Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 5 October 2020

BENKI YA NCBA YAFUNGUA MATAWI MAWILI MAPYA MKOANI MWANZA

Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa benki ya NCBA, Bi Margaret Karume.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza aitaka Benki ya NCBA kusaidia kwenye pamba, uvuvi, madini, viwanda, nishati na ufugaji


Mwanza - NCBA Bank Tanzania Limited (NCBA) ilisheherekea hatua nyingine ya kihistoria ya ujio wake nchini kwa kuzindua matawi mengine mawili mapya mkoani Mwanza mnamo tarehe 2 Oktoba. Matawi haya yanapatikana Plot No 5 – Barabara ya Nyerere Road na Jengo la Kauma – Barabara ya Kenyatta.

Hafla hii ni kati ya sherehe zinazoendelea za ujio wa Benki ya NCBA ambayo ni muunganiko wa hiari kati ya NIC Bank (T) Limited na CBA Bank (T) Limited ambapo huduma rasmi za taasisi hii mpya zilianza tarehe 8 Julai 2020 baada ya idhini ya Benki Kuu ya Tanzania.

Uzinduzi huo ulianza kwa matembezi yenye nderemo na shangwe wakitamka kauli yao mbiu iitwayo GOR FOR IT kutoka kwa wafanyakazi wa NCBA kwenye mitaa na barabara ya jiji la Mwanza kutoka tawi lao lililopo kitalu namba 5 – Barabara ya Nyerere Road hadi jengo la Kauma – Barabara ya Kenyatta na baadae kukafanyika hafla ya jioni kuhitimisha uzinduzi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza aliekuwa Mgeni Rasmi katika matukio yote mawili alitoa wito wake kwa benki ya NCBA kwa kuelezea sekta muhimu za uchumi mkoani Mwanza wenye idadi ya watu takriban milioni moja. Alikaririwa akisema, ‘…pia tunajivunia rasilimali watu kwani Mwanza ni mji wa pili kwa ukubwa nchini Tanzania wenye takriban watu milioni 1. Ni moja wapo ya miji inayokuwa kwa kasi kubwa zaidi kutokana na fursa, rasilimali na shughuli za kiuchumi katika sekta zote nilizo-zitaja, iwe madini, kilimo, mifugo, uvuvi na viwanda’.

‘Mwanza inategemea sana shughuli za uvuvi, ambayo inaongoza kwa mapato ya fedha ikiwemo zile za kigeni. Jiji hili ni makao ya viwanda 13 vya kusindika samaki zenye uwezo wa kusindika karibu tani 1,065 za samaki kwa siku, hivyo kutoa mchango mkubwa unaomarisha uchumi wa mkoa huu kwa kutoa ajira mbali mbali kwa wananchi’.

Mkuu wa Mkoa aliendelea kusisitiza kuhusu umuhimu wa kusaidia maendeleo ya sekta ya biashara kwa viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Alisema, ‘Ni imani yetu kuwa Benki ya NCBA kama taasisi ya fedha itakuwa moja ya washirika bora, watakaowezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa kusonga mbele katika hatua mpya ya maendeleo na kukuza pato la Taifa’.

Halikadhalika, Mkuu wa Mkoa hakusita kuipongeza benki ya NCBA kwa ujio wao wa kihistoria kwenye Mkoa huo na Taifa kwa ujumla. Alisikika akisema, ‘Ujio wenu kama benki mpya utasaidia sana kuanzisha na kukuza miradi mipya pamoja na kutoa programu mpya za kifedha zitakazokuza uwezo wa kiuchumi wa watu wa Mwanza na kuleta thamani zaidi katika vipaumbele vya uchumi na shughuli za uzalishaji katika mkoa wa Mwanza’.

Mkurugenzi Mkuu na Afisa Mkuu Mtendaji wa benki ya NCBA, Bi Margaret Karume aliwahakikishia wadau, wageni na wateja kuwa Benki inatoa huduma bora za kiwango cha kimataifa mahali popote walipo. Alisema, ‘Ninayofuraha ya kuwa-ha-ki-kishia wateja wetu wote kuwa wapo huru kutembelea tawi lolote lile la NCBA Bank ili kupata huduma zile zile bora kwa kiwango cha kimaitaifa, iwe hapa Mwanza ama katika miji mingine au visiwani Zanzibar. Pia, kufuatia muunganiko wetu, wateja wana uhuru na urahisi wa kutumia mashine yoyote ile ya ATM yenye nembo ya NCBA Bank ukiwa Mwanza, Arusha, Zanzibar, Dar es salaam ama katika nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda, na Ivory Coast’.

Bi. Margaret Karume, alimshukuru Mkuu wa Mkoa pamoja na waheshimiwa wageni waalikwa kwa utayari wao wa kuiunga mkono Benki ya NCBA. Margaret Karume alisisitiza umuhimu kwa Benki ya NCBA kuunga mkono mageuzi ya kiuchumi ya Mkoa wa Mwanza na Taifa kwa ujumla. Alisema, ‘Benki ya NCBA inaleta kwa pamoja ubora wa dunia mbili. Kuchanganya nguvu za taasisi mbili za awali zinaifanya benki ya NCBA kuwa benki kubwa na yenye nguvu kifedha, yenye utaalam na uwezo mkubwa unaowa-weka wateja wake mstari wa mbele katika safari yao ya mafanikio.

‘Kama benki kubwa na imara, benki ya NCBA itahakikisha tunawashika mkono wateja wetu na kutoa huduma za kipekee za kifedha zitakazo-wawe-zesha katika safari yao ya mafanikio. NCBA ni benki inayokuhudumia vilivyo leo, kwa ajili ya mafanikio yako ya kesho’.

Alimalizia kwa kusema, ‘Katika kuwahudumia wateja wetu na kufikia matarijio ya maendeleo ya kiuchumi hapa Mwanza, tunatarajia kuwa na mazungumzo ya kina na wateja wetu pamoja na wadau mbalimbali wa biashara na mandeleo ili kutengeneza mikakati imara itakayo-kidhi malengo yetu ya kuhamasisha kila mmoja kufikia malengo’.

Uzinduzi wa matawi haya mawili mkoani Mwanza ni miongoni mwa matawi 12 mapya ya Benki ya NCBA kote nchini baada ya uzinduzi wa Makao Makuu na Tawi Kuu mkoani Dar es Salaam mnamo tarehe 19 Agosti 2020, iliyofuatiwa na uzinduzi wa matawi mawili jijini Arusha mnamo tarehe 19 Septemba na tawi moja visiwani Zanzibar tarehe 26 Septemba.

Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana na;

NCBA BANK TANZANIA LIMITED

Caroline Maajabu Mbaga
Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uraia;
Barua Pepe: caroline.mbaga@ncbagroup.com
Simu: +255 (22) 2295000 / DL: +255 768 987008

Let’s GO FOR IT!

ABOUT NCBA BANK (T) LTD

NCBA Bank (T) Limited is a result of the merger of NIC Bank (T) Limited and CBA Bank (T) Limited. The merger follows through the successful acquisition of the majority of the assets and all of the liabilities of CBA by NIC. The Notice of Transfer of Assets and Liabilities was published in the Government Gazette on 17th January 2020 (as GN No.48) and in leading local newspapers. The Notice of Transfer of Assets and Liabilities was issued in line with section 4 of the Transfer of Businesses (Protection of Creditors) Act, Cap 327 R.E 2002.

The issuance of a banking license by The Bank of Tanzania paves the way for the two organizations to start operating as NCBA Bank (T) Ltd officially.

The merger creates one of the largest financial services groups in the region, a bank with the financial strength, expertise, and regional reach to support Tanzania and the regions’ economic growth aspirations. The group is strongly placed to play a bigger and more significant role in the banking sector and economies of Tanzania, the region and beyond.

It brings together the best in class retail and corporate banks with strong potential for growth in all aspects of banking and wealth management.

The merged entity will be a Universal Bank suitable and relevant for a wide demographic of customers, providing a full range of financial products and services for corporate, institutional, SME and consumer banking customers, who will benefit from strong relationship management and customer service excellence.

A proudly African Bank operating as an international bank with global standards, NCBA Bank is;

• One of the largest banks by customer numbers in Africa with a complementary base of over 40 million customers across Africa and the region, a strong digital proposition and a robust corporate and asset finance offering. NCBA Bank currently has 12 branches in Tanzania in Dar es Salaam, Arusha, Mwanza and Zanzibar.

• Amongst the largest financial institutions in the East Africa region and the 3rd largest Bank in Kenya with a total asset base over KES 444 Billion (Tsh 9,324bn) and Shareholders’ Equity of KES 65 Billion (Tsh 1,365).

No comments:

Post a Comment