s Local Currency Loan-to-Deposit Ratio
  • Build a stable, long-term funding base
  • Provide low-cost, stable funding to support high-margin MSME lending

SAMSUNG OPENS TWO NEW BRAND STORES IN KUNDUCHI AND UBUNGO, SHOWCASING THE FULL CONSUMER EXPERIENCE

Dar es Salaam, 10 February 2025 – Samsung Electronics East Africa has officially opened two new Samsung Brand Stores in Kunduchi and Ubungo, strengthening its footprint in Tanzania and reaffirming its commitment to delivering a fully connected consumer experience.

The new stores bring Samsung’s complete ecosystem closer to Tanzanian customers by integrating both Mobile and Consumer Electronics products under one roof. Designed as immersive retail spaces, the stores allow customers to experience first-hand how Samsung devices seamlessly connect to support communication, entertainment, home living, and productivity.

A Complete Samsung Ecosystem in One Space

Unlike standard retail outlets, the newly launched Brand Stores are larger, purpose-built environments that showcase Samsung’s full product range. Customers can explore the latest Samsung Galaxy smartphones, tablets, wearables, televisions, home appliances, and accessories — all within a setting that demonstrates real-life smart connectivity.

Through interactive displays and live demonstrations, visitors can see how devices sync and interact effortlessly, reinforcing Samsung’s vision of a connected lifestyle.

The official launch ceremonies were attended by key stakeholders, business partners, members of the media, and a Guest of Honour — underlining the importance of the investment in Tanzania’s growing digital and retail landscape.

Strengthening Long-Term Commitment to Tanzania

Speaking during the launch, Mgope Kiwanga, Mobile Business Head, Samsung Electronics East Africa (Tanzania), said the openings reflect Samsung’s long-term strategy in the Tanzanian market.

The opening of our Brand Stores in Kunduchi and Ubungo marks an important step in bringing the full Samsung Consumer Experience closer to our customers. These stores allow us to demonstrate how our mobile devices and consumer electronics connect as one ecosystem, making technology more practical, accessible, and relevant to everyday life,” said Kiwanga.

Tuesday, 10 February 2026

OVERSUBSCRIBED TREASURY BONDS SIGNAL UNTAPPED INVESTMENT POTENTIAL IN TANZANIA

Dar es Salaam, 10 February 2026 — Investors have shown strong confidence in Tanzania’s long-term government securities, with the recent 25-year Treasury bond attracting bids far exceeding the amount on offer. While this reflects trust in macroeconomic stability, analysts say it also highlights a growing pool of capital that remains underutilised in the wider economy.

In the mid-last-week auction, investors submitted bids worth Sh1.6 trillion, yet the Bank of Tanzania accepted only Sh300 billion, leaving approximately Sh1.3 trillion in capital seeking alternative investment opportunities.

Oversubscription is widely regarded as a vote of confidence in government instruments and fiscal management. However, market experts argue that repeated oversubscription also reveals structural gaps—particularly the limited availability of safe, long-term investment options outside government securities.

Confidence High, Options Limited

Commenting on the trend, Mr Frank Abel, Manager for Research and Analysis at Vertex International Securities, said persistent oversubscription sends a dual message.

First, investors trust government instruments and the country’s financial system,” Mr Abel noted. “Second, it indicates there are limited avenues for safe, long-term investment in the private sector. Capital is available, but attractive alternatives are few.”

He explained that Tanzania has experienced consistent demand for Treasury bonds over recent years, driven by both institutional and individual investors seeking stability and predictable returns.

According to Mr Abel, the surplus capital presents a significant opportunity to support economic growth if properly channelled.

The challenge is not liquidity or willingness,” he said. “It is about creating structured channels where this trust in government can be translated into real-economy projects.”

NEW STUDY FINDS ILLICIT ALCOHOL COSTS TANZANIA OVER TZS 1 TRILLION ANNUALLY

Dar es Salaam, February 5, 2026 – Illicit alcohol continues to pose a serious threat to public health, government revenue, and legitimate businesses in Tanzania, according to a newly released study.

The study reveals that approximately 61% of all alcohol consumed in Tanzania is illicit, resulting in an estimated annual revenue loss of TZS 1.026 trillion due to uncollected taxes.

A Regional Challenge

The findings reflect a broader regional trend. Similar studies conducted by Euromonitor International in Kenya and Uganda in 2025 showed that illicit alcohol accounted for 60% and 67% of illicit alcohol consumption, respectively.

Experts say this indicates that illicit alcohol is not only a national issue but a regional challenge that requires coordinated, long-term solutions.

What Constitutes Illicit Alcohol?

According to the study, illicit alcohol refers to beverages that do not fully comply with tax, regulatory, and legal requirements. This includes alcohol that:

  • Is not subject to proper excise duty
  • Lacks required health and safety approvals
  • Violates production standards
  • Uses unapproved or unsafe ingredients

Illicit alcohol is also distributed through unlicensed outlets, which play a significant role in alcohol markets across many developing countries.

Traditional Brews Dominate the Illicit Market

The study shows that illicit alcohol spans all categories, including spirits, beer, and wine. However, a significant share comes from illegal traditional or artisanal brews, such as Mbege, Komoni, Wanzuki, Ulanzi, and Dengerua.

While these drinks have cultural significance, their widespread consumption is largely driven by low prices. For example, gongo, which is banned, can be up to 80% cheaper than legally produced spirits. Counterfeit alcohol and smuggled products also remain a major concern, particularly in the spirits and beer segments.

PUMA ENERGY TANZANIA LAUNCHES AFRICA’S LARGEST CNG MOTHER STATION, STRENGTHENING PPPs

Prime Minister Dr. Mwigulu Nchemba (third from right) launches Puma Energy’s Compressed Natural Gas (CNG) Mother Station in Dar es Salaam, yesterday. The facility is anticipated to be Africa’s largest, with a capacity of 6.7 million standard cubic feet per day. On his left is the company’s Managing Director, Ms. Fatma Abdallah, while on his right is the Deputy Minister for Energy, Ms. Salome Makamba, alongside other officials.

Dar es Salaam, February 9, 2026 — Puma Energy Tanzania has officially commissioned Africa’s largest and most advanced Compressed Natural Gas (CNG) Mother Station, marking a major milestone in Tanzania’s journey toward clean, affordable, and reliable energy.

The landmark facility was inaugurated by Prime Minister Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba, underscoring the Government’s strong commitment to public–private partnerships (PPPs) as a driver of sustainable national development.

A Strategic Investment in Clean Energy

Located in Dar es Salaam, the state-of-the-art CNG Mother Station is designed to meet the country’s growing demand for cleaner and more cost-effective fuel alternatives. The facility will serve light vehicles, buses, and heavy-duty trucks, while also acting as a central distribution hub supplying “daughter” CNG stations across Tanzania via tube-trailers.

The project positions natural gas as a viable substitute for petrol and diesel, helping to lower transport costs, reduce emissions, and support energy diversification.

“This CNG Mother Station is more than just infrastructure; it’s a symbol of our long-term confidence in Tanzania and our commitment to creating shared value,” said Ms. Fatma Abdallah, Managing Director of Puma Energy Tanzania.
“We are proud to partner with the Government to deliver a project that will power Tanzania’s progress for years to come.”

Government Applause for a Model PPP

Speaking during the inauguration, Prime Minister Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba praised the project as a strong example of the Sixth Phase Government’s strategy to foster a conducive investment climate and leverage PPPs for national development.

“Puma Energy Tanzania stands out as a successful example of public–private partnership, delivering quality energy services while contributing to national revenues, employment creation, and strategic infrastructure development,” the Prime Minister stated.
“This investment reflects the Government’s commitment to creating a favourable business environment and aligns perfectly with our national priorities.”

Strong Returns for Tanzanians

Treasury Registrar Mr. Nehemiah Mchechu highlighted the project’s unique ownership structure, noting that government participation ensures commercial success directly benefits the nation.

“This joint venture proves that combining government participation with private-sector efficiency delivers vital infrastructure and strong financial returns for Tanzanians,” Mr. Mchechu said.