Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 8 November 2019

BENKI YA DCB YASHINDA TUZO YA SOKO LA HISA LA DAR ES SALAAM

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (wa tatu kushoto), akikabidhi tuzo ya mshindi wa tatu katika kitengo cha makampuni bora ya mwaka katika eneo la uwekezaji katika sekta za kibenki kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Benki ya Biashara ya DCB, Regina Mduma wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa wanachama wa DSE jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine pichani kutoka kushoto ni; Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es salaam, Moremi Marwa, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji na Dhamana (CMSA), Nicodemus Mkama na Ofisa katika kitengo cha Sheria wa DCB, Grace Ringo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (kulia), akishikana mikono Mkurugenzi wa Kitengo Cha Sheria was Benki ya DCB, Regina Mduma, baada ya kumkabidhi iliyoshinda benki hiyo ya mshindi wa tatu katika kitengo cha makampuni bora ya mwaka katika eneo la uwekezaji katika sekta za kibenki wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa wanachama wa DSE jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Ofisa katika kitengo cha Sheria wa DCB, Grace Ringo. 
Mkurugenzi katika Kitengo cha Sheria wa Benki ya DCB, Regina Mduma (kulia), na Ofisa wa Kitengo hicho Grace Ringo wakionesha tuzo hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha.

No comments:

Post a Comment