Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 6 May 2024

JINSI YA KUNUFAIKA NA MIKOPO YA WAJASIRIAMALI KUPITIA BENKI YA NMB


Benki ya NMB imeingia makubaliano ya miaka miwili na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa ajili ya kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wafanyabiashara ndogo ndogo kupitia Benki ya NMB.

Kupitia makubaliano haya:
  • Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 18.5 zitakazokopeshwa kwa wafanyabiashara ndogo ndogo kupitia Benki ya NMB, kwa masharti nafuu, na kwa riba ndogo ya 7% tu.
  • Mikopo hii itakopeshwa kwa wafanya biashara ndogo ndogo waliosajiliwa, na kutambulishwa kwa Benki ya NMB na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.
  • Kabla ya kuidhinisha mikopo hii, Benki ya NMB itajiridhisha kwa kuwatembelea wafanya biashara hawa katika maeneo yao, ili kuhakikisha mikopo inawafikia walengwa waliokusudiwa.
  • Mfanyabiashara atakopeshwa kulingana na mahitaji ya biashara anayoifanya.
  • Benki ya NMB kwa kushirikiana na Wizara, itahakikisha wanufaika wanapatiwa elimu ya kifedha, ili kuwajengea nidhamu ya matumizi ya fedha hizi katika kutimiza malengo yaliyokusudiwa na kuweza kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.
Makubaliano haya yamesainiwa leo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB - Bi. Ruth Zaipuna na Katibu Mkuu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum - Dkt. Seif Shekallaghe, na kushuhudiwa na Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima - Waziri katika wizara hiyo.

Kunufaika na mikopo hii, tembelea tawi lolote la NMB lililo karibu nawe.

No comments:

Post a Comment