• Ushirikiano wa kimkakati kuwawezesha wafanyabiashara kupata ujuzi, teknolojia na suluhisho za kidijitali
• Mpango huo wazinduliwa rasmi Mwanza Septemba 16
Dar es Salaam, Septemba 11, 2026: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na Vodacom Tanzania PLC zimeingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) ya miaka miwili, yenye lengo la kuimarisha uwezo wa wafanyabiashara nchini kupitia Mpango wa Maendeleo ya Wafanyabiashara wa Rejareja (Retailer Development Programme).
Mpango huo umebuniwa kuwawezesha wafanyabiashara kupata ujuzi wa vitendo katika usimamizi wa biashara, fedha na matumizi ya teknolojia, kwa lengo la kukuza biashara zao na kuongeza mchango wao katika ukuaji wa uchumi.
Ukiendeshwa chini ya kaulimbiu “Growing Innovatively Together” (GRIT), mpango huo unaonesha dhamira ya pamoja ya TBL na Vodacom Tanzania kuwawezesha wafanyabiashara wanaoshiriki katika mnyororo wa thamani wa TBL, huku wakiimarisha mchango wao katika uchumi wa Tanzania.
TBL: Wafanyabiashara ni Nguzo Muhimu
Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Masuala ya Kisheria na Uhusiano wa Kampuni wa TBL, Neema Temba, alisema ushirikiano huo unaonesha umuhimu wa kuwekeza katika uwezo wa wafanyabiashara ili kuwawezesha kukua kwa muda mrefu.
“Kwa TBL, wafanyabiashara ni nguzo muhimu ya biashara na ukuaji wa uchumi. Kupitia ushirikiano na Vodacom Tanzania, tunawekeza katika ujuzi, teknolojia na uendelevu wa biashara ili kuwawezesha kukuza shughuli zao na kunufaika na fursa mpya. Hivyo tunajenga thamani inayonufaisha biashara, familia na jamii kote nchini,” alisema Bi. Temba.
Ushirikiano huo utaunganisha mtandao wa TBL wa zaidi ya wafanyabiashara 26,000 na uzoefu wa Vodacom Tanzania katika mawasiliano, ubunifu wa kidijitali na huduma za kifedha, kwa lengo la kuwasaidia wafanyabiashara kuboresha ufanisi, uimara na uendelevu wa biashara zao.

.jpeg)



.jpeg)





.jpeg)
.jpeg)









.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)