Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 16 October 2024

VODACOM TWENDE BUTIAMA 2024 YAHITIMISHWA BUTIAMA KWA MAFANIKIO MAKUBWA


Dar es Salaam – Msafara wa kihistoria wa Vodacom Twende Butiama 2024 umekamilika rasmi mnamo tarehe 13 Oktoba kwa mafanikio makubwa, ukihitimishwa wilayani Butiama, kijijini kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere katika mkoa wa Mara. Msafara huo, uliowakutanisha waendesha baiskeli zaidi ya 100 kutoka Tanzania na nchi jirani, ulifanyika kuanzia tarehe 29 Septemba na kupita katika mikoa 12 ya Tanzania.


Mafanikio ya msafara huu ni pamoja na kutoa huduma za afya bure kwa maelfu ya wananchi katika kambi za matibabu zilizowekwa njiani. Zaidi ya madawati 1,000 yalichangwa kwa shule mbalimbali, zikiwemo shule zinazohudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum, huku miche 50,000 ya miti ikipandwa katika maeneo mbalimbali ambako msafara huu ulipita, lengo likiwa kuhifadhi mazingira.


Ubunifu huu wa Msafara wa Vodacom Twende Butiama, ulianzishwa mwaka 2018, umeendelea kuwa jukwaa muhimu la kusaidia jamii kupitia utoaji wa huduma za kijamii katika nyanja za elimu, afya, na mazingira.








No comments:

Post a Comment