Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 12 October 2022

NBC YATOA MSAADA WA MADAWATI, MIFUKO YA SARUJI ILI KUBORESHA ELIMU MKOANI MWANZA

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala (kulia) akipokea msaada wa madawati 50 kutoka kwa Meneja wa benki ya NBC Tawi la Mwanza, Thomas Lijaj (kushoto) ikiwa ni msaada kutoka benki ya Benki ya NBC tawi la Mwanza katika kusaidia jitihada za wilaya hiyo kukabiliana na changamoto ya uhaba wa madawati wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika mkoani humo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Maofisa waandamizi kutoka wilaya hiyo pamoja na benki hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala (katikati) akiwa ameketi sambamba na baadhi ya wanafunzi kutoka wilayani humo kwenye moja ya madawati yaliyotolewa na benki ya NBC tawi la Mwanza katika kusaidia jitihada za wilaya hiyo kukabiliana na changamoto ya uhaba wa madawati wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika wilayani humo.

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) tawi la Mwanza imetoa msaada wa mifuko ya saruji 200 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Samia iliyoko wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza sambamba na msaada wa madawati 50 kwa ajili ya shule za Msingi zilizopo wilayani Ilemela mkoani humo ikiwa ni hatua ya benki hiyo katika kuunga mkono juhudi za serikali pamoja na wananchi katika kuboresha elimu wilayani humo.

Akizungumza kwenye hafla za kukabidhi misaada hiyo, Meneja wa benki ya NBC Tawi la Mwanza Bw Thomas Lijaj alisema misaada hiyo inalenga kuunga mkono jitihada ambazo tayari zinaendelea kuonyeshwa na serikali pamoja na wananchi katika maeneo husika kwa kuboresha miundombinu ya elimu.

Maofisa waandamizi wa Benki ya NBC tawi la Mwanza wakiongozwa na Meneja wa tawi hilo, Thomas Lijaj (kulia) wakikabidhi stakabadhi ya malipo ya manunuzi ya mifuko ya saruji 200 kwa Mkuu wa Wilaya ya Ngamagana Bi Amina Makilagi (wa pili kushoto) kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule ya Msingi Samia iliyopo wilayani humo.


“Tunaamini kwamba mifuko ya saruji pamoja na madawati tuliyoikabidhi katika halmashauri hizi mbili zitasaidia kuunga mkono jitihada ambazo tayari zipo katika kutatua changamoto zilizopo za uhaba wa vyumba vya madarasa na madawati katika shule husika. Lengo ni kuwasaidia wanafunzi wapate mazingira bora zaidi ya kujifunzia,’’ alisema Bw Lijaj.



Aliipongeza serikali kwa jitihada inazoendelea kuzionesha katika kuboresha elimu hapa nchini huku akibainisha kuwa benki ya NBC kama mdau muhimu wa maendeleo itandelea kuunga mkono jitiha hizo huku lengo likiwa ni kuongeza kasi ya maendeleo katika sekta hiyo muhimu.


Viongozi waandamizi wa Wilaya ya Ilemela wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala (kulia) wakikagua madawati hayo.

“Lengo letu ni kuhakikisha ndoto za watoto hawa kielimu zinafikiwa na pia kumuunga mkono Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassani katika utoaji wa elimu bora. Kwa hiyo tumekabidhi madawati na mifuko ya saruji kwa ajili ya wanafunzi hawa kwa kuwa ni furaha ya NBC kuona watoto wanaondokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili hasa katika swala la elimu” aliongeza Bw Lijaj.
Viongozi waandamizi wa Wilaya ya Ilemela wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala (katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa wa benki ya NBC tawi la Mwanza pamoja na baadhi ya wanafunzi na walimu kutoka wilayani humo.


Wakizungumza mara baada ya kupokea misaada hiyo Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bi Amina Makilagi na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Bw Hassan Masala pamoja na kuishukuru benki hiyo kwa msaada huo walisema serikali imejipanga kuhakikisha inamaliza changamoto za kielimu kupitia mipango yake mbalimbali sambamba na kushirikiana na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kifedha.

“Msaada huu umekuja wakati muafaka kwasababu tunahitaji madawati kwa ajili ya wanafunzi watakaonza masomo mapema mwakani…tunawashukuru sana benki ya NBC kwa kutuunga mkono kwenye hili.’’ Alisema Bw Masala.
Muonekano wa madawati yaliyotolewa na Benki ya NBC tawi la Mwanza kwa ajili ya shule za Msingi zilizopo wilayani Ilemela mkoani humo ikiwa ni hatua ya benki hiyo katika kuunga mkono juhudi za serikali pamoja na wananchi katika kuboresha elimu wilaya humo.

Kwa upande mmoja wa wakuu wa shule hizo Bw Mbita Samson ambae ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Samia aliishukuru benki ya NBC kwa namna ilivyoguswa katika kuchangia sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa na msaada wa madawati kwa kuwa jitihada hizo zimekuwa zikisaidia kuongeza kasi ya serikali na wanachi wanaojitolea kuboresha utoaji wa elimu hapa nchini.

“Binfasi nimefarijika sana kwa msaada huu kutoka NBC na kwa kweli bado tunahitaji wadau wengine wajitoe kusaidia kama walivyofanya benki hii. Hii leo tumepokea msaada huu mifuko ya saruji itakayotusaidia sana kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa hivyo tunawashukuru sana kwa kuunga mkono jitihada za wananchi na serikali yetu…asanteni sana NBC,’’ alisema Bw Mbita.

No comments:

Post a Comment