Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 25 February 2021

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAWAPELEKEA WAKAZI WA MIKOA YA KASKAZINI BIA MPYA YA GUINNESS SMOOTH

Meneja wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Kaskazini, Msika Lumuli (kushoto) akiwa na maafisa mauzo, Nakunda Mbaga na Susan Mollel wakiongesha bia mpya ya Guinness smooth ambayo ilizinduliwa hivi karibuni jijini Arusha
Mjengoni bendi ikiwaburudisha wageni waolifika kwenye uzinduzi wa bia mpya ya Guiness smooth katika hoteli ya Mount Meru iliyopo Arusha. Bia ya Guinness Smooth sasa itaanza kupatikana katika ukanda wote wa Kaskazini kwa shilingi 1,500 tu.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti wakiifurahia bia mpya ya Guiness smooth muda mfupi baada ya kuzinduliwa hivi karibuni jijini Arusha.

Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) imeendelea kupanua wigo wa bidhaa zake sokoni baada ya kuzindua bia mpya aina ya Guinness Smooth katika mikoa ya Moshi, Arusha, Manyara na Tanga.

Katika uzinduzi wa bia hiyo mpya, wateja wa kampuni ya SBL, wauzaji wake wa bia pamoja na wenye mabaa walipata nafasi ya kuonja na kufurahia ladha ya kipekee ya bia ya Guinness smooth

Akiongea wakati wa uzinduzi huo jijini Arusha, Meneja Uvumbuzi wa SBL Bertha Vedastus alisema “Bia hii mpya kwenye familia ya Guinness ina ladha ya kipekee ambayo inamfanya kila mnywaji afurahie kila mara anapoitumia na wakati akiwa na marafiki,” alisema

Bertha aliongeza “Ikiwa imetengenezwa kwa kumjali mnywaji wa Kitanzania, bia hii ina hadhi ya kimataifa na imetengenezwa katika kiwanda chetu cha moshi huku ikitumia malighafi za Kitanzania ikiwa ni Pamoja na shayiri inayolimwa katika mikoa ya Moshi, Arusha na mingineyo,”
 

Meneja uvumbuzi huyo aliongeza kuwa familia ya Guinnness Tanzania inayo furaha kuwaletea bia hiyo wakazi wa mikoa ya Kaskazini ambao siku zote wamekuwa waaminifu kwa bidhaa za SBL na kuongeza kuwa bia ya Guinness smooth itakuwa ikipatikana kwa shilingi 1,500 tu.

“Guinness inahistoria ndefu na kongwe ya kutengeneza bia bidhaa ambazo zimefanikiwa kuteka soko la dunia na kuendelea kuwa kinara. Bia hii ni muendelezo wa Guinness kuwaleta wateja wake bidhaa ambazo zinakidhi mahitaji yao na kuenda na wakati,” alisema

Baadhi ya wateja waliohudhuria uzinduzi na kuonja bia hiyo mpya walielezea kuvutiwa na ladha ya kipekee ya bia hiyo mpya na kusema kuwa watakuwa mabalozi wazuri.

“Bia ni nzuri na huu ni ujumbe kuwa ika kila sababu ya kufanya vizuri sokoni. Kwangu mimi kama msambazi wa bia naona ni fursa ambayo nitaitumia vyema kwa ajili ya kuweza kuongeza wigo wa wateja wangu Pamoja na kukuza biashara yangu pia,” aliongeza

No comments:

Post a Comment