Blog Rebranding Teaser_030826

Blog Rebranding Teaser_030826

Stanbic Bank Banner_070826

Stanbic Bank Banner_070826

Absa Loan Campaign_160426

Absa Loan Campaign_160426

Friday, 17 June 2022

BENKI YA NMB YAKABIDHI VIFAA VYA USAFI - DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka (wa tatu kushoto) akipokea msaada wa vifaa vya kutunza taka kutoka kwa Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Juma Kimori vyenye nia ya kusaidia utunzaji wa Mazingira katika jiji la Dodoma. Wengine kwenye picha ni Naibu Meya wa Jiji la Dodoma - Emmanuel Chibago, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma - Dkt. Fatma Mganga, Afisa Mkuu Rasilimali watu - Emmanuel Akonaay na Mkuu wa Idara ya Huduma za serikali na Ofisi Ndogo za Makao Makuu Dodoma wa NMB - Vicky Bishubo.

Mkuu a Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka akiwa amebeba moja ya vifaa vya kuhifadhia taka vilivyotewa na Benki ya NMB yenye nia ya kusaidia utunzaji wa Mazingira katika jiji la Dodoma. NMB ilikabidhi vifaa 100 kwa ajili ya Mkoa wa Dodoma kwenye viwanja vya Nyerere square Jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka ameagiza Jiji la Dodoma kuharakisha sheria ndogo ndogo za mazingira ili kuweka hali ya usafi katikati ya Jiji hilo.

Mtaka alitoa agizo hilo Kwa Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Emmanuel Chibago wakati wa kupokea vifaa vya kuhifadhia taka vilivyotolewa na benki ya NMB ili kusaidia utunzaji wa mazingira.

"Siku ile tulipata aibu kubwa, niliamua kuandika kwa mkono wangu kuomba vifaa hivi kwa benki ya NMB na leo wameleta,sasa naagiza vikabidhiwe kwa maandishi ili kila mmoja awe na wajibu wa kutunza na kuvifanyia kazi," alisema Mtaka.

NMB wamekabidhi jumla ya mapipa 100 yenye thamani ya zaidi ya Sh20 milioni wakiahidi kuendeleza ushirikiano na mkoa ili kuweka mji katika hali ya usafi.

Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Juma Kimori alisema makabidhiano ya vifaa hivyo ni mipango ya benki hiyo katika kurudisha sehemu ya faida kwa wananchi baada ya kodi ambapo mwaka huu wametenga Sh.bilioni 2.9 ikiwa na ongezeko la 41% ukilinganisha na Sh.bilioni 2.05 za mwaka jana.

LIPIA KIFURUSHI CHAKO CHA DStv POA TSHS 9,900 TU



Endelea kufurahia msimu wa pili wa vipindi vyako pendwa ndani ya @dstvtanzania pekee kupitia chaneli yako pendwa ya Maisha Magic Poa, 144.
Ikiwemo Watubaki, Salama Na, Maskani Poa, Ya Walimwengu bila kusahau marudio ya Kapuni.

Hakikisha unalipia mapema kifurushi chako cha Poa TShs 9,900 tu kwa kupiga *150*53# uweze kufurahia vipindi hivi.

#DStvEwaaaaaah


 

Thursday, 16 June 2022

UBA BANK DONATES BOOKS IN CELEBRATION OF INTERNATIONAL DAY OF THE AFRICAN CHILD


June 16 every year has been set aside by the United Nations as the International Day of the African Child to celebrate children in Africa and in recognition of the courage of students who marched for their right to better education in Soweto, South Africa.


Since this day aims at raising awareness for the situation of children in Africa and highlights the need for continuous improvement in Education, United Bank for Africa Tanzania Limited (UBA), through its Read AfricaInitiative, joined the rest of the world to celebrate African children by donating literature books to Kurasini Secondary School in Dar es Salaam.


UBA Tanzania’s Head of Corporate Banking, Dora Kyungu, used the opportunity to explain what the ‘UBA Read Africa Initiative’ means and the role it plays in encouraging students across Africa to improve their vocabularies and communication skills through reading.


UBA is a global Africa bank with presence in 20 African countries, the United Kingdom, the United States of America and France. The bank recognizes how the reading culture is critical to the future of our African children and the continent as well. All children were encouraged inculcate the habit of reading and read the donated books to enrich their bank of vocabularies to enhance their learning abilities.


After receiving the books, the headmaster of Kurasini Secondary School, Amry Jaribu Fundi, acknowledged thekind gesture of United Bank for Africa Tanzania Limited (UBA) for supporting quality education across in Tanzania. He urged the students to take full advantage of the donated books to increase their knowledge and continue to build a reading habit.


The Head Girl of the school, Sonia Madaha, expressed her sincere gratitude on behalf of other students and promised to continue to lead by example by reading a lot more.


UBA has an impeccable track record of supporting the communities where it operates.



BENKI YA NMB YAKABIDHI BILIONI 30.7 GAWIO KWA SERIKALI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango (wa tatu kulia) akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 30.7 kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB - Ruth Zaipuna (wa tatu kushoto) ikiwa ni gawio kwa Serikali katika hafla iliyofanyika Jijini Dodoma. Wengine ni Waziri wa Fedha na Mipango - Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (wa pili kulia), Afisa Mkuu wa Fedha NMB(kushoto), Juma Kimori na wapili toka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NMB, Dkt. Edwin Mhede.

Benki ya NMB imekabidhi Shilingi Bilioni 30.7 kwa Serikali huku Makamu wa Rais, Mhe. Dkt Philip Isdor Mpango akisema benki hiyo imefanya siku yake na Serikali nzima kuwa yenye furaha.

Makamu wa Rais alitoa kauli hiyo kufuatia agizo lake kwa benki hiyo mwaka jana kipindi kama hiki alipopokea gawio la Sh Bilioni 20.8 ikiwa ni faida ya 2020 na kutaka waongeze nguvu na ubunifu ili waje na gawio nono.



Gawio hilo limetolewa ikiwa ni faida ya NMB kwa mwaka wa fedha ulioishia 2021 ambapo jumla ya Shilingi Bilioni 97 zilipitishwa na mkutano mkuu wa wana hisa wa Benki ya NMB kutolewa kwa wanahisa kama gawio. Serikali ikiwa inamiliki hisa 31.8%, imepokea shilingi Bilioni 30.7 kama gawio lake kutoka benki ya NMB ikiwa ni ongezeko la 40% ukilinganisha na mwaka jana.

Kwa gawio hilo, Benki ya NMB ndani ya kipindi cha miaka mitano inakua imetoa jumla ya Shilingi Bilioni 80.544 kwa Serikali.



Akipokea mfano wa hundi ya kiasi hicho, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango alisema benki hiyo imeendelea kuiheshimisha Serikali kwa kuonyesha namna gani inavyokuwa kimtaji na kuwajali wateja wake.

“Hata nitakapokwenda kumpokea Mheshimiwa Rais, hili litakuwa ni jambo la kwanza kumuambia, moyo wangu umeburudika sana, mmenifurahisha sana nasema hongereni sana,” alisema Dkt. Mpango.

Akitoa taarifa yake kwa Makamu wa Rais, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna alisema faida ya Benki baada ya kodi katika kipindi cha 2021 iliongezeka kwa asilimia 41 hadi kufikia Shilingi Bilioni 290.



Kiasi hicho ni kikubwa ukilinganisha na Shilingi Bilioni 206 ya mwaka 2020 ambapo idadi ya akaunti za wateja iliongezeka hadi kufikia Milioni tano ikilinganishwa na milioni nne za 2020.

Wednesday, 15 June 2022

GEITA GOLD FC VISITS GGML FUNDED PROJECTS IN GEITA

From left to right: Stephen Mhando, Public Relations and Communications Manager at GGML; Manace Ndoroma, Senior Manager - Partnerships at GGML; Mamoudou Berete, ASM Superintendent of AngloGold Ashanti, Siguiri, Guinea, and Regina Mabula, Social Economic Development Officer at GGML inspect the progress at the Geita Town Football Stadium.
Geita Gold Football Club Head Coach Fred Felix ‘Minziro’ and Manace Ndoroma, Senior Manager - Partnerships at GGML pictured at EPZA ahead of a tour of some of Geita Gold Mining Limited’s CSR projects.
The Geita Gold Football Team poses for a joint photo with the Moyo wa Huruma children, GGML staff and Geita Town council officials.

Geita Gold Football Club, a team funded by Geita Gold Mining Limited (GGML), on 9 June 2022 visited company - funded community projects within Geita Town Council.

Speaking during the team's visit, GGML's Senior Partnerships Manager, Manace Ndoroma said that in addition to providing sponsorship of 500 million Tanzanian shillings to the team, they have decided to invite the team to see the Company’s investments in the Geita community.

"We are very delighted to be the main sponsors of Geita Gold Football Club because their efforts to rise to the top echelons of the premier league have awakened sporting momentum within our Geita region. This team has become a solid ambassador for the Company, Town of Geita as well as our region as a whole,“ said Mr. Ndoroma.

Geita Gold Football Club Chief Executive Officer, Simon Shija commended GGML for continuing to benefit the Geita community through various development projects.

"Many people praise our team for doing well in the league standing, but the secret behind our success lies in the support of various stakeholders including GGML whom, in addition to being the main sponsor, are building a modern football stadium in Geita.

WAFANYAKAZI WA JOHARI ROTANA WACHANGIA DAMU

Ikiwa Juni 14 ya kila mwaka huadhimishwa siku ya wachangia damu duniani, wafanyakazi wa Hoteli ya Johari Rotana ya jijini Dar es Salaam wamechangia damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kuhakikisha wanaokoa maisha ya watu.






KAA TAYARI KWA WOMEN'S AFRICA CUP OF NATIONS

 


Soka linaendelea!

Kaa tayari kwa Women's Africa Cup Of Nations (AWCON) itakatoanza Julai 2 - 23 Julai 2022, huku ukipata kutazama Live mechi hizi kupitia chaneli za SuperSport.

Jiunge na @dstvtanzania kupitia ofa yao ya TShs. 59,000/= tu kwa kupiga simu 0659 07 07 07.

#DStvEwaaaaah

HERO MOTOCORP YAKABIDHI PIKIPIKI KWA JESHI LA POLISI

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo.

Dar es Salaam, 14th June 2022 - Kampuni ya Hero Motocorp ni moja kati ya watengenezaji wakubwa wa pikipiki za magurudumu mawili duniani, sasa nchini Tanzania chini ya kampuni tanzu ya Karimjee Jivanjee Ltd (KJL), imekabidhi msaada wa pikipiki tano za Hero Hunter 125cc kwa jeshi la polisi Tanzania katika hafla iliyofanyika kwenye showroom ya Hero hapo mjini.

Meneja Mkuu wa Karimjee Jivanjee Ltd, William Kadiva alitaja “Karimjee Jivanjee Limited ni biashara ya familia ya karne ya 21 inayoendeshwa na historia na mwongozo wa huduma bora, watu, wateja, washirika, jamii na biashara. Karimjee Jivanjee kwa sasa inaendesha shughuli zake katika sekta tano za biashara: Usafiri, Nishati, Huduma za Kifedha, Ukarimu na Mtaji.

Kutoka kulia - General Manager wa Karimjee Jivanjee, William Kadiva, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, ACP Richard Michael Ngole. 

Aliongeza Bw William Kadiva “tuna chapa nne chini ya mwamvuli wa Karimjee Mobility, Hero Moto corp ikiwa mojawapo ya chapa tanzu. Karimjee Mobility ilichukua jukumu la kusambaza pikipiki za Hero mwishoni mwa mwaka 2021 na hadi sasa imefanikiwa kufungua matawi 2 na kuunda mtandao wa wafanyabiashara zaidi ya 20 walioidhinishwa kote Tanzania”

Akitoa maelezo wakati wa uchangiaji huo wa pikipiki kwa mapolisi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo alisema “Pikipiki hizi za Hero zitawawezesha askari polisi kuweka ufuatiliaji katika maeneo yao na pia kuimarisha ulinzi kwa ujumla.



Naye OCD wa Chango’mbe Ariziki Mohammed Mkwaya ambaye alipokea pikipiki hizo kwa niaba ya jeshi la polisi pia alitoa pongezi kwa Meneja Mkuu wa shujaa William Kadiva na kueleza kuwa msaada huo utasaidia kuwapa motisha askari katika maeneo tofauti.

NMB TELEZA KIDIJITALI KUZINDULIWA SHINYANGA

Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magesse, akizungumza na wamachinga kuhusu faida za kampeni ya Teleza kidijitali iliyozinduliwa wilayani Kahama katika stendi ya mabasi CDT.
Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magesse (kulia) na Meneja wa NMB Tawi la Kahama, Gadiel Sawe wakipeperusha bendera hewani ikiwa ni ishara ya kuzindua kampeni ya Teleza Kidijitali iliyozinduliwa wilayani Kahama katika stendi ya mabasi CDT mkoani Shinyanga.
Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magesse (kulia) na Meneja wa NMB Tawi la Kahama, Gadiel Sawe (kushoto), wakizungumza na mamalishe kuhusu faida za kampeni ya Teleza Kidijitali.

Baada ya kuchanja mbuga mtaa kwa mtaa katika Mkoa wa Dar es Salaam na Arusha, sasa Benki ya NMB imefika Mkoa wa Shinyanga kuzindua kampeni ya 'Teleza Kidijitali' katika mikoa ya Kanda ya Magharibi.

Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya CDT Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Meneja wa Kanda ya Magharibi wa NMB, Sospeter Magesse alisema kampeni ya 'Teleza kidijitali' imeanzishwa hivi karibuni kuwaelimisha Watanzania umuhimu wa huduma zilizo chini ya kampeni hio, ambazo ni NMB Pesa Wakala, Lipa Mkononi na Mshiko Fasta.

"Kupitia huduma ya Teleza kidijitali, pia inamuwezesha mteja kufungua akaunti mara moja na kuunganishwa na huduma za NMB Mkononi papo hapo bila mahitaji ya vigezo vingi vya usajili" alisema Magesse.

Tuesday, 14 June 2022

TAARIFA YA HALI YA UCHUMI NA MPANGO WA MAENDELEO WAWASILISHWA BUNGENI

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiwasilisha Bungeni jijini Dodoma, Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kushoto) na Naibu wake, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) wakifurahia jambo baada ya kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.
Naibu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) akijibu swali bungeni jijini Dodoma, kabla ya kuwasilishwa kwa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.
Viongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Emmanuel Tutuba (kushoto), wakifuatilia uwasilishaji wa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, akifurahia jambo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) baada ya kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Lawrance Mafuru, baada ya kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.
Naibu wa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akiteta jambo na Manaibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Jenifa Omolo (kushoto) na Bi. Amina Khamis Shaaban (katikati) katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma.
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb), akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, baada ya kuwasilishwa kwa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, bungeni jijini Dodoma.

BENKI YA DCB YASHEREHEKEA MIAKA 20 YA MAFANIKIO IKIZIDI KUTOA FURSA ZA KIUCHUMI KWA WATANZANIA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati), aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa benki hiyo, Edmund Mkwawa (kulia), Katibu Muhtasi wa benki hiyo, Judith Maeda, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa, Mhasibu wa Tawi wa benki hiyo, Prisca Dona, Ofisa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Rosemary Masaga na Mwenyekiti wa Bodi Mstaafu wa benki hiyo, Prof. Lucian Msambichaka wakipiga picha ya kumbukumbu wakati wa Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omar Kumbilamoto (kulia) akisalimiana na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Hanifa Suleiman Hamza na Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (kushoto) akipokea tuzo ya shukrani ya Hayati Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ya huduma bora ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Uanzishwaji wa DCB ilikuwa moja ya ndoto za hayati Mkapa katika kuwasaidia wafanyabiashara ndogondogo waliokosa vigezo vya kupata mikopo ya mitaji kupitia mifumo rasmi ya kibenki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati) akikabidhi tuzo ya shukrani kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa benki hiyo, Edmund Mkwawa wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati) akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Mwenyekiti wa Bodi Mstaafu wa benki hiyo, Prof. Lucian Msambichaka wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa Katibu Muhtasi wa benki hiyo, Judith Maeda wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa Ofisa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Rosemary Masaga wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro (katikati) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa Mhasibu wa Tawi wa benki hiyo, Prisca Donati wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo na waalikwa wengine wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 20 ya huduma bora ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zoro akitumbuiza wakati wa Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.