“Mjasiriamali anatakiwa kufungua SimAccount kwa kupiga *150*62# na kisha kujisajili kutumia kitambulisho chake cha ujasiriamli, ambapo ataweza kunufaika na mkopo binafsi wa ‘Jiwezeshe’ au kupitia kikundi,” aliongezea Nsekela.
Nsekela alisema kwa kuzingatia mazingira ya biashara za wajasiriamali wamachinga, Benki ya CRDB imeachana na mpango wa kutoza riba kwa asilimia na badala yake mteja atatozwa kiwango kidogo cha kati ya shilingi 5,00 na 2,000 tu pindi arejeshapo mkopo.
“Tumefanya hivi ili kuwapunguzia mzigo wajasiriamali hawa wadogo, ili waweze kuwekeza zaidi faidi wanayoipata kupitia mikopo hii ya ‘Jiwezeshe’,” alisema Nsekela.
|
No comments:
Post a Comment