Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 31 March 2015

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MILIONI 10 UJENZI WA KANISA LA KKKT USHARIKA WA MATOSA

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Matosa Kimara jijini Dar es Salaam, Rabisante Lema akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei baada ya kukabidhi hundi ya sh. milioni 10 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miundombinu ya kanisa hilo wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa. Jumla ya shilingi milioni 50 zilipatikana katika harambee hiyo. (Picha na Francis Dande).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia) akimkabidhi hundi ya sh. millioni kumi Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Matosa Kimara jijini Dar es Salaam, Mhandisi Simon Kihunzi kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kanisa hilo, wakati wa harambee iliyofanyika kanisani hapo, ambapo jumla ya shillingi milioni 50 zilipatikana.
Godwin Semunyu akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charls Kimei baada ya kutoa mchango wake. Kulia ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Rabisante Lema.
Bofya hapa kwa picha zaidi

No comments:

Post a Comment