Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 27 February 2023

BANK OF AFRICA KUENDELEA KUWEZESHA BIASHARA NDOGO ZA KATI NCHINI

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Bank of Africa, Nandi Mwiyombella (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Nishati, January Makamba wakati alipotembelea banda la maonyesho la benki hiyo kwenye mkutano wa Jukwaa la Biashara la Nchi za Ulaya na Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni wafanyakazi wa Bank of Africa, Beatrice Mirigo (wa pili kushoto) na Jessica Mizambwa (wa pili kulia).

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Bank of Africa, Nandi Mwiyombella (kushoto) akimwelezea Waziri wa Nishati, January Makamba huduma zinazotolewa na Benki hiyo wakati alipotembelea banda la maonyesho la benki hiyo kwenye mkutano wa Jukwaa la Biashara la nchi za Ulaya na Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni wafanyakazi wa Bank of Africa, Beatrice Mirigo (wa pili kushoto) na Jessica Mizambwa (wa pili kulia).

Baadhi ya wageni waliotembea banda la maonyesho la Bank of Africa, wakipatiwa maelezo ya huduma zinazotolewa na benki kutoka kwa Wafanyakazi wa Benki hiyo.

Bank of Africa Tanzania, imeeleza dhamira yake ya kuendeleza Biashara ndogo na za kati nchini ili ziweze kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi kwa kasi na kuleta maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Bank of Africa Tanzania, Adam Mihayo, wakati akieleza ushiriki wa Benki hiyo katika Jukwaa la biashara la Tanzania na nchi za Ulaya (EU-Tanzania Business Forum) lililomalizika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

“Huu ni moja ya mkakati mkuu wa Benki yetu wenye lengo la kuunga mkono dira ya Serikali ya Tanzania katika ajenda ya ujumuishaji katika mfumo rasmi wa kifedha hususani katika makundi ya biashara ndogo na za kati na uwezeshaji wa Wanawake”, alisema.

Mihayo, alisema kuwa Bank of Africa, imekuwa na programu ya kuwapatia wafanyakabiashara wadogo na wa kati (SMEs) mafunzo ya uendeshaji biashara zao kwa ufanisi sambamba na kuwapatia mikopo kw ajili ya kukuza biashara zao.

Mkutano wa Jukwaa la Biashara la EU-Tanzania ulilenga kuonyesha fursa za biashara zilizopo nchini Tanzania na kueleza mikakati ya kufanikisha uwekezaji wa kibiashara kwa wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ulaya na Tanzania.

Bank of Africa, kupitia huduma zake bora na mtandao wake thabiti katika nchi 18 za Afrika imedhamiria kuendelea kufanikisha ushirikishwaji wa kifedha kupitia ubia na ushirikiano.

No comments:

Post a Comment