Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya kuwa mshirika wa kimkakati katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Zanzibar, ikiahidi kuendelea kuwawezesha wafanyabiashara, wawekezaji na wajasiriamali kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na ongezeko la uwekezaji, maendeleo ya miundombinu na ukuaji wa sekta ya utalii.
Benki hiyo imesema itaendelea kutoa suluhisho mbalimbali za kifedha zitakazowawezesha wafanyabiashara kupata mitaji, kupanua shughuli zao, kuongeza uzalishaji na kuwekeza katika fursa mpya za biashara, hususan katika maeneo yenye kasi ya ukuaji wa kiuchumi, ikiwemo Kizimkazi na Zanzibar kwa ujumla.
Akizungumza kufuatia hitimisho la Tamasha la Kizimkazi mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bw. Theobald Sabi, alisema benki hiyo inaona fursa kubwa katika mabadiliko yanayoendelea Zanzibar na imejipanga kushirikiana na sekta binafsi ili kuhakikisha fursa hizo zinageuka kuwa shughuli endelevu za kiuchumi.
“NBC itaendelea kuwa mshirika wa wafanyabiashara na wawekezaji katika kutumia fursa zinazopatikana Zanzibar, ikiwemo eneo la Kizimkazi. Tumejipanga kutoa suluhisho mbalimbali za kifedha zitakazowasaidia kupata mitaji, kukuza biashara zao na hatimaye kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa maeneo haya,” alisema Bw. Sabi.



.jpeg)
.jpeg)





















.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)









