Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Friday, 18 April 2025

DSE YASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA JUMUIYA FINTECH TANZANIA


April 17, 2025: Soko la Hisa Dar es salaam DSE limesiani Makubaliano (MOU) na jumiya ya Fintech society Tanzania yenye lengo la kukuza matumizi ya suluhisho za kiteknolojia katika ushirikiano wa masoko ya mitaji na kuwawezesha Watanzania kupata elimu ya Fedha.



Akizungumza na waandishi wa Habari Aprili 17 wakati wa kusaini Makubaliano hayo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa Bw. Peter Nalitolela Amesema ushirikiano huo utaangiza katika maeneo mbalimbali ikwemo kusaidia mabadiliko ya kidigitali katika huduma za kifedha na kujenga uwezo kwa vijana na wataalam sekta ya fedha.



"Teknolojia ya Fedha ni teknolojia ambayo imekuwa Kwa Kasi sana Kwa kujitika Kwa Kupitia mitandao ya simu kuwawezesha wadau kupata huduma za kifedha kama vile kufanya malipo kuwekeza kutuma pesa sehemu mbalimbali na kuhifadhi kuunga mkono juhudi za kiserikali za uelimishaji wa kifedha teknohama ni sehemu muhimu sana tunapunguza usumbufu" amesema Nalitolela

Ameongeza kuwa Wao kama soko la Hisa wamekuwa wanafanya jitihada hizo binafsi kupitia mtandao wao wa uwekezaji kwa kushirikiana na wadau wa fedha na kukuza juhudi za kuwafikia wananchi katika kuwekeza soko la Hisa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Fintech society Tanzania, Dr. Deniss Mwighusa amesema wamefanya tafiti mbalimbali Kwenye maswala ya teknolojia ya Fedha ni kitu ambacho kwa kiasi kikubwa sana kinakua.

"Tunajaribu kuangalia wapi na tunahitaji kufanya nini na tumefanya utafiti Katika maswala ya teknolojia ya Fedha basi Ili kuweza kufanikisha tunafanya vizuri huku tukiangazia Maswala ya Mafunzo na Moja ya maeneo ya Siri sana ambayo tunaelekea kufanya Katika mambo ambayo tutafanya na DSE" amesema Mwighusa.

No comments:

Post a Comment