Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 7 June 2024

DKT. NCHEMBA AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA TCB

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya Benki hiyo na mchango wake katika maendeleo ya Taifa, Ofisini kwa Waziri wa Fedha Treasury Square, jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya Benki hiyo na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.

Mkutano huo umefanyika Ofisini kwa Waziri wa Fedha Treasury Square, jijini Dodoma ambapo Waziri wa Fedha ameipongeza Benki hiyo kwa mafanikio inayoendelea kuyapata ikiwemo kutengeneza faida katika biashara ya sekta ya fedha.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia) akiagana na Mkurugenzi wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, baada ya kumalizika kwa mkutano wao ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya Benki hiyo na mchango wake katika maendeleo ya Taifa, uliofanyika katika Ofisi ya Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, akielezea umuhimu wa Benki hiyo katika kuchochea ukuaji wa Uchumi, wakati wa mkutano kati yake na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya Benki hiyo na mchango wake katika maendeleo ya Taifa, uliofanyika katika Ofisi ya Waziri wa Fedha Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiongoza mkutano kati yake na Mkurugenzi wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya Benki hiyo na mchango wake katika maendeleo ya Taifa, uliofanyika Wizara ya Fedha, jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment