Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Sunday, 30 March 2025

MAKAMU WA RAIS DKT. PHILIP MPANGO AZINDUA MATAWI YA NMB



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, ametoa wito kwa wananchi kuepuka wakopeshaji binafsi maarufu kama kausha damu ambao hutoza riba kubwa na kunyanyasa wateja kupitia ukamataji wa mali za wadaiwa. Amebainisha kuwa kufunguliwa kwa matawi mapya ya NMB karibu na wananchi kutatoa fursa ya upatikanaji wa huduma za kifedha kwa ufanisi, usalama, na unafuu.


Dkt. Mpango aliyasema hayo wakati akizindua rasmi Matawi ya Benki ya NMB Chanika na Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Alieleza kuwa uzinduzi wa matawi hayo utaongeza mchango wa NMB katika maendeleo ya taifa kwa kulipa kodi, kutoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja, na kusaidia usalama wa miamala kama malipo ya bili za maji, umeme, ada za shule, na mauzo ya bidhaa.


Aidha, Makamu wa Rais alitoa wito kwa NMB kuendelea kuchangia kwenye maendeleo ya kijamii hususan katika sekta za afya na elimu. Alisema kuwa uwajibikaji kwa jamii ndio msingi wa kudumu wa mahusiano bora kati ya benki na wananchi.


Kupitia kuongeza idadi ya mawakala wenu, mtakuwa mnasaidia kuzalisha ajira kwa vijana ambao ni wadau muhimu wa huduma hizi. Ninaipongeza NMB kwa juhudi hizi na nawasihi msiishie hapa, bali muendelee kuwekeza zaidi katika elimu ya fedha kwa wananchi, hasa wale wa vijijini,” alisema Dkt. Mpango.


Makamu wa Rais alisisitiza umuhimu wa kubuni mikakati bora ya kuongeza uelewa wa masuala ya fedha miongoni mwa wananchi. Aliitaka NMB kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania na Umoja wa Mabenki kubuni programu za kuongeza elimu ya kifedha, huku akitoa rai ya kupunguza gharama za huduma za kidijitali ili ziweze kufikiwa na watu wengi zaidi.


Aliongeza kuwa Sekta ya Benki na Fedha imeendelea kukua na kuonesha mafanikio makubwa, ambapo mchango wake kwenye ukuaji wa Pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.3 mwaka 2019 hadi asilimia 8.6 mwaka 2023. Dkt. Mpango alihimiza NMB kujizatiti kwa mikakati madhubuti ya kuhimili mitikisiko ya kiuchumi, magonjwa, na changamoto nyingine za kimataifa.


Saturday, 29 March 2025

STANBIC YAENDESHA DROO YA PILI YA TAP KIBINGWA, YAWAZAWADIA WATEJA

Meneja wa Kitengo cha Kadi kutoka Benki ya Stanbic, Irene Mutabihirwa (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza washindi wa droo ya pili ya kampeni ya "Tap Kibingwa" inayohamasisha wateja kutumia kadi za Visa Debit. Tukio hilo lilifanyika jijini Dar es salaam na jumla ya washindi 5 walipatikana kwa kujishindia kiasi cha Tsh 500,000 kila mmoja . Wengine katika picha ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Irene Kahwili (kushoto) na Joan Muro, kutoka kitengo cha kadi Benki ya Stanbic.
  • Ambapo washindi watano wamejishindia TZS 500,000 kilammoja katika droo ya Tap Kibingwa, ikiendelea kusherehekea hatua ya Tanzania kuelekea uchumi usiotegemea pesa taslimu.
  • Benki ya Stanbic imeendelea kuwazawadia wateja wake ambao wanatumia huduma za kibenki kupitia Kadi za Visa Debit, huku droo moja ya mwisho ya mwezi ikitarajiwa kufanyika mapema mwishoni mwa mwezi Machi, ikiwa nidroo ya mwisho ya kampeni hiyo.
  • Droo kubwa ya mwishoni mwa mwezi Machi itamshuhudia mshindi mmoja akiibuka na gari jipya aina ya Suzuki Fronx 2024, zero mileage, ikidhihirisha dhamira ya Stanbic yakukuza huduma ya benki kidijitali.
Dar es Salaam, Machi 2025 – Benki ya Stanbic imefanikiwa kuendesha droo ya pili ya mwezi ya kampeni yake ya Tap Kibingwa, ambapo wateja watano wamejishindia kiasicha TZS 500,000 kila mmoja. Kampeni hii inalenga kuchochea matumizi ya Kadi za Visa Debit kwa ajili ya miamala ya kidijitali, ikiendelea kuhamasisha urahisi na usalama wa malipo yasiyo ya pesa taslimu kote nchini Tanzania.

Washindi wa droo ya Machi ni:

Richard Muyambo
Alice Frank Mutagonda
Saddam Ally
Nabbila Abbasali Hirji
Siddharth Misra

Meneja wa Kutoa Kadi wa Benki ya Stanbic, Irene Mutabihirwa, amesisitiza dhamira ya benki hiyo ya kuendeleza malipo ya kidijitali nchini Tanzania.

"Tap Kibingwa ni sehemu ya mkakati wetu mpana wa kuimarisha ubunifu wa kifedha na ujumuishi wa kifedha. Miamala ya kidijitali huleta usalama na ufanisi, na tunafurahia kuendelea kuwazawadia wateja wetu kwa kufanya maamuzibora ya kifedha," alisema Mutabihirwa.

Tap Kibingwa ni kampeni maalum inayoendeshwa na Benki ya Stanbic inayohamasisha wateja kutumia Kadi za Visa Debit kwa malipo ya kila siku badala ya pesa taslimu. Wateja wanaofanya miamala ya angalau TZS milioni 5 kwa mwezi wanapata nafasi ya kushiriki kwenye droo za kila mwezi. Kampeni hii inaendelea hadi mwisho wa Machi 2025, ambapo droo kubwa itamshuhudia mshindi mmoja akiibuka na gari jipya aina ya Suzuki Fronx 2024, zero mileage.

NAIBU MUFTI: KUMWALIKA TAJIRI SI KAMA HUJAFUTURISHA, APONGEZA BENKI YA TCB KWA KUGUSA WOTE


Naibu Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Hassan Chizenga ameipongeza Benki ya Biashara Tanzania(TCB) kwa kufuturisha makundi mbalimbali ikiwa ni moja ya ibada muhimu katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, huku akisema hata tajiri anastahili kualikwa.



Sheikh Chizenga aliyemwakilisha Mufti Mkuu wa Tanzania, ameyasema hayo wakati wa hafla ya futari maalum iliyoandaliwa na benki hiyo Machi 28, 2025 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ambapo ilijumuisha watu mbalimbali ikiwamo viongozi wa dini, watoto yatima kutoka vituo tofauti, wateja wao, wafanyakazi wa TCB, na Jumuiya ya Watu Wenye Ulemavu wa Ngozi.



Naibu Mufti huyo amesema kuwa TCB imefanya jema kukaa na wateja wake na watu wengine kufuturu pamoja na kukiri kuwa hafla hiyo imekuwa tofauti na sehemu nyingine alizowahi kualikwa katika kipindi hiki.



Mwaliko hata kama umewahi kujadiliwa katika mitandao, kumwalika tajiri mwenzako si kama hujafuturisha, utakuwa umefuturisha si binadamu? Lakini pale utakapomwalika tajiri halafu ukamwalika na mtu ambaye huna nasaba naye hata katika mizunguko yako ya kila siku. na huna namna ya kukutana naye, ukamwalika yatima, ukamwalika mtu wa chini. Nyinyi mmepatia sana na mmeenda mahali ambapo Mungu anapopataka”, ameeleza Naibu Mufti.



Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TCB, Adam Mihayo amesema dhamira ya benki hiyo ni kushirikiana na Serikali katika kujenga uchumi imara.



Amesema kwa kutambua unyeti wa baadhi ya sekta wamekuwa wakizigusa moja kwa moja ili kupunguza mzigo kwa serikali lakini pia ni sehemu ya kurudisha kwa jamii.



TCB tunaamini kuwa benki sio tu taasisi ya fedha bali ni mshirika wa maendeleo ya jamii, tumekuwa mstari wa mbele katika kusaidia miradi yenye matokeo chanya kwa jamiia tukigusa sekta mbalimbali ikiwamo afya, elimu ,pia kusaidia taasisi za kidini katika miradi mbalimbali.



Tumeendelea kutoa misaada kwa kuimarisha miundombinu katika elimu ikiweo kusaidia madawati katika baadhi ya shule lakini pia tumetembelea katika hospitali na kutoa misaada bila kusahau makundi yenye uhitaji.” amesema Mihayo.



DTB FOSTERS UNITY AND LOYALTY WITH MEMORABLE IFTAR AT TANGA BEACH RESORT

A memorable moment captured at Diamond Trust Bank’s Iftar event, bank officials in Tanga coming together to celebrate the spirit of community and strengthen relationships.

On the evening of 27th March 2025, Diamond Trust Bank Tanzania PLC (DTBT) held a memorable Iftar event at Tanga Beach Resort in Tanga Region where over 200 valued customers gathered for a special Iftar hosted by the bank. This carefully planned event provided a unique opportunity for customers to connect, share experiences and foster deeper relationships with both each other and the bank’s leadership team.

Sheikh Juma Bakari Ilungulu addresses attendees at Diamond Trust Bank’s Iftar event in Tanga, sharing words of reflection and unity after a day of fasting, fostering a sense of community and connection.

The Iftar was honoured by the presence of the Secretary of the Union of Sheikhs in Tanga - Sheikh Juma Bakari Ilungulu, and graced by the Chief Guest, Ambassador Dr. Batilda Buriani, the Regional Commissioner of Tanga. This event, marking the breaking of the fast during the holy month of Ramadan, was not merely a meal but a symbolic representation of Diamond Trust Bank’s unwavering commitment to its customers and the broader community.

Sylvester Bahati, Diamond Trust Bank’s Head of Corporate Communications & Citizenship addresses invitees at the Iftar event, expressing gratitude and reinforcing the bank's commitment to building strong relationships with its valued customers.

During the event, customers had the chance to interact with one another and with different bank officials in a relaxed, friendly setting. This allowed for the exchange of ideas, feedback, and insights, all of which are invaluable to the bank as it continues to evolve to meet the needs of its clients.

Customers gathered at Diamond Trust Bank’s Iftar event in Tanga, for a well-deserved meal after a long day of fast.

For DTB this Iftar was a testament to the power of face-to-face engagement and the importance of listening to and supporting the customers who continue to drive the bank’s success.

With the support of these valued customers, Diamond Trust Bank looks forward to continuing its journey of growth, innovation, and community engagement, both in Tanga and beyond.

Friday, 28 March 2025

VODACOM APPOINTS DAVID TARIMO AS INDEPENDENT NON-EXECUTIVE DIRECTOR AND BOARD CHAIRMAN

AKIBA COMMERCIAL BANK BRINGS JOY TO CHAKUWAMA ORPHANAGE WITH HEARTFELT DONATION



Dar es Salaam, 28 March 2025: As part of its commitment to giving back to the community, Akiba Commercial Bank has extended support to Chakuwama Orphanage, bringing smiles to the children through a donation aimed at improving their well-being.

The donation, which includes essential supplies, reflects the bank’s dedication to making a meaningful impact in the lives of those in need and fostering hope for a brighter future. Speaking during the handover, Ms. Dora Saria, Head of Marketing and Communication at Akiba Commercial Bank, emphasized the institution’s belief in supporting communities and creating lasting positive change.


"At Akiba Commercial Bank, we believe in the power of collective support to transform lives. This donation is a step towards ensuring the well-being of these children while fostering hope for those in need and a brighter future ahead," said Ms. Saria.

Mr. Hassan Tabu, representing Chakuwama Orphanage, expressed heartfelt gratitude for the bank’s generosity, acknowledging that such support plays a crucial role in uplifting the children’s lives. “We sincerely appreciate Akiba Commercial Bank for standing with us. This donation will go a long way in ensuring the children’s needs are met while giving them a reason to smile,” he said.

Through this initiative, Akiba Commercial Bank reaffirms its commitment to corporate social responsibility, striving to make a positive and lasting impact in the communities it serves.

NBC YAITAMBULISHA “NBC SHAMBANI’’ KWA WAKULIMA SONGWE, MBEYA

Katibu Tawala Wilaya ya Mbozi Bw Mbwana Kambangwa, (alieshika mkasi) akijipongeza sambamba na wadau wengine mara baada ya kuzindua kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima mazao mbalimbali ikiwemo kahawa na ufuta katika mikoa ya Songwe na Mbeya wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika kata ya Mlowo, wilayani Mbozi mkoani Songwe. Wengine ni pamoja na Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (katikati) na wadau mbalimbali wa kilimo kutoka mikoa ya Songwe na Mbeya.
Katibu Tawala Wilaya ya Mbozi Bw Mbwana Kambangwa, (katikati) sambamba na wadau wengine wakionesha zawadi za pikipiki na kompyuta mpakato ‘laptops’ zitakazotolewa kwa washindi wa kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima mazao mbalimbali ikiwemo kahawa na ufuta katika mikoa ya Songwe na Mbeya wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika kata ya Mlowo, wilayani Mbozi mkoani Songwe.
  • Wakulima washukuru kuondokana na makato, kufungiwa akaunti
Songwe, Machi 28, 2025: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), imetambulisha kampeni yake ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ kwa wakulima wa mazao mballimbali ikiwemo Kahawa na ufuta kwenye mikoa ya Songwe na Mbeya ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuchochea kasi ya ukuaji wa sekta ya kilimo kupitia uchumi jumuishi unaochagizwa na huduma rasmi za kifedha.


Hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo ilifanyika kata ya Mlowo, wilayani Mbozi mkoani Songwe ikiongozwa na Katibu Tawala Wilaya ya Mbozi Bw. Mbwana Kambangwa, huku pia ikihushisha uwepo wa wadau mbalimbali wa sekta za kilimo na ufugaji kutoka mikoa hiyo miwili wakiwemo viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika vya wakulima na wafugaji (AMCOS), pamoja na wadau wengine wanaoshiriki kwenye mnyororo wa thamani wa sekta hiyo muhimu.


Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa aliwaongoza maofisa wengine wa benki hiyo kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo inayotoa fursa kwa wakulima na wafugaji wa mikoa ya Songwe na Mbeya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki na kompyuta mpakato ‘Laptops’


Akizungumza kwenye hafla hiyo, Bw Kambangwa pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa jitihada zake endelevu zinazolenga kuwasaidia wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali hapa nchini ukiwemo mkoa wa Songwe, alisema ujio wa kampeni hiyo kwenye mikoa hiyo utasaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wa wadau mbalimbali wa sekta hizo hususani kupitia huduma mbalimbali za kibenki zilizobuniwa mahususi kwa makundi hayo ikiwemo elimu ya kifedha na huduma za mikopo rafiki.


Ubora zaidi wa kampeni hii unaonekana pale inapohusisha utoaji wa elimu ya nidhamu ya fedha miongoni mwa wakulima mmoja mmoja na vyama vya ushirika hatua ambayo itawajengea uwezo wa kuona umuhimu wa kujiwekea akiba, umuhimu wa kutumia bima mbalimbali ikiwemo bima ya afya, bima za kilimo pamoja na kuwekeza kwenye zana za kisasa za kilimo.’’


CAREER OPPORTUNITY AT TADB BANK - MARKETING, CUSTOMER SERVICE & CORPORATE AFFAIRS MANAGER


The Manager – Marketing, Customer Service, and Corporate Affairs is pivotal in shaping TADB’s public image, strengthening stakeholder relationships, and enhancing customer experience. This role drives strategic communication, branding, and marketing initiatives, ensuring alignment with TADB’s development finance mandate and national priorities.

This position requires strong leadership, strategic execution, and adaptability to effectively position TADB as a key player in development finance.

Application deadline: Not later than 4:00 pm, 10th April 2025.

CLICK HERE TO APPLY > > >

EACOP SECURES MAJOR FUNDING AS CONSTRUCTION SURPASSES 55% MILESTONE


The East African Crude Oil Pipeline (EACOP) project has reached a significant milestone by securing the first tranche of external financing from a consortium of leading financial institutions. This consortium includes the African Export-Import Bank (Afreximbank), Standard Bank of South Africa Limited, Stanbic Bank Uganda Limited, KCB Bank Uganda, and the Islamic Corporation for the Development of the Private Sector (ICD). This financial commitment underscores confidence in EACOP's potential to transform the East African energy sector.

The project's shareholders comprise TotalEnergies (62%), Uganda National Oil Company Limited (UNOC, 15%), Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC, 15%), and China National Offshore Oil Corporation (CNOOC, 8%). Collectively, they are ensuring the project's progression towards establishing a significant export system aimed at boosting economic development in both Uganda and Tanzania.


Construction of the 1,443-kilometer pipeline—spanning 296 km in Uganda and 1,147 km in Tanzania—has surpassed 55% completion as of March 2025. The project emphasizes safety, environmental sustainability, and community engagement. Currently, over 8,000 Ugandan and Tanzanian citizens are employed, with 400,000 man-hours of training provided to equip the workforce with essential skills. Additionally, $500 million has been injected into local economies through the procurement of goods and services, reinforcing the project's positive economic impact.


Once completed, EACOP will transport up to 246,000 barrels of crude oil per day from Kabaale in Uganda's Hoima District to the Chongoleani Peninsula near Tanzania's Tanga Port. The pipeline features advanced technology, including a 24-inch insulated and buried system, six pumping stations, and two pressure reduction stations. Notably, the marine export terminal in Tanzania will incorporate a 3 MW solar plant, highlighting the project's commitment to integrating renewable energy solutions.



Adhering to high environmental and social standards, EACOP aligns with the International Finance Corporation (IFC) guidelines and the Equator Principles, ensuring socially responsible and environmentally sustainable execution. The project connects to national power grids, primarily hydro-based, to minimize its carbon footprint. EACOP represents more than just an oil pipeline; it symbolizes regional collaboration, economic development, and industrial advancement, offering long-term economic opportunities to communities along its route.

NCBA STRENGTHENS FINANCIAL INCLUSION AND COMMUNITY TIES THROUGH RAMADAN IFTAR

From left to right: NCBA Bank Tanzania Board Chairman - Dr. Fauz Abdallah Twaib, Deputy Kazh of Tanzania - Sheikh Ally Hamisi Ngeruko and NCBA Bank Tanzania Managing Director - Claver Serumaga.

NCBA Bank Tanzania recently hosted a special Iftar dinner at Serena Hotel, bringing together key stakeholders, customers, and religious leaders to celebrate the spirit of Ramadan. The event underscored the bank’s commitment to fostering financial inclusion and strengthening its ties with the community through innovative financial solutions tailored to meet the diverse needs of individuals and businesses.

NCBA Bank Tanzania Managing Director - Claver Serumaga.

Speaking at the event, NCBA Bank Managing Director, Mr. Claver Serumaga, emphasized the bank’s role in enhancing financial accessibility, particularly through digital banking and mobile-based financial solutions. He highlighted that financial inclusion is key to economic empowerment, and NCBA remains dedicated to ensuring that individuals, regardless of their background or location, can access essential financial services. Through platforms like M-Pawa and NCBA Now, the bank continues to transform the banking landscape in Tanzania, making it easier for individuals and businesses to save, access credit, and manage their finances seamlessly.

Deputy Kazh of Tanzania - Sheikh Ally Hamisi Ngeruko

The event was graced by the Guest of Honor, Deputy Kazh of Tanzania, Sheikh Ally Hamisi Ngeruko, who commended NCBA’s efforts in supporting the Muslim community and advancing financial inclusion. He highlighted the values of unity, generosity, and economic empowerment during Ramadan, acknowledging NCBA’s role in promoting financial literacy and providing accessible banking solutions. He emphasized that financial independence is crucial in fostering a prosperous society and lauded NCBA for offering digital financial solutions that empower individuals and small businesses.

NCBA Bank Tanzania Management Team.

The Iftar dinner also served as a platform to highlight the growing importance of digital financial solutions in promoting economic resilience. As one of Tanzania’s leading financial institutions, NCBA has been at the forefront of digital transformation, offering a suite of innovative products designed to meet the needs of today’s fast-evolving market. NCBA Now, the bank’s digital banking platform, allows customers to perform transactions, pay bills, and access financial services seamlessly from their mobile devices. With user-friendly features and real-time banking capabilities, NCBA Now is revolutionizing the way customers interact with their finances. M-Pawa, a flagship mobile savings and loan product, provides customers with easy access to financial services via their mobile phones. In partnership with Vodacom Tanzania, M-Pawa enables users to save securely and borrow instantly, empowering them to grow their businesses and manage personal expenses efficiently.

Thursday, 27 March 2025

BAHATI NASIBU YA TAIFA YASHIRIKIANA NA VODACOM M-PESA KUWEZESHA MIAMALA KIDIJITALI


Dar es Salaam, 27 Machi 2025: Bahati Nasibu ya Taifa ya Tanzania leo imesaini ushirikiano na jukwaa bora la huduma za kifedha kwa njia ya simu hapa nchini, Vodacom M-pesa, Ili kurahisisha miamala ya bahati nasibu ya Taifa na kupanua fursa za kibiashara kupitia mfumo wa fedha wa kidijitali.


Kuunganishwa kwa bahati nasibu ya Taifa kwenye jukwaa la M-Pesa, kutawapa watumiaji urahisi wa upatikanaji wa michezo ya bahati nasibu kupitia jukwaa salama.


Kwa kutumia mtandao mpana wa Vodacom wenye zaidi ya watumiaji milioni 26, ushirikiano huu utawezesha urahisi wa ununuzi wa tiketi za michezo ya kubahatisha, kupitia majukwaa ya kidijitali ya Vodacom, ikiwemo huduma za M-pesa kwa njia ya simu, USSD codes na aplikesheni ya M-pesa.


Mkurugenzi wa ITHUBA Tanzania, Kelvin Koka, ameelezea ushirikiano huu kuwa ni hatua kubwa katika sekta ya michezo ya kubahatisha nchini. "Ushirikiano huu na M-Pesa utahakikisha kwamba wachezaji wanashiriki kikamilifu katika michezo ya bahati nasibu, huku ukihamasisha wafanyabishara kuweza kushirikiana nasi kwa kuwa jukwaa letu linazingatia uwazi na mustakabali ujao wa bahati nasibu ya Taifa. Kwa kuwa M-Pesa ni mshirika wetu rasmi wa huduma za kifedha kwa njia ya simu, tutahakikisha kwamba tunazingatia usalama, ufanisi na uhakika wa miamala ya wateja wetu."

Mkuu wa Idara ya wa M-pesa Tanzania, Jacqueline Ikwabe, amebainisha umuhimu wa ushirikiano huu kwa kusema, "M-Pesa imejikita katika kuwezesha uvumbuzi wa kidijitali unaowanufaisha wafanyabiashara na wateja. Kwa kuiunganisha Bahati Nasibu ya Taifa kwenye jukwaa letu, tutahakikisha ushiriki salama, wa haraka na rahisi huku tukifungua fursa zaidi za ushirikiano katika sekta mbalimbali."

‘LIPA CHAPCHAP’: BENKI YA EXIM YAJA NA MAPINDUZI YA MALIPO KIDIJITALI

Mkuu wa Idara ya Wateja Wadogo na Kati wa Benki ya Exim, Bw. Andrew Lyimo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma mpya inayojulikana kama 'Lipa ChapChap', suluhisho bunifu la malipo ya kidijitali ambalo linarahisisha miamala kwa biashara na watu binafsi. Kushoto kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano, Bw. Stanley Kafu na Mkuu wa Idara ya Njia Mbadala za Kidijitali, Silas Matoi kutoka Benki ya Exim Tanzania.

Dar es Salaam – Benki ya Exim Tanzania imechukua hatua madhubuti katika kuunda mustakabali wa malipo ya kidijitali kwa kuzindua ‘Lipa ChapChap’, suluhisho la malipo yasiyotumia fedha taslimu linalorahisisha miamala kwa wafanyabiashara na wateja binafsi. Zaidi ya kuwa huduma mpya, Lipa ChapChap ni hatua muhimu katika dhamira ya benki ya kuendeleza ujumuishi wa kifedha, ubunifu, na uchumi wa kidijitali nchini Tanzania.


Sababu kubwa ya ubunifu huu ni ongezeko la mahitaji ya malipo yasiyotumia fedha taslimu na ujumuishi wa kifedha. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imekuwa ikisisitiza umuhimu wa kuhamia kwenye uchumi wa kidijitali. Kupitia Lipa ChapChap, Benki ya Exim inaendana na maono ya BoT ya kujenga mfumo wa kifedha ulio jumuishi na wa kisasa zaidi, hatimaye kupunguza utegemezi wa miamala ya fedha taslimu.


Kwa biashara nyingi, hususan biashara ndogo na ya kati (SMEs), mifumo ya kibenki ya zamani mara nyingi huweka vikwazo kama vile gharama kubwa za miamala na upatikanaji mdogo wa miundombinu ya malipo ya kidijitali. Suluhisho hili la malipo linaondoa changamoto hizi kwa kutoa njia salama na isiyo na gharama kwa wafanyabiashara, ikiwaruhusu kupokea malipo kutoka benki zote na mitandao yote ya simu.


Mkuu wa Idara ya Wateja Wadogo na Kati wa benki hiyo, Andrew Lyimo alielezea athari chanya ya mpango huu kwa kusema: "’Maliza Kirahisi, Lipa ChapChap’ ni ushuhuda wa dhamira yetu ya kuleta ubunifu na urahisi. Suluhisho hili siyo tu kwamba linaimarisha ufanisi wa malipo, bali pia linakuza ujumuishi wa kifedha kwa kuhudumia biashara zote, ikiwemo SMEs, kwa njia salama, isiyo na gharama, na inayopatikana kwa haraka. Lengo letu ni kuunda mfumo wa uchumi usiotegemea fedha taslimu unaowanufaisha wafanyabiashara na wateja binafsi."


Kwa kuongezeka kwa matumizi ya teknolojia ya simu, suluhisho hili la Benki ya Exim linahakikisha kuwa biashara za kila aina, kutoka kwa wauzaji wadogo mitaani hadi makampuni makubwa, zinapata mfumo wa malipo wa kidijitali ulio salama na wenye ufanisi.