KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YADHAMINI MBIO ZA KUHAMASISHA UTUNZAJI MAZINGIRA WILAYANI SERENGETI
Baadhi ya washiriki wa mbio za Serengeti Migration Marathon wakikimbia katika mbio hizo zilizodhaminiwa na kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) pamoja na makampuni mengine kwa ajili ya uhamasishaji wa utunzaji wa mazingira. Mbio hizo zilifanyika hivi karibuni wilayani Serengeti mkoani Mara.
Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu (wa sita kulia) akizungumza muda mfupi kabla ya uzinduzi wa mbio za Serengeti Migration Marathon. Mbio hizo zilidhaminiwa na kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) pamoja na makampuni mengine kwa ajili ya uhamasishaji wa utunzaji wa mazingira. Mbio hizo zilifanyika hivi karibuni wilayani Serengeti mkoani Mara.
Klabu ya wakimbiaji kutoka kanda ya ziwa, wakishangilia baada ya kufanikiwa kumaliza mbio za Serengeti Migration Marathon.
No comments:
Post a Comment