Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 26 July 2024

MAANDALIZI YA NBC DODOMA MARATHON 2024 YAKAMILIKA - 28 JULAI 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule (wa pili kulia) akipokea sweta maalum la mbio za NBC Dodoma Marathon kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, Godwin Semunyu (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bi Tasiana Massimba (kulia) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi mkuu wa mkoa huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mbio hizo zinalenga kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama na mtoto makabiziano hayo yamefanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dodoma leo. Kushoto ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bi Joyce Fisoo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule (katikati) akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya fulana maalum za mbio za NBC Dodoma Marathon mwaka 2024 mara baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, Godwin Semunyu (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bi Tasiana Massimba (Kulia) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi mkuu wa mkoa huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo RC Senyamule (pichani) pamoja na kuipongeza benki ya NBC kwa maandalizi hayo mazuri alisema ujio wa mbio hizo mkoani humo kwa miaka mitano sasa umekuwa ukiambatana na fursa mbalimbali ikiwemo ongezeko la mzunguko wa fedha unaotokana na ongezeko la mahitaji ya chakula, vinywaji,mavazi na malazi kutona na idadi kubwa ya watu wanaotoka mikoa mbalimbali ili kushiriki mbio hizo jijini humo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon Bi Tasiana Massimba (Pichani) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28, mwaka huu jijini Dodoma.
Awali akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, ambayo ndio inaratibu mbio hizo Bw Godwin Semunyu (pichani) alisema maandalizi yote yamekamilika na tayari washiriki mbalimbali wa mbio zinazohusisha umbali wa km5, km10, km21 na km42 wanaendelea kuingia jijini humo ili kushiriki mbio hizo.
Akizungumza kwenye mkutano huo Mkuu wa Kanda ya Kati wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Bw Joseph Sayi (pichani) alisema kampuni hiyo ikiwa kama mdau mkuu wa mawasiliano kwenye mbio hizo imejipanga kutoa huduma ya mawasiliano ya internet bure kwa washiriki wote wa mbio hizo.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon wakifutilia mkutano huo.

Dodoma, 26 Julai 2024: Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule amethibitisha kukamilika kwa maadalizi ya msimu wa tano mbio za NBC Dodoma Marathon huku akionyesha kuridhishwa na ubora wa mbio hizo sambamba na mchango wake katika kuchochea kasi ya Uchumi wa mkoa huo kupitia sekta za biashara, michezo na utalii.

Mbio zinatarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama na mtoto. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza washiriki zaidi ya 8,000 waliothibitisha kushiriki mbio hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo RC Senyamule pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa maandalizi hayo mazuri alisema ujio wa mbio hizo mkoani humo kwa miaka mitano sasa umekuwa ukiambatana na fursa mbalimbali ikiwemo ongezeko la mzuguko wa fedha unaotokana na ongezeko la mahitaji ya chakula, vinywaji,mavazi na malazi kutona na idadi kubwa ya watu wanaotoka mikoa mbalimbali ili kushiriki mbio hizo jijini humo.

“Kukamilika kwa maadalizi ya mbio hizo tena katika viwango vya kimataifa kunatoa taswira sahihi ya hadhi ya mbio hizo na jiji la Dodoma kama makao makuu ya nchi. Nitoe wito kwa wananchi wa jiji la Dodoma hususani wafanyabiashara kuchangamkia fursa mbalimbali zitokanazo na ongezeko hili la watu ambao nje ya washiriki hao 8,000 waliothibitisha kushiriki pia wapo wengine zaidi walioambatana nao.’’ Alisema.

TANZANIA BREWERIES LIMITED HOSTS 51ST ANNUAL GENERAL MEETING

TBL Board Chairman, Mr. Leonard Mususa addresses shareholders during the 51st Annual General Meeting (AGM) held at the Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam yesterday. This event highlighted TBL PLC’s financial performance, strategy and market position. With him left is the Company Secretary, Esther Kuja and Board Member, Phocus J.I. Lasway (right).

Dar es Salaam, July 25, 2024 - Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL PLC), Tanzania's leading beverage manufacturer, is delighted to announce its 51st Annual General Meeting (AGM) at the renowned Julius Nyerere International Convention Centre. This event will highlight TBL's financial performance, strategy, and market position.


The AGM, expected to be attended by various stakeholders, will cover the growth and development of TBL and the entire group, as well as the challenges faced over the past year. TBL will also showcase how their applied innovations in driving production growth.


A crucial agenda item at the AGM will be the ratification of dividends paid of TZS 537 per share (equivalent to TZS 158,445 million) for the year ended December 31, 2023, an 85% increase over the prior year. This illustrates TBL PLC's commitment in delivering consistent returns to its esteemed shareholders.


TBL Board Chairman Mr. Leonard Mususa, said, "We are proud to announce that despite the challenging operating conditions of 2023, including global geopolitical tensions and local excise duty hikes, Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL PLC) demonstrated resilient growth and delivered significant value to our shareholders. Our steadfast execution of strategic initiatives and the market's confidence in our diverse portfolio of brands resulted in a notable increase in revenue, enabling us to approve and distribute a dividend of TZS 537 per share—an impressive 85% increase over the previous year. This accomplishment underscores our commitment to creating long-term value for our shareholders and reinforces our position as one of the nation’s leading contributors to economic growth."


Furthermore, the AGM involved the approval of the appointment of PricewaterhouseCoopers as the external auditors for the upcoming financial year ending December 31, 2024, highlighting TBL PLC's unwavering dedication to sound financial governance and transparency.

WANANCHI NDANI YA DStv BOMBA; KAIZER CHIEFS vs YANGA 28 JULAI SAA 10:00

#tumewasikiliza
#mbungibampa2bampa

VODACOM YAZINDUA KAMPENI YA “NI BALAAA” KILA MTU NI MSHINDI

Ni Balaaa! George Lugata (kushoto), Mkuu wa Idara ya Mauzo na Usambazaji, Athumani Mlinga, Mkurugenzi wa Kitengo cha TEHAMA, Grace Chambua, Kaimu Mkurugenzi wa Biashara na Epimack Mbeteni, Mkurugenzi wa M-Pesa wote kutoka Vodacom Tanzania Plc wakizindua kampeni ya "Ni Balaaa" iliyofanyika tarehe 25 Julai 2024 Gerezani - Kariakoo jijini Dar es Salaam. Kampeni hiyo ya miezi minne inalenga kuwazawadia wateja wa kampuni hiyo zawadi za kila siku shilingi 100,000, wiki shilingi 500,000, mwezi shilingi milioni moja na hatimaye kuwapata washindi wakuu watano ambapo kila mmoja atapata shilingi 20 milioni.

Julai 25, 2024, Dar es Salaam: Kampuni ya Teknolojia na Mawasiliano Vodacom Tanzania Plc imezindua kampeni kabambe inayojulikana kama “Ni Balaaa” ikiwa na lengo la kuwanufaisha wateja wake na jamii nzima kiujumla. Kampeni hii kubwa na ya kitaifa inalenga kunufaisha watanzania wengi ambapo kutakuwa na washindi wa kila siku, wiki, mwezi na washindi watano wa zawadi kuu huku wote wakiondoka na zawadi kemkem ikiwemo fedha taslimu.


“Kampeni ya Ni Balaaa inalenga kuwazawadia wateja wetu kila wanaponunua kifurushi (bando) au kufanya miamala kupitia M-Pesa na pia kutoa nafasi kwa washindi wa zawadi kuu, kupendekeza Shule za Msingi katika Jamii zao na Vodacom Tanzania itafanya maboresho katika maktaba za shule hizo kama vile kuwapatia vitabu, makabati ya kuhifadhia vitabu na samani za kusomea”, alisema Grace Chambua, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara kutoka Vodacom Tanzania wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika Kariakoo-Gerezani, jijini Dar es Salaam.


Kampeni hii yenye kaulimbiu ya ‘Kila Mtu ni Mshindi’ inaanza mwezi huu wa Julai mpaka Oktoba mwaka huu huku ikiwa na washindi wa kila siku wa shilingi 100,000/-, washindi wa wiki wa shilingi 500,000/- huku wale wa mwezi wakiondoka na shilingi milioni moja, na washindi watano wa zawadi kuu ambao kila mmoja ataondoka na kibunda cha shilingi milioni 20!


Akielezea namna ya kushinda kupitia M-Pesa, Epimack Mbeteni, Mkurugenzi wa M-Pesa kutoka kampuni hiyo, alisema, “kila muamala unaoufanya kupitia M-Pesa katika kipindi cha kampeni unaongeza nafasi yako ya kushinda. Iwe unatuma pesa kwa familia, unalipia bili au unatumia M-Pesa super App kwa miamala na malipo ya kila siku.”


Mbeteni aliongezea kuwa kampeni ya ‘Ni Balaaa” itakuwa shirikishi ili kuwezesha kila mteja popote pale alipo bila kujali umbali wala hali yake ya kiuchumi kuibuka na ushindi wa aina tofauti.


“M-Pesa inamrahishia kila mtu kufanya miamala, ikiwemo wafanyabiashara kama nyie mliotuzunguka hapa Kariakoo. Yaani popote pale ulipo kila unapotumia M-Pesa basi moja kwa moja unaingia kwenye droo na hivyo kujiongezea nafasi ya kuibuka mshindi. Sisi tunasema Pesa ni M-Pesa na msimu huu “Ni Balaaa”, anamalizia Mbeteni.

Kwa kumalizia Bi. Chambua aliongezea kuwa kampeni hii itawagusa pia wamiliki wa biashara ndogo na za kati ambapo kwa kujiunga na SME Combo Bundles kutoka Vodacom sio tu zitawarahisishia shughuli zao za kibiashara, lakini pia zinawapa nafasi ya kushinda zawadi muhimu kama vile zana za usimamizi wa hesabu (inventory management system) au kamera za CCTV kwa ulinzi zaidi wa maeneo yao ya biashara.

BENKI YA EXIM YACHANGIA VITANDA KWA KITUO CHA AFYA TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Burian (kushoto) akikabidhi Cheti cha kuthamini mchango wa benki ya Exim Tanzania kwa mkoa wa Tanga kwa Stanley Kafu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano kutoka Benki ya Exim Tanzania wakati wa hafla ya makabidhiano ya msaada wa vitanda na Magodoro 21 kwa ajili ya kukamilisha mahitaji ya vitanda katika Kituo cha Afya cha Mwakidila kilichopo Jijini Tanga yaliyofanyika tarehe 25 Julai 2024.

Stanley Kafu, Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano kutoka Benki ya Exim Bank Tanzania,(wa nne kutoka kulia) akimkabidhi vitanda 21 na Magodoro 21 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt Batilda Burian kwa ajili ya kituo cha Afya Mwakidila wakati wa hafla ya makabidhiano ambayo yamefanyika katika kituo hicho Jijini Tanga tarehe 25 Julai 2024. Msaada huo umeenda kukamilisha mahitaji ya vitanda vilivyokuwa vinahitajika katika kituo hicho cha afya, Kushoto ni Fredrick Sagamiko, Mkurugenzi wa Jiji la Tanga.

Tanga: Exim Bank Tanzania imetoa jumla ya vitanda na magodoro 21 vya wagonjwa kwa kituo cha afya cha Mwakidila kilichopo jijini Tanga, mchango ambao umetatua kikamilifu tatizo la upungufu wa vitanda vya wagonjwa katika kituo hicho. Makabidhiano hayo, ambayo yamefanyika mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mh. Balozi Dkt Batilda Burian, ni sehemu ya juhudi za kuboresha huduma za afya katika mkoa huo. Kituo cha afya Mwakidila kilikuwa na vitanda 29 huku mahitaji yakiwa 50, hivyo mchango wa Exim Bank Tanzania umetatua tatizo hilo la muda mrefu katika hafla iliyofanyika mnamo tarehe 25 Julai 2024.

“Sekta ya afya nchini, ikiwemo mkoa wa Tanga, inakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo uhaba wa vifaa vya matibabu, upungufu wa vitanda, madawa, pamoja na uchache wa watoa huduma za afya ambavyo vimekuwa vikiathiri kwa kiasi kikubwa ubora wa huduma za afya,” anasema Bi Kauthar D’souza, Meneja Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano, Exim Bank Tanzania.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo jijini Tanga, Bi D’souza aliongeza, “Sisi kama Exim Bank Tanzania, tunatambua changamoto hizi na ndo maana tunajitolea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu ya afya ili kusaidia Watanzania wapate huduma bora za afya.”

Takwimu zinaonesha jitihada za ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika maeneo mbalimbali nchini ambao umewezesha vituo vya kutolea huduma za Afya kuongezeka kutoka vituo 8,549 Mwaka 2021 hadi vituo 9,693 mwaka 2024; kama taifa tumepiga hatua katika kusogeza huduma hizi muhimu karibu zaidi kwa jamii.

Thursday 25 July 2024

WASHINDI NBC DODOMA MARATHON KUIWAKILISHA TANZANIA KIMATAIFA

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akipokea sweta maalum la mbio za NBC Dodoma Marathon kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi Waziri huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama wa mtoto Makabiziano hayo yamefanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia) akimpongeza Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) baada ya kuthibitisha dahamira yake ya kukimbia km 42 kwenye mbio za NBC Dodoma Marathon zinazoratibiwa na benki hiyo kwa lengo la kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama wa mtoto. Dkt Ndumbaro amethibitisha dhamira hiyo hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akimpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon Bi Tatiana Masimba kwa maandalizi mazuri yam bio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama wa mtoto.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mbio za NBC Dodoma Marathon pamoja na mchango wa benki ya NBC katika kuendeleza sekta ya michezo nchini. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia) akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mbio za NBC Dodoma Marathon pamoja mchango wa benki ya NBC katika kuendeleza sekta ya michezo nchini. Kushoto ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro.

Dar es Salaam, 22 Julai 2024: Serikali imesisitiz dhamira yake ya kutumia mbio za NBC Dodoma Marathon kama chanzo cha kuwapata wanariadha sahihi watakaoliwakilisha taifa kwenye mashindano ya kimataifa yakiwemo mashindano ya Olympic na Mashindano ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth). Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro amebainisha dhamira hiyo ya serikali jijini Dar es Salaam huku akithibitisha nia yake ya kukimbia km 42 (full marathon) kwenye mbio hizo zinatotarajiwa kufanyika jijini Dodoma, Julai 28 mwaka huu.

Lengo kuu la mbio hizo zinazotarajiwa kuongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ni kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama wa mtoto.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya benki ya NBC akiwa sambamba na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw Theobald Sabi, Dkt Ndumbaro pamoja na kusifia jitihada za benki hiyo katika kuinua sekta ya michezo nchini, alisema kwasasa taifa linakabiliwa na uhaba mkubwa wa wanariadha wenye sifa ya kushiriki mashindano ya kimataifa hivyo serikali imejipanga kutumia mbio hizo kutambua wanariadha wenye sifa sahihi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano mbalimbali ya kimataifa.

“Kwasasa kwenye mashindano ya Olympic tunakwenda na wanariadha wachache sana kwasababu hatuna maandalizi ya kutosha. Hivyo NBC Dodoma Marathon ni moja ya chanzo cha kupata wanariadha wazuri ili baada ya mbio hizi tuweze kuwatamuba na kuwapa mafunzo zaidi ili mashindano ya ‘Commonwealth’ na Olympic na mengine mbalimbali ya kimataifa tuwe na wanariadha wengi zaidi.’’ Alibainisha Dkt. Ndumbaro huku akipongeza maandalizi ya mbio yenye kuzingatia viwango vya kimataifa.

Aidha Dkt. Ndumbaro aliipongeza benki hiyo kwa jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta ya utamaduni, sana ana michezo kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo udhamini wa michezo na huduma za kibenki zinazolenga kuwasaidia wadau mbalimbali wa sekta hizo.

BENKI YA PBZ YAZINDUA HUDUMA YA BIMA KUPITIA BENKI

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Bw Joseph Meza (kulia) na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya PBZ, Bw Arafat Haji (Kushoto) wakimkabidhi zawadi maalum Naibu Kamishna wa Bima Tanzania Bi Khadija Said wakati wa hafla ya utambulizo wa huduma ya bima kupitia benki (Bancassurance) ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuboresha zaidi huduma zake sambamba na kuongeza ujumuishaji wa jamii zaidi katika mfumo rasmi wa fedha kupitia huduma za bima. Hafla hiyo ilifanyika Zanzibar.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya PBZ, Bw Arafat Haji (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi huo.

Hafla ya utambulisho wa huduma hiyo ilifanyika Zanzibar ikiongozwa na Naibu Kamishna wa Bima Tanzania, Bi Khadija Said na kuhuduriwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya bima na wateja. Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya PBZ, Bw Arafat Haji aliwaongoza wafanyakazi wengine wa benki hiyo kwenye hafla hiyo muhimu.

Zanzibar, 24 Julai 2024: Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) imezidua huduma ya bima kupitia benki (Bancassurance) ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuboresha zaidi huduma zake sambamba na kuongeza ujumuishaji wa jamii zaidi katika mfumo rasmi wa fedha kupitia huduma za bima.

Zaidi hatua hiyo inatajwa kuwa inalenga kuunga mkono jitihada za serikali kupitia Mpango Mkakati wa Fedha wa miaka kumi (2020 -2030) unaolenga kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya watanzania wana uelewa wa kutosha kuhusu huduma za bima huku asilimia 50 wakiwa wanatumia huduma za bima.

Hafla ya utambulisho wa huduma hiyo ilifanyika jana Zanzibar ikiongozwa na Naibu Kamishna wa Bima Tanzania, Bi Khadija Said na kuhuduriwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya bima na wateja. Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya PBZ, Bw Arafat Haji aliwaongoza wafanyakazi wengine wa benki hiyo kwenye hafla hiyo muhimu.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Bi Said pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa hatua hiyo muhimu alisema huduma hiyo itasaidia kuchochea kasi ya utoaji wa huduma za kibima visiwani humo na nchi nzima kwa ujumla huku pia ikitoa fursa nyingi za kiuchumi kupitia hakikisho la usalama wa mali za wananchi hususani waliopo pembezoni.

“Hatua hii ya PBZ ni muhimu sana kwetu serikali kwa kuwa inaunga mkono utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Fedha wa miaka kumi (2020 -2030) unaolenga kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya watanzania wana uelewa wa kutosha kuhusu huduma za bima huku asilimia 50 wakiwa wanatumia huduma za bima.’’ Alibainisha huku akitoa wito kwa benki hiyo kuendelea kutoa elimu zaidi kwa wananchi kuhusu umuhimu wa huduma za bima kupitia benki.

APPOINTMENT OF PETER NALITOLELA AS CEO OF DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE


This is to inform the public that The Board of Directors of Dar es Salaam Stock Exchange PLC (DSE) during its 30th Extra Ordinary Meeting held on 24th June 2024 approved the appointment of Mr. Peter Situmbeko Nalitolela as Chief Executive Officer of DSE effective 1st August 2024.

Mr. Nalitolela brings a wealth of experience and expertise garnered from large public and private sector organisations, most recently serving as Director and Head of Treasury & Financial Markets at National Bank of Commerce (NBC). He has financial markets experience with good exposure to other major sectors of the economy. He also has international exposure with good knowledge on how global markets work and he has engaged in primary and secondary markets. His personality is endowed with leadership skills embedded in humility and mindfulness. With this background, he is poised to drive growth and innovation at DSE.

The Board of Directors of DSE are confident that the appointment of Mr. Nalitolela will strengthen DSE's ability towards achieving key strategic objectives as well as creating enduring value for all shareholders.

On behalf of the Board of Directors, I extend heartfelt congratulations to Mr. Nalitolela on his appointment.

Ellinami Minja,
Chairman,
DSE Board of Directors.

BIG BROTHER NAIJA NDANI YA DStv! ZIMEBAKI SIKU 3 TU

Piga *150*53# kulipia kifurushi chako mapema usipitwe.

#burudanibampa2bampa

CHANELI 9 DStv KUONESHA MICHUANO YOTE YA OLYMPICS 2024





#olympics2024onDStv

Wednesday 24 July 2024

NMB YASHINDA TUZO 5 ZA KIMATAIFA, YATAJWA BENKI BORA TANZANIA 2024


Benki ya NMB imepokea Tuzo 5 za kimataifa ambazo kwa ujumla wake zinaitambua NMB kama benki kiongozi nchini katika biashara, utoaji huduma za kidijitali, kufuata misingi ya utawala bora na uzingatiaji wa maslahi ya jamii katika shughuli zake.


Tuzo hizo - zilizotolewa na Jarida la Kimataifa la Euro Money katika hafla iliyofanyika jijini London, Uingereza tarehe 18 Julai 2024 - ni pamoja na:
  • Benki Bora Tanzania (Kwa mara ya 11 ndani ya miaka 12)
  • Benki Bora ya Kidijitali Tanzania
  • Benki Bora inayofuata misingi imara ya Utawala Bora, Ustawishaji wa Jamii na Utunzaji Mazingira (ESG) Tanzania
  • Benki Bora ya Wateja Maalum Tanzania
  • Benki Bora ya Wateja Wenye Uwezo Mkubwa wa Kifedha Tanzania (High Net Worth Individuals)

Tuzo hizi zimepokelewa na Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB - Alfred Shao aliyeambatana na Meneja Mwandamizi wa Mahusiano ya Wawekezaji, Edgar Ndani na Afisa Uhusiano, Bethuel Kinyori.


“Tuzo hizi ni matokeo ya ufanisi wa kiutendaji kwa ujumla, mkakati wa matumizi ya njia za kidijitali, huduma jumuishi za fedha na uendeshaji wa biashara inayomgusa kila Mtanzania,” alisema Bw. Shao.


“Tunawashukuru Watanzania, wateja wetu ,wadau na wafanyakazi wetu wote kwa ujumla kwa kuendelea kutuamini na kutufanya washirika katika kukuza shughuli zenu kupitia masuluhisho yetu bunifu,” alisema Bw. Shao.




NBC CROWNED TANZANIA'S BEST BANK FOR CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITY

The Managing Director of NBC Bank, Theobald Sabi, holds a trophy after the bank was named Tanzania's Best Bank for Corporate Social Responsibility in the Euromoney Awards for Excellence 2024 held in London over the weekend. The prestigious recognition affirms NBC Bank's dedication to the economic and social empowerment of the communities it serves.

London, July 2024 - In a momentous achievement that solidifies its position as a trailblazer in sustainable development, NBC Bank has been named the Best Bank for Corporate Social Responsibility in Tanzania at the prestigious Euromoney Awards for Excellence 2024. This esteemed recognition is a testament to the bank's unwavering dedication to the economic and social empowerment of the communities it serves.

Theobald Sabi, the visionary Managing Director of NBC Bank, expressed immense pride in this historic accolade, emphasizing the bank's role as a catalyst for community upliftment and a provider of transformative financial solutions. With their guiding principle, "Conveniently Everywhere," NBC Bank has consistently offered a comprehensive range of traditional and cutting-edge digital financial services tailored to meet the diverse needs of its customers, ultimately improving their economic and social well-being.

"Being named Tanzania's Best Bank for Corporate Social Responsibility is a testament to our unwavering commitment to making a lasting, positive impact on society," Sabi remarked. "We firmly believe in empowering our communities and contributing to their sustainable development. This prestigious recognition motivates us to continue our relentless efforts in building a better Tanzania for all."

At the heart of NBC Bank's success lies its deep-rooted mission to empower communities and drive inclusive growth. Through a diverse portfolio of innovative banking products and services, the bank has consistently sought to address the varying financial needs of its customers, from the rural smallholder farmer to the urban entrepreneur. Initiatives like NBC Shambani, Kuanasi Account, Wafugaji Account, and Johari Account have been instrumental in championing financial inclusion, ensuring access to vital financial tools and resources for all.

But NBC Bank's influence extends far beyond the realm of traditional banking. The institution's unwavering commitment to sustainable development has manifested through a comprehensive array of impactful community-centric programs and initiatives, as meticulously detailed in their inaugural Sustainability Report for 2023. Sabi proudly highlighted the bank's significant contributions to education, healthcare, youth enterprise, and environmental conservation – all of which have had a transformative impact on the communities they serve.

Thursday 18 July 2024

BENKI YA EXIM YATOA VITANDA VYA WAJAWAZITO MKOANI MOROGORO

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro - Mhe. Judith Nguli (wa pili kushoto), ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akikagua moja ya vitanda vya wodi ya wazazi vilivyokabidhiwa na Exim Bank Tanzania kwa Mkoa wa Morogoro. Wengine ni Dkt. Best Magoma (kushoto) -  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Stanley Kafu (wa pili kulia) - Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo na Ibrahim Ukwaju - Meneja wa Tawi la benki hiyo Morogoro. Vitanda hivyo ni sehemu ya kupunguza tatizo la uhaba wa vitanda vya kujifungulia wajawazito katika Mkoa wa Morogoro na tukio hilo limefanyika tarehe 18 Julai katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania - Stanley Kafu akikabidhi vitanda vya kujifungulia wajawazito kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro - Mhe. Judith Nguli ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero. Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ambapo vitanda hivyo vinaenda kupunguza changamoto za vifo vya Mama na Mtoto wakati wa kujifungua ikiwa ni sehemu ya malengo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika kusaidia jamii na kuboresha huduma za afya nchini, Exim Bank Tanzania imetoa vitanda vya hospitali kwa wodi za wazazi katika Mkoa wa Morogoro. Makabidhiano hayo yamefanyika mbele ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ikiwa ni sehemu ya mapambano ya kupunguza vifo vya wamama na watoto wakati wa kujifungua.


Benki ya Exim Tanzania imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kijamii katika sekta za mazingira, elimu, uchumi, utalii, michezo, na afya. Kwa mjibu wa taarifa za wizara ya afya, Serikali ya Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vya kina mama na watoto kutoka 556 mwaka 2016 mpaka kufukia vifo 104 mnamo mwaka 2023 ingawa bado hali sio salama sana.

Kwa kutambua changamoto hii pamoja na zingine zikiwemo uhaba wa vifaa vya matibabu, upungufu wa vitanda, madawa, na uchache wa watoa huduma za afya, benki ya E xim inaona ina nafasi kama taasisi kusaidia Serikali kupunguza tatizo la vitanda vya wajawazito.

UBONGO KUSHIRIKIANA NA VODACOM FOUNDATION NA HOPE INTERNATIONAL KUZINDUA ZIARA MARA NA ARUSHA


Dar es Salaam, Tanzania - 12 Julai 2024: Ubongo, shirika linaloongoza barani Afrika katika burudani ya elimu kwa watoto, linajivunia kutangaza uzinduzi wa ziara zake za kikanda nchini Tanzania, zinazojulikana kama; "Ziara ya Kujenga Akili," kwa ushirikiano na Vodacom Tanzania Foundation na Hope and Healing International. Ziara ya Kujenga Akili inalenga kutoa uzoefu wa kielimu unaovutia na wenye tija kubwa kwa watoto na walezi kote Tanzania.

Ziara hiyo itaanza katika mikoa ya Mara na Arusha tarehe 15 Julai 2024, ikiwaleta moja kwa moja watoto wahusika wa katuni maarufu barani Afrika na vipindi vya burudani, ikiwa ni pamoja na watoto wenye ulemavu. Iliyoandaliwa ili kuhamasisha kujifunza kupitia michezo, ziara hiyo inatoa mchanganyiko wa kipekee wa elimu na burudani.

"Katika Ubongo, tumejizatiti kutoa maudhui ya kielimu yatakayowezesha viongozi wa kizazi kijacho barani Afrika," alisema Iman Lipumba, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Maendeleo. "Ziara ya Kujenga Akili ni ushahidi wa kujitolea kwetu kufikia watoto katika kila pembe ya nchi ili kuhakikisha wanapata rasilimali na mafanikio.

Basi lenye chapa ya Ubongo litasafiri katika mikoa hiyo, likibeba wahusika wa katuni na waburudishaji kwa ajili ya kufanya maonesho katika shule na vituo vya kijamii.

Vilevile waatashirikisha watoto katika michezo ya kielimu na mashindano huku ziara hiyo ikilenga kujumuisha sherehe za Mwisho wa juma katika kila mkoa ambapo watoto na walezi wao wataweza kushiriki katika shughuli mbalimbali.

Wakati wa sherehe hizi, watoto na walezi watapokea zana maalum zitakazosaidia mchakato wa ujifunzaji.

"Tunafurahi sana kushirikiana na Vodacom Tanzania Foundation na Hope and Healing International katika ziara hii ya kukuza akili. Ushirikiano huu unathibitisha dhamira yetu ya pamoja ya kutoa uzoefu wa kielimu wa hali ya juu kwa watoto na walezi nchini Tanzania.