Benki ya NMB inaendelea kuupiga mwingi! Hivyo ndivyo unavyoweza kuelezea kutokana na hatua mbalimbali ambazo benki hiyo imeendelea kuchukua katika kusogeza huduma zake karibu na Watanzania.
Kwa kushirikiana na kampuni ya bima ya Britam, Benki ya NMB inatoa bima ya vyombo vya majini mahususi kwa ajili ya uvuvi (Mtumbwi/Jahazi) vinavyotumiwa na wavuvi wadogo wadogo, wa kati na wakubwa.
Bima hii ni kinga endapo chombo na vifaa vyake vitapata majanga kama moto, kuzama, kuvamiwa, kuibiwa, kugongwa au kugonga vyombo vingine.
Pia, kwa ajili ya mvuvi endapo atapata ajali akiwa kwenye shughuli za kivuvi ndani ya maji au kando kando ya mto, bwawa, ziwa au bahari.
Faida za ziada utakazopata katika bima hii ni;
- Kifo kitokanacho na ajali, bima italipa Tsh 2,000,000
- Ulemavu wa kudumu utokanao na ajali - Tsh 2,000,000
- Gharama za matibabu yatokanayo na ajali - Tsh 500,000
- Mkono wa pole kwa familia kama mteja atafariki na ajali- Tsh 200,000






























.jpg)



%20in%20celebration%20mood%20with%20Absa%20staff%20during%20the%20Dar%20City%20Marathon.jpg)







