Ukuaji huu unatokana na dhamira ya benki hiyo ya kusaidia wafanyabiashara na watu binafsi kwa kutoa huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji yao, huku ikizingatia usimamizi bora wa mali. Kwa mantiki hiyo, kiwango cha mikopo isiyolipwa kimesalia chini ya kiwango cha udhibiti kwa 2.7% kufikia 31 Desemba 2024. Uwekaji wa fedha kwa wateja ziliongezeka hadi TZS trilioni 2.5, ongezeko la 4.2%, ikiashiria imani ya wateja na ufanisi wa bidhaa za kifedha za Exim Bank katika kukidhi mahitaji mbalimbali ya kibenki.
Afisa Mkuu wa Fedha wa benki hiyo, Shani Kinswaga, alisisitiza uimara wa kifedha wa taasisi hiyo: “Matokeo yetu yanaonesha mfumo madhubuti wa usimamizi wa hatari na ufanisi wa uendeshaji. Ukuaji mkubwa wa mtaji wa wanahisa, ambao umeongezeka kwa 32.6% hadi TZS bilioni 412.2, unathibitisha dhamira yetu ya muda mrefu ya kutoa thamani kwa wadau wetu.”
Mapato yasiyotokana na riba, ambayo ni sehemu muhimu ya utofauti wa mapato, yaliongezeka kwa 20.1% hadi TZS bilioni 123.7. Ukuaji huu unaonesha mkakati wa benki wa kupanua huduma za kibenki za kidijitali na vyanzo mbadala vya mapato, unaochochewa na maboresho endelevu ya huduma kwa wateja kupitia mifumo salama na rahisi ya kidijitali.
Andrew Lyimo, Mkuu wa Huduma za Rejareja wa Exim Bank, alisisitiza umuhimu wa benki ya kidijitali katika kukuza ujumuishaji wa kifedha: “Tunaendelea kupanua mfumo wetu wa kibenki wa kidijitali, tukitoa huduma za kifedha salama na rahisi kwa watu binafsi na wafanyabiashara. Kipaumbele chetu ni kutumia teknolojia kuboresha uzoefu wa wateja na kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kote nchini.”
Inapoangazia mbele, Exim Bank inaendelea kujidhatiti kuimarisha nafasi yake kubwa kupitia ubunifu endelevu, ushirikiano wa kimkakati, na upanuzi wa mtandao wake kikanda. Dira ya benki hiyo kwa 2025 inajumuisha kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha, kuhamasisha uwezeshaji wa kiuchumi, na kuendelea kuongoza katika huduma za kibenki za kidijitali. Kwa msingi thabiti na mkakati wa kisasa, Exim Bank iko tayari kwa mafanikio endelevu katika mazingira ya kifedha yanayoendelea kubadilika.
Akihitimisha ripoti hiyo, Bw. Matundu alisisitiza maono ya muda mrefu ya benki hiyo: “Matokeo haya ni ushuhuda wa dhamira yetu ya kuendeleza huduma za kifedha, ubunifu, na ukuaji unaomlenga mteja. Tunapoangalia mbele, kipaumbele chetu kitasalia katika kuongeza uwezo wetu wa kidijitali, kuimarisha upanuzi wetu kikanda, na kuwawezesha watu binafsi na wafanyabiashara kote nchini. Tumejizatiti kuunda mustakabali wa benki ndani na nje ya Tanzania.”
No comments:
Post a Comment