Foreign Exchange Rates

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Tuesday, 4 February 2025

RIPOTI YA FEDHA, BENKI YA EXIM 2024 YAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu (katikati), akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza Ripoti ya Fedha ya 2024 ya benki hiyo, ikionesha mafanikio makubwa ya kifedha na ukuaji endelevu. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Rejareja, Andrew Lyimo, na Afisa Mkuu wa Fedha, Shani Kinswaga (kulia), katika hafla iliyofanyika hivi karibuni katika Makao Makuu ya Benki ya Exim jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam: Benki ya Exim Tanzania imetoa ripoti yake yenye matokeo mazuri ya kifedha kwa mwaka ulioishia tarehe 31 Desemba 2024, ikionesha ukuaji mkubwa katika viashiria muhimu vya kifedha na kama taasisi. Jumla ya mali za benki hiyo zimeongezeka kwa 4.7%, kufikia TZS trilioni 3.1, na kuimarisha nafasi yake kama mojawapo ya taasisi zinazoongoza katika sekta ya kifedha Tanzania. Kiasi cha mikopo yake kimefikia TZS trilioni 1.8, ikirekodi ongezeko la kuvutia la 19.1% kwa mwaka.


Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu, alisema, “Matokeo yetu ya 2024 yanaonesha dhamira yetu ya ukuaji endelevu na ujumuishaji wa kifedha. Tumewekeza kimkakati katika mageuzi ya kidijitali, huduma za kibenki zinazomlenga mteja, na upanuzi wa kikanda, kuhakikisha kuwa tunasalia mstari wa mbele katika ubunifu na ubora wa huduma.”


Faida ya benki kabla ya kodi ilifikia TZS bilioni 139.7, ikiwa na ongezeko la asilimia 52.7 ikilinganishwa na mwaka uliopita, huku faida baada ya kodi ikiwa TZS bilioni 90, ambayo inadhihirisha ongezeko la asilimia 48.8. "Utendaji huu wa kipekee ni matokeo ya maboresho katika operesheni zetu, uwekezaji wa kimkakati, na juhudi zetu za kuendelea kuwapatia wateja wetu huduma bora”.Tunashukuru wateja wetu kwa kuendelea kutuamini na kutuunga mkono, jambo ambalo limekuwa muhimu katika kufikia matokeo haya. "Pia, mazingira bora ya biashara yamechangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza ukuaji, na kutuwezesha kuchukua fursa zinazoendana na malengo yetu ya muda mrefu." amesema Mkurugenzi wa Fedha wa benki, Shani Kinswaga.

Ukuaji huu unatokana na dhamira ya benki hiyo ya kusaidia wafanyabiashara na watu binafsi kwa kutoa huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji yao, huku ikizingatia usimamizi bora wa mali. Kwa mantiki hiyo, kiwango cha mikopo isiyolipwa kimesalia chini ya kiwango cha udhibiti kwa 2.7% kufikia 31 Desemba 2024. Uwekaji wa fedha kwa wateja ziliongezeka hadi TZS trilioni 2.5, ongezeko la 4.2%, ikiashiria imani ya wateja na ufanisi wa bidhaa za kifedha za Exim Bank katika kukidhi mahitaji mbalimbali ya kibenki.

Afisa Mkuu wa Fedha wa benki hiyo, Shani Kinswaga, alisisitiza uimara wa kifedha wa taasisi hiyo: “Matokeo yetu yanaonesha mfumo madhubuti wa usimamizi wa hatari na ufanisi wa uendeshaji. Ukuaji mkubwa wa mtaji wa wanahisa, ambao umeongezeka kwa 32.6% hadi TZS bilioni 412.2, unathibitisha dhamira yetu ya muda mrefu ya kutoa thamani kwa wadau wetu.”

VODACOM YAWAZAWADIA MAWAKALA BORA JIJINI DODOMA

Mkurugenzi wa M-Pesa Tanzania, Epimack Mbeteni (kulia) akimkabidhi zawadi na cheti Elikira Ezekiel (katikati), kuwa wakala aliyefanya vizuri zaidi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha wa kampuni ya Vodacom kwa kanda ya kati. Viongozi wa kampuni hiyo kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam walitembelea sehemu mbalimbali katika kanda hiyo ili kuongea, kutatua matatizo ya wateja wao papo hapo na pia kuwatambua mawakala waliofanya vizuri zaidi. Hii ikiwa ni adhma yao ya kusogeza huduma karibu na wateja na kuendelea kuwaelimisha kuhusu huduma zao. Kushoto ni meneja usimamizi thamani ya mteja kutoka Vodacom, Daudi Ndovu. Tukio hili lilifanyika hivi karibuni Wilaya ya Kondoa, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa M-Pesa Tanzania, Epimack Mbeteni (kushoto) akimkabidhi zawadi na cheti Thabit Juma Idd (wa pili kutoka kushoto), kuwa wakala aliyefanya vizuri zaidi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha wa kampuni ya Vodacom kwa kanda ya kati. Viongozi wa kampuni hiyo kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam walitembelea sehemu mbalimbali katika kanda hiyo ili kuongea, kutatua matatizo ya wateja wao papo hapo na pia kuwatambua mawakala waliofanya vizuri zaidi. Hii ikiwa ni adhma yao ya kusogeza huduma karibu na wateja na kuendelea kuwaelimisha kuhusu huduma zao. Kulia ni Meneja Mauzo wa kampuni hiyo Wilaya ya Manyoni, Bernard Kombe, akifuatiwa na Afisa Mauzo wa M-Pesa wa Kanda hiyo, Musa Kushoka. Tukio hili lilifanyika hivi karibuni Wilaya ya Manyoni jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa M-Pesa Tanzania, Epimack Mbeteni akimkabidhi zawadi na cheti cha kuwa wakala aliyefanya vizuri zaidi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha wa kampuni ya Vodacom kwa kanda ya kati, Idrisa Omary Kondoa jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa M-Pesa Tanzania, Epimack Mbeteni akimkabidhi cheti cha kuwa wakala aliyefanya vizuri zaidi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha wa kampuni ya Vodacom kwa kanda ya kati, Timoth Ndeji Itigi jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa M-Pesa Tanzania, Epimack Mbeteni akimkabidhi zawadi na cheti cha kuwa wakala aliyefanya vizuri zaidi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha wa kampuni ya Vodacom kwa kanda ya kati, Roman Abed Machinga Complex jijini Dodoma.