Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 24 July 2023

WAZIRI MKUU AIPONGEZA NBC KWA KUSAIDIA AFYA YA UZAZI

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (wa pili kushoto) akishiriki katika mbio za NBC Dodoma Marathon 2023 pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Theobald Sabi (wa pili kulia). Wengine wa kwanza kulia ni mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule na kushoto ni mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri. Mbio za mwaka huu zimefanikiwa kukusanya shilingi milioni 500 zitakazotumika kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na afya ya uzazi kwa wanawake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akimpongeza Waziri wa Utamaduni. Sanaa na Michezo Pindi Chana baada ya kushiriki mbio za NBC Dodoma Marathon 2023. Wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Theobald Sabi. Mbio za mwaka huu zimefanikiwa kukusanya shilingi milioni 500 zitakazotumika kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na afya ya uzazi kwa wanawake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimvisha medali mmoja wa washindi wa NBC Dodoma Marathon 2023. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Pindi Chana (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Theobald Sabi. Mbio za mwaka huu zimefanikiwa kukusanya shilingi milioni 500 zitakazotumika kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na afya ya uzazi kwa wanawake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wadhami ni wa NBC Dodoma Marathon 2023 pamoja na viongozi wa Benki ya NBC na viongozi wa mkoa wa Dodoma muda mfupi baada ya kumalizika kwa mbio hizo. Mbio za mwaka huu zimefanikiwa kukusanya shilingi milioni 500 zitakazotumika kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na afya ya uzazi kwa wanawake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (wa nne kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 107 kwa Taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation. Fedha hizo ni sehemu ya fedha zilizopatikana kutokana na mbio za NBC Dodoma Marathon 2023 na zitakwenda kufadhili mafunzo ya wakunga ili kuongeza wataalamu watakaosaidia kuokoa vifo vinavyotokana na uzazi kwa akina mama.

Dodoma, Julai 23, 2023: Waziri Mkuu wa Jamuhuri wa Muunngano wa Tanzania Kassim Majaliwa, ameipongeza Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kuandaa mbio za NBC Marathon ambazo zinalenga kukusanya fedha kwa ajili ya kusaidia afya ya uzazi na saratani ya shingo ya kizazi.

Akiongea muda mfupi baada ya mbio hizo kumalizika jijijini Dodoma, Waziri Mkuu alisema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa sekta binafsi katika kuiunga mkono kwenye kutatua changamoto mbali mbali zinazoikabili jamii.

“Serikali inathamini mchango mkubwa unaotolewa na benki ya NBC. Tunafurahishwa na ushirikiano mzuri kati ya Taasisi ya Kansa ya Ocean Road, Taasisi ya Benjamini Mkapa pamoja na Chama cha Riadha Tanzania ambao umekuwa ukiwezesha kukusanya fedha kwa ajili ya kusaida mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na mwaka huu likiongezeka eneo la afya ya uzazi. Serikali inapongeza jitihada hizi nzuri,” alisema

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya NBC Theobald Sabi alisema baada ya kumalizika kwa mbio z mwaka huu, benki hiyo inayo furaha kuandaa mbio za mwaka ujao ikiwa ni baada ya kuandaa mbio hizo kwa mara tatu mfululizo kwa ufanisi.

“Baada ya kuandaa mbio hizi kwa mara ya nne mfululizo, tunayo furaha kuanza maandalizi ya msimu wa nne. Fedha zilizopatikana leo shilingi milioni 500 zitatumika kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi,” alisema

Aliongeza “Tunaendelea na jitiahada za kuunga mkono mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi. Mpaka sasa tumefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi milioni 500 zilizosaidia kufikia upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake zaidi ya 23,500 na matibabu kwa zaidi ya wanawake 1,300. Benki ya NBC inawapongeza na kuwashuru washiriki wote kutoka nje na ndani ya nchi kwa kuweza kufanikisha mbio za mwaka huu.

No comments:

Post a Comment