Blog Rebranding Teaser_030826

Blog Rebranding Teaser_030826

Stanbic Bank Banner_070826

Stanbic Bank Banner_070826

Absa Loan Campaign_160426

Absa Loan Campaign_160426

Saturday, 26 April 2025

WIZARA YA SHERIA YAISHUKURU NMB KWA KUIMARISHA KITUO CHA HUDUMA


Wizara ya Katiba na Sheria (MoCLA), imeishukuru Benki ya NMB kwa kukubali kuendesha mafunzo ya kukijengea uwezo Kituo cha Huduma kwa wateja cha wizara hiyo, kilichotembelea Kituo cha Huduma kwa Wateja NMB ‘NMB Contact Center,’ kujifunza mifumo ya kupokea taarifa, malalamiko, kero na changamoto za wateja na kuzitatua.



Shukrani hizo zimetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Lawrence Kabigi, aliyeongoza masafara wa watumishi wa kituo hicho, wafanyakazi wa MoCLA na Wanasheria wa Serikali, alipokuwa akitoa neno la shukrani kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna baada ya kukamilisha mafunzo yao.



Kabigi alibainisha kuwa, siku mbili za mafunzo yao NMB, hususani katika Kituo cha Huduma kwa Wateja ‘NMB Contact Center,’ yeye na washiriki wengine kutoka MoCLA wamejifunza mengi, ikiwemo namna kituo hicho na taasisi nzima inavyotoa huduma tangu kupokea malalamiko na kero za wateja wao na kuyashughulikia kwa utaratibu wa kisasa zaidi.



Tulikuja hapa pia kuona tunatofautiana vipi katika teknolojia kwenye kushughulikia changamoto za wateja wenu, tumejionea namna mlivyotengeneza mifumo bora, sahihi na ya kisasa inayoshughulikia changamoto. Mifumo mizuri ambayo haimhitaji tu mfanyakazi kujibu, bali mifumo yenyewe inajibu na kuleta suluhishi za kimahitaji.



Na sisi tunaangalia namna ya kufikia ufanisi wenu katika kuhudumia wananchi wanaosubiri kutoka kwetu ufumbuzi wa changamoto zao, tukiamini kwamba tunapopambana kumaliza kero na changamoto za wananchi bila kutumia muda wao, tuNawapa wigo mpana wa kuendelea kuwajibika na uzalishaji mwingine na kukuza pato lao na la taifa kwa ujumla.



Mwananchi ambaye tutamsaidia kumaliza changamoto zake, hata asipotulipa tutakuwa tumempa muda wa kufanya mambo mengine na kwa mantiki hiyo ataweza kulipa kodi serikalini.



Kimsingi sisi hatubagui malalamiko ya wananchi, tunayapokea yote na yaliyo ndani ya wizara yetu yanatatuliwa, na yale ya wizara ama idara za serikali, taasisi za umma na binafsi tunayapeleka na tunafuatilia ufumbuzi wake.



Tunashukuru kwa mafunzo haya, ambayo si tu yalikuwa ya nadharia, bali kwa vitendo kupitia wataalam mahiri na wabobevu wanaohudumu kwenye vitengo mbalimbali bila kuathiri usiri wa taarifa za wateja wenu,” alisema Kabigi na kutaka mashirikiano baina ya MoCLA yaendelee kwa ustawi wa maisha ya Watanzania wa kada zote.

Friday, 25 April 2025

MINISTRY OF CONSTITUTION HAILS NMB FOR EMPOWERING SERVICE CENTER


The Ministry of Constitution and Legal Affairs (MoCLA) has expressed gratitude to NMB Bank for facilitating training to bolster the capabilities of the Ministry's Customer Service Center. This was after the center visited NMB’s Customer Contact Center to learn about systems for receiving information, complaints, issues, and challenges from clients and resolving them effectively.



These thanks were given by the Assistant Director of Human Rights Monitoring at the Ministry of Constitution and Legal Affairs, Lawrence Kabigi, who led a team of the center's staff, MoCLA employees, and Government Lawyers, during his address of appreciation to NMB Bank's Chief Executive Officer, Ms. Ruth Zaipuna, after completing their training.



Kabigi noted that during the two-day training at NMB, especially at the Customer Contact Center, he and other participants from MoCLA learned a lot, including how the center and the entire institution deliver services from receiving complaints and issues to addressing them using advanced methodologies.



We also came here to understand the differences in technology used in handling customer challenges. We have witnessed how you have developed excellent, accurate, and modern systems that address these challenges. These efficient systems not only allow staff to respond but also let the system itself provide solutions where needed.



We aim to achieve your level of efficiency in serving citizens who rely on us to provide solutions to their challenges, believing that by addressing citizens’ grievances promptly, we offer them a broader scope to remain productive and ultimately boost their income and the nation's revenue.



A citizen whose problems we help solve, even if they don't pay us directly, gains more time to manage other activities and thereby contribute to government revenues through taxes.



At the core, we do not discriminate against any citizen complaints. We receive all grievances, resolve those pertaining to our ministry, and forward and follow up resolution for issues related to other governmental departments, public institutions, and even private entities.



We are thankful for this training, which was not just theoretical but practical as well, led by experienced specialists in various units while maintaining the confidentiality of your clients’ information,” Kabigi stated, emphasizing the need for ongoing collaboration for the benefit of Tanzanians across all sectors.



On her part, Ms. Zaipuna thanked MoCLA for choosing NMB to enhance the capabilities of their center’s personnel, noting that the ministry has selected the right partner to learn about customer service, especially given NMB’s significant systematic and technological advancements to ensure high-quality service delivery.



NMB is a government bank, which is why we believe in mutual understanding as we undertake many initiatives together. You have come to the right place—back in 2020, we decided to implement a ‘transformative strategic plan’ for the bank, recognizing the necessity of investing in both human resources and their environments.

TCB YAZINDUA KAMPENI YA “TOBOA KIDIJITALI” KWA AJILI YA UJUMUISHI WA KIFEDHA NA MATUMIZI YA MIAMALA YA KIDIJITI


Benki ya Biashara Tanzania (TCB) imezindua rasmi kampeni ya kitaifa ijulikanayo kama “Toboa Kidijitali”, ambayo inalenga kuhamasisha wananchi kutumia mifumo ya kisasa ya miamala ya kifedha kwa njia ya kidijiti, sambamba na kuwazawadia wateja wake wanaoshiriki kikamilifu katika matumizi ya huduma hizo.



Uzinduzi huo umefanyika siku ya Ijumaa Aprili 25, 2025, Makao Makuu ya TCB yaliyopo eneo la Makumbusho, jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau mbalimbali wa benki, wafanyakazi, wateja, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.



Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa TCB, Adam Mihayo, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi na Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati, Bi. Lilian Mtali, amesema kuwa benki hiyo imeamua kuwekeza zaidi ya shilingi milioni 200 katika kampeni hii kama sehemu ya kurudisha kwa jamii, lakini pia kama njia ya kuendelea kukuza matumizi ya teknolojia ya kifedha nchini.



Hii ni namna ya kuwarudishia wateja wetu, jamii na wafanyabiashara wadogo wanaotuzunguka. Tumepanga kuwazawadia washindi mbalimbali watakaoibuka kidedea kupitia miamala wanayofanya kwa njia ya kidijiti kwa kipindi cha miezi minne,” amesema Mtali.



Ameongeza kuwa TCB imekuwa mstari wa mbele katika kuwekeza kwenye ubunifu wa mifumo ya huduma za kifedha ili kumwezesha Mtanzania kufanya miamala kwa haraka, kwa usalama na mahali popote, bila kulazimika kufika tawi la benki.



Kwa kutumia huduma kama Popote Mobile App, Popote Visa Card, na mfumo wa Lipa Popote, mteja anaweza kufanya miamala bila usumbufu. Tunasisitiza uhuru wa kujihudumia kibenki kwa kutumia teknolojia kwa sababu muda ni pesa,” amesema Mtali.



Kwa upande wake, Jesse Jackson, Afisa Mkuu wa Huduma za Kidijiti na Ubunifu wa TCB, amesema kuwa kupitia kampeni ya Toboa Kidijitali, benki hiyo inatarajia kutoa zawadi mbalimbali kwa washindi, ikiwemo gari aina ya Mazda, simu ya iPhone 16 Pro Max, bajaji, bodaboda kila mwezi kwa kipindi cha miezi minne.



Jackson amesema kuwa kampeni hii inalenga si tu kuongeza miamala ya kidijitali, bali pia kuchochea ujumuishi wa kifedha kwa makundi yote ya Watanzania, wakiwemo wale wa vijijini na maeneo ya pembezoni.

Thursday, 24 April 2025

BENKI YA EXIM YAKABIDHI MADARASA KWA SHULE MBILI KIGOMA

Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina (kulia), ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma na Bw. Stanley Kafu (kushoto), Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania wakifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa madarasa yaliyojengwa na benki hiyo katika shule mbili za wilaya ya Buhigwe, mkoani Kigoma.

Kigoma, 22 Aprili 2025: Katika juhudi za kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu nchini Tanzania, Benki ya Exim Tanzania imekabidhi rasmi madarasa kwa shule mbili za sekondari wilayani Buhigwe katika mkoa wa Kigoma. Shule hizo, Shule ya Sekondari Kaphunya na Shule ya Sekondari Nyakitundu, zimepokea madarasa hayo yaliyokamilika yenye viti na madawati, ikiwa ni sehemu ya juhudi endelevu za benki hiyo katika kusaidia sekta ya elimu na kuboresha matokeo ya kujifunza kote nchini. Pia benki hiyo imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo kwa shule hizo mbili kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya michezo nchini.



Akizungumza katika hafla hiyo, Stanley Kafu, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim, alisisitiza dhamira ya benki hiyo katika kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini.



"Sisi kama Benki ya Exim, tunaamini kuwa elimu ni msingi wa maendeleo katika jamii yoyote ikiwemo Tanzania. Kwa kuwekeza katika mazingira ya kujifunzia, hatujengi tu madarasa na kutoa madawati haya, bali tunaunda mustakabali wa vijana wetu na kuwawezesha jamii. Tunajivunia pia kuchangia maendeleo ya sekta ya michezo kwa vijana wetu kwa kutoa vifaa vya michezo maana ni sehemu ya kuimarisha afya zao ili waweze kusoma vizuri,” alisema Kafu.



Mbali na sekta ya elimu, benki ya Exim imekuwa ikishiriki kikamilifu katika miradi mbalimbali ya uwajibikaji kwa jamii kupitia mpango wake unaojulikana kama ‘Exim Cares’. Benki hiyo imechangia kuboresha huduma za afya kwa kutoa vifaa tiba kwa hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini, imewezesha ujumuishaji wa kifedha kupitia suluhisho za benki za kidijitali, na pia kushiriki katika jitihada za utunzaji wa mazingira.



Naye Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina, kwa niaba ya Mgeni Rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, aliipongeza Benki ya Exim kwa mchango wake mkubwa katika kusaidia juhudi za serikali za kuboresha upatikanaji wa elimu bora.



"Mchango huu wa madarasa, vitu na madawati yake kutoka Benki ya Exim ni uthibitisho wa nguvu ya ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi katika kuendeleza na kufikia malengo ya taifa. Madarasa haya yatatoa mazingira bora ya kujifunza kwa watoto wetu, kuwawezesha kufaulu kitaaluma na kujenga maisha yao ya baadaye. Tunatoa wito kwa wadau wengine kuungana nasi katika kuinua sekta ya elimu," alisema Mhe. Ngayalina.



Sekta ya elimu nchini inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uchache wa walimu, ukosefu wa maabara, na upungufu wa madarasa katika shule mbalimbali zikiwemo shule ya Sekondari Kaphunya na Shule ya Sekondari Nyakitundu. Mazingira haya yanaathiri ubora wa elimu na kupunguza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi na hivyo kuathiri kiwango cha elimu nchini.



Wednesday, 23 April 2025

STANBIC YAZINDUA eMKOPO – MKOPO WA KIDIGITALI KWA WATUMISHI WA SERIKALI

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya Stanbic, Emmanuel Mahodanga (katikati) akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya eMkopo. Wengine kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Mauzo wa benki hiyo, Priscus Kavishe na Meneja wa Tawi Makao Makuu Stanbic, Anorld Moshi.

Dar es Salaam, Aprili 2025 – Stanbic Bank Tanzania imezindua rasmi huduma ya eMkopo, mkopo wa kidigitali uliobuniwa mahsusi kwa ajili ya watumishi wa umma, kupitia ushirikiano rasmi na Mfumo wa Serikali wa Watumishi Portal (https://ess.utumishi.go.tz).

Huduma hii inawawezesha watumishi wa umma nchini kuomba na kupata mkopo wa hadi TZS milioni 200, kwa kipindi cha kurejesha cha hadi miezi 108 (sawa na miaka 9), kwa njia rahisi na ya kidigitali bila kulazimika kutembelea matawi ya benki.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Emmanuel Mahondanga, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Stanbic Bank alisema:

"Uzinduzi wa eMkopo unaashiria hatua kubwa katika utoaji wa huduma za kifedha zinazozingatia mahitaji ya sasa. Kwa kuunganishwa na mfumo wa serikali wa Watumishi Portal, tunarahisisha mchakato mzima wa upatikanaji wa mikopo kwa watumishi wa umma – kwa njia ya haraka, salama na rafiki kwa mtumiaji. Hii ni sehemu ya dhamira yetu ya kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kuchochea ustawi wa wateja wetu."

Tuesday, 22 April 2025

STANBIC YAHITIMISHA KAMPENI YA TAP KIBINGWA KWA SHANGWE – WASHINDI WAKUU KUSUBIRIWA

Meneja wa Kitengo cha Kadi kutoka Benki ya Stanbic, Irene Mutabihirwa (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza washindi wa droo ya 3 ya kampeni ya Tap Kibingwa kwa wateja wa benki hiyo wanaotumia kadi zao za Stanbic Visa Debit kufanya malipo, ambapo washindi watano wamejishindia kiasi cha shilingi 500,000 kila mmoja. Wengine pichani ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Irene Kahwili (kushoto) na Joan Muro (kulia) kutoka Kitengo cha Kadi cha Benki ya Stabic.
  • TZS milioni 7.5 zimetolewa kama zawadi kwa wateja 15 waliotumia Visa Debit Card zao kwa miezi mitatu
  • Washindi wengine watano wajishindia TZS 500,000 kila mmoja katika droo ya mwisho ya mwezi
  • Mshindi wa gari jipya aina ya Suzuki Fronx kutangazwa siku chache zijazo
Dar es Salaam, 19 Aprili 2025: Benki ya Stanbic Tanzania, kwa kushirikiana na Visa, imehitimisha rasmi kampeni yake ya kuvutia ya Tap Kibingwa, ambayo imekuwa ikiwazawadia wateja waliokuwa wanafanya matumizi ya malipo ya kidijitali kupitia matumizi ya kila siku ya Visa Debit Card zao.

Katika droo ya mwisho ya mwezi iliyofanyika jijini Dar es Salaam, wateja watano—Coles Josette, Irene Charles Isaka, Chisora Kennedy, Abubakar Said Salim Bakhresa na Pietro Stella—wamejishindia TZS 500,000 kila mmoja. Washindi hao wanaungana na washindi wengine 10 kutoka droo za mwezi Februari na Machi, na kufanya jumla ya washindi kufikia 15 na jumla ya zawadi kufikia TZS milioni 7.5.

Wakati shauku ikiendelea kuongezeka, benki imethibitisha kuwa mshindi wa droo kuu ya kampeni hii—atakayeondoka na gari jipya aina ya Suzuki Fronx—atatangazwa rasmi katika siku chache zijazo. Hii itakuwa kilele cha kampeni ya Tap Kibingwa, ambayo imelenga kuwazawadia wateja waliotumia kadi zao kwaviwango vya juu na kwa uaminifu.

Tap Kibingwa imekuwa njia ya kujenga imani katika huduma za kibenki za kidijitali,” alisema Irene Mutabihirwa, Meneja wa Kadi za Malipo – Benki ya Stanbic Tanzania. “Kupitia kampenihii, tumewazawadia wateja wetu kwa uaminifu wao na pia tumesaidia kuhamasisha tabia ya kufanya miamala salama, yaharaka na rahisi. Tumefunga hatua ya droo za kila mwezi nasasa tunajiandaa kumtangaza mshindi wetu mkuu.”

Saturday, 19 April 2025

CRDB, COSTECH WASAINI MKATABA WA SHILINGI BILIONI 2.3 KUWEZESHA BIASHARA ZA VIJANA



Dar es Salaam, 17 Aprili 2025: Katika kuimarisha ubunifu na ujasiriamali miongoni mwa vijana nchini, Benki ya CRDB kupitia taasisi yake ya CRDB Bank Foundation na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) wamesaini mkataba wa shilingi bilioni 2.3 kwa ajili ya kuziwezesha biashara changa za vijana.

Makubaliano hayo yaliyoshuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda, ni sehemu ya Programu ya IMBEJU kupitia dirisha lake la IMBEJU BUNI yakilenga kuwasaidia vijana wabunifu nchini kupata elimu ya fedha na mitaji nafuu ya kukuza biashara zao.



Akizungumza katika hafla ya utiaji saini, Waziri Mkenda amesema: “Hii ni hatua ya kupongezwa inayochochea ukuaji wa uchumi wa ubunifu. Ushirikiano huu ni jibu la changamoto ya kukosekana kwa ufadhili kwa vijana wabunifu na ni kielelezo cha juhudi za serikali kujenga uchumi shindani wa viwanda wenye ubunifu.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa ameeleza kuwa ushirikiano huu una akisi dhamira ya Benki ya CRDB kushiriki kujenga uchumi jumuishi.



“Tangu kuanzishwa kwa Programu ya IMBEJU Machi 2023, tulilenga kuwafikia vijana na wanawake waliopo pembezoni na kuwapa fursa za kifedha. Kupitia mkataba huu, tunatarajia kuwafikia vijana zaidi ya 1,000 na kuwapa mitaji wezeshi, mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha ili waweze kuendesha biashara endelevu kwa mfumo rasmi hivyo kuwa rahisi kwao kukua zaidi,” amesema Tully.

Katika kipindi hiki cha ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na COSTECH, zaidi ya vijana 700 wabunifu wamefikiwa na kuwezeshwa kupitia dirisha la IMBEJU Buni ambalo ni mahsusi kwa ajili ya wabunifu wenye biashara changa kwa kuwapa mafunzo na mitaji wezeshi yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 5.



Katika utekelezaji wa mkataba uliosainiwa, kutakuwa na kamati ya pamoja ya usimamizi (Steering Committee) kati ya Benki ya CRDB, CRDB Bank Foundation na Tume ya Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya kufanya tathmini, ufuatiliaji, na usimamizi madhubuti wa utekelezaji ili kuhakikisha kunakuwa na uwazi wa kutosha kulifikia lengo lililowekwa.

Friday, 18 April 2025

DSE YASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA JUMUIYA FINTECH TANZANIA


April 17, 2025: Soko la Hisa Dar es salaam DSE limesiani Makubaliano (MOU) na jumiya ya Fintech society Tanzania yenye lengo la kukuza matumizi ya suluhisho za kiteknolojia katika ushirikiano wa masoko ya mitaji na kuwawezesha Watanzania kupata elimu ya Fedha.



Akizungumza na waandishi wa Habari Aprili 17 wakati wa kusaini Makubaliano hayo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa Bw. Peter Nalitolela Amesema ushirikiano huo utaangiza katika maeneo mbalimbali ikwemo kusaidia mabadiliko ya kidigitali katika huduma za kifedha na kujenga uwezo kwa vijana na wataalam sekta ya fedha.



"Teknolojia ya Fedha ni teknolojia ambayo imekuwa Kwa Kasi sana Kwa kujitika Kwa Kupitia mitandao ya simu kuwawezesha wadau kupata huduma za kifedha kama vile kufanya malipo kuwekeza kutuma pesa sehemu mbalimbali na kuhifadhi kuunga mkono juhudi za kiserikali za uelimishaji wa kifedha teknohama ni sehemu muhimu sana tunapunguza usumbufu" amesema Nalitolela

Ameongeza kuwa Wao kama soko la Hisa wamekuwa wanafanya jitihada hizo binafsi kupitia mtandao wao wa uwekezaji kwa kushirikiana na wadau wa fedha na kukuza juhudi za kuwafikia wananchi katika kuwekeza soko la Hisa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Fintech society Tanzania, Dr. Deniss Mwighusa amesema wamefanya tafiti mbalimbali Kwenye maswala ya teknolojia ya Fedha ni kitu ambacho kwa kiasi kikubwa sana kinakua.

Thursday, 17 April 2025

EXCITING CAREER OPPORTUNITIES AT NMB BANK PLC

We are a leading bank, committed to your growth and welfare. Join our team of best talents in the market, together we will continue to impact and transform lives through meaningful work, innovative products and solutions while driving the sustainability agenda. 

We are renowned for investing, nurturing and transforming careers. Our commitment to diversity, equity and inclusion has led us to become the first financial institution in Africa to attain the most coveted EDGE Certification (EDGE Assess). We are more than a bank.

The following vacancies are currently available;
  • Digital Sales Manager - Head Office (Closing date; 29 April 2025)
  • Officer; Consumer Special Scheme - Head Office (Closing date; 17 April 2025)
  • Operation Transformation System Developer - Head Office (Closing date; 29 April 2025)
  • Relationship Manager; Affluent - Dar es Salaam Zone, Mlimani City (Closing date; 29 April 2025)
  • Relationship Manager; SME - Nortern Zone (Closing date; 28 April 2025)
  • Senior Credit Administration Officer - Head Office (Closing date; 30 April 2025)
  • Senior Specialist; Corporate Support Quality Assurance - Head Office (Closing date; 24 April 2025)

PwC SHUTS OPERATIONS IN NINE AFRICAN COUNTRIES


April 16, 2025 (Reuters) - PwC shut operations in nine Sub-Saharan African countries last month following a strategic review, the Big Four accounting firm said, in response to a media report that said the company exited over a dozen countries to avoid scandals.

PwC, which operates as a global network of locally owned partnerships, has shut operations in the Ivory Coast, Gabon, Cameroon, Madagascar, Senegal, the Democratic Republic of Congo (DRC), Congo Republic, Republic of Guinea and Equatorial Guinea, it said in a statement published on its website on March 31, 2025.

The accounting firm directed Reuters to the statement in response to queries on a Financial Times article published earlier in the day that said PwC had exited multiple countries that were deemed too small, risky or unprofitable.

The decision came due to mounting differences with local partners, who said they lost over a third of their business in recent years after pressure from PwC's global executives to drop risky clients, the FT said, citing people familiar with the matter.

The PwC statement did not give a reason for the move.

BANK OF TANZANIA MONTHLY ECONOMIC REVIEW, MARCH 2025

Wednesday, 16 April 2025

CAPE TOWN INTERNATIONAL AIRPORT NAMED AFRICA'S BEST AIRPORT IN 2025

Cape Town International Airport has been named the Best Airport in Africa at the 2025 Skytrax World Airport Awards, reaffirming its status as the continent’s leading aviation hub.

  • Cape Town International Airport named Best Airport in Africa at 2025 Skytrax World Airport Awards.
  • The airport also received awards for Best Airport Staff Service in Africa and Cleanest Airport in Africa.
  • Singapore Changi Airport named Best Airport in the World.
Cape Town International Airport has been named the best airport in Africa at the 2025 Skytrax World Airport Awards, reaffirming its status as the continent’s leading aviation hub.

In addition to the top regional title, the airport also received awards for Best Airport Staff Service in Africa and Cleanest Airport in Africa, according to results released by Skytrax on Tuesday.

The Skytrax Awards are based on a global airport customer satisfaction survey conducted between August 2024 and February 2025.


The survey gathered responses from air travellers of over 100 nationalities and assessed more than 575 airports worldwide on metrics such as check-in, arrivals, shopping, security, and boarding experiences.

On a global scale, Singapore Changi Airport was named Best Airport in the World and also won for Best Dining, Best Washrooms, and Best Airport in Asia.

AfDB AND BANK OF AFRICA TANZANIA SIGN $7.5 MILLION FACILITY TO BOOST TRADE FINANCE


The African Development Bank and the Bank of Africa Tanzania (BOAT) have signed a $7.5 million trade finance transaction guarantee facility to boost trade finance activities of the Bank of Africa in Tanzania.

Under this facility, the African Development Bank will provide a guarantee of up to 100% to confirming banks against non-payment risks arising from letters of credit and similar trade finance instruments issued by the Bank of Africa Tanzania. The facility will support small and medium-sized enterprises (SMEs) and local corporates engaged in the import sector. The facility aligns with efforts to bolster intra-Africa trade, contributing directly to the objectives of the African Continental Free Trade Area (AfCFTA).

Speaking at the signing event in Dar es Salaam, the Bank’s Country Manager for Tanzania, Patricia Laverley, stressed the importance of the facility in addressing Tanzania’s trade finance needs, saying that given the country’s import requirements, it will aid priority sectors such as trade, agriculture, manufacturing, and energy. “This facility will support trade by enabling BOAT to play a more strategic role in the regional and international market.”

Representing BOAT’s management, Deputy Managing Director Hamza Cherkaoui lauded the strong partnership with the African Development Bank, emphasizing its role in expanding trade finance capabilities across the continent. “This partnership strengthens our ability to support businesses across various sectors by providing seamless trade finance solutions, expanding our confirmation network, and enabling access to top-tier confirming banks,” he said.

VODACOM YAZINDUA TWENDE BUTIAMA 2025 KUBORESHA ELIMU, AFYA NA MAZINGIRA

Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi. Zuweina Farah, akizungumza wakati wa uzinduzi wa msafara wa Vodacom Twende Butiama kwa mwaka 2025. Kushoto ni Mwanzilishi wa Twende Butiama, Bw. Gabriel Landa. Msafara huo utakaofanyika mwezi Julai kutoka Dar es Salaam mpaka Butiama unalenga kuenzi fikra za Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius K. Nyerere ambazo ni kuboresha elimu, afya na mazingira na unadhaminiwa na kampuni hiyo. Mkutano huo umefanyika jijini Arusha tarehe 15 Aprili 2025.
  • Yatoa msaada wa vifaa maalum kwa watu wenye ulemavu
Arusha – 15 Aprili 2025: Kwa miaka ishirini na tano, Vodacom Tanzania PLC imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuchochea maendeleo endelevu katika jamii. Msafara wa Twende Butiama wa mwaka 2025 kwa mara nyingine unadhaminiwa na Vodacom na litahusisha msafara wa umbali wa karibu kilomita 1,500 likipita katika mikoa 11 kuanzia tarehe 3 hadi 13 mwezi Julai, na kumalizika kwa kishindo katika kijiji cha Butiama mkoani Mara – mahali alipozaliwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.


Akizungumzia kuhusu msafara huo, Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania na Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Zuweina Farah, alisisitiza dhamira ya kampuni hiyo kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma katika harakati za maendeleo nchini.


Tunaamini katika kuunganisha Watanzania kwa mustakabali bora, na Twende Butiama ni moja ya njia tunayoitumia kutimiza dira hiyo. Iwe ni ujumuishaji wa kidijitali, upatikanaji wa elimu, huduma bure za afya au utunzaji wa mazingira, kampeni hii inaonesha nguvu ya ushirikiano na dhamira ya kweli,” alisema Zuweina.


Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, Twende Butiama imeboresha maisha ya maelfu ya Watanzania. Zaidi ya watu 150,000 wamenufaika na huduma za afya bure, zaidi ya miti 100,000 imepandwa katika shule mbalimbali nchini na kuhamasisha uelewa wa mazingira na kuboresha mazingira ya kujifunzia, zaidi ya madawati 1,900 yamegawiwa kwa shule za msingi 34 ili kupunguza idadi ya wanafunzi kukaa chini, na baiskeli 50 zimesambazwa kwa wanafunzi wa vijijini ili kuwapunguzia muda wa kufika shuleni na kuongeza mahudhurio.


Msafara wa mwaka huu unaendeleza mafanikio hayo kwa kuzingatia zaidi upatikanaji wa elimu jumuishi, uhifadhi wa mazingira, na utoaji wa huduma bora za afya. Aidha, kampeni hiyo itaendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum kwa kugawa vifaa vya kusaidia kama vile viti, kwa lengo la kujenga jamii jumuishi.


Msafara huo utaanza rasmi katika viwanja vya Kijitonyama jijini Dar es Salaam na kwa mara ya kwanza zitapitia mikoa ya Pwani, Tanga, Arusha, Manyara, Singida, Tabora, Shinyanga, Simiyu hadi Mara. Katika maeneo haya, waendesha baiskeli, wadau na wanajamii watahusika moja kwa moja katika shughuli za upandaji miti, msaada wa kielimu, kambi za afya na usafi wa mazingira.


Mwanzilishi wa msafara wa Twende Butiama, Bw. Gabriel Landa, alisema: “Kilichoanza kama harakati ndogo za baiskeli sasa kimekuwa harakati ya kitaifa ya kuleta mabadiliko. Kila mwaka tunapanda miti, tunatoa elimu, na kugusa maisha ya maelfu ya Watanzania. Safari ya mwaka huu kutoka Dar es Salaam hadi Butiama ni safari ya matumaini kwa taifa letu.”