Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 25 April 2024

KAMPUNI YA SIGARA - TCC YAIDHINISHA GAWIO KWA WANAHISA WAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya sigara - TCC, Takashi Araki akiongea katika Mkutano Mkuu wa 59 wa wana hisa.

Kampuni ya Sigara - Tanzania Cigarette Company (TCC) imeidhinisha Gawio la Shilingi 500 kwa Hisa kwa Wanahisa wake ikiwa ni baada ya kampuni hiyo kupata faida baada ya kodi ya Shilingi bilioni 66.2 ikiwa ni pungufu ya asilimia 4 ya faida iliyopata Kampuni hiyo kwa mwaka 2022.

Yamesemwa hayo na Mwenyekiti wa Bodi wa TCC, Paul Makanza wakati wa Mkutano Mkuu wa 59 wa Wanahisa wa Kampuni hiyo kwa mwaka 2023, ambapo amesema upungufu huo umetokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji ambazo zilisababishwa na changamoto za kiuchumi ulimwenguni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo amesema licha ya changamoto, mapato ya Kampuni hiyo yameongezeka kufikia Shilingi milioni 373,527 sawa na ongezeko la asilimia 9.7 ikilinganishwa na mwaka uliopita, ukuaji ambao umechochewa na ongezeko la asilimia 5.1 katika mauzo ya ndani ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Mwaka 2022, Kampuni hiyo ili idhininisha Gawio la jumla ya Shilingi bilioni 67 sawa na Shilingi 670 kwa hisa.

No comments:

Post a Comment