Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 15 October 2024

DKT. NCHEMBA AKUTANA NA UMOJA WA MABENKI TANZANIA (TBA)

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) akizungumza katika kikao chake na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), ofisini kwake jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma za fedha jumuishi. Kushoto ni Mwenyekiti wa TBA, Bw. Theobald Sabi.
Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Bw. Theobald Sabi, akizungumzia mchango wa Sekta ya Benki nchini katika kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Taasisi hiyo, jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma jumuishi za kifedha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiongoza kikao kati yake na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba akifafanua jambo katika kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, akielezea namna ambavyo Serikali kupitia Benki hiyo imekuwa ikisimamia Sekta ya Benki nchini wakati wa kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Na. Benny Mwaipaja, Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma jumuishi za kifedha. 

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, wakati ujumbe wa TBA uliongozwa Mwenyekiti wake, Bw. Theobald Sabi.

DKT. NCHEMBA ATETA NA MKUU WA KAMPUNI YA HEINEKEN JIJINI DODOMA

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akiwa katika picha na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya Vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford, baada ya kikao chao kilichofanyika Ofisini kwake -Treasury Square, jijini Dodoma. Katika kikao hicho walijadili kuhusu ukuaji wa Kampuni na namna ambavyo Kampuni hiyo inachangia mapato katika uchumi na maendeleo ya nchi.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akiongoza kikao kati yake na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford, alipomtembela ofisini kwake jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford aliyefika - Treasury Square, jijini Dodoma, kuzungumza na Mhe. Waziri kuhusu maendeleo ya Kampuni hiyo na namna inavyochangia katika uchumi wa nchi. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, kulia ni Kamishna Msaidizi, Idara ya Sera, Wizara ya Fedha, Bw. William Mhoja, akifuatiwa na Afisa Masoko wa Kampuni hiyo, Bi. Lilian Pascal.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akiwa na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya Vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford, aliyefika kumtembelea Ofisini kwake, Jengo la Treasury Square, Jijini Dodoma, ambapo walizungumzia kuhusu maendeleo ya Kampuni hiyo na mchango wake katika uchumi wa nchi.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (kushoto) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) na Mgeni wake, Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya Vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford na ujumbe wake, walipomtembelea Mhe. Wazir,i Ofisini kwake jijini Dodoma.
Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya Vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford na ujumbe wake, akifafanua jambo alipomtembelea Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (hayupo pichani), Ofisini kwake jijini Dodoma.

Na. Benny Mwaipaja, Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford, aliyemtembelea Ofisini kwake, Jengo la Treasury Square, jijini Dodoma, akiambatana na Afisa Masoko wa Kampuni hiyo. Bi. Lilian Pascal, ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya kampuni hiyo iliyowekeza hapa nchini na namna inavyochangia katika pato la Taifa na Uchumi wa nchi kwa ujumla.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayesimamia Sera za Uchumi, Bw. Elijah Mwandumbya na Kamishna Msaidizi, Idara ya Sera, Bw. William Mhoja, pamoja na Maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha.

VODACOM YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUPELEKA HUDUMA MTAANI

Mteja wa muda mrefu wa Vodacom Tanzania Plc, George Nyamugali (wa nne kutoka kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja, Harriet Lwakatare wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja yaliyofanyika katika Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam. Ili kusherehekea wiki ya huduma kwa Wateja, Wafanyakazi wa kampuni hiyo wamewafuata wateja ili kusikiliza changamoto zao na kuzifanyia kazi papo hapo.

Dar es Salaam, Oktoba 07, 2024 – Kampuni ya Mawasiliano na Teknolojia Vodacom Tanzania imezindua rasmi maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 2024 kwa kaulimbiu ya ‘Huduma Bora Kila Wakati’, ambapo kupitia program maalumu ya Huduma Kitaani imeanza kwa kutembelea Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la Wiki hii ya Huduma kwa Wateja ni kuimarisha mahusiano kati ya kampuni ya Vodacom na wateja wake, huku ikisisitiza umuhimu wa kutoa huduma bora unaokidhi mahitaji ya mteja.


Akizungumza katika tukio hilo, Harriet Lwakatare, Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom Tanzania, alisema, "Wiki hii ni fursa yetu ya kumshukuru kila mteja aliyekuwa nasi muda wote katika safari hii. Kupitia kaulimbiu yetu ‘Huduma Bora Kila Wakati,’ tunaleta huduma zetu moja kwa moja kwa wateja wetu, kuwasikiliza, na kuhakikisha tunawapatia huduma stahiki."


Mwaka huu, Vodacom Tanzania imeamua kuwasogezea wateja wake huduma kwa kuwafuata pale walipo kwenye shughuli zao za kila siku na kutatua changamoto zao pamoja na kupokea maoni yao kuhusu huduma za Vodacom. Harakati za huduma kitaani zitafanyika pia katika kanda za Vodacom mikoani na itaenda sambamba na utoaji wa msaada katika hospitali kadhaa ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa Vodacom kuchangia damu.


Lwakatare aliendelea kusema, "Kwetu sisi huduma kwa wateja siyo tu suala la miamala au masuala ya kiufundi ila pia ni kule kujali wateja wetu na kuhakikisha wanapata huduma zinazowasaidia katika maisha yao ya kila siku. Tunataka wateja wetu watumie mtandao wetu na wafanye biashara zao kwa amani, wakijua kuwa Vodacom ipo kwa ajili yao."

NMB CEO CHIEF GUEST AT CHARLOTTE SEC. SCHOOL GRADUATION CEREMONY


With a few days left to the Fourth Form National Examinations scheduled to be held on November 11, 2024, form four candidates at Charlotte Secondary School located at Tungi Mkwajuni, Morogoro Municipality, have been urged to put God first, have discipline, work hard, have integrity and honest, if they are to achieve more success both academically and spiritually.


The call was made by the NMB Bank Chief Executive Officer (CEO), Ruth Zaipuna during the 12th graduation ceremony held in Morogoro over the weekend and attended by the bank’s management.


The graduation ceremony began with a holy mass presided by Father Isdory Ndekumanya who later joined the event’s chief guest, Ruth Zaipuna to cut a ribbon to inaugurate the school’s library.


Speaking during the event, Zaipuna commended the school’s board for the honor offered to her to officiate as guest of honor adding that the event reminded her of her form four graduation held 33 years ago at Kilakala Secondary School in Morogoro.


"Everyone has their own life journey, but the life journeys of others have something that you could learn from which can help you too. As you graduate form four today, remember that each of you has made a stride, so I take this opportunity to ask you to continue serving and trusting God but at the same time put an extra effort into everything you do.


"I have gone through various stages of education and then embarked on work life so as I said earlier, everyone has their own life journey, and sincerely speaking some of the things that helped me achieve success personally include putting God first in everything I do and every step I take.


"You also need a high level of discipline, and ensure to work hard in everything you do, be it small or big but you need to to continue learning every day," noted Zaipuna.


Zaipuna during the event lauded the Charlotte Secondary School Board under the chairperson Vidda-Joyce Makundi for spearheading the school’s success and congratulated parents and guardians for their efforts noting that she believes that behind every young child who believes in himself/herself, there is a parent who gives him/her that confidence.


Zaipuna used the opportunity to remind parents and students of the importance of creating a positive saving culture, urging them to join the NMB Youth Forum called ‘Go na NMB’ which comes with many benefits including financial literacy and other banking solutions including health insurance.


Earlier, the Principal of Charlotte Secondary School, Sister Monica Masaure lauded the parents for their cooperation in supporting their children's education since 2021 when they joined, while congratulating the teachers and non-teaching staff for supporting the well-being of the students.


Sister Monica reiterated that the mission of her school is to scrap second and third grades and remain with 'Division One' only.

CEO NMB AWAFUNDA WAHITIMU "FORM FOUR" CHARLOTTE SEKONDARI, MOROGORO


Kuelekea mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne itakayofanyika Novemba 11, 2024, wahitimu wa Shule ya Sekondari Charlotte iliyopo Tungi Mkwajuni, Manispaa ya Morogoro, wametakiwa kumtanguliza Mungu, kuwa na nidhamu, bidii, uadilifu na uaminifu, ili kupata mafanikio zaidi kielimu, kimaisha na kiimani.


Wito huo umeetolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna, wakati wa Mahafali ya 12 ya shule hiyo inayomilikiwa na Shirika la Masista wa Kazi ya Roho Mtakatifu, yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 12, yaliyohudhuriwa pia na menejmenti ya benki hio.


Mahafali hayo yalitanguliwa na Misa Takatifu iliyoongozwa na Padre Isdory Ndekumanya wa Shirika la Mapdre wa Maisha ya Kitume wa Kazi ya Roho Mtakatifu, aliyemuongoza Mgeni Rasmi Bi. Zaipuna kukata utepe kuzindua Maktaba Mpya ya shule hiyo yenye usajili namba; S.4445.


Akizungumza wakati wa hotuba yake, Bi. Zaipuna aliishukuru Bodi ya Shule hiyo yenye wanafunzi 462 kumpa heshima ya kuwa mgeni rasmi wa tukio hilo, lililomrejeshea kumbukumbu za miaka 33 iliyopita alipokuwa akihitimu Kidato cha Nne katika Sekondari ya Kilakala mjini Morogoro.


“Kila mtu anayo safari yake ya kimaisha, lakini historia za maisha ya wengine zina kitu cha kujifunza kinachoweza kukusaidia nawe, kwa hiyo mnapohitimu kidato cha nne leo, kila mmoja wenu amepiga hatua, hivyo niwaombe muendelee kumtumikia na kumtumainia Mungu na kuweka juhudi katika kila mnachofanya.


“Nimepitia hatua mbalimbali za kielimu tangu hapo, baadaye maisha ya ajira na kama nilivyosema, kila mmoja ana safari yake, na katika safari yangu kielimu na kimaisha, vitu vilivyonisaidia kupata mafanikio ni pamoja na kumtegemea na kumtanguliza Mungu katika kila kitu, kila hatua.


“Pia, kuwa na nidhamu ya hali ya juu, bidii kwenye kila kitu ninachofanya kiwe kidogo au kikubwa, nafanya kwa bidii kubwa na maarifa makubwa, kuwa muadilifu, muaminifu, kuonesha na kusimamia ubora katika kazi ninayofanya na zaidi ni uamuzi wa kuendelea kujifunza kila siku,” alibainisha Bi. Zaipuna.


Aliupongeza uongozi wa Charlotte Sekondari na Bodi ya Shule chini ya Mwenyekiti Vidda-Joyce Makundi kwa kusimamia vema na kufanikisha elimu kwa wahitimu hao, huku akiwapongeza wazazi na walezi, akisema anaamini kuwa nyuma ya kila mtoto mdogo anayejiamini, kuna mzazi anayempa kujiamini huko.


Bi. Zaipuna alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wazazi na wanafunzi umuhimu wa kujenga utamaduni chanya wa kujiwekea akiba na kuwataka kujiunga na Jukwaa la Vijana la NMB liitwalo Go na NMB linalojumuisha elimu ya fedha, uwekaji akiba na suluhisho nyinginezo zikiwemo za bima ya afya.


Awali, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Charlotte, Sista Monica Masaure, aliwashukuru wazazi kwa ushirikiano wao katika kujenga elimu ya watoto wao tangu mwaka 2021 walipojiunga, huku akiwapongeza walimu na wafanyakazi wasiokuwa waalimu kwa kusaidia ustawi wa taaluma shuleni kwake.


Sista Monica alibainisha kuwa dhamira yao kama shule ni kufuta ufaulu wa madaraja ya pili na tatu na kubaki na ‘Division One’ tu, msukumo unaopewa nguvu sio tu na ufundishaji wa walimu, bali misingi bora na imara iliyowekwa na wadau wa elimu wa shule hiyo ikiwemo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

PRESIDENT MWINYI UNVEILS NEW PEOPLE'S BANK OF ZANZIBAR BRANCH IN MWANZA

The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Dr. Hussein Ali Mwinyi (center), cuts a ribbon to signify the inauguration of a new branch of the People's Bank of Zanzibar (PBZ) located in the Nyamagana District of Mwanza during a brief ceremony held in the city yesterday. Others in the picture include Minister of Finance for the United Republic of Tanzania, Dr. Mwigulu Lameck Nchemba (second right); Zanzibar's Minister of State-President's Office (Finance and Planning), Dr Saada Mkuya Salum (third right); the District Commissioner of Nyamagana, Ms. Amina Nassoro Makilagi (fourth right); the First Lady - Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi (to the right of President Mwinyi); Managing Director of PBZ (third left); along with other government and bank officials.
The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Dr. Hussein Ali Mwinyi (third from right), receives a special gift from the Managing Director of the People's Bank of Zanzibar (PBZ), Mr. Arafat Haji (fourth left), during a brief inauguration ceremony of the bank’s new branch located in Nyamagana district, Mwanza, held in the city yesterday. Others in attendance include Minister of Finance for the United Republic of Tanzania, Dr. Mwigulu Lameck Nchemba (third left); Minister of State in the Office of the President for Finance and Planning, Zanzibar, Dr. Saada Mkuya Salum (second right); District Commissioner of Nyamagana, Ms. Amina Nassoro Makilagi (second left); First Lady – Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi (right); along with other government and bank officials.

Mwanza: October 14, 2024 – In a momentous stride towards economic enhancement for both Zanzibar and mainland Tanzania, Dr. Hussein Ali Mwinyi, President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, inaugurated a new branch of the People's Bank of Zanzibar (PBZ) in Mwanza. This strategic establishment promises to not only broaden access to financial services but also unlock a myriad of economic opportunities for the local populace.

The launch event, held in Mwanza's Nyamagana district, was a gathering of distinguished officials and community members. Among the notable attendees were Dr. Mwigulu Lameck Nchemba, the Minister of Finance for the United Republic of Tanzania; Dr. Saada Mkuya Salum, the Minister of State in the President's Office for Finance and Planning in Zanzibar; and Ally Suleiman Ameir, the Minister of State for Zanzibar State House Affairs.

The attendees also included Mwanaasha Khamis Juma, the Chairperson of the Budget Committee of the House of Representatives, and Ms. Amina Nassoro Makilagi, the District Commissioner of Nyamagana, who represented the Regional Commissioner. Mr. Joseph Abdalla Meza, Chairman of the PBZ Board of Directors, alongside the bank’s Managing Director, Mr. Arafat Haji, completed the lineup of speakers who pledged their commitment to the community and the nation.

In his keynote address, Dr. Mwinyi urged the citizens of Mwanza and the surrounding Lakes Region to actively take advantage of the banking services now available to them. He articulated a vision where PBZ’s presence aligns with the government’s overarching goal of bringing economic unity to the nation.

"The establishment of PBZ branches across mainland Tanzania and the Zanzibar islands functions as a vital bridge for fostering unity and enhancing economic opportunities. This bank is set to unlock avenues for various groups, such as farmers, livestock keepers, entrepreneurs, traders, and public and private sector employees. I foresee robust interactions between Zanzibar and the Lakes Region flourishing as a direct result of this branch," the President emphasized.

Dr. Mwinyi also expressed his approval of the bank's commitment to quality service and its community-driven programs supporting sectors like sports, education, and healthcare. "I am hopeful that the residents of Mwanza will benefit immensely from PBZ's commitment to corporate social responsibility," he added.

Thursday 10 October 2024

BANDARI YA UVUVI YA KILWA KULETA MAPINDUZI YA SEKTA YA UVUVI TANZANIA


Dar es Salaam: Ujenzi wa Bandari ya kwanza ya uvuvi nchini Tanzania, Kilwa Masoko, iliyoko kwenye pwani ya Bahari ya Hindi katika mkoa wa Lindi, uko karibu kukamilika, ikiwa tayari imefikia asilimia 70. Mradi huu ni hatua muhimu katika mkakati wa Tanzania wa kukuza sekta ya uvuvi wa bahari kuu na kuboresha maisha ya maelfu ya wavuvi.


Mradi huu, ambao unagharimu TShs 289.5 bilioni, unatarajiwa kutengeneza ajira 30,000 na unatarajiwa kuwa kamili ifikapo Januari mwakani. Mara baada ya kukamilika, bandari hii itakuwa na uwezo wa kuchakata tani 60,000 za samaki kila mwaka, hatua muhimu katika jitihada za Tanzania za kuongeza uwezo wake wa kunufaika na soko lenye faida la uvuvi wa bahari kuu.


Mojawapo ya vipengele muhimu vya mradi huu ni kituo cha kuchakata samaki, ambacho kina lengo la kuwawezesha wavuvi wa ndani. Wavuvi watawezeshwa kuongeza mavuno yao kutoka kilo 1 hadi kilo 100 kwa siku. Ongezeko hili litaongeza faida na kuboresha hali zao za kiuchumi. Aidha, wanawake wanaoshiriki katika sekta hii wanatarajiwa kuona fursa zaidi katika kilimo cha mwani, huku uzalishaji ukitarajiwa kuongezeka kutoka tani 4,000 hadi tani 10,000 kwa mwaka, kulingana na taarifa za Wizara ya Mifugo na Uvuvi.


Mkurugenzi wa Miundombinu na Maendeleo katika Wizara hiyo, Bw George Kwandu, alisema kuwa kwa sasa Tanzania haijafaidika kikamilifu na uvuvi wa bahari kuu kwa sababu sehemu kubwa ya samaki huvuliwa na meli kubwa za kigeni au kutupwa kwa kukosa vifaa vya usafirishaji. Bandari hii mpya itasaidia kutatua changamoto hizo, kuruhusu samaki ambao uvuaji wake hawajafungwa kwenye mikataba wa aina yeyote kuletwa Kilwa Masoko, ambapo watachakatwa na kuuzwa kwa wafanyabiashara, hivyo kuunda mnyororo wa usambazaji wenye ufanisi na faida zaidi.


"Bandari hii ya uvuvi italeta mabadiliko makubwa katika sekta ya uvuvi nchini Tanzania. Itakuwa na uwezo wa kuhifadhi tani 1,800 za bidhaa za samaki kwa wakati mmoja na kuhudumia meli zenye urefu wa hadi mita 35," alisema Bw. Kwandu.


Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko inatarajiwa kuwa kitovu cha uvuvi wa bahari kuu, ikileta miundombinu muhimu itakayokuza sekta ya uvuvi nchini Tanzania na kusaidia jamii za ndani kuongeza uzalishaji wao wa kiuchumi.


Mwezi uliopita, wakati wa Mkutano wa 8 wa Mawaziri Wanaosimamia Bahari, Maji ya Ndani, na Uvuvi wa Shirika la Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega, alisema kuwa wavuvi wadogo wanachangia kwa kiasi kikubwa sekta ya uvuvi nchini. Alisema asilimia 95 ya wavuvi wa Tanzania wanafanya kazi kwa kiwango kidogo, wakichangia kwa kiasi kikubwa uchumi na usalama wa chakula.


Tanzania huzalisha tani 472,579 za samaki kwa mwaka, huku tani 429,168 zikivuliwa kutoka kwenye maji ya asili. Sekta hii inachangia Sh3.4 trilioni kwa mwaka, ikiwa na ukuaji wa asilimia 1.9 na kutoa ajira kwa watu 230,000 moja kwa moja.