Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 5 June 2024

VODACOM YAIBUKA KIDEDEA KATIKA TUZO ZA KIDIJITALI

Wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom Tanzania PLC, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Vodacom Business - Nguvu Kamando (wa pili kushoto) wakionesha tuzo walizoshinda katika wiki ya ubunifu iliyoambatana na utoaji wa tuzo za Tanzania Digital Awards ambapo Vodacom iliibuka kidedea kwa kunyakua tuzo tano.
Mkurugenzi wa Vodacom Business - Nguvu Kamando (kushoto) akipokea tuzo ya kampuni bora ya simu iliyotolewa na kampuni ya Serengeti bytes na kupigiwa kura na Watanzania.
Mkuu wa idara ya Masoko wa Vodacom Business - Aileen Meena (kulia) akipokea tuzo ya kampuni ya simu inayotoa huduma bora kwa Wateja hapa nchini.
Meneja wa mifumo mipya ya huduma za kifedha - Brenda Msola (kushoto) akipokea tuzo ya kampuni ya ubunifu wa applikesheni bora ya huduma za kifedha.
Meneja wa mifumo mipya ya huduma za kifedha - Brenda Msola (kulia) akipokea tuzo ya ubunifu wa kidijitali katika sekta ya huduma za kifedha (M-Koba).

Kampunui inayoongoza kwa huduma za teknolojia na mawasiliano nchini ya Vodacom, imetunukiwa tuzo na Kampuni ya Serengeti bytes kupitia programu ya Tanzania Digital Awards katika wiki ya ubunifu (Innovation week).

Kampuni hiyo ya Vodacom imejishindia tuzo katika vipengele vitano ambavyo ni:
  1. Kampuni bora ya simu nchini
  2. Kampuni ya simu inayotoa huduma bora zaidi nchini
  3. Applikesheni bora ya huduma za kifedha
  4. Tuzo ya ubunifu wa kidijitali katika Afya (m-mama)
  5. Tuzo ya ubunifu wa kidijitali katika sekta ya huduma za kifedha (M-Koba)

No comments:

Post a Comment