Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 15 October 2024

DKT. NCHEMBA AKUTANA NA UMOJA WA MABENKI TANZANIA (TBA)

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) akizungumza katika kikao chake na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), ofisini kwake jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma za fedha jumuishi. Kushoto ni Mwenyekiti wa TBA, Bw. Theobald Sabi.
Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Bw. Theobald Sabi, akizungumzia mchango wa Sekta ya Benki nchini katika kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Taasisi hiyo, jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma jumuishi za kifedha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiongoza kikao kati yake na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba akifafanua jambo katika kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, akielezea namna ambavyo Serikali kupitia Benki hiyo imekuwa ikisimamia Sekta ya Benki nchini wakati wa kikao kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma.
Na. Benny Mwaipaja, Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), jijini Dodoma, ambapo walijadili kuhusu mchango wa Sekta ya Benki katika uchumi wa nchi kupitia huduma jumuishi za kifedha. 

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, wakati ujumbe wa TBA uliongozwa Mwenyekiti wake, Bw. Theobald Sabi.

No comments:

Post a Comment