Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 29 August 2024

NBC YASISITIZA DHAMIRA YAKE KUCHOCHEA UKUAJI BIASHARA, UCHUMI WA BULUU ZANZIBAR

Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila akizungumza kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga (katikati) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi, Uchumi na Uwekezaji) Zanzibar, Sharif Ali Sharif (wa tano kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa biashara visiwani Zanzibar pamoja na maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Meneja wa benki hiyo tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (wa nne kushoto) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable.
Meneja Mahusiano Mwandamizi (Sekta ya Umma na Taasisi) wa benki ya NBC, Gasto Ndanu (wa pili kulia) na Meneja Mahusiano (Huduma Binafsi) wa benki hiyo, Khafsa Mohammed (kulia) wakizungumza na baadhi ya wadau wa sekta ya biashara visiwani Zanzibar wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar.
Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (kulia) na Meneja Mahusiano (Huduma Binafsi) wa benki hiyo, Khafsa Mohammed (katikati) wakizungumza na mmoja wa wadau wa sekta ya biashara visiwani Zanzibar wakati wa hafla fupi ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’.
Baadhi ya maafisa wa benki ya NBC wakifuatilia hafla fupi ya uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.
Meneja wa Benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila (wa pili kushoto) akiwa kwenye
picha ya pamojaj na maofisa wengine
waandamizi wa benki hiyo wakati wa hafla fupi
ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu
wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO
Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika
visiwani humo jana jioni. Benki hiyo ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.

Zanzibar, 29 Agosti 2024 – Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeelezea dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na wafanyabishara wadogo, wa kati na wakubwa kupitia huduma zake mbalimbali za kibenki ili kuchochea ukuaji wa uchumi na mchango wa wadau hao katika kufanikisha agenda ya Uchumi wa Buluu na uwezeshaji wa maendeleo visiwani Zanzibar.

Dhamira hiyo imesisitizwa na Meneja wa benki ya NBC tawi la Zanzibar, Abdul Karim Mkila wakati akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Theobald Sabi, kwenye hafla fupi ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’ iliyofanyika visiwani humo jana jioni.

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga aliongoza uzinduzi wa jukwaa hilo, hafla iliyohudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi, Uchumi na Uwekezaji) Zanzibar, Sharif Ali Sharif.

Jukwaa hilo liliwakutanisha pamoja viongozi wa kampuni na mashirika kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Mauritius na mataifa jirani likiwa na lengo la kuimarisha uchumi wa buluu na kuwawezesha wafanyabiashara wa ndani. Benki ya NBC ilikuwa miongoni mwa wadhamini muhimu wa jukwaa hilo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Bw. Mkila alibainisha umuhimu, nia na mchango wa benki hiyo katika kushirikiana na wafanyabiashara pamoja na wadau mbalimbali visiwani humo ili kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma zake mbalimbali zilizobuniwa mahususi kwa ajili yao ikiwemo mikopo na huduma za bima.

"Kimsingi ni kwamba NBC tumejizatiti kushirikiana na wadau wote katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Jukumu letu ni kuhakikisha tunawawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati, na wakubwa kwa kuwapatia huduma bora za kibenki, mikopo na bima, ili waweze kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi," alisema Bw. Mkila.

Aidha, aliongeza kuwa benki hiyo itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwezesha maendeleo ya kiuchumi kwa kuleta ushirikishwaji wa kifedha kwa wafanyabiashara wa sekta zote.

Mbali na wakuu wa kampuni na mashirika, jukwaa hilo lililokuwa na kaulimbiu ‘’Kuimarisha Biashara za Ndani na Kujenga Uchumi Imara wa Buluu Zanzibar,” pia liliwakutanisha wadau wengine wa biashara na uchumi wakiwemo wawekezaji. Washiriki walipata wasaa muhimu wa kubadilishana mawazo, uzoefu, na mbinu za kukuza biashara na fursa za uwekezaji visiwani Zanzibar.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri Soraga, alitoa wito kwa washiriki kuendelea kushirikiana kwa ukaribu zaidi ili kukuza uchumi wa visiwa hivyo hususani kupitia katika sekta za utalii, biashara, uvuvi na ujenzi wa makazi.

"Tukio hili ni nafasi adimu kwa wafanyabiashara, wakuu wa taasisi, na wadau mbalimbali kukutana na kujadili kwa kina masuala muhimu kuhusu uwekezaji na ukuaji wa uchumi. Serikali pia tunalitegemea jukwaa hili kama moja ya namna bora zaidi katika kutusaidia kwa kutupatia ushauri kwenye masuala mbalimbali ya kiuchumi ili kuleta maendeleo endelevu na jumuishi," alisema Waziri Soraga.

Kwa upande wake Waziri Sharif, alisisitiza umuhimu wa wakuu wa makampuni kukutana mara kwa mara ili kujadili fursa na changamoto zinazokabili sekta mbalimbali za kiuchumi kwa kuwa mijadala na maoni yao kwa kiasi kikubwa yatasaidia kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kukuza uchumi wa Zanzibar hususani kupitia agenda ya uchumi wa buluu.

“Kwa ujumla uzinduzi wa jukwaa hili la The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo huku ukisaidia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta za uwekezaji na biashara, na kuleta mchango mkubwa kwa ustawi wa uchumi wa Zanzibar.’’ Alisema.

No comments:

Post a Comment