Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 15 June 2021

WAFANYAKAZI WA BENKI YA EQUITY WAJITOLEA DAMU KATIKA SIKU YA DAMU SALAMA DUNIANI

Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa ndani wa Benki ya Equity Tanzania, Douglas Bashobeza (kushoto) akiongoza wafanyakazi wa Benki hiyo katika tukio la uchangiaji damu kwa wahitaji lililofanyika katika Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Dar es Salaam, 14 Juni 2021 - Zaidi ya wafanyakazi 20 wa Benki ya Equity Tanzania wameongoza kampeni ya kujitolea damu ili kuokoa maisha ya wengine. Wafanyakazi hao wameamua kufanya kampeni hiyo ya uchangiaji damu ikiwa ni njia ya kuwasaidia wenye uhitaji katika hafla maalum iliyofanyika katiko Chuo cha Diplomasia, Kurasini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa ndani wa benki hiyo, Douglas Bashobeza amesema wafanyakazi wameonyesha mwitikio wa kipekee na ili kuokoa maisha ya Watanzania wengi wenye uhitaji wa damu.

“Niwashukuru wafanyakazi wa benki ya Equity kwa kuonyesha moyo wa upendo na kujitolea damu hapa leo. Benki ya Equity tunaonyesha kwa vitendo kauli yetu isemayo “Tupo Pamoja” kwa kuyafikia makundi mablimbali ya jamii. Hii ni sehemu ya huduma kwa jamii ambayo benki yetu ya Equity inasikia fahari kujumuika na ninatoa wito kwa watanzania wenzetu kujitokeza kwa wingi kuja kuunga mkono,” amesema Bashobeza.

Kila tarehe 14 Juni nchi zote duniani huadhimisha siku ya kimataifa ya kuchangia damu ili kuwawezesha wote wenye kuwa na mahitaji hayo.



“Kila mtoaji damu anaweza kusaidia kuokoa maisha hadi ya watu watatu. Ishara hiyo ya upendo ni chanya sana hata katika afya zetu. Watu wenye kuwa na damu nyingi, wanaboresha pia afya yao katika kutoa zawadi hiyo na shukrani kwa vipimo maalum ambapo pia katika utoaji damu unawezekana kugundua pia ugonjwa mapema unaoanza katika mwili wako na kutibiwa mapema. Ni suala la kutengeneza uwezekano wa kutunza afya yetu na kuhisi zaidi uwajibikaji wa kuchagua mtindo wa maisha yaliyo bora” alisema mmoja wa waandaji wa hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment