Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 16 March 2015

MH. WILLIAM LUKUVI AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA NYUMBA ZINAZOJENGWA NA NHC ENEO LA BUSWELU, MWANZA

Watendaji mbalimbali wa NHC na Manispaa ya Ilemela wakimpokea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili kuweka jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu, Mwanza.
Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC, Bw. Haikamen Mlekio akitoa maelezo kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi ya mradi wa nyumba za gharama nafuu unaotekelezwa na NHC eneo la Buswelu jijini Mwanza.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akikagua nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu Mwanza kabla ya kuweka jiwe la msingi mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC, Bw. David Shambwe akitoa maelezo kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi ya mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu Jijini Mwanza.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akihutubia wananchi (hawapo pichani) waliohudhuria uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za gharama nafuu unaotekelezwa na NHC eneo la Buswelu Jijini Mwanza. Katika hotuba yake amesema Serikali inakusudia kuondoa kodi ya VAT kwenye uuzaji wa nyumba mpya zinazojengwa na NHC ili kuzifanya nyumba hizo kuwa nafuu.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akiweka jiwe la msingi kwenye nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu Jijini Mwanza. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC Bw. David Shambwe aliyemuakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NHC.
Mafundi ujenzi nao walifurahia kwa kupata fursa ya kupiga picha ya pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipokutana nao wakati wa uwekaji jiwe la msingi eneo la Buswelu.

No comments:

Post a Comment