Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Thursday, 15 May 2025

CRDB YAWAALIKA WANAHISA – MKUTANO MKUU WA 30 WA WANAHISA WAJA KWA KISHINDO!


Arusha, 14 Mei 2025: Benki ya CRDB imewataka wanahisa wake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa, unaotarajiwa kufanyika Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya mafanikio tangu kuanzishwa kwa benki hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye Hoteli ya Gran Meliá, jijini Arusha, ambapo Benki ya CRDB pia ilizindua Ripoti yake ya Mwaka 2024, inayoonyesha maendeleo makubwa ya kifedha, kiutendaji na kijamii yaliyopatikana katika kipindi hicho.



Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, amesema kuwa Mkutano Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa kipekee kwani utatanguliwa na semina maalum kwa wanahisa na umma, itakayofanyika Ijumaa, tarehe 16 Mei 2025, katika ukumbi wa Simba, AICC. “Semina hii ya kihistoria itakuwa chini ya kaulimbiu yetu ya mwaka huu: ‘Miaka 30 ya Ukuaji wa Pamoja,’ na itafunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio yetu ya pamoja, changamoto tulizozishinda, na mwelekeo wetu wa miaka ijayo,” amesema Dkt. Laay.

Ajenda mbalimbali zitajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB ni pamoja na uchaguzi wa wajumbe wa bodi, kuteua wakaguzi wa hesabu, kujadili mapendekezo ya maboresho ya Katiba ya Benki, kujadili na kupokea Taarifa ya Bodi ya Wakurugenzi, na Taarifa ya Hesabu zilizokaguliwa, pamoja na gawio kwa mwaka 2024 ambapo pendekezo la gawio la Sh 65 kwa hisa litawasilishwa.



Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa yamekamilika kwa asilimia 100. Nsekela amesema mkutano huo utafanyika kwa njia mseto “Hybrid Meeting” ili kutoa fursa kwa wanahisa wengi zaidi kushiriki moja kwa moja na kwa njia ya kidijitali. “Tumeweka muongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yetu ya www.crdbbank.co.tz, mitandao yetu ya kijamii, lakini pia maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa Wanahisa,” amesema Nsekela huku akiwahakikishia kuwa Benki hiyo vizuri katika kuhakikisha wanashiriki bila chanagamoto yoyote.



Nsekela amewahamasisha wanahisa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu huo wa kihistoria, akisisitiza kuwa uwepo wao ni muhimu kwa ajili ya kushuhudia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika miaka 30. “Tumejenga taasisi imara inayotoa huduma bora, tumeongeza thamani kwa wanahisa, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa letu. Hii ni fursa adhimu kwa kila mwanahisa kujivunia sehemu yake katika mafanikio haya na kushiriki kuamua mustakabali wa benki yetu katika miaka ijayo,” amesisistiza.



Wednesday, 14 May 2025

TANZANIA HOSTS FIRST-EVER CUSTOMER EXPERIENCE CONFERENCE TO ADVANCE ECONOMIC AGENDA

Managing Director of Real Interactiv Inc. - Caroline Maajabu Mbaga, speaks to participants at the conference.

Historic gathering positions customer experience as key driver for Tanzania's economic transformation

Dar es Salaam, May 10, 2025: The inaugural Annual Customer Experience Conference, hosted by Real Interactiv Inc. in partnership with CX Academy Africa, successfully convened on May 9, 2025 at Hyatt Regency Hotel, sparking a transformative national conversation about customer experience as Tanzania's next economic frontier. The landmark event brought together more than 100 C-suite executives and public sector leaders from Tanzania's most influential organizations, including Vodacom, CRDB Bank, NBC Bank, Equity Bank, KCB, TANESCO, Helios, Strategis Insurance, Bumaco Insurance, Engie Mobisol, ZIC Takful and NSSF, to establish customer-centric strategies as fundamental to national growth.


The conference opened with powerful keynote addresses from globally recognized CX pioneers. Mandisa Makubalo, Founder and CEO of South Africa's Unlimited Experiences Group, captivated attendees with her presentation "The Voice of the Voiceless Customer," demonstrating how authentic customer understanding drives market leadership across African economies. Her insights were complemented by Jonathan Daniels, Managing Director of UK-based CX Centric, who delivered a compelling analysis of global customer-centricity trends and their specific applications for Tanzanian businesses seeking competitive advantage.


A conference highlight was CRDB Bank, Yolanda Uriyo, Head of Customer Experience as one of the sponsors, delivery of an inspiring keynote address titled "Customer Experience as Tanzania's Engine for Growth and Differentiation." With compelling examples from CRDB's transformation journey, Uriyo galvanized the audience by demonstrating how customer-centric strategies had directly contributed to the bank's market leadership and financial performance. "In today's competitive landscape, customer experience isn't just about satisfaction - it's our most powerful engine for sustainable growth and meaningful differentiation," Uriyo declared.


A pivotal moment occurred during the fireside chat "Customer Experience as a National Economic Catalyst," moderated by Caroline Maajabu Mbaga, Managing Director of Real Interactiv Inc. The discussion featured Tanzania Tourist Board Director General Ephraim Mafuru, who articulated how exceptional visitor experiences directly contribute to Tanzania's tourism sector, which accounts for nearly one-fifth of the nation's GDP. "Every interaction - from airport arrivals to hotel stays - represents either an opportunity to enhance Tanzania's global reputation or a risk to our economic potential," Mafuru emphasized. His perspective was reinforced by Felix John, Investment Promotion Manager at Tanzania Investment Center, who presented compelling data showing that investor decisions increasingly prioritize service quality alongside traditional economic factors.


The conference's practical sessions saw Tanzanian business leaders share real-world implementations of CX excellence. Vodacom's Customer Experience Operations Director Harriete Lwakatare and G4S Tanzania General Manager Imelda Lutebinga led an engaging panel on embedding customer-centric cultures within large organizations, while Dorothy Ndazi, Partner at Hilton Law Group, provided crucial guidance on balancing personalized experiences with data protection requirements.


David Makoha, Country Manager for IPSOS Tanzania, grounded the discussions in empirical evidence, presenting research demonstrating that Tanzanian companies with mature CX programs outperform sector averages by significant margins. These insights were put into practice during interactive workshops where cross-industry teams collaborated on customer journey mapping exercises under the guidance of international experts.


As the conference concluded, organizers announced several strategic initiatives to maintain momentum, including the establishment of annual Tanzania CX Innovation Awards and quarterly leadership roundtables. A complimentary resource toolkit, "50 Practical Ways to Elevate Customer Experience," was released to all attendees and made available for public download.

Tuesday, 13 May 2025

VODACOM YAZINDUA MSIMU WA 4 WA DIGITAL ACCELERATOR: BIASHARA 15 ZA KIBUNIFU KUCHUANA

Vinara 15 wa Vodacom Digital Accelerator Season 4 Watangazwa! Washindi wa msimu wa 4 wa bunifu za kampuni changa (Startups), inayoandaliwa na Vodacom Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na timu ya kampuni hiyo baada ya kutangazwa katika tukio lililofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
  • Kufundishwa ujasiriamali na Wataalamu wa Kimataifa kutoka Marekani
Dar es Salaam, Mei 9, 2025: Vodacom Tanzania PLC, kwa kushirikiana na Huawei Tanzania, imezindua rasmi Msimu wa 4 wa Vodacom Digital Accelerator (VDA), hatua nyingine katika kusaidia ubunifu na ujasiriamali nchini.

Mwaka huu, biashara bunifu 15 zimechaguliwa kushiriki katika programu ya siku 5 ya Design Sprint, itakayoendeshwa na wataalam wa kimataifa kutoka programu ya MassChallenge ya nchini Marekani.

Lengo la Design Sprint ni kuboresha biashara zinazochipukia, kuimarisha ufanisi wa bidhaa sokoni na kuongeza maandalizi yao kwa ajili ya kuvutia uwekezaji. Kati ya hizi, biashara 10 zenye uwezo mkubwa wa kufanikiwa zitachaguliwa kwa safari ya miezi 3 ya kuendelezwa, ambapo zitapata ushauri wa kitaalam, msaada wa maendeleo ya biashara, na fursa mahususi za kufikia masoko ya ndani na ya kimataifa.


Msimu wa 4 wa VDA unaendeshwa kupitia ushirikiano wa kimkakati unaoendelea kati ya Vodacom na Huawei, jambo litakalowezesha wabunifu hao kushiriki kwenye safari ya kujifunza nchini China mwezi Juni. Wakati wa ziara hiyo ya kimataifa, wabunifu hao watakutanishwa na kampuni kubwa za teknolojia za nchini China, ili kujifunza mifumo ya ubunifu wa kisasa na pia kuwasilisha bunifu zao mbele ya wawekezaji binafsi na mashirika.

Katika hatua kubwa ya kuwaendeleza wajasiriamali chipukizi, msimu huu utakuwa na uwekezaji wa fedha taslimu zitatolewa kwa biashara tatu bora, ili kusaidia kukuza bunifu zao na hivyo kuwaongezea uwezo wa ushindani ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

"VDA ni jukwaa la ukuzaji wa kizazi kijacho cha wavumbuzi wa Kitanzania. Na kwa mara nyingine tunachanganya ubunifu wa ndani na uzoefu wa kimataifa tukiwasaidia vijana wabunifu katika kujenga biashara zinazoweza kupanuka, kupata uwekezaji na kuingia kwenye majukwaa ya kimataifa," alisema Zuweina Farah, Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania.

Monday, 12 May 2025

STANBIC YAIMARISHA "PRIVATE BANKING" KWA WATEJA WA ARUSHA

  • Benki ya Stanbic yazindua huduma za Private Banking jijini Arusha, ikiwa ni muendelezo wa upanuzi wa huduma zake nje ya Dar es Salaam, baada ya mafanikio ya matukio kama haya Mwanza na Mbeya mapema mwaka huu.
  • Upanuzi huu wa Arusha unaonesha dhamira ya Benki ya Stanbic kuwasogezea wateja wake huduma za kifedha za hali ya juu, na kuwapa fursa wajasiriamali, wataalamu na familia za wafanyabiashara nje ya Dar es Salaam kunufaika na Private Banking.
  • Tukio hili limeangazia kaulimbiu ya Stanbic ya “Ujasiriamali Hauishi”, likilenga kuwawezesha wateja kwa mipango ya kifedha ya muda mrefu, huduma mahususi za Private Banking, na njia za kujenga urithi wa kifamilia wa kifedha.
Arusha, 8 Mei 2025 – Benki ya Stanbic imezindua maboresho ya huduma zake za wateja maalum rasmi huduma ya Private Banking Client Value Proposition (CVP) jijini Arusha, ikionyesha dhamira yake ya kuwawezesha Watanzania wenye ukwasi mkubwa kwa kuwapatia suluhisho bora za kifedha za kiwango cha kimataifa. Uzinduzi huu unafuatia mafanikio ya matukio kama haya yaliyofanyika Mwanza na Mbeya mapema mwaka huu, na kuonyesha mkakati wa benki wa kupeleka huduma bora za kifedha nje ya Dar es Salaam.


Kupitia huduma hii, wakazi wa Arusha wananufaika kwa kuunganishwa na suluhisho za kifedha zinazowiana na mahitaji ya kipekee ya mkoa huu. Kwa kuwa Arusha ni kitovu cha biashara ya utalii, biashara ya madini, kilimo cha mazao ya biashara , na biashara za kifamilia, Private Banking inaleta thamani halisi kwa watu wanaojenga urithi wa kifamilia kupitia kazi zao za kila siku.


Arusha imechaguliwa kwa ajili ya tukio hili muhimu kutokana na umuhimu wake wa kiuchumi na kijamii. Kama kitovu cha utalii, diplomasia, kilimo, na biashara zinazokua kwa kasi, Arusha ina jamii yenye nguvu ya viongozi wa biashara, wawekezaji na wataalamu wanaotafuta huduma za kifedha za kiwango cha juu. Pia ni lango kuu la Afrika Mashariki na makao ya taasisi nyingi za kimataifa, hivyo kuifanya kuwa soko muhimu kwa huduma za Private Banking.

Tukio la Arusha limewakutanisha wateja maalum wa Benki wa Private Banking, wajasiriamali na wadau wakuu kujadili jinsi huduma hizi zinavyoweza kusaidia kukuza, kusimamia, na kulinda utajiri wa kifamilia kwa vizazi vijavyo. Kwa kauli mbiu ya 'Ujasiriamali Hauishi,' tukio hili limeangazia umuhimu wa mipango ya kifedha ya muda mrefu, urithi wa kifedha, na huduma za kipekee zinazolenga tabaka la juu la Tanzania.

Arnold Shirima, mtoa huduma za utalii kutoka Usa River, alishiriki uzoefu wake;

Huduma hii imenisaidia kupanga kwa mikakati zaidi kuhusu mustakabali wa biashara yangu. Kama mtu anayesimamia mapato ya msimu, nafasi nyingi za kuhudumia wateja, na gharama kubwa za uendeshaji, nimejifunza jinsi ya kutenganisha fedha za binafsi na za biashara bila kuathiri ubora wa huduma au ukuaji wa biashara. Kupitia msaada wa Benki ya Stanbic, sasa najisikia kuwa na udhibiti zaidi wa fedha zangu na nina uwezo bora wa kukuza biashara kwa njia endelevu". Arnold Shirima, mkulima wa mazao ya biashara katika maeneo ya Usa River, anasema: “Huduma hii imenisaidia kupanga mikakati ya kifedha ya muda mrefu. Kwa sasa ninafahamu namna ya kutenganisha fedha za biashara na matumizi binafsi bila kuathiri ukuaji wa shamba langu.”

STANBIC YAZINDUA KAMPENI YA “SALARY SWITCH” KWA ZAWADI NA MANUFAA MAALUM


  • Benki ya Stanbic Tanzania yazindua kampeni mpya ya Salary Switch, inayotoa zawadi za kila siku za pesa taslimu na mikopo ya mshahara kwa wafanyakazi waliopata ajira rasmi.
  • Kampeni inalenga kuimarisha uthabiti wa kifedha wa muda mrefu kwa kuhamasisha kuweka akiba kwenye akaunti za watoto, na kukuza utamaduni wa kuokoa.
  • Droo za bahati nasibu zinatoa fursa kwa wafanyakazi kote Tanzania kujishindia zawadi kubwa za pesa kwa urahisi kwa kutumia huduma za Stanbic Bank.
Dar es Salaam: Benki ya Stanbic Tanzania imezindua rasmi kampeni mpya ya Salary Switch, inayolenga kuwazawadia Watanzania waliopo kwenye ajira rasmi kwa zawadi za kila siku za pesa taslimu, mikopo ya mshahara ya kidigitali, na upatikanaji rahisi wa mikopo hadi TZS milioni 150. Kampeni hiyo ya miezi mitatu itaanza tarehe 1 Mei hadi 30 Julai 2025, na inalenga wafanyakazi wa sekta binafsi na ya umma, kuwapatia urahisi wa kifedha wa haraka, motisha, na huduma bora za kidigitali.

Kupitia kampeni hii, wateja watakaohamishia mishahara yao Stanbic Bank wataweza kushiriki kwenye droo za bahati nasibu za kila siku (Jumatatu hadi Ijumaa), zenye zawadi za pesa taslimu zinazotofautiana kati ya TZS 100,000 hadi TZS 500,000 kulingana na siku.

Zaidi ya hayo, wateja wanaofungua Akaunti ya Akiba ya Mtoto (Hatua) watazawadiwa na benki kwa kulinganisha kiasi cha awali kilichowekwa hadi TZS 250,000, ili kuwapa watoto wao mwanzo mzuri wa kifedha. Kwa wateja waliofungua akaunti hiyo tayari, kuweka amri ya kudumu ya kujiwekea akiba pia kutaleta zawadi kama hiyo – benki italinganisha kiasi kinachowekwa hadi TZS 250,000.

VISA APPOINTS NEW COUNTRY MANAGER FOR TANZANIA, UGANDA, BURUNDI AND RWANDA


12th May 2025, Dar es Salam – Visa, a world leader in digital payments, has appointed Victor Makere as the new Country Manager for Tanzania, Uganda, Burundi and Rwanda. Victor will be responsible for driving Visa’s strategic growth, enhancing client relationships, and expanding digital payment solutions across these key markets.

Victor will manage a diverse client portfolio across the four countries, aiming to boost Visa's strategic value, increase revenue for both clients and Visa, and strengthen executive relationships. He will also set business objectives and lead key projects, including new product and service implementation.

Chad Pollock, Vice President and General Manager for East Africa at Visa, commented on the appointment: “We are delighted to welcome Victor to the Visa East Africa leadership team. With his distinguished track record in digital financial services, merchant acquiring, and strategic business development, we look forward to his significant contributions to Visa’s efforts to enhance financial inclusion and expand digital commerce across Tanzania, Uganda, Burundi, and Rwanda. His leadership and expertise will be invaluable as we continue to build a resilient and inclusive digital payments ecosystem in the region.”

Victor expressed his enthusiasm for the new role: “I am excited to join Visa and play a key role in accelerating the growth of digital payments across Tanzania, Uganda, Burundi, and Rwanda. Visa’s commitment to financial innovation and inclusion aligns perfectly with my vision for transforming the payments landscape. I look forward to collaborating with our clients, partners, and stakeholders to deliver cutting-edge, secure, and seamless payment solutions that drive economic growth and empower businesses and consumers across the region.”

BENKI YA NMB YAANDIKA HISTORIA KWA KUSHINDA TUZO SITA KUBWA


Dar es Salaam: Benki ya NMB inatangaza mafanikio ya kihistoria ya ushindi wa tuzo sita za kimataifa kutoka kwa majarida mawili mashuhuri duniani - jarida la Euromoney linalochapishwa London, Uingereza, na Global Banking & Finance Magazine lenye makao makuu yake New Jersey, Marekani.


Ushindi huu mkubwa unaashiria kutambuliwa kwa ubora wa huduma, ubunifu na mchango wa Benki ya NMB katika kuchangia maendeleo endelevu ya kiuchumi nchini.


Miongoni mwa tuzo hizo ni ile ya heshima ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika” inayodhibitisha mafanikio na maendeleo makubwa ya NMB na tasnia nzima ya fedha nchini.


Tuzo ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika”, iliyotolewa hivi karibuni jijini London katika hafla ya Euromoney Private Banking Awards 2025, imeweka historia kwa kuwa ya kwanza kutolewa kwa Benki ya Kitanzania. Hii ni hatua kubwa ya kutambua mchango wa Tanzania katika eneo nyeti la uendelevu, ambalo lina umuhimu mkubwa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na mazingira duniani kote.


Ushindi huu unadhihirisha jitihada za Benki ya NMB za kuongoza mabadiliko na dhamira yake ya dhati za kuyafanya masuala ya mazingira, jamii na utawala bora (ESG) kuwa sehemu ya msingi katika shughuli zake za kiutendaji na dira yake ya kimkakati.


Benki ya NMB pia ilinyakua tuzo mbalimbali kama kinara wa kitaifa katika sekta ya benki kutoka kwa majarida hayo mawili kama ifuatavyo:

Euromoney:
  • Benki Bora ya Uendelevu Tanzania
  • Benki Bora ya Wateja Maalum Tanzania (kwa mwaka wa tatu mfululizo)
Global Banking and Finance Magazine:
  • Benki Salama Zaidi Nchini Tanzania
  • Kinara wa Uwajibikaji kwa Jamii Tanzania 2025
  • Afisa Mtendaji Mkuu Bora wa Benki Tanzania 2025 (Tuzo hii ilitolewa kwa CEO Ruth Zaipuna)
Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi Ruth Zaipuna alipongeza kwa tuzo hizo huku akisema : “Ni hatua ya kihistoria kwa tasnia ya fedha nchini. Aidha, alisisitiza kuwa tuzo hizi ni hatua muhimu katika kuisaidia Tanzania kujipambanua kama kiongozi wa kikanda wa ufadhili endelevu na utoaji wa huduma bora za kifedha.

NMB CLINCHES SIX TOP AWARDS, INCLUDING "AFRICA’S BEST BANK FOR SUSTAINABILITY"


Dar es Salaam: NMB Bank PLC is proud to announce a landmark achievement for securing six prestigious awards from two renowned international bodies: London-based Euromoney and Global Banking & Finance Magazine from New Jersey, U.S.A. This historic recognition includes receiving the Africa's Best Bank for Sustainability award, marking a pivotal moment for NMB Bank and the Tanzanian financial sector.


The Africa's Best Bank for Sustainability award, presented at the recent Euromoney Private Banking Awards ceremony in London, is the first time a Tanzanian Bank has received continental recognition in this vital area that has a global impact. This underscores NMB Bank's pioneering efforts and deep commitment to integrating environmental, social, and governance (ESG) principles into its core operations and strategic vision.


NMB Bank also received multiple accolades as a national leader in the Banking Sector by the two institutions as follows,

Euromoney
  • Tanzania’s Best Bank for Sustainability
  • Tanzania’s Best Private Bank (for the third consecutive year)
Global Banking and Finance Magazine
  • Safest Bank in Tanzania
  • Best Corporate Social Responsibility Initiative Tanzania 2025
  • Best Banking CEO Tanzania 2025 (awarded to CEO Ruth Zaipuna)

Announcing these significant achievements in Dar es Salaam, NMB Bank CEO Ruth Zaipuna hailed the recognition as a historic breakthrough for Tanzania's financial sector. She emphasised that the awards represent a significant step in positioning the country as a regional leader in sustainable finance and service excellence.

Friday, 9 May 2025

ABSA BANK CHAMPIONS FINANCIAL LEADERSHIP AT 10TH CFO EAST AFRICA SUMMIT


Dar es Salaam, 8 May 2025: Absa Bank Tanzania reaffirmed its commitment to advancing financial leadership across the region by participating as a Principal partner at the 10th CFO East Africa Summit, held at the Serena Hotel in Dar es Salaam.


The annual summit brought together over 100 senior finance executives from across East Africa, offering a vital platform for knowledge exchange, regional networking, and dialogue on emerging financial trends. Topics ranged from the evolving role of the CFO, digital transformation, and ESG integration to strategic growth and capital optimization.


In his keynote address, Mr. Obedi Laiser, Managing Director of Absa Bank Tanzania, underscored the bank’s rationale for supporting the CFO East Africa Summit, citing its relevance in today’s evolving economic climate.


As sponsors of this summit, we recognize the critical role finance leaders play in shaping the future of organizations across East Africa,” Mr. Laiser remarked. “The CFO role is no longer confined to traditional financial stewardship, it has expanded to include driving innovation, strategic transformation, and long-term value creation.”


He emphasized that Absa Bank Tanzania is committed to equipping finance executives with the tailored financial solutions and strategic advisory they need to help their organizations thrive in uncertain times. “We stand ready to partner with CFOs, providing insights, capital, and expertise to support their ambitions and unlock new growth opportunities.”


Absa Bank Tanzania's active participation in the summit aligns with its overarching purpose: to Empower Africa’s tomorrow, together….one story at a time, by shaping the future of finance through collaboration, innovation, and thought leadership. With a footprint in over 10 African countries with representative offices in Nigeria, Namibia, London and New York, Absa continues to play a pivotal role in driving economic growth and financial inclusion across the region.

ABSA GROUP CHAIRMAN STEPS DOWN; HANDS OVER REINS TO THE NEXT PHASE OF LEADERSHIP

Mr Sello Moloko.
  • Mr Sello Moloko will step down as Chairman and Independent Non-Executive Director of the Board of Absa Group on 15 July 2025
  • Mr René van Wyk will succeed Mr Moloko as Group Chairman, subject to regulatory approval
  • The Absa Group Board thanks Mr Moloko for his leadership and service during his tenure
  • Mr Moloko will work with Mr van Wyk in the coming months to ensure a smooth transition
Absa Group has announced that Mr Sello Moloko will be stepping down as Chairman of the Board and an Independent Non-Executive Director, effective 15 July 2025. Moloko, who has led the strategic work of the board, will be handing over the reins for the next phase of leadership and for him to focus on his family, personal business interests, and community commitments.

Mr René van Wyk will succeed Mr Moloko as Chairman of the Board effective 15 July 2025, subject to regulatory approval.

Moloko says, “I feel honoured to have worked alongside such a talented and dedicated Board and with a management team that has shown invaluable resilience. The Board dealt with several challenges in 2024, and as a result did work to reposition the Group for a more sustainable performance trajectory which included appointing a permanent Chief Executive and initiating the restructure of our retail operating model”.

These challenges have got me to reflect on the demands on myself and on my time. I feel the time is ripe now for me to refocus my attention on my family, my community commitments and the several personal business initiatives outside the Group that I need to drive. This will, naturally, adversely affect my ability to devote the requisite time to a group of the scale of Absa. Indeed, it has been a great privilege to serve as Chairman of the Absa Group Board,” concludes Moloko.

ABSA BANK HOSTS INVESTMENT BANKING BREAKFAST TO EMPOWER CORPORATE CLIENTS



Dar es Salaam, May 8, 2025: Absa Bank Tanzania hosted an exclusive Investment Banking Breakfast event at the Zanzibar Room of the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam. The event, attended by over 100 corporate clients, is part of the bank’s ongoing commitment to equip businesses with timely insights and financial solutions that enable sustainable growth across sectors.


The event featured presentations from senior investment banking experts from Absa Bank Tanzania and Absa Group, covering critical themes including Debt Capital Markets, Strategic Partnerships, and M&A opportunities across East Africa.


In his opening remarks, Mr. Obedi Laiser, Managing Director of Absa Bank Tanzania, reaffirmed the bank’s commitment to supporting clients in navigating a dynamic economic landscape.


Our goal is to keep our clients ahead of the curve by sharing valuable insights and bespoke solutions that unlock capital and drive business transformation,” said Mr. Laiser. “Absa’s investment banking franchise is not only award-winning - it is deeply rooted in understanding the local context while leveraging our continental reach.”


The bank’s purpose - “Empowering Africa’s tomorrow, together, one story at a time” - was emphasized throughout the event. Mr. Laiser also reiterated Absa’s brand promise: “Your story matters,” underscoring the bank’s dedication to building lasting relationships with clients through tailored financial support.


Adding her voice to the session, Ms. Nellyana Mmanyi, Corporate Director at Absa Bank Tanzania, highlighted the strength and diversity of the bank’s investment banking capabilities.


Our Investment Banking offerings are designed to meet our clients where they are and take them where they aspire to go. From project and asset finance to M&A advisory and capital markets solutions, we provide end-to-end support that is responsive to the realities of doing business in Tanzania and the rest of continent. The real value for our clients lies in our ability to bring global capabilities and deep regional insights into every solution we deliver. We’re not just offering products - we're offering strategic partnerships.” said Ms. Mmanyi.


Absa’s Investment Banking arm has garnered numerous awards over the past three years, including:
  • Best M&A Bank in Africa, Best Investment Bank for Infrastructure (2025),
  • Green Finance Bank for Pan Africa (2024),
  • Most Innovative Investment Bank in multiple African markets (2023), and
  • Best Investment Bank in Africa (2023), among others.

With a strong presence in over 17 African countries, Absa continues to deliver strategic advisory, financing, and capital-raising solutions that power growth across the continent.


TRA & SICPA LEAD THE CHARGE IN MODERNIZING TAX COMPLIANCE WITH SMART DAS TRAINING


In a continued effort to modernize tax administration and enhance compliance among producers of excisable goods, the Tanzania Revenue Authority (TRA), in partnership with SICPA Tanzania, has commenced a nationwide training program focusing on the newly introduced Smart DAS (Huisha Kidijitali) mobile application. The initiative is part of the broader strategy to simplify the Electronic Tax Stamp (ETS) declaration process, reduce human error, and improve efficiency for both taxpayers and regulators.

The Smart DAS app, now available on Android and iOS platforms, offers a streamlined solution for taxpayers. Instead of manually entering stamp serial numbers—a process that was time-consuming and prone to errors—producers can now simply scan the first and last stamp used in a batch. The application automatically captures the necessary data and submits it directly to TRA’s central system, greatly reducing declaration time and improving accuracy in reporting.

This application is a direct response to the needs of our taxpayers,” said Mr. Abyud Tweve, ETS Project Manager from TRA Headquarters’ Domestic Revenue Department. “We listened to their challenges and responded with a practical, easy-to-use solution that not only simplifies compliance but also enhances our own ability to manage and verify production data in real-time.”

To ensure the effective rollout of the app, TRA recently hosted a comprehensive training session in Dar es Salaam, bringing together 92 officers from across the country. The officers, who oversee the ETS and Electronic Fiscal Device (EFD) sections in their respective regions, were given practical demonstrations on the use of the Smart DAS app and how it integrates with existing tax compliance tools.

During the training, officers also participated in workshops where key action points were agreed upon—including the need for a cascade training model. Each officer is now expected to conduct regional-level taxpayer workshops to ensure all producers are familiar with the new system and can adopt it with minimal disruption to their operations.

The success of Smart DAS depends on awareness and accessibility,” added Mr. Tweve. “Our officers are now fully equipped to guide taxpayers, address concerns, and ensure that every user understands the advantages of going digital.”

Thursday, 8 May 2025

NBC YAZINDUA "NBC SHAMBANI" KWA WAKULIMA WA UFUTA PWANI

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Bw Nickson Simon (alieshika mkasi) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima zao la ufuta mkoani Pwani wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika mapema jana wilayani Kibaha, mkoani Pwani. Wengine ni pamoja na Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (kulia), na wadau mbalimbali wa kilimo kutoka mkoa huo.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Bw Nickson Simon (pichani) akizungumza na wadau wa kilimo wakiwemo wakulima kutoka mkoa wa Pwani wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima zao la ufuta mkoani Pwani iliyofanyika wilayani Kibaha.
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (pichani) akizungumza na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakiwemo wakulima na viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’.
Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Pwani, Bw Abdillahi Mutabazi (pichani) akizungumza na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakiwemo wakulima na viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’.
Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Majanga wa Benki ya NBC Bw Godliving Maro (pichani) akizungumza na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakiwemo wakulima na viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika.

Kibaha, Pwani - Mei 7, 2025: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), imetambulisha kampeni yake ya ‘Wekeza NBC Shambani Ushinde’ kwa wakulima wa zao la ufuta mkoa wa Pwani ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuchochea kasi ya ukuaji wa sekta ya kilimo kupitia uchumi jumuishi unaochagizwa na huduma rasmi za kifedha.


Hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo ilifanyika wilayani Kibaha ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Bw Nickson Simon ‘Nikki wa Pili’ huku pia ikihushisha uwepo wa wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo kutoka mkoa huo akiwemo Mrajisi Msaidizi wa Mkoa huo Bw Abdillahi Mutabazi, viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika vya wakulima na wafugaji (AMCOS), pamoja na wadau wengine wanaoshiriki kwenye mnyororo wa thamani wa sekta hiyo muhimu.


Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa aliwaongoza maofisa wengine wa benki hiyo kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo inayotoa fursa kwa wakulima wa zao la ufuta mkoa wa Pwani kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki na kompyuta mpakato ‘Laptops’