Kitomari Banking & Finance Blog is a premier site for banking, finance, business, economic, investment and stock market news as well as selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the World. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.
Thursday, 29 May 2025
BENKI YA NBC YASHIRIKI MKUTANO MKUU MAALUM WA CCM, YATOA HUDUMA ZA KIFEDHA KWA WAJUMBE
Dodoma: Mei 29, 2025: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeshiriki kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) - Taifa uliofanyika jijini Dodoma, kama sehemu ya juhudi za benki hiyo kutoa huduma za kifedha kwa wateja wake sambamba na kuendelea kujenga mahusiano na wadau wake kibiashara.
Mkuu wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano wa NBC Bw. Godwin Semunyu, aliungana na timu ya wafanyakazi kutoka tawi la benki hiyo jijini Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa Kanda ya Kati wa benki ya NBC, Bw Miraji Msuya katika ushiriki huo.
“Ushiriki wetu kwenye Mkutano huu unatokana na mahusiano yetu kibiashara na wadau wa mkutano huu wakiwemo wanachama mmoja mmoja na chama pia kama taasisi. Pamoja na kufuatilia mkutano huu, NBC kama wageni waalikwa pia tunatoa huduma zetu za kibenki kwa wateja wetu waliohudhuria mkutano hu kupitia timu yetu iliyoweka kambi kwenye eneo hili la mkutano,’’ alisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment