Foreign Exchange Rates

DStv Advert_010224

DStv Advert_010224

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 24 December 2021

EQUITY BANK NAMES ISABEL MAGANGA AS NEW BOSS


Dar es Salaam, 24th December 2021 – Equity Bank Tanzania has announced the appointment of Ms. Isabel Maganga as the new Managing Director in an acting capacity with effect from 23rd December 2021.

Ms. Maganga is a career banker with over fifteen years of experience. She holds a Master of Science in Finance and Investments from Coventry University, a Bachelor's degree in Environmental Science and Management from Sokoine University of Agriculture. She also holds a Diploma in Banking from Milpark Business School. She is a certified Professional Banker and Certified Expert on SME Finance. Prior to her appointment, Ms. Maganga was the Head of Commercial at the Bank.

The announcement, which was made by the Board of Directors, follows the coming to an end of Mr. Robert Kiboti's tenure as the Managing Director at Equity Bank Tanzania, who was appointed in 2018. He will be transiting back to the Group Head Office.

Wednesday 15 December 2021

LIPIA KIFURUSHI CHA DStv POA KWA TSHS 9,900 TU!



Mtaalam wa elimu anaitwa Mwalimu sisi tunamuita MASTER.

Karibuni kwenye meza ya #SalamaNaHenryKulaya kuna mizinga mingi ya kudaka kwenye show hii. Alhamis saa tatu kamili usiku kwenye @maishamagicpoa on @dstvtanzania pekee!

Let’s Learn!

Piga *150*53# kulipia kifurushi cha Poa kwa TShs 9,900 tu.

#ZigoLaSikukuu
#DStvJoy
#ZigoKamaLote

USIKOSE ARSENAL VS WEST HAM LIVE NDANI YA DStv



London Derby ni 🔥🔥
🔥

Tofauti ya pointi 2 tu baina ya timu hizi kutoka London, mbio za Top 4 ni za moto, Arsenal Vs West Ham Live ndani ya @dstvtanzania.

Ni kupitia kifurushi chako cha Compact TShs 51,000 tu ili uweze kutazama mbungi hili.

Lipia sasa kwa kupiga *150*53#

#Birianiiendelee
#DStvJoy
#ZigolaSikukuu

Friday 10 December 2021

USIKOSE LIVERPOOL VS ASTON VILLA JUMAMOSI HII

 


Akiwa kama kocha wa Aston Villa Steven Gerald, Jumamosi hii na kikosi chake watakuwa dimbani kufuana na Liverpool timu ambayo aliwahi kuwa mchezaji wake.

Ukiwa kama mdau wa soka tuambie ni upi mtazamo wako juu ya mechi hii.

Kwa TShs 21,000/= tu @dstvtanzania inakupa kutazama mechi hii Live. Hakikisha hupitwi kwa kulipia mapema kifurushi chako.

Piga *150*53# ili usikose burudani hii.


#BirianiIendelee
#ZigoLaSikukuu
#DStvJoy

Monday 6 December 2021

AIRTEL LAUNCHES CHRISTMAS CUSTOMER DRIVE PROMOTION

Airtel Money Director, Isack Nchunda (left) and Airtel Corporate Communications Manager, Jackson Mmbando inaugurating the Holiday Offer through Airtel Money, send money FREE campaign today at Airtel Head office Dar es Salaam.
  • Customers can now send money Airtel to Airtel free to their families, friends and loved ones during Christmas holiday.
  • Solidarity levy to remain the same
Dar es Salaam. Monday 6 December 2021: Airtel Tanzania the Smartphone Network through its Airtel Money service has announced Christmas customer drive promotion with Airtel Money, customers can now send money Airtel to Airtel free during the Christmas festivals.

Speaking today in Dar es Salaam while announcing the Airtel Money the drive, Airtel Money Director Isack Nchunda said that, ‘Airtel is very committed on offering customers with freedom to communications. As we approach Christmas festivals, this where most of Tanzanians use the opportunity to show love and care to their families, friends and loved ones. For that reason, Airtel Money is announcing send money free to Airtel Money customers and this will give their life easier as they will be charged zero costs when sending money whether for family, business or to their loved ones’.

Nchunda added, ‘As we understand that during this festival seasons most of customers will be travelling from one place to another, and most especially from town to rural areas, Airtel Tanzania is now embarking on network infrastructure where now we are unveiling 4G sites to areas which were not covered previously. Said Nchunda adding that as for now, Airtel network is very stable and available country wide, whether 2G, 3G or 4G.

BENKI YA CRDB YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA TUZO ZA NBAA

Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo akipokea tuzo ya mshindi wa jumla kwa uwasilishaji bora wa Taarifa za Fedha Nchini kwa viwango vya kimataifa, kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali, Leonard Mkude (kushoto), katika hafla ya utoaji tuzo kwa washindi wa Shindano la Uandaaji Bora wa Hesabu kwa Viwango vya Kimataifa kwa mwaka 2020. Shindano hilo liliandaliwa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) na lilifanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA Bunju Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita. Kulia ni Mtaalamu wa Uendeshaji wa Fedha wa Benki ya CRDB, Neema Maganja.

 
Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo (wa saba kushoto) akiwa pamoja na wafanyakazi wa Idara ya Fedha wa Benki ya CRDB wakiwa wa tuzo ya mshindi wa jumla kwa uwasilishaji bora wa Taarifa za Fedha nchini kwa viwango vya kimataifa, waliyoipata katika Shindano la Uandaaji Bora wa Hesabu kwa Viwango vya Kimataifa kwa mwaka 2020 lililoandaliwa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA Bunju Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Wafanyakazi wa Benki ya CRDB Idara ya Fedha wakifurahia tuzo zao walizopata katika Shindano la Uandaaji Bora wa Hesabu kwa Viwango vya Kimataifa kwa mwaka 2020 ambapo Benki ya CRDB iliibuka kinara, lililoandaliwa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA Bunju Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.


Benki ya CRDB imeibuka kinara katika tuzo zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu (NBAA) kama taasisi ya fedha iliyoongoza kwa kuwasilisha Taarifa ya Fedha bora kwa mwaka 2020 kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Akizungumza wakati kukabidhi tuzo hiyo, Mhasibu Mkuu wa Serikali, Leonard Mkude aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuendelea kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa katika utayarishaji wa taarifa zake za kifedha.

Mkude alisema kuandaa ripoti za mwaka za Mashirika na Taasisi za Umma kwa viwango vya kimataifa kunawapatia wananchi fursa ya kupima ufanisi wa utendaji kazi wa taasisi husika, kuona namna gani yanawajibika ipasavyo katika kutumia rasilimali.

“Hongereni sana Benki ya CRDB kwa kuibuka kinara wa jumla na kwa upande wa taasisi za fedha, hii inadhihirisha ni jinsi gani Benki hii imewekeza katika mifumo ya kisasa ya kutoa huduma kwa wateja lakini pia na kuwezesha kupata taarifa za kiwango,” alisema Mhe.Mkude.

Kwa upande wake Afisa Mkuu wa Fedha Benki ya CRDB, Fredrick Nsekanabo, alisema kuwa Benki ya CRDB inatambua umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kupitia mifumo inayozingatia viwango vya kitaifa na kimataifa. Alisema kitendo cha kupata tuzo hizo kunaifanya benki hiyo kuendelea kuongeza jitihada ili kubaki katika nafasi hiyo.

JICA CELEBRATES COMPLETION OF THE FIRST THREE TANZANIAN START-UPS OF THE NEXT INNOVATION WITH JAPAN (NINJA) START-UP INITIATIVE

DCB YASHINDA TUZO ZA CONSUMER CHOICE AWARDS AFRICA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa (kulia), akipokea tuzo ya mshindi wa pili katika Benki zinazotoa huduma bora kwa wateja kutoka kwa Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Elisha Manya wakati wa hafla ya utoaji zawadi kwa washindi wa Tuzo za Chaguo la Mtumiaji Afrika zilizofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo baada ya kupokea tuzo ya mshindi wa pili katika Benki zinazotoa huduma bora kwa wateja katika hafla ya utoaji zawadi kwa washindi wa tuzo za chaguo la watumiaji Afrika zilizofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Elisha Manya.

Benki ya Biashara ya DCB imeibuka mshindi kwa kutwaa tuzo ya Benki pendwa Tanzania inayotoa huduma bora kwa wateja katika kinyang’anyiro cha mwaka huu cha tuzo za Consumer Choice Awards Afrika 2021 (CCAA).

Hafla ya kukabidhi tuzo hizo za Consumer Choice Awards Africa 2021 zilifanyika jijini Dar es Salaam, lengo kuu ikiwa ni kuleta ushindani kati ya makamapuni na biashara mbali mbali barani Afrika, kuhamasisha utoaji huduma na bidhaa bora kwa wateja pamoja na kutambua kazi bora za watoa huduma.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa alisema "ushindi wa DCB katika kipengele cha benki inayotoa huduma bora kwa wateja ni faraja kubwa sana kwa benki hiyo kwani ushindi wa tuzo hizi unapatikana kwa kupigiwa kura na wateja, hii imeonyesha imani kubwa walionayo wateja wetu juu ya benki ya DCB".

“Hii ni mara ya kwanza DCB inashiriki katika kinyang’anyiro hiki, Tanzania ina idadi ya benki nyingi tu, kwa benki yetu kupata ushindi huu si kitu kidogo kwetu, ni imani yetu wateja wetu na watanzania kwa ujumla wataendelea kutuunga mkono ili tuweze kufanya vizuri zaidi.

WAFANYAKAZI WA NYANZA BOTTLERS LTD WAFURAHIA UZINDUZI WA KAMPENI YA 'MAAJABU HALISI NA COCA-COLA'

Meneja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola Tanzania, Kabula Nshimo akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya Nyanza Bottling Ltd (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘Maajabu Halisi’ uliofanyika mkoani Mwanza mwishoni mwa wiki iliyopita. Uzinduzi kama huo pia unatarajiwa kufanyika katika mikoa mingine ambapo utaambatana na shughuli tofauti za kusisimua zitakazowahusisha wateja maeneo mbalimbali na kudumu mpaka kipindi cha msimu wa sikukuu na mwaka mpya.
Meneja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola Tanzania, Kabula Nshimo (kushoto) pamoja Meneja wa Mauzo na Masoko wa Nyanza Bottling Ltd, Samwel Makenge (kulia) wakizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya Nyanza Bottling Ltd wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘Maajabu Halisi’ uliofanyika mkoani Mwanza. Uzinduzi kama huo pia unatarajiwa kufanyika katika mikoa mingine ambapo utaambatana na shughuli tofauti za kusisimua zitakazowahusisha wateja maeneo mbalimbali na kudumu mpaka kipindi cha msimu wa sikukuu na mwaka mpya.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Nyanza Bottling Ltd wakifurahia nyakati mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘Maajabu Halisi’ uliofanyika mkoani Mwanza mwishoni mwa wiki iliyopita. Uzinduzi kama huo pia unatarajiwa kufanyika katika mikoa mingine ambapo utaambatana na shughuli tofauti za kusisimua zitakazowahusisha wateja maeneo mbalimbali na kudumu mpaka kipindi cha msimu wa sikukuu na mwaka mpya.

Sunday 5 December 2021

ZANTEL YAZINDUA DUKA JIPYA MICHENZANI MALL - UNGUJA

Mkuu wa Wilaya ya Mjini-Unguja, Rashid Msaraka akikata utepe kuzindua duka jipya la Zantel lililopo eneo la biashara la Michenzani Mall. Kulia ni Mkuu wa Zantel-Zanzibar Mohammed Khamis Mussa na Emmanuel Joshua, Mkuu wa Mauzo, Usambazaji na Huduma kwa wateja. Duka hilo ni la tatu kwa Unguja na la tano kwa Zanzibar litakalosaidia kusogeza huduma karibu na wateja.
  • Mkuu wa Wilaya aipongeza kwa kuboresha huduma za Mawasiliano
Unguja. 2 Desemba 2021 - Katika kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa urahisi, Kampuni ya Zantel imezindua duka jipya la huduma kwa wateja lililopo Michenzania Mall mjini unguja.

Uzinduzi wa duka hilo ulifanyika hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashid Msaraka na kushuhudiwa na wadau mbalimbali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Zantel-Zanzibar Mohammed Khamis Mussa alisema duka hilo litasaidia kuongeza huduma za mawasiliano karibu na wateja kwani duka hilo lipo katikati ya mji.

“Duka hili litakuwa msaada mkubwa katika kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa wateja wetu hapa Unguja. Eneo hili la Michenzani ni rahisi zaidi kufikika kwa wateja wote wa maeneo ya karibu na wanaotembelea eneo hili,” alisema Mussa.

Saturday 4 December 2021

CRDB YAAHIDI MITAJI NA MIKOPO KWA WAWEKEZAJI WA ITALIA

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Bw. Abdulmajid Nsekela akitoa hotuba yake kwa Wafanyabiashara na Wawekezaji walioshiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.

Sehemu ya Wafanyabiashara na Wawekezaji walioshiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Chama cha Wawekezaji katika Sekta ya Hoteli Zanzibar, Paulo Rosso walipokutana katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.


Benki ya CRDB imewahakikishia wafanyabiashara na wewekezaji wa Tanzania na Italia utayari wake wa kutoa mikopo na mitaji ya kutosha watakapo kuwa tayari kuwekeza nchini Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Italia liloandaliwa na Ubalozi wa Tanzania lililofanyika Jijini Roma, nchini Italia.

Nsekela amesema Benki ya CRDB ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Sita pamoja na wawekezaji katika kuhakikisha kuwa changamoto zinazoendana na huduma za kibenki zinatatuliwa.

“Nawahakikishia kuwa Benki ya CRDB itawawezesha mikopo ya kuwekeza katika sekta mbalimbali hivyo msiwe na wasiwasi kuhusu mitaji ya kuwekeza ipo karibuni sana tuijenge Tanzania,” amesema Nsekela.

Nsekela ameongezea kuwa Benki ya CRDB inafarijika kuona wawekezaji wengi wameonesha nia ya kuwekeza zaidi Tanzania, huku akimpongeza Balozi wa Tanzania nchini Itali, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo kwa kuandaa Jukwaa hilo ambalo limetoa fursa ya kueleza sekta mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana Tanzania.

Friday 3 December 2021

USIKOSE LONDON DERBY JUMAMOSI HII NDANI YA DStv

 


London Derby, kinara vs namba 4 kwenye msimamo, Chelsea wanasema, "kama mnaweza tushusheni ", je Moyes ataweza Jumamosi hii?

Ni Live bila chenga ndani ya @dstvtanzania pekee kupitia kifurushi cha Poa sh 9,900 tu.

Lipia sasa kifurushi chako mapema kwa kupiga *150*53#

#DStvJoy
#ZigolaSikukuu
#Birianiiendelee

Thursday 2 December 2021

BENKI YA DCB YASHIRIKI KONGAMANO LA UELEWA NA FURSA ZILIZOMO KATIKA MIRADI YA MAENDELEO YA KIUCHUMI

Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Core Securities Limited, George Fumbuka wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).
Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kushoto), akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Nicodemus Mkama, wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).
Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kulia), akibadilishana mawazo na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa Mfuko wa Mendeleo ya Mitaji (UNCDF), Peter Malika wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).
Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kushoto), akishikana mikono na Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Ofisi ya Rais TAMISEMI, John Cheyo, wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).
Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kushoto), Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Ofisi ya Rais TAMISEMI, John Cheyo, na Afisa Mtendaji Mkuu, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Nicodemus Mkama wakifurahia jambo wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).

Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Fauzia Bairu (kulia), akimsikiliza Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF), Peter Malika wakati wa kongamano la wadau kuhusu utaratibu mbadala wa kugharamia miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia hati fungani uliofanyika jijini Arusha jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF).

SERENGETI LAGER YAWAKUTANISHA MASHABIKI WA MBEYA USO KWA USO NA TAIFA STARS

Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa tayari kwa ajili ya kujibu maswali ya mashabiki katika tukio la kampeni ya ‘Nje ya Dimba na Taifa Stars’ lililofanyika jijini Mbeya ambapo mashabiki walikutana uso kwa uso na baadhi ya nyota wa timu ya taifa.
Mchezaji wa Taifa Stars Kibwana Shomari, akijibu moja ya swali kutoka kwa mashabiki wa soka wakati wa tukio lililowakutanisha wacheza wa timu hiyo ya taifa na washabiki wao lililofanyika jijini Mbeya chini ya kampeni ya Nje ya Dimba na Stars inayoendeshwa na bia ya Serengeti Lager.
Baadhi ya mashabiki wa Taifa Stars mkoani Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu hiyo ya taifa, muda mfupi baada ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na bia ya Serengeti Lager ikiwa ni sehemu ya kampeni ya ‘Nje ya Dimba na Taifa Stars’.

Bia ya Serengeti Lager leo imewakutanisha uso kwa uso baadhi ya wachezaji wa Taifa Stars na mashabiki katika hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika jijini Mbeya ikiwa ni muendelezo wa kampeni ya ‘Nje ya Dimba na Stars’

Kampeni ya 'Nje ya Dimba na Stars' inalenga kuwapa nafasi mashabiki wa Taifa Stars kukutana na nyota wanaowapenda katika baa zao na pia watapata fursa ya kuwauliza maswali kuhusu maisha yao nje ya soka pamoja kupiga nao picha za ukumbusho. Kampeni hiyo ya nchi nzima itadumu kwa miezi mitatu.

Akiongea wakati wa hafla hiyo, meneja masoko wa kanda za juu kusinini wa SBL Denis Tairo alisema bai ya Serengeti lager ikiwa kama shabiki mkuu wa Taifa Stars inajivunia kuwaletea mashabiki wa Taifa Stars mkoani Mbeya nyota inaowapenda na kuwapa nafasi kuzungumza nao na hivyo kuwafahamu kwa undani zaidi.

Wednesday 1 December 2021

BENKI YA CRDB YAZINDUA KAMPENI YA “TISHA NA TEMBOCARD VISA,” WATEJA 4 KUPELEKWA KUSHUHUDIA AFCON 2022 NCHINI CAMEROON

Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa (katikati) akionyesha aina mpya ya kadi za ‘TemboCard’ wakati wa hafla ya uzindunzi wa kampeni ya Tisha na TemboCardVisa ulioenda sambamba na uzinduzi wa kadi hizo uliofanyika leo katika Makao Makuu ya Benki hiyo, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Mkuu wa Idara wa Masoko wa Benki ya CRDB, Joseline Kamuhanda (Kulia) na Kaimu Meneja Mwandamizi wa Biashara ya Kadi wa Benki hiyo, Erica Mwaipopo.

Benki ya CRDB kwa kushirikiana na kampuni ya Visa international leo imezindua kampeni ya “Tisha na TemboCard Visa” inayolenga kuhamasisha wateja kujenga utamaduni wa kutumia kadi zao za TemboCardVisa huku wakijiwekea nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwamo kushuhudia kombe la mataifa ya afrika AFCON litakalofanyika nchini Cameroon mwakani 2022.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya CRDB Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Wateja wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Rabala alisema zawadi zitatolewa kwa wateja ambao watafanya miamala mingi zaidi kupitia TemboCardVisa zao katika kipindi chote cha kampeni ambayo inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi Machi 2022.


“Lengo letu ni kuona wateja na Watanzania wanajenga utamaduni wa kutumia kadi zao kufanya malipo ya manunuzi na kuachana na utaratibu wa kutumia pesa taslimu ambazo sio salama. Katika kipindi hiki cha kampeni tutatoa zawadi kwa washindi zaidi ya 80 ambapo kila mwezi tutao zawadi kwa washindi 20,” alisema Raballa.

Akielezea kuhusu zawadi zitakazotolewa katika kampeni hiyo, Raballa alisema wateja watapata zawadi mbalimbali ikiwamo kurudishiwa asilimia 5 ya kiasi walichotumia, kulipiwa bili ya malipo ya manunuzi, simu janja, tablet, televisheni, sofa set, home theatre, pamoja na safari ya kitalii kwenda Zanzibar au Serengeti. “Kubwa zaidi ni zawadi ya safari ya kwenda Cameroon kushuhudia michuano ya AFCON kwa wateja 4 ambao watakuwa na miamala mingi zaidi katika kipindi cha Desemba na Januari. Washindi wataruhusiswa kwenda na wenza au rafiki zao” alisema Rabala.


Raballa alitoa rai kwa wateja wa Benki hiyo na Watanzania kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika kampeni hiyo kwa kutumia kadi zao za TemboCardVisa kufanya malipo huku akiwasihi kuendelea na utamaduni huo hata baada ya kampeni kwani lengo ni kufanya matumizi ya kadi kuwa sehemu ya kawaida ya miamala ya malipo ikiwa ni mkakati wa kujenga jamii yenye matumizi machache ya pesa taslimu “cashless society”.

“Kwa wale ambao hawana akaunti niwashauri wafungue akaunti ili waweze kuunganishwa na TemboCardVisa na kuanza kufurahia huduma huku wakijiwekea nafasi ya kujishindia zawadi kemkem. Kama mnavyojua sasa hivi zoezi la kufungua akaunti tumelirahisisha sana…”

“…kama una simu janja unachotakiwa kufanya ni kupakua SimBanking App na kufuata hatua za kufungua akaunti kwa kutumia namba ya NIDA na kisha utaomba kupata TemboCard yako, kwa wale wa sio na simu janja wanaweza kutembelea kwa CRDB Wakala wakiwa na kitambulisho cha NIDA kufunguliwa akaunti na kupata TemboCardVisa kwa urahisi. Tunatamani kuona watu wengi zaidi wakishiriki ili kwa pamoja tuweze kufikia lengo,” aliongezea.


Awali akielezea namna ya kushiriki katika kampeni hiyo na kuibuka mshindi, Kaimu Meneja Mwandamizi wa Biashara ya Kadi Benki ya CRDB, Erica Mwaipopo alisema wateja wanatakiwa kutumia kadi zao za TemboCardVisa kulipia manunuzi na huduma katika maduka, supermarkets, migahawa, hoteli na vituo vya mafuta kupitia vifaa vya manunuzi (POS), pamoja na malipo ya mitandaoni ikiwamo kulipia tiketi za ndege au malipo ya kuagiza bidhaa nje ya nchi.

Uzinduzi huo wa kampeni hiyo ya “Tisha na TemboCardVisa” ulienda sambamba na uzinduzi na muonekano mpya wa kadi za Benki ya CRDB ‘TemboCard’ ambazo zimeboreshwa zaidi ili kuwapa wateja uzoefu bora zaidi pindi watumiapo kadi zao. Akielezea kuhusu ujio wa kadi hizo mpya za TemboCardVisa, Mkuu wa kitengo cha Masoko, Joseline Kamuhanda alisema kadi hizo zimetengenzwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa itakayowawezesha wateja kutumia kadi zao kwa urahisi kufanya malipo popote pale.


Benki ya CRDB ilikuwa benki ya kwanza kuanzisha huduma za kadi ‘TemboCard’ nchini mwaka 2002, ikilenga kuwapa wateja wake urahisi na unafuu wa upatikanaji wa huduma popote walipo. Mpaka sasa Benki ya CRDB imefanikiwa kutoa zaidi ya TemboCard milioni 3 ikiungana na mifumo ya malipo ya kimataifa ya Visa, MasterCard na Union Pay. Huduma za Tembocard zimechangia kwa kiasi kikubwa kusaidia jitihada za serikali katika kuimarisha mfumo wa malipo nchini na kuongeza ujumuishi wa kifedha “Financial Inclusion”.








VODACOM TANZANIA FOUNDATION KWA KUSHIRIKIANA NA UNEP, UNICEF, DORIS MOLLEL FOUNDATION WAANGALIA NAMNA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI HUCHANGIA ONGEZEKO LA KUZALIWA KWA WATOTO NJITI NCHINI

Mratibu wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia mazingira (UNEP) Clara Makenya (kushoto) akipokea mti wa matunda kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel (kulia) mara baada kumalizika kwa semina iliyojadili namna ambavyo athari za mabadiliko ya tabianchi huchangia ongezeko la kuzaliwa kwa watoto njiti, huku pia ikisababisha vifo vya akina mama wajawazito. Kulia ni Meneja wa Tasisi ya Vodacom Tanzania Foundation Sandra Oswald ambao ni wadau katika kusaidia juhudi za kuhifadhi mazingira na kusaidia juhudi za serikali katika sekta ya afya nchini.

 


I&M BANK LAUNCHES A NEW RELOCATED BRANCH IN ARUSHA

The Arusha Regional Commissioner, John Mongella unveils the new I&M Bank relocated branch in Arusha yesterday. Behind him, is the Bank Chief Executive officer, Mr. Baseer Mohammed and the Retail Banking Manager, Ms. Lilian Mtali. The branch will provide a range of services including the Select Banking for affluent clients.
The Arusha Regional Commissioner, John Mongella speaks during unveiling of the newly relocated branch in Arusha yesterday.  The branch will provide a range of services including the Select Banking for affluent clients expecting to boost business operations in the region.
The Arusha Regional Commissioner, John Mongella in a jovial mood with I&M Bank CEO, Mr. Baseer Mohammed and the Retail Banking Manager, Ms. Lilian Mtali during unveiling of the newly relocated branch in Arusha yesterday.
  • Customers to enjoy convenience with a range of customized services including select Banking for affluent clients
Arusha. 30th November, 2021 - I&M Bank customers in Arusha will now enjoy convenience through the new relocated branch with state-of-the-art features including the Select Banking lounge for the affluent clients.

The branch was launched by the Arusha Regional Commissioner, John Mongella witnessed by different leaders and stakeholders on Tuesday 30th November 2021 at the new premises.

Speaking during the opening ceremony, the Bank Chief Executive Officer, Baseer Mohammed said the move aimed at ensuring easy accessibility of bank’s services to the customers in the region.

“This initiative aimed at bringing convenience to our customers since the new branch is in city center offering easy accessibility. This branch has state-of-the-art features including the Select Banking Lounge that will serve the affluent clients, modern facilities, and safe deposit lockers, bureau de change etc. this is all to ensure that our customers are enjoying the banking experience while visiting our newly relocated branch” he said.