Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 21 May 2021

NMB BONGE LA MPANGO - MKAZI WA CHAMWINO ANYAKUA GARI AINA YA TATA ACE

Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Benki ya NMB - Benedicto Baragomwa akimkabidhi kadi ya gari aina ya Tata Lifan alimaarufu Kirikuu, Jacqline Kihongozi, aliyepokea kwa niaba ya mshindi wa kampeni ya bonge la Mpango inayoendeshwa na NMB, Hadija Idd Mkazi wa Chamwino Mkoani Dodoma ambaye ndiye mshindi wa kwanza kujishindia zawadi ya gari aina ya Tata Ace kwenye kampeni hii. Akishuhudia ni Meneja wa NMB Kanda ya Kati - Nsolo Mlozi.

Kwa niaba ya mshindi wa kwanza wa gari aina ya Tata Ace kwenye kampeni ya Bonge la Mpango - Hadija Idd Mkazi wa Chamwino Mkoani Dodoma, ambaye ndiye mshindi wa kwanza kujishindia zawadi ya gari aina ya Tata Ace kwenye kampeni hii - Jacqline Kihongozi akifungua gari hilo (Lifan) baada ya kukabidhiwa na Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Benki ya NMB - Benedicto Baragomwa katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Tawi la NMB Chamwino. Akishuhudia ni Meneja wa NMB Kanda ya Kati - Nsolo Mlozi.

Hadija Iddi mkazi wa Chamwino mkoani Dodoma amekuwa mshindi wa kwanza kuzawadiwa gari aina ya TATA Ace maarufu kama Kirikuu yenye thamani ya sh. Millioni 25, baada ya kushinda katika kampeni ya Bonge la Mpango inayoendeshwa na Benki ya NMB.

Akimkabidhi gari hiyo Bi. Hadija, Kaimu Afisa Mkuu Ukaguzi wa Ndani wa NMB, Benedicto Baragomwa alisema, Bonge la Mpango inaendelea nchini kote na zawadi mbakimbali zinaendelea kutolewa, hivyo wateja wanaendelee kufungua akaunti na kuweka hela kuanzia sh. 100,000 kwenye akaunti zao za NMB ili waweze kuingia katika kinyanganyiro cha Zawadi mbalimbali zinazotolewa katika kampeni hii ikiwemo, gari ya kifahari aina ya Toyota Fortuner mpya yenye thamani ya Sh.169 milioni, gari ya miguu mitatu(Lifan) na pesa taslimu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa gari hilo, Hadija aliishukuru benki ya NMB na kusema kuwa gari hilo litamsaidia katika shughuli zake za kujiongezea kipato lakini pia akawashauri watanzania kuwekeza katika benki hiyo kwani ndiyo benki bora Tanzania na pia inawajali wateja wake kwani amekuwa shahidi.

"Nimeamini kuwa yanayozungumzwa ni kweli,nimekabidhiwa gari mpya,nimepewa ufunguo na Kadi ya gari vikiwa kamili kabisa, kweli NMB ndiyo mpango mzima,"alisema Hadija.

Wakati huo huo, Meneja wa NMB Kanda ya Kati - Nsolo Mlozi na mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania walichezesha droo nyingine kwa ajili ya kuwapata washindi wa wiki, ambapo watu mbalimbali walipata fedha taslimu wakati na Henry Semwanza kutoka Chamwino and Faustine Nyawigrika wa Biharamulo wakijishindia gari ya mataili matatu (Lifan) mpya kila mmoja.

Hadi sasa, NMB imetoa zawadi zenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 145 zikiwemo; fedha taslimu, pikipiki za miguu mitatu aina ya LIFAN na Tata Ace kwa washindi wa Bonge la Mpango.

No comments:

Post a Comment