Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Monday, 28 April 2025

NCBA BANK PLANTS 5,000 TREES TO RESTORE MPIJI RIVERBANK IN BUNJU B, DAR ES SALAAM

NCBA Bank Acting Managing Director, Alex Mziray.

25 April 2025 - In a bold demonstration of corporate environmental responsibility, NCBA Bank Tanzania led a major tree-planting initiative along River Mpiji in Bunju B, Dar es Salaam. The campaign involved the planting of 5,000 trees and was attended by the Bank’s Acting Managing Director, Mr. Alex Mziray, alongside regional government officials, community leaders and environmental stakeholders.


River Mpiji, a key waterway in Kinondoni District, has for years suffered from environmental degradation caused by deforestation, waste dumping, informal settlement growth, and unchecked urban expansion. The result has been eroded riverbanks, reduced water quality, and compromised biodiversity. Recognizing the ecological urgency, NCBA Bank took a proactive step with this intervention to help rehabilitate the river’s fragile ecosystem and safeguard it for future generations.


Speaking at the event, Mr. Mziray emphasized that the Bank’s commitment to sustainability goes beyond rhetoric:

We believe in acting with purpose. By planting these 5,000 trees, we are helping to rebuild a critical water ecosystem, fortify community resilience, and underscore the role the private sector must play in climate action. It is not enough to talk about sustainability we must live it.”


The initiative aligns with NCBA’s broader environmental goal of planting over 10,000 trees nationwide by the end of 2025, a target the Bank is steadily pursuing. Prior campaigns have already seen trees planted in Zanzibar, Arusha, Mwanza, and Dar es Salaam’s Jangwani area, each designed to address different ecological needs coastal erosion, urban green cover, and hospital-area beautification and resilience.


The planting in Bunju B included indigenous and climate-resilient species chosen specifically for their ability to stabilize soil, absorb excess water, and support the native flora and fauna. Experts on-site also trained volunteers on how to care for the trees after planting, ensuring the effort results in long-term survival and growth.


What set this campaign apart was the deep community involvement. Over 300 participants, including schoolchildren, local residents, and environmental clubs, were actively involved in the day’s activities. “This is not just an event. It is a movement,” said one community elder. “We now feel responsible for protecting this river.

Sunday, 27 April 2025

NMB YADHAMINI BONANZA LA WIKI YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI



Katika kuadhimisha Wiki ya Maonesho ya Kitaifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Benki ya NMB imedhamini na kushiriki bonanza maalum lililoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) mjini Singida.

Bonanza hilo, lililofanyika katika Uwanja wa VETA - Singida, lilikutanisha makampuni kutoka sekta binafsi na ya umma yaliyoshindana katika michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete na kuvuta kamba, likiwa na lengo la kuhimiza afya na usalama kazini kupitia michezo.



Mgeni rasmi katika hafla hii alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, ambaye aliipongeza Benki ya NMB kwa mchango wake mkubwa katika kufanikisha tukio hilo muhimu. Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mhe. Dendego alisisitiza umuhimu wa mazoezi katika kuboresha afya za wafanyakazi, akieleza kuwa ustawi wa wafanyakazi ni msingi wa uzalishaji bora na maendeleo ya taifa.



Kauli mbiu ya mwaka huu katika Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ni “Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahali Pa Kazi,” ikilenga kuhimiza matumizi ya teknolojia na ubunifu wa kidijitali katika kulinda afya na usalama wa wafanyakazi.



Mbali na kushiriki katika bonanza, Benki ya NMB pia imeweka banda maalum katika Viwanja vya Maonesho vya Mandewa ambapo wananchi wanapata fursa ya kujifunza namna benki hiyo inavyohakikisha usalama mahali pa kazi, pamoja na kupata elimu ya kifedha na huduma nyingine za kibenki.



Benki ya NMB inajivunia kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono jitihada za kuimarisha afya na usalama wa wafanyakazi nchini, ikiendelea kushirikiana na taasisi za umma na binafsi katika kujenga mazingira bora ya kazi.









Saturday, 26 April 2025

WIZARA YA SHERIA YAISHUKURU NMB KWA KUIMARISHA KITUO CHA HUDUMA


Wizara ya Katiba na Sheria (MoCLA), imeishukuru Benki ya NMB kwa kukubali kuendesha mafunzo ya kukijengea uwezo Kituo cha Huduma kwa wateja cha wizara hiyo, kilichotembelea Kituo cha Huduma kwa Wateja NMB ‘NMB Contact Center,’ kujifunza mifumo ya kupokea taarifa, malalamiko, kero na changamoto za wateja na kuzitatua.



Shukrani hizo zimetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Lawrence Kabigi, aliyeongoza masafara wa watumishi wa kituo hicho, wafanyakazi wa MoCLA na Wanasheria wa Serikali, alipokuwa akitoa neno la shukrani kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna baada ya kukamilisha mafunzo yao.



Kabigi alibainisha kuwa, siku mbili za mafunzo yao NMB, hususani katika Kituo cha Huduma kwa Wateja ‘NMB Contact Center,’ yeye na washiriki wengine kutoka MoCLA wamejifunza mengi, ikiwemo namna kituo hicho na taasisi nzima inavyotoa huduma tangu kupokea malalamiko na kero za wateja wao na kuyashughulikia kwa utaratibu wa kisasa zaidi.



Tulikuja hapa pia kuona tunatofautiana vipi katika teknolojia kwenye kushughulikia changamoto za wateja wenu, tumejionea namna mlivyotengeneza mifumo bora, sahihi na ya kisasa inayoshughulikia changamoto. Mifumo mizuri ambayo haimhitaji tu mfanyakazi kujibu, bali mifumo yenyewe inajibu na kuleta suluhishi za kimahitaji.



Na sisi tunaangalia namna ya kufikia ufanisi wenu katika kuhudumia wananchi wanaosubiri kutoka kwetu ufumbuzi wa changamoto zao, tukiamini kwamba tunapopambana kumaliza kero na changamoto za wananchi bila kutumia muda wao, tuNawapa wigo mpana wa kuendelea kuwajibika na uzalishaji mwingine na kukuza pato lao na la taifa kwa ujumla.



Mwananchi ambaye tutamsaidia kumaliza changamoto zake, hata asipotulipa tutakuwa tumempa muda wa kufanya mambo mengine na kwa mantiki hiyo ataweza kulipa kodi serikalini.



Kimsingi sisi hatubagui malalamiko ya wananchi, tunayapokea yote na yaliyo ndani ya wizara yetu yanatatuliwa, na yale ya wizara ama idara za serikali, taasisi za umma na binafsi tunayapeleka na tunafuatilia ufumbuzi wake.



Tunashukuru kwa mafunzo haya, ambayo si tu yalikuwa ya nadharia, bali kwa vitendo kupitia wataalam mahiri na wabobevu wanaohudumu kwenye vitengo mbalimbali bila kuathiri usiri wa taarifa za wateja wenu,” alisema Kabigi na kutaka mashirikiano baina ya MoCLA yaendelee kwa ustawi wa maisha ya Watanzania wa kada zote.

Friday, 25 April 2025

MINISTRY OF CONSTITUTION HAILS NMB FOR EMPOWERING SERVICE CENTER


The Ministry of Constitution and Legal Affairs (MoCLA) has expressed gratitude to NMB Bank for facilitating training to bolster the capabilities of the Ministry's Customer Service Center. This was after the center visited NMB’s Customer Contact Center to learn about systems for receiving information, complaints, issues, and challenges from clients and resolving them effectively.



These thanks were given by the Assistant Director of Human Rights Monitoring at the Ministry of Constitution and Legal Affairs, Lawrence Kabigi, who led a team of the center's staff, MoCLA employees, and Government Lawyers, during his address of appreciation to NMB Bank's Chief Executive Officer, Ms. Ruth Zaipuna, after completing their training.



Kabigi noted that during the two-day training at NMB, especially at the Customer Contact Center, he and other participants from MoCLA learned a lot, including how the center and the entire institution deliver services from receiving complaints and issues to addressing them using advanced methodologies.



We also came here to understand the differences in technology used in handling customer challenges. We have witnessed how you have developed excellent, accurate, and modern systems that address these challenges. These efficient systems not only allow staff to respond but also let the system itself provide solutions where needed.



We aim to achieve your level of efficiency in serving citizens who rely on us to provide solutions to their challenges, believing that by addressing citizens’ grievances promptly, we offer them a broader scope to remain productive and ultimately boost their income and the nation's revenue.



A citizen whose problems we help solve, even if they don't pay us directly, gains more time to manage other activities and thereby contribute to government revenues through taxes.



At the core, we do not discriminate against any citizen complaints. We receive all grievances, resolve those pertaining to our ministry, and forward and follow up resolution for issues related to other governmental departments, public institutions, and even private entities.



We are thankful for this training, which was not just theoretical but practical as well, led by experienced specialists in various units while maintaining the confidentiality of your clients’ information,” Kabigi stated, emphasizing the need for ongoing collaboration for the benefit of Tanzanians across all sectors.



On her part, Ms. Zaipuna thanked MoCLA for choosing NMB to enhance the capabilities of their center’s personnel, noting that the ministry has selected the right partner to learn about customer service, especially given NMB’s significant systematic and technological advancements to ensure high-quality service delivery.



NMB is a government bank, which is why we believe in mutual understanding as we undertake many initiatives together. You have come to the right place—back in 2020, we decided to implement a ‘transformative strategic plan’ for the bank, recognizing the necessity of investing in both human resources and their environments.

TCB YAZINDUA KAMPENI YA “TOBOA KIDIJITALI” KWA AJILI YA UJUMUISHI WA KIFEDHA NA MATUMIZI YA MIAMALA YA KIDIJITI


Benki ya Biashara Tanzania (TCB) imezindua rasmi kampeni ya kitaifa ijulikanayo kama “Toboa Kidijitali”, ambayo inalenga kuhamasisha wananchi kutumia mifumo ya kisasa ya miamala ya kifedha kwa njia ya kidijiti, sambamba na kuwazawadia wateja wake wanaoshiriki kikamilifu katika matumizi ya huduma hizo.



Uzinduzi huo umefanyika siku ya Ijumaa Aprili 25, 2025, Makao Makuu ya TCB yaliyopo eneo la Makumbusho, jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau mbalimbali wa benki, wafanyakazi, wateja, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.



Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa TCB, Adam Mihayo, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi na Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati, Bi. Lilian Mtali, amesema kuwa benki hiyo imeamua kuwekeza zaidi ya shilingi milioni 200 katika kampeni hii kama sehemu ya kurudisha kwa jamii, lakini pia kama njia ya kuendelea kukuza matumizi ya teknolojia ya kifedha nchini.



Hii ni namna ya kuwarudishia wateja wetu, jamii na wafanyabiashara wadogo wanaotuzunguka. Tumepanga kuwazawadia washindi mbalimbali watakaoibuka kidedea kupitia miamala wanayofanya kwa njia ya kidijiti kwa kipindi cha miezi minne,” amesema Mtali.



Ameongeza kuwa TCB imekuwa mstari wa mbele katika kuwekeza kwenye ubunifu wa mifumo ya huduma za kifedha ili kumwezesha Mtanzania kufanya miamala kwa haraka, kwa usalama na mahali popote, bila kulazimika kufika tawi la benki.



Kwa kutumia huduma kama Popote Mobile App, Popote Visa Card, na mfumo wa Lipa Popote, mteja anaweza kufanya miamala bila usumbufu. Tunasisitiza uhuru wa kujihudumia kibenki kwa kutumia teknolojia kwa sababu muda ni pesa,” amesema Mtali.



Kwa upande wake, Jesse Jackson, Afisa Mkuu wa Huduma za Kidijiti na Ubunifu wa TCB, amesema kuwa kupitia kampeni ya Toboa Kidijitali, benki hiyo inatarajia kutoa zawadi mbalimbali kwa washindi, ikiwemo gari aina ya Mazda, simu ya iPhone 16 Pro Max, bajaji, bodaboda kila mwezi kwa kipindi cha miezi minne.



Jackson amesema kuwa kampeni hii inalenga si tu kuongeza miamala ya kidijitali, bali pia kuchochea ujumuishi wa kifedha kwa makundi yote ya Watanzania, wakiwemo wale wa vijijini na maeneo ya pembezoni.

Thursday, 24 April 2025

BENKI YA EXIM YAKABIDHI MADARASA KWA SHULE MBILI KIGOMA

Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina (kulia), ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma na Bw. Stanley Kafu (kushoto), Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania wakifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa madarasa yaliyojengwa na benki hiyo katika shule mbili za wilaya ya Buhigwe, mkoani Kigoma.

Kigoma, 22 Aprili 2025: Katika juhudi za kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu nchini Tanzania, Benki ya Exim Tanzania imekabidhi rasmi madarasa kwa shule mbili za sekondari wilayani Buhigwe katika mkoa wa Kigoma. Shule hizo, Shule ya Sekondari Kaphunya na Shule ya Sekondari Nyakitundu, zimepokea madarasa hayo yaliyokamilika yenye viti na madawati, ikiwa ni sehemu ya juhudi endelevu za benki hiyo katika kusaidia sekta ya elimu na kuboresha matokeo ya kujifunza kote nchini. Pia benki hiyo imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo kwa shule hizo mbili kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya michezo nchini.



Akizungumza katika hafla hiyo, Stanley Kafu, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim, alisisitiza dhamira ya benki hiyo katika kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini.



"Sisi kama Benki ya Exim, tunaamini kuwa elimu ni msingi wa maendeleo katika jamii yoyote ikiwemo Tanzania. Kwa kuwekeza katika mazingira ya kujifunzia, hatujengi tu madarasa na kutoa madawati haya, bali tunaunda mustakabali wa vijana wetu na kuwawezesha jamii. Tunajivunia pia kuchangia maendeleo ya sekta ya michezo kwa vijana wetu kwa kutoa vifaa vya michezo maana ni sehemu ya kuimarisha afya zao ili waweze kusoma vizuri,” alisema Kafu.



Mbali na sekta ya elimu, benki ya Exim imekuwa ikishiriki kikamilifu katika miradi mbalimbali ya uwajibikaji kwa jamii kupitia mpango wake unaojulikana kama ‘Exim Cares’. Benki hiyo imechangia kuboresha huduma za afya kwa kutoa vifaa tiba kwa hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini, imewezesha ujumuishaji wa kifedha kupitia suluhisho za benki za kidijitali, na pia kushiriki katika jitihada za utunzaji wa mazingira.



Naye Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina, kwa niaba ya Mgeni Rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, aliipongeza Benki ya Exim kwa mchango wake mkubwa katika kusaidia juhudi za serikali za kuboresha upatikanaji wa elimu bora.



"Mchango huu wa madarasa, vitu na madawati yake kutoka Benki ya Exim ni uthibitisho wa nguvu ya ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi katika kuendeleza na kufikia malengo ya taifa. Madarasa haya yatatoa mazingira bora ya kujifunza kwa watoto wetu, kuwawezesha kufaulu kitaaluma na kujenga maisha yao ya baadaye. Tunatoa wito kwa wadau wengine kuungana nasi katika kuinua sekta ya elimu," alisema Mhe. Ngayalina.



Sekta ya elimu nchini inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uchache wa walimu, ukosefu wa maabara, na upungufu wa madarasa katika shule mbalimbali zikiwemo shule ya Sekondari Kaphunya na Shule ya Sekondari Nyakitundu. Mazingira haya yanaathiri ubora wa elimu na kupunguza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi na hivyo kuathiri kiwango cha elimu nchini.