Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 5 December 2018

DKT. KIGWANGALLA NA DKT. NDUMBARO WAFANYA MKUTANO WA PAMOJA NA WAANDISHI WA HABARI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akitoa neno la ufunguzi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Maiasili na Utalii, Mhe. Dkt. Khamis Kigwangalla kuongea na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo. Viongozi hao walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari kuelezea mikakati inayochukuliw na Serikali ya awamu ya tano ya kuvutia utalii nchini. Mikakati hiyo imeanza kuzaa matunda ambapo wnanchi wa Urusi wameichagua Tanzania kuwa eneo bora zaidi kwa utalii duniani na kutoa Tuzo maalum kwa serikali. Aidha, Mikakati iliyofanywa nchini China hivi karibuni imewezesha kuingiwa kwa Mkataba wa kuleta watalii elf 10 kutoka Shangai mwaka 2019. Kushoto ni Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Yuri popov.
Dkt. Kigwangalla akizungumza na Waandishi wa Habari hawapo pichani ambapo alitumia fursa hiyo kuwaeleza namna Watalii wanavyoongezeka kuja nchini kwa wingi. Alisema sekta ya utalii ndiyo inayoongoza kuingizia Taifa hili fedha za kigeni ambapo kitakwimu sekta hiyo inachangia asilimia 25 ya fedha zote za kigeni. Aidha. alitoa pongezi zake za dhati kwa balozi zetu zilizopo nje ya nchi kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuwa zimekuwa zikifanya jitihada kubwa katika kutangaza Vivutio vilivyopo nchini Tanzania ambapo kutokana na juhudi hizo Tanzania inapokea watalii wapatao Milioni 1.3 na malengo waongezeke zaidi kila mwaka.
Balozi wa Urusi naye akizungumza na Waandishi wa Habari.
Read More >>

No comments:

Post a Comment