Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 19 April 2023

DCB ELIMU MPANGO MZIMA NA MAMA SAMIA YAZIDI KUPAA

Ofisa Elimu Manispaa ya Temeke, Abdul Buhety (kushoto), akipokea msaada wa madawati 30 Kwa niaba ya Shule ya Msingi Sandali kutoka Kwa Kaimu Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya DCB, Ruth Mpangalala yaliyotolewa na benki hiyo, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kusaidia elimu ya DCB Elimu Mpango Mzima na Mama Samia katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Temeke, jijini Dar es Salaam.

Msimamizi wa Huduma za Wateja na Masoko wa Benki ya DCB, Elizabeth Ntulu (kulia), na Ofisa Mahusiano wa Benki hiyo, Dalila Issa (kushoto), wakikabidhi sehemu ya madawati 30 yaliyotolewa na DCB kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Sandali kupitia kampeni yao ya DCB Elimu Mpango Mzima na Mama Samia, shuleni hapo, temeke, Dar es Salaam.

Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya DCB, Caroline Gabriel (kulia) katika hafla ya makabidhiano ya msaada wa madawati 30 yaliyotolewa na DCB kwa Shule ya Msingi Sandali kupitia kampeni yao ya DCB Elimu Mpango Mzima na Mama Samia, shuleni hapo, Temeke, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi wa Shule ya Msingi Sandali, Yohana Ndunguru (kushoto), akipokea msaada wa madawati 30 Kwa niaba ya shule hiyo kutoka Kwa Kaimu Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya DCB, Ruth Mpangalala yaliyotolewa na benki hiyo, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kusaidia elimu ya DCB Elimu Mpango Mzima na Mama Samia katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Temeke, jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Shule ya Msingi Sandali, Bakari Jaribu, akizungumza katika hafla hiyo. Wengine kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Biashara wa DCB, Ruth Mpangalala, Ofisa Elimu wa Manispaa ya Temeke, Abdul Buhety na Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi wa shule hiyo, Yohana Ndunguru.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Sandali wakimpa mkono wa shukurani Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB, Ruth Mpangalala baada ya kukabidhiwa msaada wa madawati.

No comments:

Post a Comment