Foreign Exchange Rates

Absa Loan Campaign_160426

Absa Loan Campaign_160426

CRDB Bank Advert_070325

Sunday, 5 July 2026

YAS YAZINDUA KAMPENI YA KUSHINDA SIMU ZA ZTE KUPITIA YAS APP


Dar es Salaam, Julai 3, 2026 – Watanzania sasa watapata fursa ya kujishindia simu janja aina ya ZTE A35 kila wiki baada ya Yas Tanzania kuzindua kampeni ya "Register, Login and Win", inayolenga kuongeza matumizi ya huduma za kidijitali kupitia Yas App.

Kampeni hiyo imezinduliwa leo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SabaSaba), ambapo Watanzania wanaotembelea banda la Yas wanaweza kujisajili kwenye Yas App na kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kila wiki ya kushinda simu janja aina ya ZTE A35. Kampeni hiyo itadumu kwa siku 90, huku washindi wanne wakipatikana kila wiki.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa Huduma za Vijana na Wateja Maalum wa Yas Tanzania, Ikunda Ngowi, alisema kampeni hiyo inalenga kuwahamasisha Watanzania kutumia Yas App kupata huduma mbalimbali za mawasiliano kwa urahisi.

"Kupitia Yas App, wateja wanaweza kupata huduma muhimu popote walipo na wakati wowote. Kupitia kampeni hii tunawapa Watanzania sababu zaidi ya kutumia huduma za kidijitali huku tukiwazawadia simu janja," alisema Ngowi.

 

Aliongeza kuwa kupitia Yas App, wateja wanaweza kununua vifurushi vya intaneti, dakika na SMS, kuangalia salio na kusimamia huduma zao zote za Yas kwa urahisi.

"Tunawaalika Watanzania wote wanaotembelea Maonesho ya SabaSaba kufika banda la Yas, kupakua Yas App na kujisajili ili kupata nafasi ya kushinda simu mpya ya ZTE A35 kila wiki," alisema.

MIXX, SERIKALI YA ZANZIBAR KUSHIRIKIANA KULETA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KWA VYAMA VYA USHIRIKA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Sera Uratibu na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Hamza Hassan Juma akishuhudia utuaji Saini mkataba baina ya Mkurugenzi wa Uzingatiaji wa Sheria Mixx Tanzania Abdallah Nguba (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Vijana Ajira na Uwezeshaji, Salama Mbarouk Khatib, wakati wa maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani 2026, huko katika kiwanja cha kufurahishia Watoto Tibirinzi Chake Chake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Sera Uratibu na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Hamza Hassan Juma akizungumza kwa niaba ya Makamu wa Pili wa Rais, wakati wa wakati wa maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani 2026, huko katika kiwanja cha kufurahishia Watoto Tibirinzi Chake Chake.

Pemba, Julai 4, 2026 – Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema matumizi ya teknolojia katika sekta ya ushirika yataongeza uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika huduma za kifedha, kufuatia kutiwa saini kwa makubaliano ya ushirikiano kati ya Mixx by Yas na Idara ya Maendeleo ya Ushirika Zanzibar.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo katika maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani, Mgeni Rasmi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar anayeshughulikia Sera, Uratibu na Shughuli za Baraza la Wawakilishi, Mhe. Hamza Hassan Juma, alisema ushirikiano huo unaendana na dhamira ya Serikali ya kuharakisha mageuzi ya kidijitali yatakayowezesha vyama vya ushirika kuwa na mifumo ya kisasa, salama na yenye tija.

"Mageuzi ya kidijitali katika sekta ya ushirika yataongeza uwazi, kuimarisha uwajibikaji na kuwapa wananchi huduma bora zaidi za kifedha. Ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi ni muhimu katika kufanikisha maendeleo jumuishi na kujenga uchumi wa kisasa unaomgusa kila Mwananchi," alisema.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kunufaisha maelfu ya wanachama wa vyama vya ushirika, vikundi vya kijamii na wajasiriamali Zanzibar kwa kuwezesha usimamizi wa fedha kwa njia za kidijitali, kuongeza usalama wa miamala na kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha.

Mkurugenzi wa Uzingatiaji wa Sheria Mixx, Bw. Abdallah Nguba alisema ushirikiano huo unaweka msingi wa mageuzi yatakayoboresha namna vyama vya ushirika vinavyosimamia fedha na kutoa huduma kwa wanachama wake kupitia teknolojia.

"Makubaliano haya yanaweka msingi wa mageuzi makubwa katika vyama vya ushirika kwa kuboresha usimamizi wa fedha, kuongeza uwazi na kurahisisha huduma kupitia teknolojia. Kupitia Mixx Kikoba, wanachama wataweza kuweka akiba, kuchangiana, kufanya malipo, kununua hisa, kupokea gawio na hata kuomba mikopo moja kwa moja kupitia simu zao," alisema.

Saturday, 4 July 2026

NBC YAKABIDHI AZAM FC KOMBE LA UBINGWA WA LIGI YA VIJANA U20 2025/2026

Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Nassor Idrissa (katikati) na Mkuu wa Kitengo cha Wajasiriamali, Vijana na Wanawake wa Benki ya NBC, Gaudence Shawa (kulia – alievaa suti) wakikabidhi kombe la Ligi ya NBC ya Vijana chini ya miaka 20 (NBC U20 Youth League) kwa nahodha wa timu ya Azam FC (U20) Rajabu Somvi baada ya timu hiyo kuwa bingwa wa ligi hiyo kwa msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe la ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es Salaam kufuatia mechi ya fainali baina ya mabingwa hao na wenzao Yanga SC (U20).
Wachezaji wa timu ya Azam FC (U20), viongozi na wadau mbalimbali wakijipongeza baada ya timu hiyo kukabidhiwa rasmi kombe la ubingwa wa Ligi ya NBC ya Vijana chini ya miaka 20 (NBC U20 Youth League) msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe la ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es Salaam kufuatia mechi ya fainali baina ya mabingwa hao na wenzao kutoka Yanga SC (U20) mechi hiyo iliisha kwa timu ya Azam FC (U20) kuibuka na ushindi wa 2-1.

Dar es Salaam, Julai 2, 2026 – Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), mdhamini mkuu wa Ligi ya NBC Vijana chini ya Miaka 20 (NBC U20 Youth League), imekabidhi rasmi kombe la ubingwa wa msimu wa 2025/2026 kwa Azam FC (U20) baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Yanga SC (U20) katika mchezo wa fainali uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Chamazi Complex, jijini Dar es Salaam.

Kabla ya mchezo huo wa fainali, Mbeya City FC (U20) ilitwaa nafasi ya tatu baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya JKT Tanzania (U20), kufuatia timu hizo kutoka sare katika muda wa kawaida.

Hafla ya kukabidhi kombe hilo iliongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Wajasiriamali, Vijana na Wanawake wa Benki ya NBC, Gaudence Shawa, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi. Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa soka nchini akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Nassor Idrissa, Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Oscar Milambo, Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Lameck Nyambaya, viongozi wengine wa TFF pamoja na Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars, Miguel Gamondi.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Shawa aliwapongeza mabingwa Azam FC (U20), washindi wa pili Yanga SC (U20), washindi wa tatu Mbeya City FC, vilabu vyote vilivyoshiriki, mabenchi ya ufundi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kufanikisha msimu ulioonyesha kiwango cha juu cha ushindani na maendeleo makubwa ya kiufundi.

Alisema ubora wa michezo ulioshuhudiwa msimu huu unaonesha wazi kuwa uwekezaji katika maendeleo ya soka la vijana unaanza kuzaa matokeo yanayotarajiwa, huku ukitoa matumaini makubwa ya kuimarika zaidi kwa ligi za ndani na timu za taifa katika miaka ijayo.

"NBC tunaamini kwamba mafanikio ya soka la kulipwa huanzia kwenye uwekezaji madhubuti katika maendeleo ya vijana. Ndiyo sababu tuliamua kuwa sehemu ya safari hii ya kujenga kizazi kipya cha wachezaji wenye uwezo wa kuleta ushindani mkubwa katika Ligi Kuu ya NBC, NBC Championship na hatimaye kuiwezesha Tanzania kuwa na timu za taifa zenye ushindani wa kimataifa. Tunafurahishwa kuona kiwango cha ushindani na ubora wa soka katika ligi hii vinaendelea kuimarika kila msimu, jambo linalotupa imani kuwa uwekezaji huu unaendelea kuleta matokeo chanya," alisema Shawa.

ABSA BANK DONATES TZS 20 MILLION TO SUPPORT LIFE-SAVING HEART TREATMENT FOR CHILDREN

Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second left), and Executive Director of Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), Dr. Peter Kisenge, exchange signed Memorandum of Understanding (MoU) documents, shortly after formalising the partnership between the two institutions. During the ceremony, Absa Bank Tanzania also donated TZS 20 million to support cardiac treatment for children from underprivileged families. From left are Absa Bank Tanzania Company Secretary, Mr. Desmond Malyi, and Global Medicare General Manager, Mr. Daniel Lazaro.

Dar es Salaam, Tanzania – Reinforcing its commitment to creating a positive social impact through corporate citizenship, Absa Bank Tanzania has donated TZS 20 million to support the treatment of children living with heart disease across Tanzania.

The funding will be channelled through the Heart Team Africa Foundation (HTAF), a non-governmental organisation established by the Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI). The initiative is aimed at helping children from vulnerable families gain access to specialised, life-saving cardiac treatment and care.

The donation was formalised through the signing of a Memorandum of Understanding (MoU) in Dar es Salaam, marking the beginning of a partnership focused on improving access to quality healthcare for children with heart conditions.

Absa Reaffirms Its Commitment to Being a Force for Good

Speaking during the signing ceremony, Absa Bank Tanzania Managing Director, Obedi Laiser, said the partnership reflects the Bank's purpose of being a Force for Good by making a meaningful difference in the lives of Tanzanians.

"Our purpose is to be a Force for Good in everything we do, and this partnership is a reflection of that commitment in action. We recognize the remarkable work undertaken by the Jakaya Kikwete Cardiac Institute in providing specialized cardiac care to children and families across Tanzania."

 

He noted that by partnering with JKCI through the Heart Team Africa Foundation, Absa is helping to expand access to life-saving treatment for children living with heart disease while offering hope to families facing both medical and financial hardships.

"Every child deserves the opportunity to live a healthy and productive life. By investing in their health today, we are investing in their future stories, the well-being of their families and the long-term prosperity of our communities. We are honoured to partner with the Jakaya Kikwete Cardiac Institute in this important initiative and contribute to improving the lives of children across Tanzania," Laiser added.

JKCI Welcomes the Support

Receiving the donation, Jakaya Kikwete Cardiac Institute Executive Director, Dr. Peter Kisenge, praised Absa Bank Tanzania for its contribution, describing it as timely and impactful for children requiring specialised heart treatment.

According to Dr. Kisenge, heart disease continues to rise globally and in Tanzania, with children increasingly affected. He noted that more than 70 percent of paediatric heart disease cases are congenital, while others develop after birth.

"This support comes at a crucial time for many children and families in need of specialized cardiac care. Beyond helping us save lives, it highlights the important role that partnerships between the private sector and healthcare institutions can play in strengthening healthcare delivery and improving patient outcomes in Tanzania."

VODACOM TANZANIA YANG’ARA KWENYE UZINDUZI WA MAONESHO YA 50 YA SABASABA 2026

  • Yatwaa tuzo mbili ikiwemo mshindi wa tatu wa jumla 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire (kulia), kuhusu huduma ya simu mpya ya smati kitachi inayouzwa na kampuni hiyo ili kuwawezesha Watanzania kuingia katika ulimwengu wa kidijitali wakati Marais hao walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA). Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo wakipokea maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa maonesho hayo. Maonesho hayo yamefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili, ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), wakifurahia ushindi baada ya kampuni yao kutunukiwa tuzo mbili: Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi Julai 3, 2026, na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye kabla ya hafla ya ufunguzi aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutembelea banda la Vodacom na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitazama huduma mbalimbali zilizokuwepo ndani ya banda la Vodacom, wakati wa kutembelea banda hilo muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), baada ya kupata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma zinazotolewa na kampuni hiyo. Rais Samia aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho hayo. Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Tukio hilo lilifanyika Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

TANZANIA BREWERIES SHAREHOLDERS APPROVE 2025 ACCOUNTS AFTER STRONG YEAR OF PROFITABLE GROWTH

From left: Ami R. Mpungwe, Interim Chairman of the Board of Tanzania Breweries PLC (TBL), Michelle Kilpin, Managing Director of TBL (centre), and Avito Swai, Finance Director of TBL (right) speaking with shareholders during the TBL Annual General Meeting, where shareholders approved the company's 2025 audited financial statements following a year of profitable growth.

Dar es Salaam, Tanzania — Thursday, 2 July 2026: Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL Plc) has successfully held its 53rd Annual General Meeting (AGM) at the Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) in Dar es Salaam, with shareholders also participating virtually via an online meeting platform.

The AGM provided shareholders with an opportunity to review the company’s performance for the financial year ended 31 December 2025, approve key governance resolutions, and engage directly with the Board of Directors and Management on the company’s strategic direction.

Strong shareholder approvals and governance resolutions

During the meeting, shareholders approved the minutes of the 52nd AGM and formally adopted the Directors’ Report, Auditors’ Report, and audited financial statements for the year ended 31 December 2025.

The AGM also ratified the interim dividend paid during the year, reaffirming shareholder confidence in the company’s performance and capital allocation approach.

In addition, shareholders approved the appointment of PricewaterhouseCoopers (PwC) as external auditors for the financial year ending 31 December 2026, reinforcing TBL Plc’s commitment to strong governance and transparency.

Strong financial performance in 2025

TBL Plc reported a solid year of profitable growth, supported by strong demand across its beer and spirits portfolio, disciplined cost management, and continued investment in brand building and route-to-market efficiency.

Key highlights include:

  • Revenue growth of 13%
  • Operating profit increase of 35%
  • Improved execution across distribution and customer channels
  • Ongoing brand investment across core and premium segments

This performance reflects sustained consumer demand and the company’s ability to navigate a dynamic operating environment while strengthening profitability.

Leadership confidence in long-term growth

Speaking at the AGM, Ambassador Ami R. Mpungwe, Interim Chairman of the Board, emphasized the importance of governance, accountability, and long-term value creation.

He noted that the AGM remains a critical platform for transparency and engagement with shareholders, reaffirming the Board’s focus on safeguarding value and supporting sustainable business growth.

TBL Plc Managing Director, Michelle N. Kilpin highlighted the strength of the company’s ecosystem, pointing to its brands, people, customers, and partners as key drivers of performance.

She reaffirmed the company’s commitment to continued investment in consumer brands, digital platforms, local sourcing, and operational efficiency, while maintaining a strong focus on responsible and sustainable growth.

NMB YASOGEZA HUDUMA ZA BIMA KIDIJITALI KUPITIA UMEBIMA MINI APP

DAR ES SALAAM – Benki ya NMB imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za bima kwa njia ya kidijitali kupitia Umebima Mini App, huduma iliyounganishwa ndani ya programu ya NMB Mkononi, inayowawezesha wateja kununua bima kwa urahisi, usalama na haraka kupitia simu zao za mkononi.

NMB ilitoa taarifa hiyo wakati wa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo benki hiyo imeendelea kuonesha ubunifu wa huduma za kifedha zinazochochea uchumi wa kidijitali, sambamba na kauli mbiu ndogo ya maonesho ya mwaka huu, "Biashara za Tanzania Kidijitali Zaidi."

Akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho hayo, Mkuu wa Idara ya Bima wa Benki ya NMB, Martin Massawe, alisema kuwa Umebima Mini App ni sehemu ya mkakati wa benki wa kurahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa Watanzania kupitia teknolojia.

Alieleza kuwa huduma hiyo imeondoa ulazima kwa mteja kufika katika tawi la benki au ofisi za kampuni za bima ili kupata huduma. Badala yake, mteja anaweza kuchagua na kununua bima inayokidhi mahitaji yake popote alipo kupitia programu ya NMB Mkononi.

"Kwa kutumia Umebima Mini App, mchakato wa kupata bima umekuwa rahisi zaidi, salama na wa haraka, hivyo kuwawezesha wateja kupata kinga ya kifedha kwa urahisi kupitia simu zao," alisema Massawe.

Alisisitiza kuwa bima ni nyenzo muhimu ya usalama wa kifedha kwa watu binafsi, familia na biashara, kwani huwasaidia kukabiliana na athari za majanga na matukio yasiyotegemewa ambayo yanaweza kusababisha hasara kubwa za kifedha.

Kwa kutambua mahitaji tofauti ya wateja, NMB imeendelea kubuni bidhaa mbalimbali za bima zinazolenga makundi mbalimbali ya jamii. Miongoni mwa bidhaa hizo ni Matching Insurance, inayolenga wafanyabiashara wadogo na wamiliki wa biashara ndogo ndogo kwa kuwapatia kinga ya bima kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kidijitali.

NMB STRENGTHENS DIGITAL INSURANCE ACCESS THROUGH UMEBIMA MINI APP

DAR ES SALAAM – As Tanzania continues to embrace digital transformation across industries, financial institutions are expanding innovative solutions that make essential services more accessible to customers. Reinforcing this commitment, NMB Bank has enhanced access to digital insurance services through its Umebima Mini App, an integrated platform within the NMB Mkononi mobile banking application that enables customers to purchase insurance conveniently from their smartphones.

The announcement was made during the 50th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF), popularly known as Sabasaba, where NMB showcased its growing portfolio of digital financial solutions in line with this year's sub-theme, "Digitalizing Tanzanian Businesses."

Speaking to journalists at the exhibition, Martin Massawe, Head of the Insurance Department at NMB Bank, said the Umebima Mini App reflects the bank's commitment to supporting Tanzania's digital economy by making insurance products simpler, faster, and more accessible to all customers.

According to Massawe, the platform eliminates the need for customers to visit a bank branch or insurance office. Instead, users can browse, select, and purchase insurance policies that best suit their personal or business needs directly through the NMB Mkononi app, wherever they are.

He noted that the fully digital process offers customers a secure, convenient, and efficient way to access insurance services, supporting the country's broader financial inclusion agenda.

Expanding Financial Protection

Massawe emphasized that insurance remains one of the most important tools for financial security, helping individuals, families, and businesses protect themselves against unforeseen risks and financial losses.

To address the diverse needs of Tanzanians, NMB has developed a range of insurance products tailored to different customer segments. Among these is Matching Insurance, a specialized product designed for small-scale entrepreneurs and micro-business owners, providing affordable protection for their businesses through a simple digital application process.

Thursday, 2 July 2026

VODACOM YAIMARISHA MCHANGO KATIKA UKUAJI WA UCHUMI KUELEKEA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Dar es Salaam – Vodacom Tanzania Plc, kampuni pekee ya mawasiliano iliyoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), imetambuliwa kuwa mmoja wa walipa kodi wakubwa nchini, hatua inayoakisi dhamira yake ya kuendesha biashara kwa uwazi, uwajibikaji na kwa kuzingatia sheria huku ikiendelea kuchangia maendeleo ya uchumi wa Tanzania.

Tuzo hiyo, iliyotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inatambua mchango mkubwa wa Vodacom Tanzania katika ulipaji wa kodi pamoja na nafasi yake muhimu katika kuchochea maendeleo ya taifa kupitia uwekezaji na ubunifu.

Akipokea tuzo ya Mlipakodi Bora katika Sekta ya Mawasiliano wakati wa hafla ya utoaji wa Tuzo za Walipa Kodi iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire alisema mafanikio ya kampuni hayaishii katika kutoa huduma bora za mawasiliano pekee, bali pia yanajidhihirisha kupitia mchango wake katika maendeleo ya taifa.

Alieleza kuwa Vodacom imeendelea kuchangia ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupitia ulipaji wa kodi, uwekezaji katika miundombinu ya kidijitali, kuendeleza ubunifu, pamoja na kukuza rasilimali watu ili kuimarisha uchumi wa kidijitali.

Kwa mujibu wa kampuni hiyo, utambuzi huo unaimarisha dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuharakisha mageuzi ya kidijitali yanayowanufaisha Watanzania wote.

Wakati Tanzania ikiendelea kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Vodacom Tanzania imeahidi kuendelea kuwekeza katika teknolojia za kidijitali, miundombinu ya mawasiliano na maendeleo ya ujuzi wa kidijitali ili kuharakisha ujumuishi wa kidijitali, kuongeza tija na kuchochea ukuaji wa uchumi shirikishi.

PUMA ENERGY HONOURED WITH PRESIDENTIAL BEST TAXPAYER AWARD FOR OUTSTANDING TAX COMPLIANCE

Dar es Salaam, Tanzania – Puma Energy Tanzania has been honoured with the prestigious Presidential Best Taxpayer Award, earning recognition as the Best Wet Cargo Importer during the Presidential Awards for Best Taxpayers held as part of the Tanzania Revenue Authority's (TRA) 30th anniversary celebrations.

The award recognizes Puma Energy Tanzania as one of the country's most diligent and largest contributors of taxes and duties, underscoring the company's unwavering commitment to tax compliance, corporate governance, and national development.

The awards ceremony, presided over by the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan, brought together leading taxpayers from all 35 regions of the country in recognition of their vital role in strengthening domestic revenue collection and supporting Tanzania's economic transformation. Puma Energy Tanzania's award was presented by the President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, H.E. Dr. Hussein Ali Mwinyi.

A Strong Commitment to National Development

For many years, Puma Energy Tanzania has played a significant role in Tanzania's socio-economic development through consistent tax payments, dividend contributions to the Government as a shareholder, and strategic investments that enhance reliable, safe, and efficient energy services across the country.

Speaking after receiving the award, Puma Energy Tanzania Managing Director Fatma Abdallah described the recognition as a testament to the company's unwavering commitment to accountability, integrity, transparency, and full compliance with Tanzanian laws.

"This award is a great honour to us and gives us the motivation to continue fulfilling our responsibilities effectively. It reflects the collective efforts of our employees, our strong partnership with the Government, and our commitment to conducting business transparently and in full compliance with the country's laws," she said.

HALOTEL AND SAMSUNG ELECTRONICS PARTNER TO LAUNCH DEVICE FINANCING SOLUTION AT SABA SABA 2026

Dar es Salaam, Tanzania – 2 July 2026

Halotel Tanzania and Samsung Electronics East Africa have officially unveiled a new device financing solution bundled with affordable mobile packages, designed to make smartphone ownership more accessible to Tanzanians. The launch took place at the Halotel Booth during the 50th Dar es Salaam International Trade Fair (Saba Saba 2026).

The initiative marks a major milestone in advancing digital inclusion in Tanzania by enabling customers to acquire Samsung smartphones through flexible financing plans combined with Halotel connectivity bundles. The offer ensures users are not only able to access modern devices but also remain connected from the moment of purchase.

Driving Digital Inclusion and Connectivity

As Tanzania continues to accelerate its digital transformation across key sectors such as education, business, and public services, access to smartphones remains a critical enabler. This partnership directly addresses affordability barriers by introducing structured payment options tailored to different customer segments.

The solution is expected to significantly expand smartphone penetration, particularly among students, young professionals, entrepreneurs, and families seeking reliable access to digital services.

Through this collaboration, Halotel reinforces its commitment to ensuring that more Tanzanians are included in the digital economy by providing affordable connectivity and device accessibility under one integrated offering.

Empowering Youth and the Digital Economy

A key focus of the initiative is youth empowerment. By improving access to smartphones and data services, the partnership is expected to support learning, innovation, entrepreneurship, and participation in the growing digital economy.

The bundled packages are designed to offer both affordability and convenience, helping users maximize the value of their devices while staying connected through Halotel’s nationwide network.

Leadership Perspectives

Speaking during the official launch, Halotel Tanzania Deputy Managing Director Madam Tran Thi Thuy Dung emphasized the company’s mission to expand digital access:

At Halotel, we believe that everyone should have the opportunity to experience the benefits of digital connectivity. Through this partnership with Samsung Electronics East Africa, we are making quality smartphones more affordable and accessible to Tanzanians, particularly the young generation, while ensuring they enjoy reliable and affordable connectivity through Halotel bundles. This initiative reflects our commitment to empowering communities and supporting Tanzania's digital transformation.”

NMB, UNCDF OPEN NEW GROWTH PATHWAY FOR TANZANIA’S DIGITAL START-UPS

NMB Bank Chief Technology and Digital Transformation Officer, Kwame Makundi (seated left) and United Nations Capital Development Fund (UNCDF) Executive Secretary, Pradeep Kurukulasuriya sign a Memorandum of Understanding in Dar es Salaam to advance the third phase of the PesaTech programme, aimed at strengthening Tanzania’s fintech and start-up ecosystem. Looking on is Paola Trevisani (centre), Head of Infrastructure and Regional Cooperation at the European Union Delegation to Tanzania and the East African Community, alongside other officials.
NMB Bank Chief Technology and Digital Transformation Officer, Kwame Makundi (centre) exchanges signed Memorandum of Understanding documents with UNCDF Executive Secretary Pradeep Kurukulasuriya in Dar es Salaam. The agreement advances the third phase of the PesaTech programme, through which fintechs and start-ups will receive mentorship, market linkages and opportunities to integrate their solutions into the NMB digital ecosystem. Looking on is Paola Trevisani, Head of Infrastructure and Regional Cooperation at the European Union Delegation to Tanzania and the East African Community.

DAR ES SALAAM – NMB Bank has strengthened its commitment to Tanzania's digital innovation agenda by signing a strategic partnership with the United Nations Capital Development Fund (UNCDF) aimed at accelerating the growth of technology-driven start-ups through financing, mentorship, regulatory support, and access to markets.

The new collaboration seeks to create a stronger innovation ecosystem by connecting entrepreneurs with financial institutions, investors, government agencies, and business opportunities, enabling digital solutions to grow into sustainable enterprises that address real economic and social challenges.

The Memorandum of Understanding (MoU) was signed in Dar es Salaam by NMB Bank Chief Technology and Digital Transformation Officer, Kwame Makundi, and UNCDF Executive Secretary, Pradeep Kurukulasuriya.

Building on the Success of PesaTech

The agreement expands a partnership first launched in 2022 through the PesaTech Programme, an initiative designed to nurture technology start-ups developing innovative solutions for financial services and other key sectors of Tanzania's economy.

Speaking during the signing ceremony, Mr. Makundi said the collaboration has entered a new growth phase following the encouraging performance of the programme's first two cohorts.

According to him, 20 start-ups have already benefited from the programme, with five currently working directly with NMB Bank.

KADI MPYA YA NMB YAFUNGUA FURSA ZA MITAJI KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA KATI

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi (katikati), Mkurugenzi wa Mastercard anayesimamia biashara Afrika Mashariki, Imelda Ngunzu, na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, wakizindua rasmi kadi maalumu ya NMB SME World Business Credit Card jijini Arusha.

ARUSHA – Benki ya NMB, kwa kushirikiana na Mastercard, imezindua NMB SME World Business Credit Card, bidhaa mpya ya kifedha inayolenga kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) kupata mtaji wa haraka, kufanya malipo ya ndani na kimataifa kwa urahisi, na kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika jijini Arusha, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema kadi hiyo imebuniwa kukidhi mahitaji ya wafanyabiashara wanaohitaji mtaji wa muda mfupi ili kuendeleza shughuli zao za kila siku.

Alieleza kuwa kadi hiyo inatoa mkopo wa hadi Shilingi milioni 50, kulingana na uwezo wa kifedha wa mteja, pamoja na kipindi cha hadi siku 53 bila riba, endapo deni litarejeshwa ndani ya muda huo. Mfumo huo unawapa wafanyabiashara nafasi ya kuongeza bidhaa, kulipa wasambazaji kwa wakati na kushughulikia changamoto za mtaji bila kuathiri mzunguko wa biashara zao.

Mbali na huduma ya mkopo, NMB SME World Business Credit Card inaweza kutumika kupitia mtandao wa Mastercard katika mamilioni ya maeneo duniani, hivyo kuwawezesha wafanyabiashara kufanya malipo ya kimataifa kwa usalama na urahisi.

Kadi hiyo pia inakuja na manufaa mbalimbali yanayoongeza thamani kwa watumiaji wake, ikiwemo bima ya matibabu ya safari yenye thamani ya hadi Dola za Marekani 100,000, bima ya mizigo, huduma za VIP Lounge katika zaidi ya viwanja vya ndege 400 duniani, pamoja na punguzo maalumu katika hoteli na huduma nyingine mbalimbali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mastercard anayesimamia biashara za SMEs Afrika Mashariki na Visiwa vya Bahari ya Hindi, Imelda Ngunzu, alisema uzinduzi wa kadi hiyo unaonesha dhamira ya Mastercard na NMB ya kusaidia ukuaji wa biashara ndogo na za kati kupitia suluhisho za kisasa za kifedha.

TRADE MINISTER VISITS NMB PAVILION AT 50TH DAR ES SALAAM INTERNATIONAL TRADE FAIR

Minister for Industry and Trade, Hon. Judith Kapinga (MP) (left), is welcomed by NMB Bank’s Head of Branch Network and Sales, Donatus Richard, during her visit to the bank’s pavilion at the ongoing 50th Dar es Salaam International Trade Fair.

DAR ES SALAAM – The Minister for Industry and Trade, Hon. Judith Kapinga (MP), visited the NMB Bank pavilion at the ongoing 50th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF), where she received an overview of the bank's innovative banking solutions designed to support businesses, expand financial inclusion, and accelerate Tanzania's digital economy agenda.

The Minister was received by NMB Bank's Head of Branch Network and Sales, Donatus Richard, who welcomed her to the bank's exhibition pavilion and highlighted the institution's commitment to providing accessible, technology-driven financial services for individuals, entrepreneurs, and businesses of all sizes.

During the visit, Hon. Kapinga was briefed on NMB's wide range of banking products and digital financial solutions that are empowering businesses to grow, enhancing access to formal financial services, and supporting the Government's vision of building an inclusive and digitally enabled economy.

The discussions also focused on the bank's continued investment in digital banking platforms, customer-centric innovations, and tailored financial solutions that enable enterprises to improve operational efficiency while expanding their participation in Tanzania's rapidly evolving economic landscape.

NMB's presence at the 50th DITF underscores the bank's strategic role in promoting entrepreneurship, facilitating trade, and providing financial services that contribute to sustainable economic development. Through its participation, the bank continues to engage with customers, investors, and business stakeholders while showcasing solutions that respond to the changing needs of Tanzania's growing economy.

The Dar es Salaam International Trade Fair remains one of Tanzania's premier business and investment platforms, bringing together local and international exhibitors to showcase products, services, innovations, and investment opportunities that drive industrialization and economic growth.

NMB YASOGEZA HUDUMA KAMILI ZA KIBENKI KWA WANANCHI KATIKA SABA SABA 2026

Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, William Nkuna (katikati, mwenye shati jeupe), akimwelekeza Afande Bwakiswa Mwakeja kuhusu huduma zinazopatikana katika Tawi la NMB Saba Saba katika kipindi chote cha maonesho. Kushoto ni Jumanne Magige Richard, Afisa Mauzo wa Benki ya NMB.

Dar es Salaam – Benki ya NMB imezindua rasmi huduma za Tawi la NMB Saba Saba, likiwa kituo kamili cha huduma za kibenki ndani ya Viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, hatua inayolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi, wafanyabiashara na waoneshaji katika kipindi chote cha maonesho.

Tawi hilo, lililopo katika makutano ya Mitaa ya Mabalozi na Carnivore, Kitalu Na. 24C, litatoa huduma kuanzia Juni 28 hadi Julai 13, 2026, likihudumia maelfu ya wageni wanaotembelea maonesho hayo ya kila mwaka.

Huduma zinazopatikana katika tawi hilo ni pamoja na kufungua akaunti mpya, kuweka na kutoa fedha, kufanya malipo mbalimbali ya Serikali, huduma za bima, ushauri wa mikopo pamoja na huduma za kidijitali zinazorahisisha miamala ya kifedha.

Mbali na huduma za kibenki, NMB pia inaendelea kutoa elimu ya fedha kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya fedha, umuhimu wa kuweka akiba, ukopaji wenye uwajibikaji pamoja na usalama wa miamala ya kidijitali. Aidha, tawi hilo lina mashine ya ATM yenye uwezo wa kuweka na kutoa fedha, huku mawakala wa NMB wakisambazwa katika maeneo mbalimbali ya viwanja vya maonesho ili kuongeza urahisi wa upatikanaji wa huduma.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hizo, Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, William Nkuna, alisema hatua hiyo inawezesha wananchi, wafanyabiashara na waoneshaji kupata huduma zote muhimu za kibenki bila kulazimika kutoka nje ya Viwanja vya Saba Saba.

"Tawi la NMB Saba Saba linafanya kazi kama tawi kamili katika kipindi chote cha maonesho. Tumefungua rasmi huduma zake kwa umma ili wananchi, wafanyabiashara na waoneshaji wapate huduma za kibenki, elimu ya fedha na ushauri wa kitaalamu," alisema Nkuna.

Aliongeza kuwa wataalamu kutoka vitengo mbalimbali vya benki wanapatikana kutoa ushauri kuhusu mikopo ya biashara, kilimo na ujenzi, huduma za bima, ufunguzi wa akaunti pamoja na matumizi ya huduma za kidijitali za NMB Mkononi Super AppNMB Tap to Pay na NMB UmeBIMA.

NMB BRINGS FULL BANKING SERVICES TO SABA SABA AS TRADE FAIR OPENS OPPORTUNITIES FOR BUSINESSES

DAR ES SALAAM, Tanzania – NMB Bank has officially commenced full banking operations at its dedicated Saba Saba Branch pavilion within the Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) grounds, providing exhibitors, traders, businesses and thousands of visitors with comprehensive banking services throughout the 2026 exhibition.

The fully operational branch, located at the junction of Mabalozi and Carnivore Streets (Plot 24C), will serve customers from June 28 to July 13, 2026, offering convenient access to a broad range of banking products and financial advisory services without requiring customers to leave the exhibition grounds.

The initiative reinforces NMB's commitment to bringing financial services closer to Tanzanians while supporting commercial activities during one of the country's largest annual trade exhibitions.

Comprehensive Banking Services at the Fair

The temporary branch functions like any permanent NMB outlet, providing customers with a full suite of banking services, including:

  • Opening new bank accounts
  • Cash deposits and withdrawals
  • Government payments
  • Insurance services
  • Loan advisory and financing solutions
  • Digital banking support

To further improve convenience, the branch is equipped with a cash deposit and withdrawal ATM, complemented by NMB banking agents strategically stationed across the exhibition grounds to facilitate seamless transactions.

Financial Literacy at the Heart of the Initiative

Beyond transactional banking, NMB is using the Saba Saba platform to promote financial inclusion through practical financial education.

Visitors are receiving guidance on budgeting, saving, responsible borrowing and the safe use of digital financial services, helping individuals and entrepreneurs make informed financial decisions while embracing modern banking technologies.

Bringing Banking Closer to Customers

Speaking during the commencement of operations, NMB Acting Dar es Salaam Zonal Manager William Nkuna said the decision to establish a fully operational banking branch at the exhibition reflects the bank's commitment to improving customer convenience and supporting economic activity during the trade fair.

"The NMB Saba Saba Branch is operating as a fully functional banking outlet throughout the exhibition. We have officially opened its services to the public so that residents, businesses and exhibitors can access banking services, financial education and professional guidance," said Mr. Nkuna.

VODACOM TANZANIA YADHIHIRISHA DHAMIRA YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI ZA WATEJA

Mkurugenzi wa Sheria wa Vodacom Tanzania PLC, Olaf Mumburi (wa pili kulia), akizungumza wakati wa mkutano wa kwanza wa mwaka wa Ulinzi wa Faragha na Taarifa Binafsi, akiwa mmoja wa wazungumzaji katika majadiliano kuhusu ulinzi wa taarifa za kifedha na uchumi wa kidijitali. Mjadala huo uliwahusisha Wakili Dirontsho Mohale kutoka Taasisi ya Baakaedi Profesional Practice (Pty) Ltd - Afrika Kusini (kushoto), Mwakilishi kutoka Benki ya Stanbic Tanzania, Winston Ishengoma (wa pili kushoto), na Mwakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania Abdallah Thabiti.
Mkurugenzi Mtendaji Idara ya Taarifa Binafsi wa Vodacom Group Afrika Kusini, David Smuts (wa pili kushoto), akizungumza wakati wa mdahalo uliofanyika katika Mkutano wa Kwanza wa Mwaka wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Mdahalo huo pia uliwashirikisha Mkuu wa Idara ya Sheria na Faragha katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Doreen Mwamtangala (kulia); Mkuu wa Uzingatiaji wa Sheria na Utawala wa Benki ya CRDB Plc, Paulo Mwiru (wa pili kulia); na Mkurugenzi wa Usajili na Uzingatiaji wa Sheria katika Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Mhandisi Steven Wangwe (kushoto).

Ni katika mkutano wa kwanza wa mwaka wa ulinzi wa faragha ulioandaliwa na PDPC

Dar es Salaam, Tanzania – Juni 30 hadi Julai 1, 2026

Vodacom Tanzania PLC imeonesha uongozi wake katika kuendeleza majadiliano ya kitaifa na kikanda kuhusu ulinzi wa taarifa binafsi, uaminifu wa kidijitali na ubunifu unaowajibika, kupitia ushiriki wake katika Mkutano wa Kwanza wa Mwaka wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo mkubwa uliwakutanisha wadhibiti wa sekta, viongozi wa taasisi za kifedha, wataalamu wa sheria na wadau wa teknolojia kujadili mustakabali wa usimamizi wa taarifa binafsi katika uchumi unaozidi kuendeshwa kidijitali.

Kuimarisha Usimamizi wa Faragha katika Uchumi wa Kidijitali

Akizungumza katika moja ya majadiliano ya ngazi ya juu, Mkurugenzi wa Sheria wa Vodacom Tanzania PLC, Olaf Mumburi, alishiriki kama mmoja wa wazungumzaji katika mjadala uliolenga ulinzi wa taarifa za kifedha na uchumi wa kidijitali.

Mjadala huo uliwahusisha pia Wakili Dirontsho Mohale kutoka Baakedi Professional Practice (Pty) Ltd ya Afrika Kusini, mwakilishi wa Benki ya Stanbic Tanzania Winston Ishengoma, pamoja na mwakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Abdallah Thabiti.

Washiriki hao walisisitiza umuhimu wa kulinda taarifa za kifedha katika kipindi ambacho huduma za kifedha kidijitali zinaendelea kukua kwa kasi nchini Tanzania na katika ukanda wa Afrika Mashariki.