Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 25 September 2023

VODACOM KULIPA TZS 22.3 KWA WANAHISA

  • Vodacom Tanzania imeonyesha ukuaji mkubwa wa mapato ukiongozwa kwa kiasi kikubwa na ukuaji wa matumizi ya Data na M-Pesa.
  • Wanahisa wameidhinisha gawio la TZS 9.95 kwa kila hisa kwa mwaka wa fedha unaomalizika Machi 31, 2023.
Vodacom Tanzania PLC, kampuni ya mawasiliano na teknolojia pekee iliyoorodheshwa kwenye soko la hisa nchini Tanzania, imefanya Mkutano Mkuu wa Mwaka tarehe 22 Septemba, uliohudhuriwa na wanahisa kutoka maeneo tofauti kupitia mtandaoni. Wakati wa mkutano huo, Ripoti ya Ujumuishaji ya kila mwaka kwa mwaka unaomalizika Machi 2023 iliwasilishwa kwa wanahisa. Ripoti hiyo ilionyesha mafanikio makubwa ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Vodacom ilirekodi mapato ya huduma ya TZS 1054.8 bilioni, ambayo yalitokana kwa kiasi kikubwa na matokeo mazuri kutoka kwa huduma za data za simu, kuimarika kwa M-Pesa, na ukuaji wa haraka wa huduma za uunganishwaji. Mapato ya M-Pesa yaliongezeka kwa 8.4% na kuleta TZS 357.1 bilioni kwenye mapato ya Vodacom wakati mapato ya data yaliongezeka kwa kiasi kikubwa cha 34.2% na kuleta jumla ya TZS 273.7 bilioni.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya Mkutano Mkuu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Vodacom Tanzania, Jaji Mstaafu Thomas B. Mihayo, alielezea imani yake katika uimara wa kampuni, ukiwa umeoneshwa na ukuaji wake wa mwaka hadi mwaka.

"Matokeo yetu bora kifedha na kiendeshaji ni uthibitisho wa ubora wa mkakati wa kampuni unaosimamiwa na kujielekeza kwenye kusudi na uwezo wake wa kutekeleza mpango uliolenga kuwaunganisha watu kwenye mustakabali bora. Licha ya mabadiliko ya kiuchumi ulimwenguni na mazingira ya ushindani wa soko kwa kiasi kikubwa, kampuni ilifanya vizuri kifedha na kuendelea kuwa kiongozi katika kushiriki soko na kiashiria cha kuridhika kwa wateja," alisema Jaji Mihayo.

Kampuni imeendelea na mikakati yake ya kuboresha huduma, kusaidia juhudi za serikali katika kuongeza huduma za mawasiliano maeneo ya vijijini kwa kuweka minara 302 katika kipindi cha muongo uliopita. Pia tumesaidia shughuli za kiuchumi kwa kutengeneza zaidi ya ajira 150,000 za kujitegemea kwa Watanzania na kusaidia kilimo kwa kusajili zaidi ya wakulima milioni 3.1 kwenye huduma yetu ya M-Kulima ambayo inarahisisha kielektroniki mnyororo wa kilimo. Aidha, kwa kusaidia utekelezaji wa serikali wa mfumo wa m-mama, ambao sasa upo kwenye mikoa takriban 31 ya Tanzania bara na visiwani Zanzibar, tumesaidia usafiri wa dharura kwa wajawazito, kuokoa maisha ya mama na watoto na kuwa mfano kwa nchi kama Kenya na Lesotho.

Wakati huo huo, Bwana Philip Besiimire, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, ambaye alijiunga na kampuni mwaka jana, anasema amevutiwa na ubora wa timu ya uongozi na wafanyakazi na utekelezaji imara wa mkakati. Chini ya uongozi wake, kampuni imeendelea kuongeza mapato na wateja mwaka hadi mwaka.

"Mkakati wetu unaosimamiwa na kusudi unachochea ukuaji chanya, na utekelezaji mzuri kwenye nguzo za mkakati. Tunaendelea kushikilia nafasi yetu ya uongozi kwenye soko la simu na 30% ya wateja, tukishuhudia ukuaji mzuri wa 8.9% katika msingi wa wateja na ongezeko kubwa la 15.1% kwa watumiaji wa data, kuweka msingi wa mafanikio ya baadaye. Zaidi ya hayo, bidhaa yetu ya M-Pesa imecheza jukumu muhimu katika kusaidia ukuaji wa kijamii na kiuchumi nchini Tanzania, na msingi wetu wa wateja ukipanda kwa 20% mwaka hadi mwaka hadi kufikia milioni 8.2. Tumeongeza mfumo wetu wa M-Pesa na kujitolea kwetu kuwajumuisha kiuchumi, tumesaidia shughuli zenye thamani ya TZS trilioni 6 na kutoa mikopo midogo midogo yenye thamani ya trilioni kwa mwaka huu," alisema Philip.

Katika mwaka wa fedha uliopita, Vodacom Tanzania ilizindua mtandao wa kwanza wa 5G nchini Tanzania na kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika miundombinu ya mtandao wake, ambayo ililipa kwa kampuni kurekodi ukuaji wa 34.2% kwa mapato ya Data na msingi wa wateja.

"Kwa lengo la kuendeleza ajenda yetu ya 'Kudigitisha Tanzania', tumewekeza TZS156.0 bilioni katika kuongeza uwezo wa mtandao, upanuzi, na uboreshaji wa miundombinu ya teknolojia na mawasiliano. Hii ilijumuisha kuongeza vituo vipya vya 4G 390 na vituo vipya vya 3G 228, ikiboresha kwa kiasi kikubwa ueneaji wa mkongo wa taifa. Tulizindua mtandao wa 5G na vituo 231 vinavyosaidia teknolojia hii. Mwezi wa Oktoba 2022, tulifanikiwa kununua masafa manne ya spekta ya viwango vya chini na kati kupitia mnada, tukiwekeza dola za Marekani milioni 63.2. Uwekezaji huu wa kimkakati utaharakisha mipango yetu ya kuongeza mtandao kwa siku za usoni na kufungua fursa za ukuaji, hasa kwa upatikanaji wa mtandao ikiwa ni kiungo cha kudumu. Uwekezaji huu, pamoja na ongezeko la matumizi ya simu za mkononi na ugawaji wa spekta, ulisababisha ukuaji wa kipekee wa 57.1% katika matumizi ya data ya 4G," alisema, Phillip.

Wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka (AGM), wanahisa pia walichagua na kuwarejesha wakurugenzi wasio watendaji tofauti kwenye bodi ya kampuni. Kwenye biashara maalum, wanahisa waliidhinisha ununuzi wa 100% ya hisa zilizotolewa katika Kampuni ya Smile Communications Tanzania Limited na kukubaliana na ushirikiano wa pamoja na washirika wa kimkakati kutekeleza ufungaji wa faiba na kutoa huduma zinazohusiana pamoja na kuongeza miundombinu ya minara vijijini ili kuongeza uwepo wa mtandao wa kiungo cha kudumu na simu za mkononi nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment