Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba (wa tatu kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Mwanga Hakika Bank, Eng. Ridhiwan Mringo (wa pili kushoto) wakifungua Kitambaa cha jiwe la Msingi kuashiria Ufunguzi wa tawi jipya na la kisasa jijini Arusha. Wanaoshuhudia pembeni kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya MHB, Jagjit Singh, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtehengerwa na Mstahiki meya Arusha Maximilian Iranghe. Hafla ya uzinduzi ilifanyika hivi karibuni.
Baadhi ya wageni waalikwa na wafanyakazi wa Benki ya Mwanga Hakika wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba.
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Mwigulu Nchemba (kulia) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa tawi jipya na la kisasa jijini Arusha. Wanaoshuhudia pembeni ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Mwanga Hakika Bank, Eng. Ridhiwan Mringo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya MHB, Jagjit Singh, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtehengerwa na Mstahiki meya Arusha Maximilian Iranghe.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Mwanga Hakika Bank Eng. Ridhiwan Mringo akitoa hotuba katika hafla ya ufunguzi wa tawi jipya Jijini Arusha.
Arusha. Aprili 28, 2023: Benki ya Mwanga Hakika (MHB) imezindua tawi jipya na la kisasa jijini Arusha, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kutanua mtandao wake wa huduma za kifedha nchi nzima. Tawi hilo jipya lililopo katika jenga la Central Plaza, barabara ya Sokoine jirani na Clock tower jijini Arusha, linafanya idadi ya matawi ya benki hiyo kufikia saba. Matawi mengine yapo Dar es Salaam, Moshi, Dodoma, Mwanga na Same.