Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

Wednesday, 23 July 2025

NBC, VODACOM NA SUNDERLAND WAZINDUA MFUMO WA KUNUNUA JEZI ZA TAIFA STARS KWA NJIA YA MTANDAO

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ (katikati), akikabidhi jezi ya timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kwa mmoja wa wadau wa habari wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mfumo wa mauzo ya jezi za timu ya Taifa kwa njia ya mtandao. Mfumo huo unaratibiwa kwa ushirikiano wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) pamoja na wadau wengine wakiwemo Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania na Kampuni ya Sunderland. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo, ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), wadau wa mpango huo, pamoja na wanahabari.

Dar es Salaam, Julai 23, 2025 — Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania na kampuni ya Sunderland, wamezindua rasmi mfumo wa kisasa wa mauzo ya jezi za timu ya taifa, Taifa Stars, kwa njia ya mtandao. Hatua hii inalenga kurahisisha upatikanaji wa jezi hizo kwa wananchi wote hususan kuelekea mashindano ya CHAN 2025.

Uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam, ukiongozwa na Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (Mwana FA), na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa TFF na washirika wa mpango huo. Benki ya NBC iliwakilishwa na Mkuu wa Idara ya Miamala, Bw Mangire Kibanda.

Mhe. Mwinjuma amepongeza hatua hiyo na kutoa wito kwa taasisi mbalimbali nchini kuanzisha siku maalum ambapo wafanyakazi wao wataweza kuvaa jezi za Taifa Stars kama sare rasmi ya kazini.

“Hili ni wazo zuri kwa sababu michezo huleta mshikamano wa kitaifa. Naomba taasisi zizingatie kuwahamasisha na hata kuwanunulia wafanyakazi wao jezi hizi kwa kutumia mfumo huu wa kidijitali,” alisema Mhe. Mwinjuma.

Kwa upande wake, Bw. Kibanda alisema mfumo wa e-commerce wa NBC unawawezesha Watanzania kununua jezi za Taifa Stars bila kufika dukani.

“Unaweza kulipia moja kwa moja kwenye akaunti ya Sunderland ndani ya NBC, au kupitia matawi yetu, mawakala, na huduma za kidijitali kama NBC Kiganjani na NBC Connect,” alifafanua.

Alisisitiza pia umuhimu wa wafanyabiashara kufungua akaunti ya biashara NBC ili kunufaika na malipo kwa njia ya VISAMasterCard, na njia nyingine za kimataifa.

Uzinduzi huu ni sehemu ya mikakati ya kuendeleza uzalendo, kukuza mauzo ya jezi na kukuza matumizi ya mifumo ya kidijitali nchini.

Mkuu wa Idara ya Miamala wa Benki ya NBC, Bw. Mangire Kibanda (kushoto), akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mfumo wa mauzo ya jezi za timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kwa njia ya mtandao. Mfumo huo unaratibiwa kwa ushirikiano kati ya Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na wadau wengine wakiwemo Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania na Kampuni ya Sunderland. 



No comments:

Post a Comment