Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 14 February 2020

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA CRDB UKIONGOZWA NA MWENYEKITI WA BODI YA CRDB

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Ndg. Ally Hussein Laay, akitoa maelezo ya mafanikio ya Benki ya CRDB wakati wa mazungumzo hayo na kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa CRDB Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela. Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar,13-2-2020.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Ndg. Ally Hussein Laay, alipowasili katika ukumbi kwa mazungumzo na Ujumbe wa CRDB uliuofika Ikulu Jijini Zanzibar tarehe 13-2-2020 kwa mazungumzo na kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa CRDB Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na mgeni wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela, na (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Ndg. Ally Hussein Laay, wakitoka katika ukumbi baada ya kumaliza mazungumzo yao alipofika kujitambulisha Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na wageni wake (kushoto kwa Rais) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB. Ndg. Ally Hussein Laay na (kulia kwa Rais) Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB.Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Ndg. Ally Hussein Laay (kulia kwa Rais) na (kushoto kwa Rais) Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB. Ndg. Abdulmaji Mussa Nsekela.

No comments:

Post a Comment