Ukuaji huu unatokana na dhamira ya benki hiyo ya kusaidia wafanyabiashara na watu binafsi kwa kutoa huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji yao, huku ikizingatia usimamizi bora wa mali. Kwa mantiki hiyo, kiwango cha mikopo isiyolipwa kimesalia chini ya kiwango cha udhibiti kwa 2.7% kufikia 31 Desemba 2024. Uwekaji wa fedha kwa wateja ziliongezeka hadi TZS trilioni 2.5, ongezeko la 4.2%, ikiashiria imani ya wateja na ufanisi wa bidhaa za kifedha za Exim Bank katika kukidhi mahitaji mbalimbali ya kibenki.
Afisa Mkuu wa Fedha wa benki hiyo, Shani Kinswaga, alisisitiza uimara wa kifedha wa taasisi hiyo: “Matokeo yetu yanaonesha mfumo madhubuti wa usimamizi wa hatari na ufanisi wa uendeshaji. Ukuaji mkubwa wa mtaji wa wanahisa, ambao umeongezeka kwa 32.6% hadi TZS bilioni 412.2, unathibitisha dhamira yetu ya muda mrefu ya kutoa thamani kwa wadau wetu.”