Foreign Exchange Rates

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

Friday, 31 January 2025

BENKI YA NBC YAKABIDHI BMW X1 KWA MSHINDI WA KAMPENI KARIAKOO

Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Biashara wa benki ya NBC Bw Joseph Lyuba (kushoto) akikabidhi kadi ya gari kwa Bw Darius Kweka ambae ni mfanyabiashara mdogo ‘Machinga’ kwenye Soko la Kariakoo jijini Dar es salaam alieibuka mshindi wa zawadi ya gari aina BMW X1 kupitia kampeni ya ’Shinda mechi zako Kinamna yako’ inayoendeshwa na NBC wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya zawadi hiyo sambamba na kuhitimisha kampeni hiyo iliyofanyika tawi la NBC Kariakoo jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni Mke wa Bw Kweka Bi Miriamu Kwema (wa pili kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Vipaji na Mafunzo wa NBC Bi Priscilya Othman (kulia).
Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Biashara wa benki ya NBC Bw Joseph Lyuba (kushoto) akikabidhi ufunguo wa gari kwa Bw Darius Kweka ambae ni mfanyabiashara mdogo ‘Machinga’ kwenye Soko la Kariakoo jijini Dar es salaama alieibuka mshindi wa zawadi ya gari aina BMW X1 kupitia kampeni ya ’Shinda mechi zako Kinamna yako’ inayoendeshwa na NBC.
Mfanyabiashara kwenye Soko la Kariakoo jijini Dar es salaama Bw Darius Kweka ambae ni mshindi wa zawadi ya gari aina BMW X1 kupitia kampeni ya ’Shinda mechi zako Kinamna yako’ inayoendeshwa na NBC akionesha funguo za gari hiyo baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Biashara wa benki ya NBC Bw Joseph Lyuba (kushoto). Wengine ni Mke wa Bw Kweka Bi Miriamu Kwema (wa pili kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Vipaji na Mafunzo wa NBC Bi Priscilya Othman (kulia).
Balozi wa Benki ya NBC, Bw Conrad Kennedy, maarufu kwa jina ‘Coy Mzungu’ (katikati) akikabidhi ufunguo wa gari kwa Bw Darius Kweka ambae ni mfanyabiashara mdogo ‘Machinga’ kwenye Soko la Kariakoo jijini Dar es salaama alieibuka mshindi wa zawadi ya gari aina BMW X1 kupitia kampeni ya ’Shinda mechi zako Kinamna yako’ inayoendeshwa na NBC. Wengine ni Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Kariakoo Bw Mohamed Tegalila (kushoto).

Dar es Salaam - Januari 31, 2025: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imehitimisha rasmi kampeni yake ya ’Shinda mechi zako Kinamna yako’ kwa kukabidhi zawadi ya gari ya pili aina BMW X1 kwa Bw Galus Peter Casto maruufu kama “Kweka” ambae ni mfanyabiashara mdogo ‘Machinga’ kwenye Soko la Kariakoo jijini Dar es salaama alieibuka mshindi wa zawadi hiyo kuu.


Kampeni hiyo iliyolenga kuchochea ukuaji wa uchumi miongoni mwa wateja wa benki hiyo kupitia uwekaji wa akiba, ilizinduliwa April mwaka jana ambapo pamoja na kutoa gari aina BMW X1 mbili kwa washindi wakuu pia ilitoa fursa kwa wateja hao kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu, simu za mikononi, ‘laptops’, friji, ‘tablets’ za watoto, bima za afya pamoja na majiko ya kisasa ya kupikia.


Hafla ya makabidhiano ya zawadi hiyo imefanyika mapema leo kwenye tawi la Benki ya NBC Soko la Kariakoo ikiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Biashara wa benki hiyo Bw Joseph Lyuba pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo akiwemo Meneja wa tawi hilo Bw Mohamed Tegalila.


Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi hiyo Bw Lyuba pamoja na kuwapongeza wateja waliofanikiwa kuibuka washindi wa zawadi mbalimbali za kampeni hiyo akiwemo Bw Kweka, alisema kampeni hiyo iliyodumu kwa miezi 10 imehitimishwa kwa mafanikio makubwa kufuatia muitikio ilioupata kutoka kwa wateja kupitia uwekaji akiba.


Pamoja na kukabidhi zawadi mbalimbali kwa wateja wetu zikiwemo gari hizi mbili, mafanikio ya kampeni hii yanathibitishwa kupitia ufikiwaji wa lengo letu kuu la kampeni hii ambalo ni kuchochea kasi ya watanzania katika kujiwekea akiba. Kupitia kampeni hii tumeweza kuwafikia Watanzania wa makundi yote kiumri na kiuchumi na hiyo ndio sababu mshindi wetu wa gari hii ya pili ametoka kwenye kundi la wafanyabiashara wadogo kupitia akaunti yake ya Malengo,’’ alibainisha.


Kwa mujibu wa Bw Lyuba jumla ya zawadi zenye thamani ya TSh milioni mia mbili zimetolewa kwa washindi mbalimbali wa kampeni hiyo tangu kuanzishwa kwake.

Zaidi ya aina 8 ya zawadi zilizotolewa kupitia kampeni hii zilikuwa zipo kimkakati zaidi tukilenga ziwasaidie wateja wetu kwenye kufanikisha majukumu yao kiuchumi ambayo ndio maana hali ya ‘Shinda mechi zako’ zikiwemo nyenzo za biashara na vitendea kazi vitakavyoweza kuwarahisishia kazi zao,’’ aliongeza

Thursday, 30 January 2025

NMB BANK REPORTS RECORD FINANCIAL PERFORMANCE FOR THE YEAR 2024

Chief Executive Officer of NMB Bank, Ms. Ruth Zaipuna.

The record financial results were driven by a discipline execution of the Bank’s strategy and continuous investment in digital capabilities:
  • Profit Before Tax: TZS 931 Bln, up 20% YoY
  • Profit After Tax: TZS 644 Bln, up 18% YoY
  • Total Income: TZS 1.64 trillion, up 16% YoY
  • Total Assets: TZS 13.7 trillion, up 13% YoY
  • Cost to Income Ratio (CIR): 38%
Dar es Salaam, January 30, 2025: In 2024, NMB Bank Plc maintained a trajectory of accelerated growth, achieving outstanding financial and operational results driven by strong balance sheet growth, enhanced operational efficiencies, and significant improvement in loan portfolio quality.

NMB Bank achieved a record profit before tax of TZS 931 billion, a significant increase of 20% compared to TZS 775 billion in the financial year 2023, with a strong return on equity of 28%. The solid growth in profitability was driven by robust revenue growth, significant efficiency gains, and a notable improvement in loan portfolio quality. Total revenue rose by 16% to TZS 1.6 trillion, supported by the growth of Net Interest Income and Non-funded Income by 13% and 23%, respectively.

Furthermore, the cost-to-income ratio improved by 100 basis points year-on-year to 38% in 2024, well below the regulatory maximum limit of 55%. This improvement was driven by streamlined operations, disciplined cost management, and strategic investments in people and Digital technology, positioning the Bank to sustain growth and deliver value across its core businesses. These efforts underscore the Bank’s ability to balance efficiency with innovation, ensuring a solid foundation for future success.

The Bank’s Balance Sheet continued to grow, with total assets increasing by 13% year-on-year to TZS 13.7 trillion driven by solid growth in both loans & advances and customer deposits. Net loans and advances to customers grew by 10% to TZS 8.5 trillion, and customer deposits recorded broad-based growth, rising by 13% to TZS 9.5 trillion. The continued steady growth in the Balance Sheet demonstrates NMB’s commitment to; driving financial inclusion which has enabled the onboarding of new customers and broader access to credit, enhanced customer experience and confidence, and continued delivering innovative and accessible financial solutions to customers across.

The bank maintained strong credit portfolio quality, with the NPL ratio improving to 2.9% in 2024 compared to 3.2% recorded in 2023. This reflects strong credit origination and a robust credit monitoring process.

NMB remains well-capitalized, underpinned by strong earnings growth and efficient capital deployment, contributing to a well-capitalized status. As of December-end, the capital adequacy ratio stood at 23%, well above the regulatory minimum requirement. This solid capital position supports future investments, lending growth, and long-term stability.

NMB YAVUNJA REKODI YA UFANISI KWA MATOKEO YA KIHISTORIA YA MWAKA 2024

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna.

Matokeo haya mazuri ya kifedha yamechagizwa na utekelezaji makinii wa mkakati wa Benki na uwekezaji endelevu katika kutumia uwezo wa teknolojia za kidijitali:
  • Faida Kabla ya Kodi: TZS bilioni 931, ongezeko la 20% kwa mwaka
  • Faida Baada ya Kodi: TZS bilioni 644, ongezeko la 18% kwa mwaka
  • Jumla ya Mapato: TZS trilioni 1.64, ongezeko la 16% kwa mwaka
  • Jumla ya Mali: TZS trilioni 13.7, ongezeko la 13% kwa mwaka
  • Uwiano wa mapato na matumizi (CIR): 38%
Dar es Salaam, Januari 31, 2025 - Mwaka 2024, Benki ya NMB iliendeleza kasi ya ukuaji, ikipata matokeo ya kipekee ya kifedha na kiutendaji, yaliyochochewa na ukuaji imara wa mizania, ufanisi wa uendeshaji, na umakini mkubwa katika ukopeshaji.

Benki ya NMB ilipata faida kubwa ya kabla ya kodi kuwahi kupatikana katika historia yake kwa kufikia TZS bilioni 931 ambao ni ukuaji wa kasi wa 20% ikilinganishwa na TZS bilioni 775 za mwaka wa fedha 2023. Hii ilipelekea kupatikana kwa uwiano wa Faida na Mtaji wa 28%.Ukuaji huu imara wa faida ulitokana na ongezeko la mapato, ufanisi mkubwa wa uendeshaji, na mwendelezo wa kuimarisha ubora wa mkopo. Jumla ya mapato iliongezeka kwa 16% hadi TZS trilioni 1.6, kutokana na ongezeko la Mapato ya Riba Halisi kwa 13% na Mapato Yasiyo ya Riba kwa 23%.

Uwiano wa mapato na matumizi (CIR) uliimarika kwa pointi za asilimia 100 hadi 38%, ambao ni chini ya ukomo wa kikanuni wa 55%. Maboresho haya yalichangiwa na ufanisi zaidi wa uendeshaji, usimamizi makini wa matumizi, na uwekezaji wa kimkakati kuendeleza rasilimali watu na katika teknolojia za kidijitali. Hii iliiwezesha benki kuendeleza ukuaji, na kuhakikisha ufanisi na thamani vinapatikana katika shughuli zake zakifedha za msingi. Juhudi zote hizi zinathibitisha uwezo wa Benki ya NMB katika kupata uwiano mzuri kati ya ufanisi na ubunifu, huku ikijenga msingi imara wa mafanikio ya baadaye.

Aidha, Mizania ya Benki iliendelea kukua, huku jumla ya mali ikiongezeka kwa 13% kwa mwaka mzima wa 2024 hadi TZS trilioni 13.7. Mikopo halisi kwa wateja ilikua kwa 10% hadi TZS trilioni 8.5, huku amana zikiongezeka kwa 13% hadi TZS trilioni 9.5. Ukuaji huu thabiti unaakisi dhamira ya NMB katika kuendeleza ujumuishaji wa kifedha, ambao umesaidia kuongeza idadi ya wateja wapya na kiwango cha mikopo, kuboresha huduma kwa wateja na imani yao kwetu, huku tukindelea kuja na masuluhisho mapya bunifu na rahisi ya kifedha.

STANDARD CHARTERED OUTLINES AFRICAN INFRASTRUCTURE PROJECTS AT HEADS OF STATE ENERGY SUMMIT

STANBIC ADVOCATES ENERGY INVESTMENT & REGIONAL INTEGRATION AT EA-ECS 2025

Stanbic Bank Tanzania Vice President for Energy & Infrastructure, Mr. Joe Mwakanjuki (center), shares his insights during a panel discussion on the topic “Enhancing Energy Systems – Integrating Natural Gas into the Grid” at the East Africa Energy Cooperation Summit in Arusha yesterday. The summit brought together key stakeholders to discuss regional energy collaboration, was primarily sponsored by Stanbic. Looking on from the left are Clarke Energy Deputy General Manager, Mr. Tarak Jani, and Taqa Arabia Vice President for Africa & New Ventures, Mr. Adly Kafafy.
Stanbic Bank Tanzania Senior Vice President, Public Sector, Noella Kimaro (third left), with other participants, attend the East Africa Energy Cooperation Summit in Arusha yesterday, which was primarily sponsored by Stanbic Bank Tanzania.
  • Stanbic Bank Tanzania underscores its dedication to driving energy investment and infrastructure financing at the 5th EA-ECSEast Africa Energy Cooperation Summit (EA-ECS)2025 in Arusha
  • The summit serves as a platform to accelerate regional collaboration and energy integration, focusing on expanding access, leveraging renewable resources, and enhancing industrialization
  • Stanbic Bank continues to play a key role in supporting Tanzania’s energy sector, providing financial solutions that promote sustainable growth and economic resilience
Thursday, 30th January 2025 - Arusha: As East Africa moves toward a new era of energy transformation, Tanzania is taking a leading role in shaping the future of the region’s energy sector. At the 5th East Africa Energy Cooperation Summit (EA-ECS) 2025, Stanbic Bank Tanzania has reaffirmed its commitment to enabling investment, financing critical infrastructure, and supporting industrialization as key drivers of economic progress.

With the theme “Empowering East Africa: Unlocking Tanzania’s Energy Potential for a Regional Power Market,” EA-ECS 2025 brings together government leaders, investors, and energy experts to discuss solutions for expanding energy access, integrating sustainable power sources, and strengthening regional energy cooperation. As Tanzania positions itself as an energy hub within the East African Community (EAC), investment in energy security, infrastructure, and innovative financing models will be critical to unlocking the sector’s full potential.

Stanbic Bank Tanzania recognizes the role of strategic financing in transforming the energy landscape. By leveraging expertise from Standard Bank Group, the bank has played a key role in structuring financial solutions that de-risk investments, facilitate partnerships, and accelerate the development of large-scale infrastructure projects. The bank has contributed to major energy initiatives, including conducting the Tanzania LNG: Macroeconomic Study. Beyond Tanzania, Standard Bank Group has supported transformative energy investments across the continent, including financing the Seriti Green Wind Project in South Africa, expanding renewable energy solutions through CrossBoundary Energy, and refinancing Kenya’s Lake Turkana Wind Power Project, Africa’s largest wind farm.

TANZANIA MAKES SIGNIFICANT PROGRESS IN THE ABSA AFRICA FINANCIAL MARKETS INDEX 2024

Governor of the Bank of Tanzania, Mr. Emmanuel Tutuba (center), Managing Director of Absa Bank Tanzania, Mr. Obedi Laiser (left), and Director of Financial Markets at Absa Tanzania, Ms. Irene Rwegalulira, showcasing the book containing the Absa Africa Financial Markets Index 2024 report, shortly after its launch in Dar es Salaam today.
Governor of the Bank of Tanzania, Mr. Emmanuel Tutuba (third left), cuts a ribbon during launch of the Absa Africa Financial Markets Index 2024 report in Dar es Salaam today. From the left are Absa Managing Director Global Markets, Africa Regional Operations - Mr. Anthony Kirui; Absa Tanzania Director of Financial Markets - Ms. Irene Rwegalulira; Managing Director of Absa Bank Tanzania - Mr. Obedi Laiser; Chief Economist and Head of FIC Research - Mr. Jeff Gable; and a Board Member of the Bank - Mr. Richard Magongo.

Dar es Salaam, 30 January 2025 – Absa Bank Tanzania today hosted an exclusive breakfast event to launch the Absa Africa Financial Markets Index (AFMI) 2024, an influential annual report that evaluates the development and performance of financial markets across Africa. The event, held in Dar es Salaam, brought together key stakeholders, policymakers, industry leaders, and financial experts for an interactive session to explore the report’s insights and implications for Tanzania’s financial markets.

The Guest of Honor, Hon. Emmanuel Tutuba, Governor of the Bank of Tanzania, graced the occasion alongside esteemed panelists and keynote speakers, including: Mr. Peter Situmbeko Nalitolela - Chief Executive Officer, Dar es Salaam Stock Exchange; Mr. Charles Philip Shirima - Manager Public Relations, Capital Markets and Securities Authority (CMSA); Mr. Lameck M. Kakulu - Manager of Foreign Markets, Directorate of Financial Markets; Mr. Anthony Kirui - Managing Director Global Markets, Absa Regional Operations; and Mr. Jeff Gable - Absa Bank’s chief economist and head of FIC Research, Absa Regional Office.

Senior representatives from Absa Group, including Mr. Anthony Kirui, Managing Director Global Markets, Africa Regional Operations, and Mr. Jeff Gable, Chief Economist and Head of FIC Research, delivered keynote addresses. They shared insights into emerging trends reshaping Africa’s financial landscape, including advancements in ESG frameworks, digital technologies, and efforts to strengthen legal and regulatory regimes.

Tanzania’s Performance in AFMI 2024

This year’s AFMI report highlights significant progress for Tanzania. The country’s overall score improved from 50 to 52, ranking 12th among 29 African nations evaluated. Key achievements include:
  • Pillar 2: Access to Foreign Exchange – A notable improvement from 53 to 60, attributed to the Bank of Tanzania’s publication of the Interbank Foreign Exchange Market code of conduct, aligning with 52 out of 55 FX Global Code principles.
  • Pillar 5: Macroeconomic Environment and Transparency – The score increased from 80 to 85, driven by greater transparency, including public access to the monetary policy meeting schedule, low inflation, and a reduced non-performing loan ratio.
  • Pillar 1: Market Depth – Gains were linked to new corporate bond issuances totaling $300 million and the introduction of diverse financial instruments, including ESG-linked and Islamic financial products.
However, the report identifies areas for improvement:
  • Pillar 4: Pension Fund Development – Despite a slight score increase, Tanzania’s pension fund assets per capita remain significantly below the index average, signaling the need for enhanced local investor capacity.
  • Pillar 6: Legal Standards and Enforceability – Efforts are underway to address gaps in close-out netting legislation and regulatory frameworks to boost investor confidence.
Remarks by Key Speakers

Hon. Emmanuel Tutuba commended Absa Group for its commitment to promoting transparency and efficiency in African financial markets through the AFMI. “The progress highlighted in this report is a testament to the collaborative efforts of the government, the Bank of Tanzania, and market participants in strengthening our financial markets,” he stated.

FINANCIAL INSTITUTIONS TO CONTINUE SUPPORTING DEVT. OF THE ENERGY SECTOR

Stanbic Bank Tanzania Chief Executive Officer, Mr. Manzi Rwegasira (left), listens to CRDB Bank Managing Director, Mr. Abdulmajid Nsekela (right), during the recently concluded Mission 300 Africa Energy Summit at Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam. Looking on is Geita Gold Refinery CEO, Ms. Sara Masasi.
Stanbic Bank Tanzania Chief Executive Officer, Mr. Manzi Rwegasira (third right), attends the recently concluded Mission 300 Africa Energy Summit at Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam.

NMB 2024 FINANCIAL HIGHLIGHTS - SOLID GROWTH & SUSTAINABLE VALUE CREATION

MUHTASARI WA TAARIFA ZA KIFEDHA NMB MWAKA 2024 - UKUAJI IMARA & ENDELEVU

Wednesday, 29 January 2025

BENKI YA EXIM YAENDELEA KUJIIMARISHA KWA UNUNUZI WA CANARA BANK

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu (katikati) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kutangaza ununuzi wa Canara Bank Tanzania ambayo rasmi inakuwa sehemu ya Benki ya Exim Tanzania. Ununuzi huu ni wa tatu kufanywa na Benki ya Exim ndani ya miaka sita iliyopita ikiwa sehemu ya juhudi zake katika kuboresha sekta ya kibenki ndani na nje ya Tanzania. Kushoto ni Afisa Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Shani Kinswaga na Mkuu wa Idara ya Uwekezaji Kimkakati, Sumit Shekhar wakiwa katika tukio hilo lililofanyika Makao Makuu ya Exim Bank jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 29 Januari 2025.

Dar es Salaam: Benki ya Exim Tanzania inayofuraha kutangaza kukamilika kwa ununuzi wa Canara Bank Tanzania Limited. Huu ni ununuzi wa benki ya tatu ambao umefanyika na Benki ya Exim ndani ya miaka sita iliyopita, ikizidi kuimarisha nafasi yake kama mdau muhimu katika sektaya benki nchini Tanzania.


Ununuzi huu ulianza kwa kusainiwa kwa makubaliano mnamo mwaka 2024 na kufuatiwa na kibali kutoka Benki Kuu ya Tanzania, na sasa umekamilika rasmi. Hatua hii ni ishara ya dhamira ya Benki ya Exim ya kukua, kuleta ubunifu, na kuboresha huduma zinazolenga mahitaji ya wateja.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu alisema “Tuna furaha kubwa kuwakaribisha wateja wa Canara Bank Tanzania kwenye familia ya Benki ya Exim. Ununuzi huuni ushahidi wa dhamira yetu ya kutoa suluhisho za kifedha zenye ubunifu na huduma za kipekee, tukihakikisha mabadiliko chanya kwa wadau wetu.”



Ununuzi huu ni hatua ya kimkakati katika safari yetu ya kuboresha sekta ya kibenki ndani na nje ya Tanzania. Pamoja, tutaendelea kubuni, kukua, na kutoa suluhisho zenye huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu yanayo badilika huku tukichangia maendeleo endelevu ya Uchumi,” aliongeza Matundu.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 1997, Exim Bank imekuwamoja ya benki tano kubwa zaidi nchini, ikiendeleza upanuzi wa ndani na nje ya Tanzania kupitia ununuzi wa kimkakati. Safari hii ilianza kwa ununuzi wa benki moja nchini Uganda mwaka 2016, ikafuatiwa na ununuzi wa UBL Bank Tanzania mwaka 2019, FNB Bank Tanzania mwaka 2022, na sasa Canara Bank Tanzania mwaka 2024. Benki hiyo pia ina ofisi ya uwakilishi nchini Ethiopia, ikithibitisha matarajio yake ya kikanda.

Kuungana na ununuzi wa benki ni muhimu katika kuongeza ufanisi na kuimarisha sekta ya benki. Ununuzi wa kimkakati wa Benki ya Exim umesaidia kupunguza benki ndogo zisizo na tija, kuzalisha benki kubwa zaidi zenye ushindani, na kuongeza uwezo wa fedha, kupanua masoko mapya, kuboresha mseto wa bidhaa, kuongeza uimara wa sekta dhidi ya misukosuko ya mitaji, na kupunguza gharama za usimamizi na teknolojia. Hatua hii inaendana na maono ya Benki ya Exim ya kuwa taasisi kubwa ya kifedha kikanda ikiwa pia ni sehemu ya kuunga mkono mpango wa Benki Kuu ya Tanzania wa kupunguza benki ndogo ndogo kwa lengo la ufanisi zaidi.


Monday, 27 January 2025

SERIKALI YAIPONGEZA NMB KWA BIL. 100/- ZA KUKOPESHA WASAMBAZAJI NISHATI SAFI


Serikali imeipongeza Benki ya NMB kwa kuzindua Mfuko Maalum uliotengewa Sh. Bilioni 100 za kukopesha wasambazaji na wauzaji wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Watanzania, na kwamba Serikali itaingia kifua mbele katika Mkutano Mkuu wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika (Mission 300), unaofanyika Januari 27 na 28 jijini Dar es Salaam.



Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri Mkuu, Dk. Doto Biteko, wakati wa uzinduzi wa mfuko huo, aliobeba dhamira chanya ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) na kwamba tukio hilo ni uthibitisho tosha wa ushirikiano uliopo baina ya Serikali na Sekta Binafsi katika kustawisha jamii ya Watanzania.



Kwa niaba ya Serikali na Wizara ya Nishati, Dk. Biteko aliishukuru NMB kwa wazo hili na kwamba wako tayari kuwaunga mkono ili jambo hilo likatimizwe, huku akisema wazo la kuhakikisha mawakala na wasambazaji wa nishati safi za kupikia wanapata mitaji ili kufikisha huduma mijini na vijijini, litasaidia kuchochea upatikanaji na matumizi ya nishati hiyo.



“Hakika mpango huu wa NMB kutenga Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya jambo hili, unastahili pongezi kubwa sana, hasa ikizingatiwa kuwa kama benki ina njia nyingi sana za biashara, ambazo wangeweza kuwekeza fedha hizo sehemu nyingine ili kuweza kuendelea kujizalishia faida zaidi.



“Lakini, msukumo huu wa kuja kuweka kiasi hiki kwenye Nishati Safi ya Kupikia inaonesha dhamira ya dhati ya benki kuchangia maendeleo endelevu kwa taifa letu la Tanzania, lakini ni kielelezo tosha cha uzalendo wa kweli uliopo kati yenu Menejimenti pamoja na wafanyakazi wa benki hii.



“Mtendaji Mkuu wa NMB tayari ameeleza hapa faida mbalimbali za matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na mimi nisisitize kuwa, faida hizo za Afya Bora, Mazingira Safi, Kuboresha Uchumi na Ufanisi wa Nishati hizi na ukweli kuwa nishati safi ni salama, ndio maana hata Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kinara wa hili nchini, Afrika na duniani kote.



“Wote tunafahamu kwamba, licha ya ukosefu wa mitaji, changamoto kubwa ya wananchi kuendelea kutumia nishati isiyo safi ya kupikia, ni ukosefu wa elimu juu ya nishati safi ya kupikia, hivyo suala la NMB kuanza pia kutoa elimu ya hili ni jambo zuri na la kipekee sana kwa ustawi wa matumizi ya nishati hii safi.” Alisema Dk. Biteko.

Alibainisha kuiwa shukrani na pongezi kwa NMB hazitaishia tu katika Nishati Safi ya Kupikia tu, bali zinaenda pia kwa mambo makubwa ambayo imekuwa ikifanya kwa manufaa kwa taifa letu la Tanzania, ikiwemo misaada mbalimbali mashuleni, zahanati, vituo vya afya na hospitali na kuchagiza maendeleo endelevu kwa jamii, sambamba na upandaji miti.

Januari 27 na 28, Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano uliopewa jina la Mission 300 kuakisi dhamira ya kuwafikia watu milioni 300 barani Afrika kuhakikisha wanatumia Nishati Safi, ambapo zaidi ya marais 25, Mawaziri wa Fedha na Nishati 60 wa Afrika, watashiriki mkutano huo, mweji akiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

NMB BACKS GOVT’S CLEAN COOKING AGENDA WITH 100BN/- SOFT LOAN FACILITY


In a ground-breaking move to tackle Tanzania's energy challenges and advance the government's green agenda, NMB Bank has unveiled a TZS 100 billion loan fund to financially empower Tanzanians to embrace clean cooking solutions.



Announcing the financing initiative on Saturday in Dar es Salaam, CEO Ruth Zaipuna said the loans will carry an interest rate of 1% per month, equivalent to an annual credit cost of 12%, to make them affordable and attractive to borrowers.


The maximum loan an individual borrower can access from any NMB branch nationwide is TZS 1 billion, the seasoned banker told Deputy Premier Dotto Biteko, who presided over the inauguration of the novel lending package.


Lauding the lender backing the government’s cleaning cooking agenda, Dr Biteko said the low-cost loans are a timely intervention to support national efforts to transition majority people away from harmful and polluting fuels.


He stated the soft loans will be crucial in promoting the widespread availability of sustainable alternatives, pointing out that official figures show that only 16% of households in Tanzania were currently using clean cooking sources.


"This special credit facility being officially launched by NMB Bank today marks a significant milestone for the renewable energy sector. It is a timely financing initiative that aligns perfectly with President Dr Samia Suluhu Hassan's vision of transforming Tanzania into a model nation with universal access to affordable, reliable, and sustainable energy sources," Dr Biteko, who also serves as the Minister of Energy, remarked.


Ms Zaipuna said the loans are set at a highly competitive interest rate to not only make them affordable and user-friendly but also ensure they accelerate distribution of clean energy solutions and enable many Tanzanians to adopt them.

Saturday, 25 January 2025

SWAHIBA (CRDB) AWAKUTANISHA MAAFISA WAKUU WA FEDHA NA KUYAJENGA



Benki ya CRDB, ambayo hivi karibuni imepokea tuzo ya Mwajiri Kinara na kutajwa kama moja ya walipakodi waliofanya vizuri kwa mwaka 2023/2024, inaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya taifa kwa kushirikiana na wadau wa sekta mbalimbali ambapo Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo, ameongoza jukwaa maalum lililolenga kupeana uzoefu katika masuala ya fedha, pamoja na kusimamia mipango endelevu.



Kwa ukarimu wa kipekee, viongozi wakuu wa Benki ya CRDB akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela na Afisa Mkuu Uendeshaji, Bruce Mwile nao pia walishiriki jukwaa hili ambapo walipata nafasi ya kutoa uzoefu wao, kubadilishana mawazo na kujenga mahusiano. Katika jukwaa hili, waalikwa walipitishwa na kujionea mandhari nzuri ya jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB na wenyeji wao ambao ni viongozi na wafanyakazi wa Benki. 



#crdbbank
#tunakusikiliza

BENKI YA NMB MLIPA KODI MKUBWA ZAIDI NA BORA ZAIDI TANZANIA


Katika kuendelea kuwa mshirika mkubwa wa maendeleo nchini, Benki ya NMB imetunukiwa tuzo 3 na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ikiwa ni sehemu ya juhudi za TRA kuthamini mchango wa walipa kodi katika maendeleo ya Taifa. Tuzo hizo zinazoitambua Benki ya NMB kama mlipa Kodi Mkubwa Zaidi na Bora Zaidi nchini Tanzania kwa mwaka wa kifedha 2023/2024 ni: 


  1. Mshindi wa Kwanza; Taasisi inayolipa kodi kubwa na inayozingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi (sekta ya kibenki).
  2. Mshindi wa Kwanza; Mchangiaji bora wa ukusanyaji kodi nchini. 
  3. Mshindi wa kwanza; Taasisi inayolipa kodi kubwa zaidi nchini na kuzingatia kanuni za ulipaji kodi (sekta zote nchini).

Tuzo hizi zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kwenye Siku ya Shukrani na tuzo kwa Mlipa Kodi na kupokelewa kwa niaba ya Benki na Afisa Mtendaji Mkuu wetu, Bi. Ruth Zaipuna. 



Mafanikio haya kwa benki ya NMB ni matokeo ya kuzingatia kanuni bora za ulipaji kodi, ufanisi katika kujiendesha na ubunifu wa suluhishi bora za kifedha zenye manufaa kwa Wateja na Taifa letu.


Dhamira yao ni kuendelea kuendesha biashara ya kutoa huduma za fedha kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchi ili kuchangia kikamilifu ujenzi wa uchumi wa Tanzania.

Friday, 24 January 2025

HOW EFDs & ETS SYSTEMS LED TRA TO EXCEED Q1 REVENUE TARGETS


Dar es Salaam, January 2025: The Tanzania Revenue Authority (TRA) has credited its remarkable first-quarter revenue collection performance for the 2024/25 financial year to the effective use of advanced technology systems, specifically the Electronic Fiscal Devices (EFDs) and the Excise Tax Stamp (ETS) system.

Speaking in Dar es Salaam, TRA Commissioner General, Yusufu Mwenda emphasized that these technologies were instrumental in helping the authority surpass its revenue collection targets.

The government had tasked TRA with collecting Sh29.415 trillion for the fiscal year, part of the national Sh49.3 trillion budget approved by Parliament in June.

This required the authority to collect an average of Sh2.45 trillion each month.

However, in the first three months of the financial year, TRA collected a total of Sh7.79 trillion, exceeding the target with an average monthly collection of Sh2.6 trillion.

Mr Mwenda attributed the success to stricter oversight in the use of EFDs and the ETS system.

"These systems have significantly contributed to ensuring we meet and even exceed our targets," he explained.

PUMA ENERGY YASHINDA TUZO NNE USIKU WA HAFLA YA WALIPAKODI 2023/24


Dar es Salaam: Kampuni ya Puma Energy Tanzania, imeshinda tuzo nne wakati wa usiku wa utoaji tuzo kwa wafanyabiashara waliofanya vizuri kwa mwaka wa fedha 2023/24!



Tukio hili la kipekee lilifanyika wakati wa Usiku wa Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Walipakodi lililofanyika katika ukumbi wa the Super Dome Masaki, Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 



Viongozi wa kiserikali, wakiwemo: Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson (Mb), Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA Tanzania) Bw. Yusuph Juma Mwenda, pamoja na viongozi wengine waandamizi wa serikali na dini walikuwepo pia kushuhudia wakati taasisi na biashara zaidi ya 100 zikitunukiwa na kutambuliwa kwa weledi wao.

Ikiwakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Bi. Fatma Abdallah, kampuni hiyo kinara katika usambazaji na uuzaji wa huduma na bidhaa za mafuta na nishati imejinyakulia tuzo katika vipengele vya weledi wa ulipaji kodi katika sekta ya Uuzaji na Usambazaji wa Mafuta na Gesi kwa mwaka wa fedha 2023/24, kampuni bora zaidi iliyozingatia sheria katika ulipaji wa kodi ngazi ya kitaifa kwa mwaka wa fedha wa 2023/24, kampuni bora katika ulipaji wa wakati wa Kodi na Ushuru, na mshindi wa jumla katika ulipaji Kodi na Forodha uliolipwa katika Mwaka wa Fedha wa 2023/24 kwenye sekta ya Ushuru na Forodha.