Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 17 October 2024

SERIKALI NA SHIRIKA LA FEDHA LA KIMATAIFA (IMF), ZAHITIMISHA TATHMINI

Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa pili kushoto), Gavana wa Benki kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa kwanza kushoto), Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bi. Sauda Msemo (wa kwanza kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (wa pili kulia), wakizungumza jambo wakati wa kikao kati ya Serikali na Ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), cha kuhitimisha tathmini ya Awamu ya Nne ya utekelezaji wa Program ya Extended Credit Facility-(ECF), inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii pamoja na kufanya mapitio na tathmini ya kwanza (1st Review) ya Program mpya ya Serikali ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia Dirisha la Resilient and Sustainable Fund (RSF).
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akishiriki kikao cha kuhitimisha tathmini kati ya Serikali na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa njia ya mtandao, akiwa jijini Dodoma, ambapo timu hiyo ya IMF imefanya Tathmini ya Awamu ya Nne ya utekelezaji wa Program ya Extended Credit Facility-(ECF), inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii pamoja na kufanya mapitio na tathmini ya kwanza (1st Review) ya Program mpya ya Serikali ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia Dirisha la Resilient and Sustainable Fund (RSF).
Ujumbe wa Tanzania (kushoto) ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kwa njia ya mtandao) na ujumbe wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), wakiwa katika kikao cha kuhitimisha tathmini ya Awamu ya Nne ya utekelezaji wa Program ya Extended Credit Facility-(ECF).
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (kushoto), akiagana na Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, baada ya kutamatika kwa kikao kati ya Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani) aliyeshiriki kwa njia ya mtandao.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (katikati aliyeketi) na Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides (wa pili kushoto aliyeketi), wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Serikali na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), baada ya kutamatika kwa kikao kati ya Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani) aliyeshiriki kwa njia ya mtandao.

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha kuhitimisha tathmini kati ya Serikali na Ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ulioongozwa na Bw. Charalambos Tsangarides, kwa njia ya mtandao, akiwa jijini Dodoma.

Timu hiyo ya wataalamu kutoka IMF imekuwa nchini kwa majuma kadhaa ikifanya Tathmini ya Awamu ya Nne ya utekelezaji wa Program ya Extended Credit Facility-(ECF), inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii pamoja na kufanya mapitio na tathmini ya kwanza (1st Review) ya Program mpya ya Serikali ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia Dirisha la Resilient and Sustainable Fund (RSF).

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, Manaibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bi. Sauda Msemo na Dkt. Yamungu Kayandabila, na Maafisa wengine waandamizi wa Serikali ambao walishiriki Mkutano huo wa kuhitimisha tathimini wakiwa Ukumbi wa Mikutano wa Mount Meru wa Benki Kuu ya Tanzania, Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment