Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 20 June 2022

TANZANIA COMMERCIAL BANK YAPATA FAIDA YA BILIONI 19.7

 
Mwenyekiti wa bodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021 hatua inayo tajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa Benki ya TPB na TIB Corporate Bank.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza faida ya shilingi bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021.

 Mwenyekiti wa bodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 19.7 iliyopata benki hiyo. Wa pilikulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Sabasaba Moshingi pamoja na maafisa wengine wa benki hiyo.

Tanzania Commercial Bank (TCB) imetangaza kupata faida ya shilingi Bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021 hatua inayotajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa Benki ya TPB na TIB Corporate Bank.

Mwenyekiti wabodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa ametoa taarifa hiyo katika mkutano wa mwaka wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar esSalaam na kusema kuwa faida hiyo ni kabla ya kodi.

Faida iliyopatikana mwaka 2021 inatajwa na uongozi wa benki kuwa ni kubwa kufuatia ile ya mwaka 2020 ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa Benki ya TCB takriban miaka 95 iliyopita.

Amepongeza uongozi pamoja na wafanyakazi wa Tanzania Commercial Bank kwa kuchangia mafanikio hayo licha ya changamoto za mdororo wa uchumi uliosababishwa na wimbi la ugonjwa wa UVOKO-19 ambao pia umeathiri uchumi wa mataifa mengi duniani.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Sabasaba Moshingi amesema kufuatia mafanikio hayo, wanahisa wamekubaliana kutoa gawio la hisa na kuelekeza kwenye kuimarisha mtaji wa Benki hiyo.

Mafanikio hayo pia wamewezesha amana za wateja kuongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 1.18 mwaka 2021 kutoka shilingi trilioni 1.04 huku mikopo nayo ikiongezeka hadi kufikia shilingi bilioni 718.6 kutoka bilioni 617.81

Tanzania Commercial Bank imekuwa ikifanya kazi na wafanyabiashara kuanzia mfanyabiashara mdogo, wa kati na mkubwa na kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma kutoka benki ya TCB kila kona ya Tanzania na mipaka yake.

No comments:

Post a Comment