Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 30 August 2024

USIKOSE ARSENAL vs BRIGHTON 31 AGOSTI NDANI YA DStv PEKEE


NMB YAINGIA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA K-FINCO YA KOREA KUSINI


Benki ya NMB leo imesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) ya kushirikiana na Shirika la Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la Korea Finance for Construction (K-FINCO).


Lengo la makubaliano hayo ni kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania ambapo NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza miradi hiyo. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Benki ya NMB na K-FINCO zitakuwa na jukumu muhimu la kuvutia miradi mikubwa ya ujenzi itakayosaidia kuboresha maisha ya Watanzania. Ushirikiano huu pia unatarajiwa kuendeleza ukuaji wa mitaji, kutengeneza ajira, na kuifanya Tanzania kuwa kinara wa miundombinu katika ukanda huu.


Hafla ya utiaji saini ya ushirikiano huo imeshuhudiwa na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Mheshimiwa Togolani Mavura. Ujumbe wa NMB uliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), Bi Ruth Zaipuna, huku ujumbe wa K-FINCO ukiongozwa na Dkt. Eunjae Lee, ambaye ni CEO wa taasisi hiyo na mwenyekiti wa bodi yake ya wakurugenzi.


Mkataba huo, ambao unatarajiwa kuimarisha maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, unazichagiza taasisi hizo mbili kufanya kazi kwa karibu zaidi ili kuchangia kikamilifu ukuaji wa uchumi wa Tanzania na jitihada za ujenzi wa Taifa.


Tunaimani kuwa hatua hii itaimarisha mahusiano ya kiuchumi na kidiplomasia kati ya Tanzania na Korea Kusini, na kukuza urafiki kati ya wananchi wa mataifa haya mawili.

NMB BANK & SOUTH KOREA'S K-FINCO FORGE STRATEGIC PARTNERSHIP


NMB Bank PLC and Korea Finance for Construction (K-FINCO) have officially signed a strategic partnership agreement to boost infrastructure development in Tanzania!


In the Memorandum of Understanding, NMB Bank shall provide bank guarantees to support K-FINCO members in financing and executing construction projects across Tanzania.


The agreement was signed in Seoul, South Korea today by NMB Bank’s CEO, Ruth Zaipuna, and K-FINCO’s CEO and Chairperson, Dr. Eunjae Lee, with the ceremony attended by Tanzania’s Ambassador to South Korea, H.E Ambassador Togolani Mavura, as well as other dignitaries from NMB Bank, K-FINCO, and the Tanzanian embassy.


This partnership marks a significant step in enhancing Tanzania’s infrastructure, creating job opportunities, and driving socio-economic development. It also strengthens the bilateral ties between Tanzania and South Korea, fostering collaboration and friendship between our nations.


The agreement comes few months after a successful diplomatic mission by the President of the United Republic of Tanzania. H.E Dr. Samia Suluhu Hassan in South Korea back in June 2024.


NMB Bank will leverage its strong heritage in Tanzania, deep local knowledge, world-class expertise, and financial solutions to ensure the success of this partnership.


BENKI YA EXIM YACHANGIA HUDUMA ZA AFYA WILAYANI KAHAMA

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita (watatu kutoka kushoto), akipokea vifaa tiba kutoka kwa Stanley Kafu, Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim ukiwa ni mchango wa benki hiyo katika jitihada za kuboresha huduma za afya katika makabidhiano ambayo yamefanyika katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga mnamo tarehe 29 Agosti, 2024.

Shinyanga: Benki ya Exim Tanzania imetoa msaada wa vifaa tiba ya afya kama sehemu ya mchango wake katika jitihada za kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga.


Makabidhiano hayo ambayo yamefanyika mbele ya Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mboni Mhita, yanalenga kusaidia kupunguza changamoto za huduma za afya katika wilaya hiyo katika tukio ambalo limefanyika katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama mnamo tarehe 29 Agosti, 2024.

“Takwimu zinaonesha kama taifa tumepiga hatua katika kuongeza na kuboresha miundominu katika vituo vya afya nchini, lakini changamoto ya vifaa tiba pamoja na wataalamu wa afya bado ipo. Utoaji huu wa vifaa tiba ni sehemu ya mpango wetu mkubwa katika kuboresha huduma za afya nchini,” anasema Stanley Kafu, Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania.


Kupitia mpango wa ujulikanao kama ‘Exim Cares’, benki ya Exim imekuwa ikichangia katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo katika sekta za elimu, mazingira, utalii, Uchumi, na afya. Hii ni sehemu ya dhamira yake ya kuboresha maisha ya kila Mtanzania popote alipo nchini.


Kafu anaongeza kuwa, “Tumekuwa tukishiriki katika mikakati mbalimbali ya kuboresha huduma za afya. Mfano mwaka huu, tumeshiriki katika kampeni ya kitaifa ya uchangiaji damu katika mikoa mbalimbali, vilevile tumetoa vitanda vya kujifungulia wajawazito Mkoani Morogoro pamoja na vitanda vya hospitali Mkoani Tanga na kufanikiwa kumaliza tatizo la uhaba wa vitanda katika kituo cha afya, Mwakadila.”

Benki ya Exim Tanzania ni moja kati ya benki kubwa tano hapa nchini yenye matawi yake katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini Tanzania. Benki hiyo pia inajivunia kuwa benki ya kwanza ya Kitanzania kuvuka mipaka na mpaka sasa wanapatikana katika nchi za Djibouti, Comoro, na Uganda.

USIKOSE MECHI ZA PREMIER LEAGUE WIKIENDI HII NDANI YA DStv PEKEE

CRDB, VISA KUTOA PUNGUZO LA ASILIMIA 22 KWA ABIRIA WA QATAR AIRWAYS


Dar es Salaam, Tarehe 26 Agosti 2024: Benki ya CRDB kwa kushirikiana na wabia wake wa kimkakati ambao ni kampuni ya Visa International imetangaza kutoa nafuu ya nauli ya asilimia 22 kwa abiria wa Shirika la Ndege la Qatar wanaolipia tiketi zao kwa kutumia kadi za Tembocar Visa. 

Nafuu hiyo inajumuisha punguzo la asilimia 12 litakalotolewa na kampuni ya Visa International pamoja na asilimia 10 ya fedha taslimu itakayorudishwa kwenye akaunti ya mteja wa Benki ya CRDB baada ya kulipia tiketi yake.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa wakati wa kuzindua kampeni hiyo itakayodumu kwa miezi sita, Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wa Awali na Kati wa Benki ya CRDB, Muhumuliza Buberwa amesema ushirikiano huu unalenga kujunga utamaduni kwa wateja kutumia kadi kufanya malipo na kuachana na matumizi ya fedha taslimu. 

“Punguzo hili la asilimia 22 ni sehemu ya motisha kwa wateja kujenga utamaduni wa kutumia kadi kufanya malipo. Nitumie nafasi hii kuwakaribisha wateja wetu wanaotaka kusafiri kutumia ndege za Shirika la Ndege la Qatar ili kunufaika na punguzo hili ili. ,” amesema Paul huku akibainisha kuwa punguzo hilo pia linatosha kwa abiria kununua zawadi kwa ajili ya wapendwa wao pindi wawapo safarini.


Kaimu Mkurugenzi huyo amesema ushirikiano wa Benki ya CRDB, Visa International na Shirika la Ndege la Qatar unazijumuisha taasisi mbili kubwa zenye ubora unaotambulika ndani na kimataifa uliozifanya zitunukiwe tuzo za aina tofauti.

Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2000, Paul amesema Benki ya CRDB imetunukiwa takriban tuzo 200 a ndani na kimataifa ikiwamo tuzo za utoaji wa huduma bora za Visa, wakati Shirika la Ndege la Qatar likishinda tuzo ya shirika bora la ndege zinatolewa na kampuni ya Skytrax mara nane kati ya mwaka 2011 mpaka mwaka 2024.

Shirika hilo pia limeshinda tuzo ya shirika lenye daraja bora la biashara duniani (world’s best bisness class), ukumbi bora wa daraja la biashara duniani (world’s best business class lounge) na shirika bora la ndege ukanda wa Mashariki ya Kati.

“Benki ya CRDB na Shirika la Ndege la Qatar pia tunafanana kwenye ubunifu. Benki yetu ndio kiongozi katika ubunifu wa huduma na bidhaa zinazokidhi mahitaji na matarajio ya wateja wetu vivyo hivyo kwa Shirika la Ndege la Qatar ambalo limeshinda tuzo za kimataifa kutokana na ubunifu wake. Vilevile, sisi sote wawili tunajali na kuyatunza mazingira,” ameeleza Buberwa.


Meneja Mkazi Shirika la Ndege la Qatar, Isaack Wambua amesema ndege zao zenye makao makuu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad uliopo jijini Doha ambao umeshishinda tuzo ya uwanja bora wa ndege duniani mara tatu kuanzia mwaka 2021, zinatua katika viwanja vingine 170 duniani kote hivyo kuwapa abiria wao uhakika wa kufika popote wapatakapo huku Benki ya CRDB ikiwahakikishia kukamilisha safari zao kwa gharama nafuu. 

VIONGOZI WA DINI WAPONGEZA UZINDUZI WA AKAUNTI YA SADAKA CRDB


Dar es Salaam, 27 Agosti 2024:
Viongozi wa dini nchini wameipongeza Benki ya CRDB kwa kuzindua Akaunti ya Sadaka mahsusi kwa ajili ya taasisi za dini kukusanya sadaka, zaka na michango mingine inayolenga kuwarahisishia waumini kumtolea Mwenyezi Mungu wakati wa ibada au hata wanaposhindwa kuhudhuria ibada. 
 
Akizungumza kuhusu Akaunti ya Sadaka Naibu Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Chesco Msaga amesema nimapinduzi yatakayosaidia kuwakumbusha Wakristo kumtolea Muumba wao ili kukamilisha kazi kubwa ya uenezi wa Injili nchini na duniani kwa ujumla.


“Maisha ya mwanadamu hayana maana yoyote hapa duniani asipomwabudu Muumba wake na kumtolea zaka na sadaka kama ilivyoagizwa katika Biblia Takatifu. Nawapongeza Benki ya CRDB kwa ubunifu huu na nawaomba Wakristu kote nchini kuiona fursa hii ya kumtolea Bwana kirahisi,” amesema Padre Msaga.

Naibu katibu huyo wa TEC amesema fursa zinazoletwa na maendeleo ya sayansi na teknolojia zinapaswa kutumiwa na Wakristu kuimarisha ukaribu wao na Mwenyezi Mungu na kumtolea sadaka na zaka pamoja na michango mingine ni kati ya njia kuu za kutimiza agano na kuieneza Injili Takatifu.


Akizungumza kwa niaba ya Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dkt. Abubakary Zubery Bin Ally, Sheikh Hilal Shaweji almaarufu kama Sheikh Kipozeo naye amepongeza ubunifu uliofanywa akisema utawafaa sana Waislamu kushiriki kutoa sadaka ambayo ni kati ya nguzo muhimu za dini ya Kiislamu.
 
“Waislamu tumeagizwa kutoa sadaka na zaka. Tumeagizwa kutoa sadaka kwa ajili ya kuwasaidia wasiojiweza na kuendeleza Uislamu duniani. Ubunifu uliofanywa na Benki ya CRDB unaturahisishia kutimiza msingi huu muhimu kwa imani yetu. Tusiwe tena na sababu ya kuwa mbali na Mwenyezi Mungu,” amesema Sheikh Kipozeo.  

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema siku zote wamekuwa wakijitahidi kubuni huduma na bidhaa zinazokidhi mahitaji na matarajio ya wateja ukigusa sekta tofauti ukiwamo utamaduni na imani za watu watu wanaowahudumia.
 

“Maneno Matakatifu yanasema binadamu aliumbwa ili amtukuze Muumba wake. Hili ni jukumu letu wanadamu kwa kipindi chote cha maisha yetu hapa duniani. Katika kumtukuza Mwenyezi Mungu, tunakumbushwa kumtolea sadaka na zaka pia. Azma ya Benki yetu ya CRDB siku zote imekuwa kukidhi matarajio na mahitaji ya wateja wetu na jamii tunayihudumia kwa ujumla. Katika kufanikisha hili tumekuwa tukibuni huduma na akaunti zinazoendana na misingi ya imani pamoja na maeneo mengine mfano biashara, uwekezaji na utunzaji akiba,” amesema Nsekela.

Katika jitihada hizi, Nsekela amesema tayari Benki ya CRDB imebuni Huduma za Al Barakah zinazoendana na imani ya Kiislam lakini bado kuna fursa ya kuwahudumia zaidi waumini wote pamoja na taasisi za dini kwa ujumla ndio maana sasa imeleta Akaunti ya Sadaka.

Thursday 29 August 2024

NMB BANK DONATES DESKS & HEALTH FACILITIES TO KILOSA DISTRICT


Morogoro: NMB Bank has donated medical equipment to Kimamba Health Center and desks, chairs, and tables valued at TZS 33.1 million to the Kilosa district. This gesture demonstrates the bank's commitment to reinvesting its profits into the Morogoro community.


During separate handover ceremonies at Kimamba Health Center and Chanzulu Secondary School, NMB Bank’s Central Zonal Manager, Janet Shango emphasized the bank’s dedication to collaborating with the government to tackle various challenges. This support extends to the education, health, and emergency response sectors.


Shango detailed the contributions made to the Kilosa district, which included 235 desks distributed among four primary schools—Dakawa Centre, Mbigiri, Malangali, and Tindiga—each receiving 65 desks. Furthermore, Chanzulu Secondary School was provided with 50 tables and 50 chairs.

“Our donations are part of our commitment as a bank to support community development. We are obligated to ensure that our surrounding community benefits from our profit returns by aiding education, health, and emergency sectors. At Kimamba Health Center, NMB has donated 60 mattresses, 60 bed sheets, and a blood pressure machine,” Shango elaborated.

She mentioned that for over a decade, the bank has been dedicating 1% of its earnings back to the community.

Dr. Alfred Chiponda, the Chief Medical Officer at Kimamba Health Center, conveyed his appreciation to the bank’s management, thanking them for providing 60 mattresses, 60 bed sheets, and three blood pressure monitors, amounting to TZS 8.1 million.

NBC YASISITIZA DHAMIRA YAKE KUCHOCHEA UKUAJI BIASHARA, UCHUMI WA BULUU ZANZIBAR

Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila akizungumza kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga (katikati) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi, Uchumi na Uwekezaji) Zanzibar, Sharif Ali Sharif (wa tano kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa biashara visiwani Zanzibar pamoja na maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Meneja wa benki hiyo tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (wa nne kushoto) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable.
Meneja Mahusiano Mwandamizi (Sekta ya Umma na Taasisi) wa benki ya NBC, Gasto Ndanu (wa pili kulia) na Meneja Mahusiano (Huduma Binafsi) wa benki hiyo, Khafsa Mohammed (kulia) wakizungumza na baadhi ya wadau wa sekta ya biashara visiwani Zanzibar wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar.
Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (kulia) na Meneja Mahusiano (Huduma Binafsi) wa benki hiyo, Khafsa Mohammed (katikati) wakizungumza na mmoja wa wadau wa sekta ya biashara visiwani Zanzibar wakati wa hafla fupi ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’.
Baadhi ya maafisa wa benki ya NBC wakifuatilia hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.
Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (wa pili kushoto) akiwa kwenye
picha ya pamojaj na maofisa wengine
waandamizi wa benki hiyo wakati wa hafla fupi
ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu
wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO
Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika
visiwani humo jana jioni. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.

Zanzibar, 29 Agosti 2024 – Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeelezea dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na wafanyabishara wadogo, wa kati na wakubwa kupitia huduma zake mbalimbali za kibenki ili kuchochea ukuaji wa uchumi na mchango wa wadau hao katika kufanikisha agenda ya Uchumi wa Buluu na uwezeshaji wa maendeleo visiwani Zanzibar.

Dhamira hiyo imesisitizwa na Meneja wa benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila wakati akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Theobald Sabi, kwenye hafla fupi ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo jana jioni.

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga aliongoza uzinduzi wa jukwaa hilo, hafla iliyohudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi, Uchumi na Uwekezaji) Zanzibar, Sharif Ali Sharif.

Jukwaa hilo liliwakutanisha pamoja viongozi wa kampuni na mashirika kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Mauritius na mataifa jirani likiwa na lengo la kuimarisha uchumi wa buluu na kuwawezesha wafanyabiashara wa ndani. Benki ya NBC ilikuwa miongoni mwa wadhamini muhimu wa jukwaa hilo.

Wednesday 28 August 2024

DR. MPANGO URGES NMB TO SPREAD INSURANCE KNOWLDGE TO ROAD USERS

Vice President of the United Republic of Tanzania, Hon. Dr. Philip Mpango, hands over an award to NMB Bank’s Head of Bancassurance, Martine Massawe in recognition of the Bank’s contribution towards the success of the Road safety week exhibition and 50 years commemoration of the National Road Safety Council as the main sponsor. On the left is the Minister of Internal Affairs, Hon. Eng. Hamad Masauni.

Dodoma: Vice President of the United Republic of Tanzania, Hon. Dr. Philip Mpango has urged NMB Bank to extend its reach to a larger audience to provide education on insurance, particularly targeting operators and users of motor vehicles.

Dr. Mpango gave this directive on the August 26, 2024, during his visit to the NMB exhibition booth as part of the 50th anniversary celebrations of the National Road Safety Council, culminating at the Jamhuri Stadium in Dodoma.

In collaboration with Sanlam and Reliance Insurance Company Tanzania Ltd, NMB Bank served as the main sponsor for the celebrations, marking the third consecutive year of their sponsorship.


The Vice President emphasized the importance of insurance for motor vehicle users, noting that many people lack adequate knowledge about its significance. He stated that NMB has the capacity to reach more Tanzanians as it is a trusted institution.

"Many people don't see the value of insurance. If nothing happens in the first to fourth year, they tend to drop it. NMB, you can effectively handle this task. I urge you to take it on because the protection of a motor vehicle lies in insurance, and nothing else," said Dr. Mpango.

He pointed out that some perceive that insurance primarily benefits banks and companies, which is not true. He urged for more educational initiatives, particularly targeting motorcycle operators known as Bodaboda, declaring NMB the appropriate partner for this effort.

Tuesday 27 August 2024

VODACOM, HUAWEI WAZINDUA MPANGO WA UJUZI WA KIDIGITALI KWA WOTE


DigiTruck, darasa la kidijitali linalotembea, ushirikiano kati ya Huawei na Vodacom Tanzania, litazinduliwa nchini Tanzania mnamo August 2024 kabla ya Vodacom Twende Butiama Cycling Tour 2024. Mpango huu unalenga kuwapatia Watanzania ujuzi wa msingi wa kidijitali na kuwaboreshea ujuzi na maarifa, ukilenga wanafunzi zaidi ya 5,500, wanawake, na vijana katika mikoa 10.


Darasa hili la kidijitali linalotembea linaonesha kujitolea kwao kuwawezesha Watanzania kupata ujuzi muhimu wa kidijitali, hususani kwa maeneo na watu walio na upungufu wa fursa. Kupitia programu maalum kwa shule za sekondari, vijana waliojiajiri, na wanawake wajasiriamali, DigiTruck inalenga kuwawezesha Watanzania na nyenzo wanazohitaji ili kufanikiwa katika ulimwengu unaozidi kuwa wa kidijitali.




EXIM BIMA FESTIVAL: BURUDANI YENYE NIA YA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA AKILI

Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano, Stanley Kafu (kati) kutoka Benki ya Exim Tanzania, akizungumza wakati wa kutangaza ujio wa tamasha la Exim Bima Festival 2024, likiwa na kaulimbiu ‘Amsha Matumaini’, ambalo litafanyika terehe 28 Septemba 2024 katika Viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Tike Mwakyoma, Meneja kutoka Idara ya Bima na Kauthar D’souza, Meneja Mkuu kutoka Idara ya Masoko na Mawasiliano, wakiwa Makao Makuu ya Exim Bank jijini Dar es Salaam mnamo Agosti 23, 2024.

Dar es Salaam: Mwezi Septemba mwaka huu, Benki ya Exim Tanzania inawakaribisha Watanzania wote na wadau mbalimbali kujumuika pamoja kwa ajili ya jambo muhimu na la kipekee; Afya ya Akili. Ikiwa inasherehekea miaka 27 ya kuwahudumia Watanzania tangu kuanzishwa kwake, benki ya Exim inakuja na Exim Bima Festival 2024, ikiwa na kaulimbiu ‘Amsha Matumaini’, ambayo itafanyika mnamo tarehe 28 Septemba 2024 katika Viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.


Hili ni zaidi ya tamasha, ni wito kwa kila Mtanzania kuchukua hatua kuongeza uelewa na msaada kwa watu wenye tatizo la afya ya akili. Wakati changamoto za afya ya akili zikiongezeka nchini, tamasha hili ni fursa ya kipee kwa watu binafsi, wadau, taasisi, na sekta mbambali kuungana katika kukusanya fedha kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wale wanaoathirika na tatizo la afya ya akili.


Exim Bima Festival 2024 ni moja ya malengo ya mpango wa ‘Exim Cares’ wa Exim Bank Tanzania. Tamasha la mwaka huu limepanga kuelekeza nguvu zake katika kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa wa bima katika jamii yetu huku likijikita katika kusaidia kuongeza upatikanaji wa huduma za afya ya akili na ustawi wa jamii ya Watanzania kote nchini. Benki ya Exim imejiwekea lengo la kukusanya jumla ya TZS milioni 300 ndani ya miaka mitatu ijayo ili kugharamia huduma muhimu na maboresho ya miundombinu katika vituo vya afya ya akili.

“Tatizo la afya ya akili sio tu ugonjwa, ni suala la kijamii zaidi. Wanaoathirika ni familia zetu, marafiki zetu, mfanyakazi mwenzako, na jamii zetu. Kwa pamoja, tunaweza kubadirisha hadithi hii. EXIM BIMA FESTIVAL 2024 sio tu kwa ajili ya kujumuika na kufurahia pamoja; pia tunalenga kuongeza uelewa na kubadilisha maisha ya Watanzania,” anasema Stanley Kafu, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania.

Kafu anaongeza, “Tunapojumuika pamoja, tunavunja ukimya, tunaondoa unyanyapaa, na kujenga jamii ambayo inalipa suala la afya ya akili kipaumbele na kuhakikisha waathirika wanapata huduma bora wakati zinapohitajika. Karibu tuungane Kuamsha Matumaini Yao.”

NI BALAA, KILA MTU NI MSHINDI NA VODACOM TANZANIA!!!

Mshindi wa droo ya nne ya kampeni ya Ni Balaa, Kila Mtu Ni Mshindi kutoka Vodacom Tanzania Plc, Khalid Mohamed kutoka Temeke (kulia), akipokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 1 kutoka kwa Caleb Majo Meneja Biashara na Masoko wa kanda ya Dar es Salaam na Pwani (kushoto) Vodacom, katika Duka la Vodacom Mlimani City mwishoni mwa wiki iliyopita. Kupitia kampeni hii wateja wa Vodacom wanajiongezea nafasi za kushinda kila wakinunua vifurushi au kufanya miamala kupitia M-pesa Super App au kwa kupiga *150*00#
Meneja Biashara na Masoko kutoka Vodacom Tanzania, Caleb Majo (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi ya Shilingi milioni 1 mshindi wa droo ya nne ya Kampeni ya Ni Balaa, Kila Mtu ni Mshindi kutoka Vodacom Bi. Zulfa Said kutoka Goba (kulia) katika Duka la Vodacom Mlimani City mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mshindi wa kampeni ya Vodacom Tanzania Plc ‘Ni Balaa, Kila Mtu ni Mshindi' Omary Mohamed Abdallah kutoka Tuangoma, Dar es Salaam (kulia), akipokea mfano wa hundi ya TZS 500,000 kutoka kwa Caleb Majo (kushoto), Meneja Biashara na Masoko kanda ya Dar es Salaam na Pwani kutoka Vodacom, katika Duka la Vodacom lililopo Mlimani City. Endelea kufanya miamala mingi zaidi kwa kutumia M-pesa Super App au kupiga *150*00# pamoja na kununua vifurushi ili kujiongezea nafasi ya kushinda.
Mshindi wa kampeni ya Vodacom Tanzania Plc ya ‘Ni Balaa, Kila Mtu ni Mshindi’, Rajabu Mrisho Rajabu kutoka Kinondoni (kulia), akipokea mfano wa hundi ya Shilingi 500,000 kutoka kwa Caleb Majo (kushoto), Meneja Biashara na Masoko kanda ya Dar es Salaam na Pwani kutoka Vodacom, katika Duka la Vodacom lililopo Mlimani City Ijumaa wiki iliyopita.
Mshindi wa kampeni ya Ni Balaa! kutoka Vodacom Tanzania Plc Bernado Osward kutoka Kawe (kulia), akipokea mfano wa hundi ya TZS 500,000 kutoka kwa Caleb Majo (kushoto), Meneja Mauzo na mkakati wa biashara kanda ya Dar es Salaam na Pwani kutoka Vodacom Tanzania, katika Duka la Vodacom Mlimani City wiki Ijumaa wiki iliyopita.