Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 6 October 2020

BENKI YA ACB YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUTOA ZAWADI KWA WATEJA WAKE

Meneja wa Benki ya ACB, Tawi la Tegeta Godlove Ernest, Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki ACB, Dora Saria (wa pili kulia) pamoja na maofisa wengine na wateja wa Benki hiyo wakikata keki kuashiria uzinduzi rasmi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja wa Benki ya ACB ikihamasisha kufanya kazi kama timu katika kufikia malengo ya kutoa huduma bora kwa wateja wake. Hafla ya uzinduzi huo ulifanyika katika Tawi la Benki hiyo lililopo Tegeta jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Benki ya ACB, Tawi la Tegeta Godlove Ernest (wa pili kulia), akimlisha keki mteja wa Benki hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja wa Benki ya ACB huku ikiwahakikishia wateja kufanya kazi kama timu katika kufikia malengo ya kutoa huduma bora kwa wateja wake.
Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki ACB, Dora Saria (katikati), akizungumza na wateja wa benki hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja.

Mteja wa Benki ya ACB, Tawi la Tegeta, Jude Lymo akitoa neno la shukrani kwa Benki hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa wiki ya mteja iliyofanyika katika Tawi la Benki hiyo lililopo Tegeta jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment