Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 1 July 2022

VODACOM YAKABIDHI VIFAA KWA SHULE YA WASICHANA

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis(wan ne kushoto) akikabidhi baadhi ya vitabu kwa Mkuu wa shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, Hollness Moshi (kushoto) ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388. Kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria, Agapinus Tax na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis(wa tano kushoto), akikata utepe wakati wa Hafla yakukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika Shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax, uongozi wa shule pamoja na maofisa wengine wa Vodacom.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akisalimiana na Mkuu wa shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, Hollness Moshi wakati walipo kwenda kutoa msaada katika shule hiyo.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakitoa burudani ya ngoma za asili wakati wa kampuni ya Vodacom walipokwenda shuleni hapo kwa ajili ya kutoa misaada ya vifaa mbalimbali.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akikabidhi baadhi ya vitabu kwa wanafunzi shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.

Vodacom Tanzania Yakabidhi Vifaa kwa Shule ya WasichanaVodacom Tanzania Foundation leo imekabidhi vifaa na samani kwa Shule ya Wasichana ya Bethsaida mjini Dar es Salaam ambavyo kampuni ilishinda katika mashindano ya makampuni ya Vodacom duniani.

Akiongea wakati wa makabidhiano, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Vodacom Tanzania, Vivienne Penessis alisema, “Elimu ni msingi pekee ambao unampatia mtu kianzio cha kujenga miasha bora.

Hii ni kweli zaidi kwa Watoto yatima ambao tegemeo lao ni elimu pekee.”Shule ya Wasichana ya Bethsaida ilichaguliwa kupokea msaada huu kwa kuwa ni moja ya shule chache zinazotoa elimu ya sekondari kwa Watoto yatima wa kike nchini.

Mkurugenzi wa Vodacom pamoja na wafanyakazi wengine wa kampuni waliikabidhi shule hiyo viti 100, vitabu Zaidi ya 300 pamoja na vifaa 20 vya kuzalisha umeme wa jua. Bi penessis alielezea Imani yake kuwa msaada huo utatumika ipasavyo kwani kampuni ya Vodacom ilijiridhisha juu ya utaalam na moyo wa kujitoa wa wafanyakazi wa shule ya Bethsaida.

Msaada huu unaendana na malengo ya Vodacom Tanzania kuongeza ujumuishwaji katika elimu. Hivi karibuni, kampuni ya Vodacom ilizindua mpango wa kupanua wigo wa mfumo wa E-Fahamu kufikia nchi nzima. E-Fahamu ni huduma inayotoa mawaidha ya elimu yenye viwango vya kimataifa na vyenye kukidhi miongozo ya serikali juu ya elimu.

Kuhusu Vodacom Tanzania FoundationThe Vodacom Tanzania Foundation ni sehemu ya kampuni ya Vodacom Tanzania PLC yenye mamlaka ya kutoa huduma za kijamii zikiwa zinawalenga zaidi wanwake na vijana. Foundation inajumuisha utoaji wa hisani na kutumia uwezo utakanao na teknolojia kuleta suluhisho kwa mahitaji ya kijamii.Ikishirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali, Vodacom Tanzania Foundationimesaidia zaidi ya miradi 120 hadi sasa ikiwa imewekeza zaidi ya Shilingi bilioni 15 kuboresha Maisha ya watanzania.Kwa maelezo zaidi, tafadhali tembelea:

No comments:

Post a Comment