- Stanbic Tanzania imethibitisha tena dhamira yake ya kusaidia kukuza biashara, kufadhili miundombinu, na ushirikiano wa kikanda wakati wa huu nyeti wa usafirishaji shehena na uchukuzi kwa ujumla
- Benki hii ya tatu kwa ukubwa wa faida inayo masuluhisho ya kifedha ya kuboresha ufanisi wa uchukuzi, kupanua wigo wa masoko, na kuhamasisha fursa za kibiashara nje ya nchi
- Kushirikiana na wafanybiashara na Serikali kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na uchukuzi barani Afrika
![]() |
Stephen Mpuya, Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa kwa Biashara, Benki ya Stanbic akizungumza kwenye Mkutano wa Wadau wa Usafirishaji Afrika Mashariki uliofanyika Alhamisi wiki iliyopita Jijini Dar es salaam. |
Uwekezaji na ushirikiano wa wadau mbalimbali, hasa katika kuboresha miundombinu na kufadhili upatikanaji wa mitaji, umewezesha kuunganisha wafanyabiashara kutoka mataifa tofauti wa eneo hili na kuimarisha nafasi yake kama lango kuu la biashara katika nchi za Afrika Mashariki, Kati, na Kusini mwa Afrika.
Benki ya Stanbic Tanzania, taasisi inayoongoza katika ufadhili wa biashara na uwekezaji katika miundombinu, imethibitisha utayari wake wa kuwa sehemu ya maono haya ya Tanzania wakati wa Mkutano wa East Africa Cargo Connect Summit (EACCS) 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki jana.
Kupitia kaulimbiu ya “Tanzania: Kinara wa Mustakabali wa Kuunganisha Mitandao ya Biashara Mashariki na Kusini mwa Afrika,” mkutano wa EACCS 2025 ulisisitiza umuhimu wa kuboresha miundombinu, kuwezesha upatikanaji wa ufadhili unaofaa, na kutekeleza sera za biashara zinazowezesha miamala ya biashara kufanyika bila vikwazo kati ya mataifa mbalimbali.
Benki ya Stanbic imekuwa kiongozi katika kusaidia wafanyabiashara kushindana kwa ufanisi katika masoko ya kikanda na kimataifa. Kupitia ushirikiano na serikali na sekta binafsi, tunatoa masuluhisho maalum ya kifedha yanayolenga kukabiliana na mahitaji yanayobadilika ya sekta ya uchukuzi na usafirishaji wa shehena.
Moja ya mifano mizuri ya juhudi zetu ni programu yetu ya Vehicle Asset Financing (Ufadhili wa Mali za Magari), ambayo inawasaidia wateja kupata vifaa wanavyohitaji kwa gharama ya awali ndogo na malipo rahisi ya kila mwezi yanayolingana na mtiririko wao wa kifedha. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, imetoa ufadhili wa aina hii wenye thamani ya zaidi ya TZS bilioni 220.
“Kwetu sisi Benki ya Stanbic, Tanzania ni nyumbani, na tunajivunia kushiriki kikamilifu katika ukuaji na maendeleo yake. Hii si kauli tu – ni ahadi tunayothibitisha kwa vitendo. Katika kipindi cha miaka miwili pekee, tumetoa ufadhili wa zaidi ya dola bilioni 1 za Marekani, tukichangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo yake ya kiuchumi,” alisema Bw. Stephen Mpuya, Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa kwa Biashara wa Benki ya Stanbic Tanzania.
“Huu ni mwaka wa kipekee kwetu, kwani tunasherehekea miaka 30 ya uwepo wetu nchini. Imekuwa ni safari iliyojaa ustahimilivu, mafanikio, na mchango mkubwa katika kusaidia biashara kuimarika, huku tukichangia kwa kiwango kikubwa katika ujenzi wa miundombinu bora, na hivyo kuchochea ukuaji na maendeleo ya taifa letu kwa ujumla,” aliongeza huku akishauri kuwa:
“Ili Tanzania itimize uwezo wake kama kitovu cha biashara na uchukuzi, tunapaswa kuharakisha uwekezaji katika miundombinu, kurahisisha michakato ya biashara, na kuwapa wafanyabiashara uwezo wa kifedha unaostahili.”
Kauli hiyo iliungwa mkono na washiriki wa mkutano wa pili wa EACCS, akiwemo muwakilishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bi Fatima Rajabu, aliyekuwa mgeni rasmi wa mkutano wa siku moja uliofanyika Mlimani City tarehe 27/03/2025 kwa niaba ya Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa TPA.
“Mkutano huu unafanyika katika kipindi nyeti kwa ukanda wetu, unaoshuhudia ukuaji mkubwa, fursa nyingi, na changamoto katika mnyororo wa thamani wa usambazaji duniani. Kadri Afrika Mashariki inavyoendelea kuwa mshiriki muhimu katika biashara ya kimataifa, ni muhimu kuitumia nafasi yetu ya kijiografia, rasilimali, na miundombinu inayokua haraka ili kuhamasisha ushirikiano wa kikanda na kuimarisha mitandao ya biashara ya kimataifa kwa ajili ya maendeleo endelevu,” alibainisha Bi Rajabu.
Mjumbe kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw Daudi Stephano Riganda, alisema: “Usafirishaji ni muhimu katika ukuaji wa kiuchumi, kutengeneza ajira na kuunganisha watu na huduma muhimu. Miundombinu imara ya usafiri ni kipengele muhimu katika kuvutia Uwekezaji wa Moja kwa Moja kutoka Nje (FDI) kwa sababu inarahisisha biashara, kupunguza gharama, na kuboresha ushindani wa kiuchumi.”
Mwenyekiti wa Baraza la Wasafirishaji Shehena Tanzania (TSC), Bw alisisitiza umuhimu wa miundombinu bora na ushiriki wa tasnia ya fedha katika maendeleo ya sekta ya usafirishaji. Mbali na kudhamini mkutano huu, mchango wa Benki ya Stanbic ni muhimu kwani maendeleo ya sekta hii yanahitaji ufadhili na ushiriki mkubwa wa taasisi za fedha.
No comments:
Post a Comment