 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa Vodacom Tanzania Plc, Abednego Mhagama, wakati alipowasili katika hafla ya makabidhiano ya madarasa mawili yaliyojengwa katika Shule ya Msingi Mahilo, mkoani Ruvuma, kupitia programu ya Vodacom Tanzania Foundation.
Madarasa hayo yanalenga kuwapatia wanafunzi na walimu mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, na ni sehemu ya juhudi za kampuni hiyo za kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto kupitia ujenzi na ukarabati wa madarasa.
Katika awamu hii, shule tatu za msingi za umma katika mikoa ya Pwani, Ruvuma na Morogoro zimenufaika na mpango huo. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Agosti 20, 2026, katika Shule ya Msingi Mahilo, mkoani Ruvuma. |
No comments:
Post a Comment